Urais 2015, hoja ya jinsia na udhaifu wa BAWACHA

Magesi

JF-Expert Member
Jul 10, 2012
2,587
573
Uchaguzi wa 2015 C.C.M ni kama wanasema ushindi ni lazima kwa njia yoyote ile ili kuendelea kutawala.Makundi ndani ya C.C.M ni changamoto kubwa kwake kuendelea kubaki madarakani au kukabidhi nchi kwa upinzani hususani CHADEMA.

Kwa hali inayoendelea ndan ya C.C.M changamoto ya ndani ya chama na makundi yanayopambana kuanzia ngazi ya chini mpaka ndani ya baraza la mawaziri kiasi kwamba Mwenyekiti anajaribu kupunguza nguvu za makundi kwa kuanzia kumfunga mdomo Nape kuhusiana na swala la kuvua GAMBA ni katika kujaribu kutuliza au kupunguza hasira na mipango haramu dhidi ya wanachama wasio na upande katika swala la URAIS mwaka 2015.

MIPANGO YA MWENYEKITI KWANZA KUPUNGUZA NGUVU YA MAKUNDI AMA WOTE KUWA KITU KITU AMBACHO HAKIWEZEKANI.LAKINI MWENYEKITI ANA KETE MOJA YA JINSIA HII NI MUHIMU BILA KUJALI UWEPO WA MAKUNDI NDANI YA C.C.M MAMA ASHA ROSE MIGIRO ANAKUWA MTU MUHIMU BILA HATA KUJALI NGUVU YA CHADEMA.MWANAMKE AKIWEZESHWA ANAWEZA NDIO KAULI MBIU 2015.

SWALA LANGU HAPA NI UDHAIFU WA BARAZA LA WANAWAKE CHADEMA (BAWACHA) SIJUI WANAFAIDA GANI NDANI YA CHADEMA AU NI KWA AJILI YA UBUNGE WA VITI MAALUMU HILI NI LAZIMA UONGOZI WA C.D.M ULIFANYIE KAZI AU KUUONDOA UONGOZI WOTE KWA MASLAH MAPANA YA CHADEMA BILA KUANGALIANA USONI KWANI WAPIGAKURA WENGI WA TANZANIA NI WANAWAKE.

TUNAHITAJI BAWACHA ISIMAME KAMA BARAZA NDANI YA C.D.M LIFANYE KAZI YA KUWAUNGANISHA WANAWAKE WAWE NA MWAMKO WA KUIUNGA MKONO CDM.MWANAMKE AKIWEZESHWA ANAWEZA VIONGOZI CHADEMA LIANGALIENI HILI KWA MASLAH YA CHAMA.
 
Kama kuna eneo CDM inatakiwa kuliangalia kwa makini ni BAWACHA,naona wapo kwa ajili ya
ubunge wa viti maalim tu si zaidi ya hapo.Nimetoka kijijini kwetu sehemu za Singida hivi karibuni
nikagundua how BAVICHA wamefanya kazi kubwa,tatizo bado lipo kwa akina mama nilijaribu
kuwaelewesha wajiunge na CDM wanachojibu kuwa viongozi wanaowaongoza pale wanawake ni
CCM hivyo hawatapata msaada hata wa ushauri,wanasema labda CDM wakituwekea viongozi
wanawake huku pia tutajiunga maana tunaipenda CDM.Nilitamani niache kazi nikawe mwanasiasa
ili nisaidie chama changu ktk eneo hili lakini bado sijajiweka sawa.
 
Viongozi wa bawacha ni mzigo na janga ndani ya chadema utendaj wao ni mbovu
 
msiwalaumu bawacha,hawapewi nafac ya kutosha kwenye chama,cdm ni chama changu bt wanaendekeza sana mfumo dume,swala la kuwaweka wanawake pemben litawacost ikizingatiwa wanawake ndio wapiga kura wazuri.nauasa uongozi wa cdm ulifanyie marekebisho hili wawezeshwe wapewe rasiliman fedha watafute wanawake wa shoka wa kusimamia bawacha wafungue mataw nchi nzima wafanye semina na mikutano kutafuta wanachama wapya wa level zote za elimu na utendaji ili kukipa chama nguvu mpaka ngaz ya familia.2nahitaj wanawake type ya migiro na tibaijuka bawacha ili kuhamasisha kura za kinamama 2015
 
msiwalaumu bawacha,hawapewi nafac ya kutosha kwenye chama,cdm ni chama changu bt wanaendekeza sana mfumo dume,swala la kuwaweka wanawake pemben litawacost ikizingatiwa wanawake ndio wapiga kura wazuri.nauasa uongozi wa cdm ulifanyie marekebisho hili wawezeshwe wapewe rasiliman fedha watafute wanawake wa shoka wa kusimamia bawacha wafungue mataw nchi nzima wafanye semina na mikutano kutafuta wanachama wapya wa level zote za elimu na utendaji ili kukipa chama nguvu mpaka ngaz ya familia.2nahitaj wanawake type ya migiro na tibaijuka bawacha ili kuhamasisha kura za kinamama 2015
Najua viongozi wangu mnapita humu BAWACHA NI CHOMBO MUHIMU KULIKO CHOCHOTE NDANI YA CDM KUELEKEA KUSHIKA DOLA 2015
 
[
Tatizo kubwa ndani ya CDM ni ndugunization. Akina mama wengi wanaopewa uongozi ktk chama chetu hiki hususan ktk ngazi ya Ubunge wa kuteuliwa wanatokana na viongozi wenyewe. Ama uwe mke wa kiongozi wa juu au hawala yake au uwe na jamaa wa karibu kifamilia au kiukoo aliye ngazi ya juu ndani ya uongozi wa juu wa CDM ndipo utapewa mamlaka au utaruhusiwa kuongoza. Sasa nidhahiri kwa kila mtu kuwa chama hiki kinaelekea pabaya kutokana na ukabila.Tusilaumu sana dada zetu hawa. CDM kwafukuta ndani kwa ndani. Ukabila na hata ufuska ndo chanzo cha CDM
kufa kifo cha mende. acha kife tutauda kingine bora zaidi.
 
Back
Top Bottom