Uropokaji huu wa Membe utaibua upya mzozo wa kidiplomasia kati ya Rwanda na Tanzania

Tanzania kwa mara ya Kwanza imesema inayo uhakika kuwa waasi wa M23 walioondolewa nchini Jamuhuri ya Kongo ni ni raia Rwanda.Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Benard Membe ameliambia Bunge la Tanzania kuwa anao uhakika kuwa waasi M23 walitokea nchini Rwanda.

Hii ni Mara kwanza kwa Tanzania kukiri hadharani kuwa inao uhakika kuwa waasi hao ni raia wa Rwanda.
Taarifa zinazohusiana

Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimepeleka majeshi Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo kwa kushirikiana na yale ya umoja wa Mataifa yaliwaondoa waasi hao DRC

Benard Membe Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania

Matamshi hayo ya Waziri huyo aliyatoa wakati alipokuwa akiwasilisha hotuba ya Bajeti ya Wizara yake ambapo pia alikiri kuwa bado uhusiano wa Tanzania na Rwanda sio mzuri.

Hata hivyo upande wa Upinzani mlishambulia Waziri huyo wa Mambo ya nje Benard Membe wakidai kwamba Waziri huyo anachochea kuvurugika kwa uhusiano wa Watanzania na Rwanda kwa kuhisi kuwa M23 ni Wanyarwanda nahata kutaka achukuliwe adhabu kali.

Mbali na tuhuma hizo Waziri Membe alizidi kusisitiza kuwa waasi wa M23 ni raia wa Rwanda akisema hiyo ni ripoti ya Umoja wa Mataifa.

Mbali na waziri baadhi ya wabunge wanamuunga mkono waziri Membe kuwa waasi wa M23 ni raia wa Rwanda.

Matamshi haya Waziri wa Tanzania kuhusu M23 bado haijulikana ni kwa namna gani utaathiri uhusiano wa Tanzania na Rwanda kama utakuwepo huenda ukajulikana hapo baadae.

View attachment 160985
Waziri Membe akiropoka bungeni
Source: BBC

kitu kama kweli M23 ni wanyarwanda taabu ipo wapi? Kama alichosema Membe ni uongo uuthibitishe uongo wake. Na hawa wapinzani hamjawajua bado, wanatafuta umaarufu na kutetea wananchi waliowapeleka bungeni. Think Big.
 
Membe karefer report ya UN sasa sijui tatizo liko wapi.Halafu uwe unapenda pia kujisomea ili ujue kuliko kutumia mawazo ya watu maana nina uhakika ungesoma kuhusu march 23 nadhani ungewaelewa sana
 
Repory ya UN ndio inasema M23 ni watusi,sasa wewe una mwandama membe kwa vile ni shemeji yako
 
Mtoa mada umekurupuka! UN ndiyo ya kwanza na mpaka report ilitolewa, marekani ikaionya Rwanda, hata Obama alipokuja mwandishi wa habari wa Congo Silaji Kalyango alimuuliza Obama anachukua hatua gani waasi na kundi la Rwanda kuivamia Congo kubaka wanawake na mauaji. Obama akaahidi hatua kuchukuliwa maana Kagame Alisha onywa.
You know nothing about Americans attitude toward Rwanda, They are much closer than you think!You can't separate France from the DRC conflict too!!
 
Mnacho kosea Chadema ni kutaka kupinga kila kitu! Kuna siku mtapinga kuwa Boko Haram sio Wanigeria!
That's absurd,Really! I hope you also noticed how foolish you sound with such stupid remarks if you have any brain left in your pumpkin like head! Didn't you?
 
Jamani tuwe waangalifu wakati wa kuishi na majirani na Wah MaRais Kikwete na Kagame wanaendelea vizuri katika maongezi yao na kidiplomasia bado wako vizuri. Hayo ya Membe it's totally uncalled for ni vema tukawa waangalifu na jinsi tutumiavyo ndimi zetu ulimi wa membe utatuponza sie watu wa chini....hakina kitu kibaya kama vita.....bado hatujafungua mikanda tangu ya Idd Amin...mwenye macho haambiwi tazama KARAGABAHO.
 
Niliwahi kuandika hapa juu ya maovu ya ndugu Kagame, ni mvivu pekee wa kusoma ambaye hatoamini kua M23 walnafadhiliwa na Kagame na kaka yake Museven, CIA ambao ndo walijifanya waandishi wa habari walilifanya hili kwa ustadi mkubwa sana na baadhi ya mawasiliano ya Kagame na viongozi wa M23 ylinaswa muda mrefu na vikao vya Kagame na ndugu zake vingi vilifanyika Gisenyi nyakati za usiku au katika wilaya ya Nyagatare ndo walifanyia vikao vyao.
 
Weka hiyo ripoti tuione
Mtoa mada umekurupuka! UN ndiyo ya kwanza na mpaka report ilitolewa, marekani ikaionya Rwanda, hata Obama alipokuja mwandishi wa habari wa Congo Silaji Kalyango alimuuliza Obama anachukua hatua gani waasi na kundi la Rwanda kuivamia Congo kubaka wanawake na mauaji. Obama akaahidi hatua kuchukuliwa maana Kagame Alisha onywa.
 
Suala la Chadema kumfagilia Kagame ni kutaka ufadhili wa uchaguzi mkuu kama walivoanza mazungumzo na maafisa usalama wa Rwanda na hili linafahamika wazi, hakuna diplomasia tena kwa mtu anaewatesa Watanzania wanatumia mpaka wake au waishio kwake tena huku wakijisifu kukomesha na janja yake ya maafisa wake kutumia Passport za Uganda ili kuingia TZ kirahisi ilishagunduliwa asidhani haifahamiki vyema, lazima ukweli usemwe na usibembeleze urafiki na adui asiependa muafaka na wewe huo ni utumwa.
 
Huyu Membe ningemshauri ajaribu kufanya mawasiliano na kina Joshua Arap Sang na wenzake wampe mwongozo wa kinachoendelea pande za THE HEGUE ili walau apate tips za kinachojili huko kwani ulimi ni kiungo kidogo sana ila kisivyotumika sawa sawa kinaweza kukuletea majanga.
 
Naipenda CHADEMA, ila hapa nimekuwa na wasiwasi mkubwa. Kauli si ya Membe ni ya UN. Alichosema Membe hata Lipumba (team UKAWA) aliunga Mkono MUNUSCO. Nimeionea huruma CDM
 
Hapa sasa naona kwa mbaaaaali vita kamili vya nchi na nchi na ukizingatia ile mikwara ya juzi kati kwenye sherehe za Muungano!. Nahisi kitu.
 
Everybody knows kwamba wale ni wanyarwanda swali la msingi:kulikuwa na haja ya kutaja jana bungeni kwamba m23 ni wanyarwanda?
 
mtoa mada naona una ushabiki wa kisiasa maana umeamua kuchagua ya kuandika. cha kushangaza zaidi unaleta mada kwa kusikia hotuba ya membe bila ya kufanya uchambuzi wa kutosha. gazeti la serikali la rwanda linaisema tanzania na familia ya rais vibaya kwa makala zisizo na miguu wala kichwa. tanzania na rais anatukanwa halafu unaleta ushabiki maandazi. haya ni mambo ya kitaifa hayana chama. rais ni taasisi na tanzania ni yetu sote. watu kama wewe + upinzani maandazi = janga la tiafa
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom