Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
KATIKA historia ya chaguzi zote, mikoa yenye idadi kubwa ya watu ya Kanda ya ziwa, kanda ya Nyanda za Juu kusini na mkoa wa Dar es Salaam ndipo ambako chama tawala kimekua kikipata ushindi wa kishindo. Kwa uchaguzi wa mwaka huu, mambo yamekua tofauti.
Pamoja na kuwa kuna utata wa ajabu katika baadhi ya majimbo (mfano Hai na Iringa) ambako kura zimejichanganya (mfano Mbowe 118 Kikwete 118, Fuya 77, Slaa 75) bado Chadema imejikita na kufanya vyema katika mikoa ya kanda ya ziwa, ya Mwanza, Kagera, Mara na Shinyanga na mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ya Mbeya na Iringa na kugawana kura na CCM mikoa ya Ruvuma, Kigoma na Rukwa huku CCM ikipata ushindi mkubwa katika mikoa ya Pwani, Tanga, sehemu ya Dar es Salaam (wanakogawana na Chadema na CUF) na mikoa ya Lindi na Mtwara (wanakogawana na CUF), mikoa ambayo ina idadi ndogo ya watu, pamoja na mikoa ya Zanzibar na Pemba ambako nako CCM na CUF wanagawana.
Mikoa mingine yenye idadi ndogo ya watu ya Morogoro, Singida na Dodoma nako CCM imefanya vizuri lakini Chadema nako imeambulia kura, kama vile jimbo la Singida Mjini ambako ni ngome kuu ya CCM, JK amepata kura zaidi ya 19,000 na Chadema kuyra 5,000, hizo si haba kabisa ukilinganisha na matokeo ya kanda ya ziwa na Nyanda za Juu Kusini.
Ukiangalia matokeo yanayotangazwa na NEC utaona wamechukua kwa kiasi kikubwa matokeo ya mikoa ya Zanzibar na Pemba, na mikoa ambayo CCM imefanya vizuri. Jambo la ajabu sana hata Arusha na MWanza ambako wametangaza matokeo ya Ubunge, wanaruka kutangaza matokeo ya Urais.
Katika majimbo ya Ubungo na Kawe, wamezidi kuchelewesha kama walivyofanya Arushwa, Nyamagana na Ilemela na Hananga matokeo yanachanganya ambako Mary Nagu anaelezwa kwamba ameshinda kwa tofauti ya kuyra 45 kama ilivyo matokeo tata ya Kigoma Mjini, ambako Peter Serukamba, yamewachanganya watu wa Kigoma.
Kwa uchambuzi huo, hali si shwari kabisa na kama MWanza, Arusha, Ubungo na Kawe wamekuwa wagumu kukubali matokeo, haijulikani hali ikoje kwenye matokeo ya Urais wa Muungano na kule Zanzibar.
Pamoja na kuwa kuna utata wa ajabu katika baadhi ya majimbo (mfano Hai na Iringa) ambako kura zimejichanganya (mfano Mbowe 118 Kikwete 118, Fuya 77, Slaa 75) bado Chadema imejikita na kufanya vyema katika mikoa ya kanda ya ziwa, ya Mwanza, Kagera, Mara na Shinyanga na mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ya Mbeya na Iringa na kugawana kura na CCM mikoa ya Ruvuma, Kigoma na Rukwa huku CCM ikipata ushindi mkubwa katika mikoa ya Pwani, Tanga, sehemu ya Dar es Salaam (wanakogawana na Chadema na CUF) na mikoa ya Lindi na Mtwara (wanakogawana na CUF), mikoa ambayo ina idadi ndogo ya watu, pamoja na mikoa ya Zanzibar na Pemba ambako nako CCM na CUF wanagawana.
Mikoa mingine yenye idadi ndogo ya watu ya Morogoro, Singida na Dodoma nako CCM imefanya vizuri lakini Chadema nako imeambulia kura, kama vile jimbo la Singida Mjini ambako ni ngome kuu ya CCM, JK amepata kura zaidi ya 19,000 na Chadema kuyra 5,000, hizo si haba kabisa ukilinganisha na matokeo ya kanda ya ziwa na Nyanda za Juu Kusini.
Ukiangalia matokeo yanayotangazwa na NEC utaona wamechukua kwa kiasi kikubwa matokeo ya mikoa ya Zanzibar na Pemba, na mikoa ambayo CCM imefanya vizuri. Jambo la ajabu sana hata Arusha na MWanza ambako wametangaza matokeo ya Ubunge, wanaruka kutangaza matokeo ya Urais.
Katika majimbo ya Ubungo na Kawe, wamezidi kuchelewesha kama walivyofanya Arushwa, Nyamagana na Ilemela na Hananga matokeo yanachanganya ambako Mary Nagu anaelezwa kwamba ameshinda kwa tofauti ya kuyra 45 kama ilivyo matokeo tata ya Kigoma Mjini, ambako Peter Serukamba, yamewachanganya watu wa Kigoma.
Kwa uchambuzi huo, hali si shwari kabisa na kama MWanza, Arusha, Ubungo na Kawe wamekuwa wagumu kukubali matokeo, haijulikani hali ikoje kwenye matokeo ya Urais wa Muungano na kule Zanzibar.