FRANC THE GREAT
JF-Expert Member
- May 27, 2016
- 5,329
- 7,702
Urusi Yakataa Ombi La Irani Kuuziwa Mfumo Wa Ulinzi Wa Makombora Wa S-400
Urusi imekataa ombi la Irani kuuziwa mfumo wa ulinzi wa anga wa S-400, kukiwa na wasiwasi kuwa uuziwaji huo ungeweza kuongezeka zaidi mvutano katika eneo la Mashariki ya Kati.
Ombi hilo lilikataliwa na Rais Vladimir Putin, kwa kile kinachoelezwa kuwa, kwa kukubali ombi hilo la Irani huenda kungechochea zaidi mivutano na migogoro katika eneo la Mashariki ya Kati. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif alitembelea Moscow Mei 7.
Mauzo ya mifumo hii ya Makombora yamekuwa na utata katika Mashariki ya Kati huku Uturuki, mwanachama wa NATO na mshirika wa Marekani, akihatarisha hatua za adhabu za utawala wa Trump kwa kukubali kununua mitambo hiyo.
Rais wa Urusi, Vladimir Putin akiendesha mkutano wa kijeshi wa maswala ya anga huko Sochi, Urusi, Mei 15, 2019. (Reuters)
Mgomo wa Urusi kwa ombi la Irani unaonesha uwiano wa kinguvu katika Ghuba ya Uajemi, ambako kumekuwa na mvutano mkubwa kati ya Jamhuri ya Kiislamu kwa upande mmoja, na Umoja wa Mataifa na washirika wake wa Ghuba ya Uarabu kwa upande mwingine. Rais Donald Trump alikubali mwezi huu kutuma majeshi zaidi katika eneo hilo ikiwa ni baada ya Marekani kudai Irani kuhusika kwenye mashambulizi ya mitambo ya mafuta ya Saudia pamoja na meli nne.
Viongozi wa Irani wamekana kuhusika kwa Irani katika mashambulizi hayo.
Kuimarisha Uhusiano
Urusi na Irani wamekuwa na uhusiano wa karibu wa kisiasa na kijeshi katika miaka ya hivi karibuni, ingawa kuna ishara kwamba Moscow inatafuta kupunguza hatua za Iran katika eneo la Mashariki ya Kati ikiwa ni kutafuta kulinda uhusiano wake na mamlaka nyingine za kikanda kama Saudi Arabia na Israeli.
"Uimarishaji wowote wa kweli au wa kufikirika wa Irani unaweza kusababisha ongezeko - ikiwa Urusi imeikatalia Irani ombi kama hilo, inamaanisha kuwa Urusi inataka kuendelea kufanya kazi katika mahusiano na Saudi Arabia, Israeli na kuweka fursa ya mazungumzo na Trump," Ruslan Pukhov, mkuu wa Kituo cha Uchambuzi wa Mikakati na Teknolojia huko Moscow, alisema. "Ikiwa Urusi itaamua kuipatia Irani Mifumo ya S-400, itakuwa changamoto moja kwa moja kwa Saudi Arabia na Israeli, hivyo itakuwa kinyume na maslahi ya kitaifa ya Urusi."
Urusi ni mojawapo ya nchi zinazotetea mkataba wa nyuklia wa mwaka 2015 na Irani, ambapo Marekani iliachana nao mwaka jana kabla ya kurejesha vikwazo vya kiuchumi kwa Irani. Nchi hizo mbili pia zilimsaidia Rais wa Syria Bashar al-Assad kurejesha udhibiti wa maeneo karibia yote ya Syria baada ya miaka minane ya vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vilisababisha mamia ya maelfu ya watu kupoteza maisha.
S-400 ni Mfumo wa Makombora wa Ulinzi wa Anga ambao unauwezo wa kulenga shabaha katika umbali wa hadi kilomita 400 (maili 249).
Chanzo: The Moscow Times::Russia Rejected Iran S-400 Missile Request Amid Gulf Tension
Urusi imekataa ombi la Irani kuuziwa mfumo wa ulinzi wa anga wa S-400, kukiwa na wasiwasi kuwa uuziwaji huo ungeweza kuongezeka zaidi mvutano katika eneo la Mashariki ya Kati.
Ombi hilo lilikataliwa na Rais Vladimir Putin, kwa kile kinachoelezwa kuwa, kwa kukubali ombi hilo la Irani huenda kungechochea zaidi mivutano na migogoro katika eneo la Mashariki ya Kati. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif alitembelea Moscow Mei 7.
Mauzo ya mifumo hii ya Makombora yamekuwa na utata katika Mashariki ya Kati huku Uturuki, mwanachama wa NATO na mshirika wa Marekani, akihatarisha hatua za adhabu za utawala wa Trump kwa kukubali kununua mitambo hiyo.
Rais wa Urusi, Vladimir Putin akiendesha mkutano wa kijeshi wa maswala ya anga huko Sochi, Urusi, Mei 15, 2019. (Reuters)
Mgomo wa Urusi kwa ombi la Irani unaonesha uwiano wa kinguvu katika Ghuba ya Uajemi, ambako kumekuwa na mvutano mkubwa kati ya Jamhuri ya Kiislamu kwa upande mmoja, na Umoja wa Mataifa na washirika wake wa Ghuba ya Uarabu kwa upande mwingine. Rais Donald Trump alikubali mwezi huu kutuma majeshi zaidi katika eneo hilo ikiwa ni baada ya Marekani kudai Irani kuhusika kwenye mashambulizi ya mitambo ya mafuta ya Saudia pamoja na meli nne.
Viongozi wa Irani wamekana kuhusika kwa Irani katika mashambulizi hayo.
Kuimarisha Uhusiano
Urusi na Irani wamekuwa na uhusiano wa karibu wa kisiasa na kijeshi katika miaka ya hivi karibuni, ingawa kuna ishara kwamba Moscow inatafuta kupunguza hatua za Iran katika eneo la Mashariki ya Kati ikiwa ni kutafuta kulinda uhusiano wake na mamlaka nyingine za kikanda kama Saudi Arabia na Israeli.
"Uimarishaji wowote wa kweli au wa kufikirika wa Irani unaweza kusababisha ongezeko - ikiwa Urusi imeikatalia Irani ombi kama hilo, inamaanisha kuwa Urusi inataka kuendelea kufanya kazi katika mahusiano na Saudi Arabia, Israeli na kuweka fursa ya mazungumzo na Trump," Ruslan Pukhov, mkuu wa Kituo cha Uchambuzi wa Mikakati na Teknolojia huko Moscow, alisema. "Ikiwa Urusi itaamua kuipatia Irani Mifumo ya S-400, itakuwa changamoto moja kwa moja kwa Saudi Arabia na Israeli, hivyo itakuwa kinyume na maslahi ya kitaifa ya Urusi."
Urusi ni mojawapo ya nchi zinazotetea mkataba wa nyuklia wa mwaka 2015 na Irani, ambapo Marekani iliachana nao mwaka jana kabla ya kurejesha vikwazo vya kiuchumi kwa Irani. Nchi hizo mbili pia zilimsaidia Rais wa Syria Bashar al-Assad kurejesha udhibiti wa maeneo karibia yote ya Syria baada ya miaka minane ya vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vilisababisha mamia ya maelfu ya watu kupoteza maisha.
S-400 ni Mfumo wa Makombora wa Ulinzi wa Anga ambao unauwezo wa kulenga shabaha katika umbali wa hadi kilomita 400 (maili 249).
Chanzo: The Moscow Times::Russia Rejected Iran S-400 Missile Request Amid Gulf Tension