Don Clericuzio
JF-Expert Member
- Dec 8, 2017
- 16,936
- 40,518
Kwa washabiki wa mpira watakumbuka jinsi washabiki wa Manchester United walijikuta hawana jinsi isipokuwa kumshabikia adui jirani.
Hii ni kwa sababu wasingependa hasimu wao mkubwa Liverpool FC achukue ubingwa na kuwakaribia.
Hali waliyokuwa nayo washabiki wa Man United tunaenda kukutana nayo kwenye uchaguzi wa Rais 2020.
Rais aliyepo madarakani amekuwa adui kwa walio wengi, tena adui mkuu.
Upinzani mpaka sasa unajua kwa sababu ya kutokuwepo tume huru CCM lazima itashinda.
Sasa hivi ameibuka Membe, wote tunajua hana tofauti na CCM wenzake lakini kwa jinsi ambavyo nchi inaenda mahali kusiko julikana, ni bora tumpe Membe hata kama tunajua hana tofauti na CCM wengine.
Kama kuna kada haijaathiriwa na sera potofu za Magu, hiyo itakuwa ni kada ya kimalaika.
Natamani Magu aendelee kuwanyoosha CCM ili akili iwakae sasa kwa kipindi hiki kidogo kilichobaki, wafanye maamuzi ya liwalo na liwe.
Hii ni kwa sababu wasingependa hasimu wao mkubwa Liverpool FC achukue ubingwa na kuwakaribia.
Hali waliyokuwa nayo washabiki wa Man United tunaenda kukutana nayo kwenye uchaguzi wa Rais 2020.
Rais aliyepo madarakani amekuwa adui kwa walio wengi, tena adui mkuu.
Upinzani mpaka sasa unajua kwa sababu ya kutokuwepo tume huru CCM lazima itashinda.
Sasa hivi ameibuka Membe, wote tunajua hana tofauti na CCM wenzake lakini kwa jinsi ambavyo nchi inaenda mahali kusiko julikana, ni bora tumpe Membe hata kama tunajua hana tofauti na CCM wengine.
Kama kuna kada haijaathiriwa na sera potofu za Magu, hiyo itakuwa ni kada ya kimalaika.
Natamani Magu aendelee kuwanyoosha CCM ili akili iwakae sasa kwa kipindi hiki kidogo kilichobaki, wafanye maamuzi ya liwalo na liwe.