Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Lancanshire

JF-Expert Member
Sep 20, 2014
14,043
10,326
Habari za muda mabibi na mabwana!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza nawashauri wanachama wenzangu na wananchi kwa ujumla. Mwaka 2020 tusipoteze tena kama ilivyotokea mwaka 2015. Haya yote ni kwa sababu hatukutulia vizuri katika mchujo wa kumpata kiongozi bora.

Karibuni kwa maoni yenu.
1581065214084.png

====

Naomba niwaambieni kwa wale wambao mnafikiri ndani ya CCM hapawezi kua na mabadiliko yeyote ni kujidanganya kwa ssbabu ya mazoea ya nyuma, kwa vijana mliokua juzi yawezekana hamjui kitu ndio maana mnajipa matumaini kwa msilolijua. Hamuelewi na hamwezi kujua.

Siasa sio ubabe wala vitisho bali ni ufundi wa mtu kulingana na utashi wake. Ndani ya CCM kuna wanachama wenye kadi na katiba ya chama, wameisoma katiba na wanaelewa yaliyomo ndani yake na yanayoendelea hivi sasa. Ili kuepusha mgogoro ndani ya CCM ya sasa ni bora watu waachwe wateme nyongo zao kiliko kutumia mabavu na kukaa na mambo nyoni.

Kwa msiojua ni kwamba haya ya utawala huu wa sasa ni kwa sababu ya siasa za Bernard Membe ndani ya CCM, anajua ni wapi alijisahau na aliteleza na sasa anajiweka sawa asirudie makosa. Katiba ya chama inamruhusu kufanya hivyo, hayo mengine ya mwenyekiti wa sasa kurudi kugombea tena ni taratibu ilizo nje ya katiba na sio lazima.Waliofikiri asingeweza sasa wameina ni bora ngekua yeye kuliko tulikofikia.

Vijana wenzagu mkae mkitafakari kua Bernard Membe haya mawazo ya kutaka kua kiongozi wa taifa hili 2020 sio yake peke yake,atakua ameshauriwa na wazalendo wakongwe ambao tayari hawaridhishwi na upepo wa siasa za sasa. Mtu wa aina hii kutajwa sana sio kitu kidogo, kutakua na msukumo Mkubwa sana tena wa watu wanaojua ni wapi tupo hivi sasa.

Bernard Kamilius Membe akifanya mazoezi makali sana ya kukimbia

Habari wakuu

Kutokana na hali inavyoenda ya uendeshaji wa nchi ni wazi rais anatakiwa abadilishwe kupitia sanduku la kura mwaka 2020

Hivyo sisi watanzania tunapenda na tunatamani kusikia sauti ya kiongozi wetu mpendwa mwenye nia ya kulivusha taifa kwa hapa lilipokwamia, ndugu, mheshimiwa na mwanadiplomasia Benard Membe

Jitokeze wazi tusikie kauli yako watanzania tufarijike kwani mwaka 2020 ni jirani sana

Nawasilisha

Kuna watu tukisema Membe aongoze nchi 2020 wanabeza
Wengine wanatuita sisi ni vibaraka Wa Membe kitu ambacho sio cha kweli, Mimi sio kibaraka Wa Membe wala mheshimiwa Membe Mimi hanijui

Kitu ninachoamini ndicho nitaendelea kuamini, kwa sasa watanzania tumebadilika japo tume ya uchaguzi na vyombo vya Dora ndio hawataki kubadilika wanaturudisha nyuma

Ile kanuni ya kwamba Raisi lazima atawale miaka kumi imepitwa na wakati
Tukikupa miaka mitano ikakushinda basi kaa pembeni waachie wengine wanaoweza

Kwa miaka mitatu tu hii mambo yanaenda kombo

Vijana hawana ajira, tangu nchi kupata Uhuru awamu hii ya tano ndio awamu ambayo vijana wengi wamerandaranda mitaani bila ajira hata zile ajira za ualimu, nursing, udaktari hazipo tena

Ndani ya miaka hii mitatu watu wamefukuzwa kazi hovyo hovyo wamekua tegemezi, watu wamerudishwa kwenye Lindi la umaskini, watumishi Wa umma hawajapanda madaraja wala kuongezwa mishahara, kila siku uhakiki uchwara usio na kikomo

Ndani ya miaka mitatu ahadi zimeshindwa kutekelezeka zimebaki ni ahadi hewa, milioni hamsini kila kijiji imekua longolongo tu, ajira kwa vijana kama mnavyojionea mwenyewe,

Ndani ya miaka mitatu tumeshuhudia kauli za kibabe zisizo na mashiko kwa wananchi na viongozi wengine, wananchi wananangwa, viongozi wanatishwatishwa hovyo hovyo kama watoto wadogo

Kwa miaka hii mitatu tumeshuhudia mtu mmoja kuwa one man show, kila kitu anataka awe fonti fedi sijajua ni kupenda sifa au ni nini

Ndani ya awamu hii ndio tumeshuhudia taifa linaingia kwenye gharama za mauchaguzi uchwara yasiyo na tija kodi za wananchi zinachezewa, wananchi tumefanywa wajinga kupindukia,

Kwahayo machache yapo mengine mengi japo yapo na mambo mazuri yaliyofanyika lakini tunasema asante na yatosha sasa

2020 yafaa kwenda na mtu mwingine naye ni Bernard Membe

Bernard Membe unafaa kutuongpza
Iwe mvua liwe jua tutakua nyuma yako

Hatuwezi tena kuwasapoti watu wasio na shukrani

2020 Twende na BENARD MEMBE✔

#MEMBE_FOR_PRESIDENT2020
 
Habari za muda mabibi na mabwana! Kama kichwa cha habari kinavyojieleza nawashauri wanachama wenzangu na wananchi kwa ujumla. Mwaka 2020 tusipoteze tena kama ilivyotokea mwaka 2015. Haya yote ni kwa sababu hatukutulia vizuri katika mchujo wa kumpata kiongozi bora.Karibuni kwa maoni yenu.
Mkuu vitu vingine unapaswa utafakari sana. Hivi unadhani kwamba Raisi Magufuli kama Mwenyekiti wa CCM atajiweka kwenye mazingira ya CCM kuteua mgombea wa CCM mbadala wake? HUyu Magufuli ninayemfahamu au mwingine? Au hujaona tayari ameshajiwekea mazingira kwamba hilo lisiwezekane hata kidogo?
 
Habari za muda mabibi na mabwana!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza nawashauri wanachama wenzangu na wananchi kwa ujumla. Mwaka 2020 tusipoteze tena kama ilivyotokea mwaka 2015. Haya yote ni kwa sababu hatukutulia vizuri katika mchujo wa kumpata kiongozi bora.

Karibuni kwa maoni yenu.
Tukaletewa kichaa!
 
34 Reactions
Reply
Back
Top Bottom