Urusi yakabiliwa na vikwazo kutokana na mzozo wake wa kuivamia Ukraine

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
1645608374000.png

Bunge la Urusi limepitisha agizo la Rais Vladimir Putin la kutambua uhuru wa maeneo ya waasi mashariki mwa Ukraine, siku moja baada ya Rais Putin kutia saini agizo hilo na kuamuru wanajeshi kuingia katika maeneo hayo. Huku haya yakijiri Urusi inakodolea macho vikwazo kutoka nchi za magharibi kuhusiana na mgogoro unaoendelea kufukuta kati yake na Ukraine.

Agizo hilo limeungwa mkono kwa kauli moja katika baraza la wawakilishi mjini Moscow. Mabalozi wa Urusi katika mataifa kadhaa ya Ulaya, yakiwemo Austria na Uingereza, wametakiwa kufika katika wizara za mambo ya kigeni za mataifa hayo kujieleza kuhusiana na agizo la jana la Rais Vladimir Putin.

Taarifa kutoka kwa wakuu wa Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen, na Charles Michel imesema umoja huo unatafakari kuwekea vikwazo benki za Urusi zilizo na matawi katika maeneo ya majimbo yanayodhibitiwa na waasi wa Ukraine ya Luhansk na Donetsk. Hata hivyo vikwazo hivyo vitahitaji ridhaa kutoka kwa nchi zote 27 wanachama.

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema Uingereza itaweka vikwazo kwa benki tano za Urusi na watu watatu "wenye hadhi ya juu" kufuatia kutumwa kwa wanajeshi katika mikoa miwili inayoungwa mkono na Moscow.

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz ametangaza kuwa mchakato wa kuidhinisha matumizi ya bomba la gesi la Nord Stream 2 umesimamishwa. Ujenzi wa bomba hilo linaloziunganisha Ujerumani na Urusi kupitia chini ya bahari umekamilika, lakini utata unaolizunguka umelizuia kuanza kufanya kazi hadi sasa.

Aidha kansela Scholz amesema "Rais wa Ukraine Zelenskiy anastahili heshima yetu kubwa, kwamba nchi yake haikubali kuchokozwa na Urusi, kwa sababu ndicho hasa Rais wa Urusi anachosubiri, ili kuwa na kisingizio cha kuteka Ukraine nzima."
 
Tatizo Mwamerika huyu aliyeingia juzi anatumia njia za karne ya BC kupambana na vita vya Post-Modernism!
 
Mimi mrusi mweusi niliyeko huku Tandahimba nasema vikwazo sisi tumeshazoea , na kabla hata hatujaingia Ukraine tulijua kuwa tukiingia tutawekewa vikwazo lakini Wala hatukujali , Kama wao ni wanaume kweli wasogee Ukraine tupambane waone kilicho mtoa kanga manyoya
 
Safi wao waweke vikwazo tu hawakuanza leo. TAARIFA MBAYA KWAO NI KWAMBA QATAR INASEMA HAKUNA NJIA NYINGINE YA KUPITISHA BOMBA LA GESI ZAIDI YA RUSSIA. ukiziba uwani napita sebuleni. Ufm habari.
Raha Sana
 
Ukiachana na mengine yote ila Putin ana sauti kwa kuweza kuzinukyamazusha baadhi ya nchi.
 

Bunge la Urusi limepitisha agizo la Rais Vladimir Putin la kutambua uhuru wa maeneo ya waasi mashariki mwa Ukraine, siku moja baada ya Rais Putin kutia saini agizo hilo na kuamuru wanajeshi kuingia katika maeneo hayo. Huku haya yakijiri Urusi inakodolea macho vikwazo kutoka nchi za magharibi kuhusiana na mgogoro unaoendelea kufukuta kati yake na Ukraine.

Agizo hilo limeungwa mkono kwa kauli moja katika baraza la wawakilishi mjini Moscow. Mabalozi wa Urusi katika mataifa kadhaa ya Ulaya, yakiwemo Austria na Uingereza, wametakiwa kufika katika wizara za mambo ya kigeni za mataifa hayo kujieleza kuhusiana na agizo la jana la Rais Vladimir Putin.

Taarifa kutoka kwa wakuu wa Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen, na Charles Michel imesema umoja huo unatafakari kuwekea vikwazo benki za Urusi zilizo na matawi katika maeneo ya majimbo yanayodhibitiwa na waasi wa Ukraine ya Luhansk na Donetsk. Hata hivyo vikwazo hivyo vitahitaji ridhaa kutoka kwa nchi zote 27 wanachama.

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema Uingereza itaweka vikwazo kwa benki tano za Urusi na watu watatu "wenye hadhi ya juu" kufuatia kutumwa kwa wanajeshi katika mikoa miwili inayoungwa mkono na Moscow.

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz ametangaza kuwa mchakato wa kuidhinisha matumizi ya bomba la gesi la Nord Stream 2 umesimamishwa. Ujenzi wa bomba hilo linaloziunganisha Ujerumani na Urusi kupitia chini ya bahari umekamilika, lakini utata unaolizunguka umelizuia kuanza kufanya kazi hadi sasa.

Aidha kansela Scholz amesema "Rais wa Ukraine Zelenskiy anastahili heshima yetu kubwa, kwamba nchi yake haikubali kuchokozwa na Urusi, kwa sababu ndicho hasa Rais wa Urusi anachosubiri, ili kuwa na kisingizio cha kuteka Ukraine nzima."
hivi zombokoo Urusi kabisaa waiwekee vikwazo?? haina cha kupoteza saaaana wameipunguzia kuipeleleza!!! NATO wasumbufu sana wkt zao zinahesabika u super power sasa unaingia kwa Mchina!! NATO wana jua china na urusi damudamu na mchina ana hela mbaya!!

NATO WAkijipendekeza tu watapigwa mpaka wapoteze mwelekeo wa huo u super power wao!! na wanajua hilo?... lkn akitokea mlevi mmmoja wa vihepe akalikoroga ndo NATO ina kufa kibudu!!...subiri tu
 
Bana weee!!! huwezi kuwekea jabali vikwazo!!! ni kuutesa moyo wako tu!!! .......ukijaribu yeye anaziba kabisaaaa! kimyaaa!! ni km vile tu tangu nyerere aikatae israel!! wao israel walichomoa betrii mazimaaaa mpaka leo!!...hawaji! hamuendi!! wako hukoo!!

mkiwataka wao balozi wao yuko kenyaaaaaaaa!!...ila wenu yuko Tel aviv!...Hata mjipendekeze vipi hawaji huko!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom