Urafiki wa Zitto na Lissu , hofu yatanda CHADEMA. Mbowe amfuata Lissu Ubelgiji

TataMadiba

JF-Expert Member
Feb 7, 2014
9,866
5,742
1568178466445.png

Habari za Uchunguzi wa mambo ya siasa zinasema kuwa ukaribu wa Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Zuberi Kabwe na aliyewahi kuwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Antipas Lissu umezua hofu ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA. Taarifa hizo zinasema kuna uwezekano mkubwa wa Tundu Lissu kuhamia ACT-Wazalendo na kutengeneza Muunganiko imara wa kukabiliana Chanma tawala CCM katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Mwaka 2020. Sababu hasa za LIssu kufikia uamuzi wa kukitosa Chama chake bado hazijafahamika ingawaje ukaribu wa Zitto Kabwe kwa Lissu kuliko mtu yeyote hasa katika kipindi hiki ambacho Lissu amekuwa kwenye matatizo makubwa ya kiafya inatajwa kuwa moja ya sababu. Lissu anaamua kuuenzi msemo usemao "Äkufaaye wakati wa dhiki ndiye rafiki wa kweli".

Hali hiyo imepelekea Viongozi wa Chadema kuchukua hatua kadhaa ili kujaribu kunusuru Lissu kuhamia ACT-wazalendo.
Mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe amelazimika kusafiri kwenda Ubelgiji anakotibiwa Mhe. Lissu kwa kile kinachodaiwa ni kwenda kuuzima moto aliouwasha Zitto wa kumshawishi Lissu ahamie kwenye chama chake. Inasemekana Zitto amekuwa na safari za mara kwa mara Ubelgiji ambapo baadhi ya safari hizo zimekuwa ni siri na hazikuripotiwa na vyombo vya habari.


1568178514425.png

Mwanachama kindakindaki kijana Yeriko Nyerere kupitia akaunti yake ya Twitter , ameponda kile kinachoitwa ni Muungano Mkubwa 2020 (GrandCoalition2020) unaoenenzwa na Zitto. Yeriko amemshutumu Zitto kuacha kushughulikia kesi iliyopekeka Diwani wake wa Kata Mwanga Kaskazini Manispaa ya Kigoma Ujiji Clayton Chipanda maarufu kama Baba Levo kushindwa rufaa iliyokuwa ikipinga kufungwa jela miezi mitano na kuongezewa muda wa kifungo hadi mwaka mmoja. Duru za kisiasa zinasema Yeriko na Kundi la vijana wenzake ambao ni wakongwe ndani ya Chadema wanaona kumruhusu Zitto ajihusishe na Chadema ni kusaliti Vijana wenzao waliokuwa wapambanaji wa kweli ambao leo hii hawaonekani akiwemo Ben Saanane.

1568178432533.png

ba
 
Enzi za akina Ben Saanane, Gj Malisa Bob Chacha Wangwe, Zitto alikuwa hafurukuti kukichokonoa Chadema. Tulikuwa wengi na makini. Chadema imekufa
 
Tatizo la CHADEMA wanakuww wwnahamishia akili zao kwa Changamoto ndani ya CCM na kusahau yao. CCM ni mama Wa siasa Afrika hakuna linaloharibika huko.
 
Tatizo la CHADEMA wanakuww wwnahamishia akili zao kwa Changamoto ndani ya CCM na kusahau yao. CCM ni mama Wa siasa Afrika hakuna linaloharibika huko.
ccm wanaijua vyema cdm kuliko cdm inavyojijua.
 
Lisu anaona Hana future chadema alikuwa anautaka uenyekiti kakwaa kisiki Mbowe kadinda.Zitto kabwe alienda kumwomba Tundu Lisu awe mwenyekiti taifa was ACT wazalendo.
 
hizo ndio siasa katika ubora wake bana.
lakini kuna washamba humu kutokea maporini huko,wako tayari wakutukane matusi ya nguoni kisa lissu
Watakuwa wnnanionea maana hilo liko wazi kwamba ZITTO na LISSU kuna kitu wanakitengeneza
 
Inasikitish sana jinsi vijana wa CHADEMA wanavyopambana na hii issue ila nnafuraha kuona hakuna kiongozi mwandamizi wa CHADEMA aliezungumzia hii kitu busara imetewala. Naona Yericko anauchungu sana na Zitto ila ukweli unabaki pale pale CHADEMA hawawezi kushinda uchaguzi huu pekee yao kamwe wanaihitaji Zanzibar maana yake wanamuhitaji Zitto, pia kwasasa kwenye hizi siasa za panga na shoka ni Zitto na Lissu tu kwa huku bara ndo wameonesha ujasiri wakuweza kupamba bila woga.

Nafkiri la msingi kwa sasa Zitto wala viongozi wachadema wasijibu mambo ya mitandaoni kama wanania ya kuitetemesha CCM muungano nilazima si hiyari. Umoja ni nguvu utengano ni dhaifu maana kwa hali ilivyo sasa ACT hawana chakupoteza watasimama wao kama wao na watashinda Zanzibar huku CHADEMA wanaweza wasipate wabunge wakutosha huku ikafanya ACT kuwa chama cha kikuu cha upinzani ambayo ni mbaya sana kwa CHADEMA.

Kwenye siasa kuna element za kutokuaminiana ila haizui kufanya kazi pamojakwa hali ilivyo sasa CHADEMA na ACT kila mtu anamuhitaji mwenzie na busara ni kufanya kazi pamoja ila kama wataruhusu chuki kuongoza kuna mmoja atapoteza zaidi na nahoifi mpotezaji atakuwa CHADEMA.
 
Siasa bana hautakiwi kuiamini sana pia ukiingia sehemu unatakiwa ujue misingi yake.
 
hizo ndio siasa katika ubora wake bana.
lakini kuna washamba humu kutokea maporini huko,wako tayari wakutukane matusi ya nguoni kisa lissu
Tena usijaribu, watakumiminia mvua ya matusi mpk utalowa, kuna watu wako tayali kuwatukana mama zao matusi ya kunguoni kisa tu Lisu amesemwa!
 
Back
Top Bottom