Urgent Please!! Nataka kununua Nissani Civilian Bus

Original Pastor

JF-Expert Member
Nov 14, 2007
1,274
50
Wana JF habari wakubwa??

Naomba Ushauri nataka kununua Nissani Civilian Bus ili nifanya daladala sasa naomba ushauri kwa mwenye kujua aina nzuri ya Magari hayo maana mimi nataka kununua Engine ya BW40. year 1997 CC 3500 sasa aina ni nyingi sana. Sasa ili nisije kushindwa kulipa huu mkopo nataka nipate kitu nikae nacho miaka Mitano. Naomba ushauri tafadhali.
 
OP, mambo ya fungu la kumi nini? kweli wa madhabauni atakula madhabahuni
 
Tafuta engine bw 32..itakutoa sana ni roho ya paka...inahimili sana vishindo!!
 
OP, mambo ya fungu la kumi nini? kweli wa madhabauni atakula madhabahuni
acha ujuha hiyo ni elimu pana, hujajua kama madhabahu huajiri watenda kazi? maana imeandikwa asiyefanya kazi na asile, na kashi ya madhabahu ni kukesha kwa maombi kwa ajili wasyoijua elimu ya maandiki kama wewe
 
Wana JF habari wakubwa??

Naomba Ushauri nataka kununua Nissani Civilian Bus ili nifanya daladala sasa naomba ushauri kwa mwenye kujua aina nzuri ya Magari hayo maana mimi nataka kununua Engine ya BW40. year 1997 CC 3500 sasa aina ni nyingi sana. Sasa ili nisije kushindwa kulipa huu mkopo nataka nipate kitu nikae nacho miaka Mitano. Naomba ushauri tafadhali.
wasiliana na nasi kwa +971 50 8522237 au +971 50 6553398 usaidiwe zaidi
 
Mkuu why unataka kununua Nissan Civillian?mimi kwa ushauri wangu kama unataka gari ukae nayo muda mrefu kama daladala nakushauri ununue toyota Coaster,chukua huo mkopo uongezee hela kidogo tu ununue coaster manake nissan civillian huwa matatizo yake makubwa ni kuchemsha!kama ukipata usajili wa Mwenge Mbagala ROUTE hutamaliza siku bila hiyo gari kuchemsha na ukalazimika kurudisha nauli kwa abiria wako.

Na katika hii industry ya madaladala kulikoni uwe na gari mbovu ni bora usiwe nayo kabisa manake hata kama haijachemsha dereva na konda wanakupiga changa kwa kukudanganya!

Nakushauri mkuu coaster unapata kuanzia 25million had 40million depends on the engine type.Bora ununue coaster mkuu.
 
Wana JF habari wakubwa??

Naomba Ushauri nataka kununua Nissani Civilian Bus ili nifanya daladala sasa naomba ushauri kwa mwenye kujua aina nzuri ya Magari hayo maana mimi nataka kununua Engine ya BW40. year 1997 CC 3500 sasa aina ni nyingi sana. Sasa ili nisije kushindwa kulipa huu mkopo nataka nipate kitu nikae nacho miaka Mitano. Naomba ushauri tafadhali.

Mkuu mimi sio mtaalam wa mambo ya magar lkn siku moja nilikua nimekaa somewhere nikasikia konda wa daladala anapiga stori na wenzake flan.
Alikua anamkandia jamaa 1 kua kwa nini amenunua gari ya aina gani sijui. Akawa anasema wee mtu mlalahoi kwa nini usinunue DCM.
In short mazungumzo yake yalikua yakimaanisha ni bora m2 ununue DCM kwa daladala kwa wale wanaoanza biashara hii.
Wataalam wa hilo labda mtatoa mchango zaidi.
 
Kwanza hongera kwa kuwa na wazo kama hilo na pia kuomba ushauri.....!
Nunua ili ifanye kazi na utoe ZAKA,SADAKA,CHANGIZO LA WATAKATIFU,FUNGU LA KUMI ,N.K....!
Tatizo la nissan civilian ni GEAR BOX......! ambayo hupatikana kwa kati ya laki sita hadi saba kwa iliyotumika maeneo ya temeke....!
Ni bora pia kama hujaagizia bado, ukawaomba wakuwekee katika gari hiyo watakayotuma GEAR BOX za akiba kama mbili au tatu......!
NAWE UTASHANGAA.....!
 
Back
Top Bottom