Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

C C M, C C M, C C M, Sikilizeni kilio cha Wananchi.

Wananchi tunateseka na Shida huku mtaani.
Je hamuoni siku hizi wananchi hawafanyi mambo ya maendeleo kwakuwa hawana uwezo.

Mfano, ukizunguka hapa jijini Daresalaamu,
Shughuri za Ujenzi wa Nyumba za kuishi hakuna.
Badala take siku hizi watu wanaziuza nyumba zao tena kwa bei che kabisa.
Nendeni Chamazi mkajionee karibu kila nyumba inauzwa, mafundi ujenzi hawana kazi tena kwa sasa.
Hapo tunajumlisha mafundi uashi, rangi, bomba, kuezeka, sakafu, marumaru nk.
Jambo hili linathibitisha kushuka kwa uwezo wa kunua wa wananchi, ( purchasing power )

C C M, ni lazima muingilie kati kwa jambo hili.
Wananchi wamekuaminini na kukuchagueni kwa miaka mingi ili muwanasue na huu mkwamo wao.

Ukweli ndio huu,
Unapo kataa kumpandishia mfanyakazi mshahara kwa miaka mingi, unampunguzia mwananchi uwezo wa kiuchumi kwa kiasi kikubwa na sio mfanyakazi tu.

Kumbuka mfanyakazi akijenga nyumba mafundi wata inua kipato chao.
Akishona nguo, au kulipa ada ya mtoto, anawaongezea kipato hao wateja wake.
Nakadharika.

Hivi ikitokea mmepata Raisi anayetesa RAIA wake namna hii bado mtampa awamu ya pili kugombea kiti cha uraisi ?

Kama anasera ya kufunga mkanda ili ajenge miundombinu, basi ilibidi kwanza aweke mjadala wa wazi ili kila MTU tu aridhie kuufunga huo mkanda Bali pia ajiandae na huo mkanda wake.

Na sio tu kumlazimisha mwananchi bila ridhaa yake huku tukishuhudia baadhi ya wananchi wakijitapa tena hadharani kuwa wanaishi maisha ya raha mustarehe kwa sasa.

Kama hamumpendekezi Membe, basi mpeni kijiti, Januari Makamba au Masele. Mbona mna watu wengi waadirifu na wema kwa raia.

Tatizo LA upinzani naona kwa kipindi chote hiki bado hawajajipanga katika ngazi ya mgombea uraisi.
Mkituuliza wananchi kwa sasa wala hatujui Upinzani umemwandaa nani kugombea kiti cha Uraisi.

C C M, C C M, C C M, Chama Cha Mapinduzi, Sikieni kilio Cha Wananchi Wenu.

Naipenda Nchi Yangu Tanzania na Sina pa Kukimbilia, Hakika Ningekimbilia.
Walikuwa wapigadili wacha waisome namba. Hakuna tena mambo ya dili
 
Haya yaliyofanyika Jana ya kuandaa maandamano ya kubumba ni aibu kubwa na fedheha .

Hii imetudhalilisha kama taifa, huu ni uthibitisho tosha kuwa tumeishiwa viongozi walio wabunifu na weledi katika mambo ya kidiplomasia.

Haingii akilini kabisa kuwa jambo liko mahakamani wewe huku unakwenda kushinikiza ubalozi uchukue hatua za kuingilia muhimili wa mahakama.

Pia huu ni uthibitisho tosha kuonyedha jinsi nchi yetu inavyo usigina utawala wa kisheria, tunayo fanyiwa humu kwetu (kupindisha pindisha sheria wanavyo taka wao kama watawala ) wanadhani kuwa yanaweza kupokelewa na mataifa mengine.

Kama serikali haihusiki katika hili basi ni mategemeo yetu kuona kuwa wale wahuni wote walio ratibu maandamano pamoja na waliohusika kuandamana wote wanasakwa na kuchukuliwa hatua Kali ili iwe fundisho.

Ila kama watakaa kimya tutajua kuwa ni mpango ulio pangwa toka ngazi za juu. Na hapo ndipo tunapoona umuhimu wa kuwa na watu walio bobea kwenye mambo ya kidiplomasia kama Membe ili watuondolee aibu kama hizi. Membe jiandae kuzoa kura nyingi 2020.

MUNGU IBARIKI TANZANIA ILI TUONDOKANE NA AIBU KAMA HIZI.
 
Acheni kujitoa akili watu waliandamana south africa kupinga tu kauli ya Makonda kuhusu ushoga hamkushangaa itakuwa sisi kuandamana kuhusu ndege
 
Jamaa tukomae nae tu ili akili zisogee maana watanzania akili zao zinahitaji watu wa namna hii.hakuna cha membe wala nani tukomae na jamaa hadi kieleweke G Clamp ikikazwa vizuri tutajifunza kuandamana au vipi wajomba.
 
Kama ni upinzani ni kwanini? Je kama ni chama tawala ni kwa nini? Hebu wabobebezi wa masuala ya kisiasa njooni tuchambue kwa kina
 
Mambo yataeleweka tu. Mjomba nyoosha nchi tu. Umeshavuka wami bado kidogo tu chuma kilainike. 2020 ongeza 20 tena tiyari tutakuwa tumekuelewa. Hakuna membe wala pembe ya kukutisha
 
Mashabiki na waimba mapambio wengi wa mambo ya sasa hawapo kwenye utumishi wa umma. Kama wapo ni wale ambao wanakula
 
Labda kama mnatafuta sura nzuri lakini he is one of the most hopeless people i ever know.
 
Tunaenda na Magu mpaka 2022 ( Miaka 7 awamu ya kwanza) then anatuchukua awamu ya pili mpaka 2029 akimaliza hana cha kuongeza muda then ndio tunaanza kujadili wengine wa kumrithi
Moshi wa Ruangwa hauwezi kusubiria hadi huko
 
Tunaitaka Tanzania yenye furaha na amani, tunaitaka Tanzania ile yenye viongozi wanaoheshimu sheria na katiba ya nchi yetu, Tanzania iliyosifika kwa uimara wa diplomasia na Ushirikiano wa kimataifa , Tunaitaka Tanzania yenye viongozi wanaohezhimu wananchi wake, viongozi wanaoheshimu utu na faragha ya wananchi, tunaitaka Tanzania ile yenye viongozi wanaoheshimu haki za binadamu.
 
Back
Top Bottom