Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,783
- 1,822
Kevin-Prince Boateng ni raia wa Ghana na Ujerurumani, kwa vile baba yake ni Mghana na Mama yake ni Mjerumani. Mchezaji huyu alikuwa akiichezea timu ya vijana ya Ujerumani na alikuwa tegemeo kubwa sana kwa timu hiyo.
Ni tarehe 5 mwezi wa 6 mwaka huu ndio Uzalendo wa Ghana ulipomzidi na kuamua kuifungia pasport ya Ujerumani katika sanduku na Kuiinua mbele ile pasport ya Ghana na kuamua kuichezea Ghana katika kombe la Dunia. Uamuzi wake ulimkatisha tamaa sana kocha wa ujerumani ambaye alikuwa na mipango mahsusi juu ya maisha ya soka ya mchezaji huyu ndani ya Ujerumani. Lakini kwa vile ana haki ya kisheria ya kuchagua ni nchi gani achezee, bado uamuzi unakuwa ni wa kwake mwenyewe.
Leo Ghana ndio nchi pekee miongoni mwa nchi za Afrika ambayo imefanikiwa kufikia 1/8 na hatimaye 1/4 fainali kwa msaada wa goli la kwanza la Mjerumani/Mghana Kevin-Prince Boateng. Faida kama hizi zitokanazo na uraia wa nchi mbili ni nyingi katika maeneo tofauti hasa katika wakati huu wa utandawazi. Na kwa maana hii ndio maana nchi nyingi za Afrika kwa miaka mingi zilisharuhusu uraia wa nchi mbili.
Kama Ghana ingefunga milango kwa waghana waishio nje kama Tanzania, basi kamwe isingeweza kuitumia nafasi hiyo. Hii ni fundisho kubwa kwa Tanzania ambaye suala la Uraia wa nchi mbili limekiuwa likizungumziwa kwa takriban zaidi ya miaka 10, na kupoteza faida nyingi ambazo nchi yetu ingepata. Uamuzi wa Serikali uliotangazwa na Waziri wa mambo ya nje, Mheshimiwa Membe ni uamuzi wa busara. Lakini ni lazima tuendelee kuwaelimisha watanzania waliokuwa wakifikiri eti ni Watanzania wenye asili ya kihindi tu ndio wataofaidika zaidi. Hii si kweli, na mfano halisi ni kama tulivyoona Nchini Ghana.
Ninachoiomba serikali isipoteze muda mrefu katika kutia maamuzi muhimu kama haya na mengineyo ambayo seriali haihitaji kutumia pesa nyingi kufikia maamuzihayo. Ni vikao kadhaa tu vya bunge vinatosha kupitisha mswaada kama huo kwa kipindi cha mwaka mmoja tu na sio zaidi ya miaka kumi. Lazima tujue kuwa wakati wenzetu wanatembea yabidi sisi tukimbie ili angalau kuwakaribia.
Ushindi wa Ghana ni ushindi kwa Afrika na ni mfano kwa Tanzania. Ili tuendelee kwa kasi ni muhimu tujifunze toka kwa wenzetu vile vile. Hii ndio faida ya Utandawazi.
Ni tarehe 5 mwezi wa 6 mwaka huu ndio Uzalendo wa Ghana ulipomzidi na kuamua kuifungia pasport ya Ujerumani katika sanduku na Kuiinua mbele ile pasport ya Ghana na kuamua kuichezea Ghana katika kombe la Dunia. Uamuzi wake ulimkatisha tamaa sana kocha wa ujerumani ambaye alikuwa na mipango mahsusi juu ya maisha ya soka ya mchezaji huyu ndani ya Ujerumani. Lakini kwa vile ana haki ya kisheria ya kuchagua ni nchi gani achezee, bado uamuzi unakuwa ni wa kwake mwenyewe.
Leo Ghana ndio nchi pekee miongoni mwa nchi za Afrika ambayo imefanikiwa kufikia 1/8 na hatimaye 1/4 fainali kwa msaada wa goli la kwanza la Mjerumani/Mghana Kevin-Prince Boateng. Faida kama hizi zitokanazo na uraia wa nchi mbili ni nyingi katika maeneo tofauti hasa katika wakati huu wa utandawazi. Na kwa maana hii ndio maana nchi nyingi za Afrika kwa miaka mingi zilisharuhusu uraia wa nchi mbili.
Kama Ghana ingefunga milango kwa waghana waishio nje kama Tanzania, basi kamwe isingeweza kuitumia nafasi hiyo. Hii ni fundisho kubwa kwa Tanzania ambaye suala la Uraia wa nchi mbili limekiuwa likizungumziwa kwa takriban zaidi ya miaka 10, na kupoteza faida nyingi ambazo nchi yetu ingepata. Uamuzi wa Serikali uliotangazwa na Waziri wa mambo ya nje, Mheshimiwa Membe ni uamuzi wa busara. Lakini ni lazima tuendelee kuwaelimisha watanzania waliokuwa wakifikiri eti ni Watanzania wenye asili ya kihindi tu ndio wataofaidika zaidi. Hii si kweli, na mfano halisi ni kama tulivyoona Nchini Ghana.
Ninachoiomba serikali isipoteze muda mrefu katika kutia maamuzi muhimu kama haya na mengineyo ambayo seriali haihitaji kutumia pesa nyingi kufikia maamuzihayo. Ni vikao kadhaa tu vya bunge vinatosha kupitisha mswaada kama huo kwa kipindi cha mwaka mmoja tu na sio zaidi ya miaka kumi. Lazima tujue kuwa wakati wenzetu wanatembea yabidi sisi tukimbie ili angalau kuwakaribia.
Ushindi wa Ghana ni ushindi kwa Afrika na ni mfano kwa Tanzania. Ili tuendelee kwa kasi ni muhimu tujifunze toka kwa wenzetu vile vile. Hii ndio faida ya Utandawazi.