Judgement
JF-Expert Member
- Nov 13, 2011
- 10,327
- 4,779
Wana wa Bodi, awali ya yote niseme poleni na mishemishe za kutwa ya leo.
Nikiwa nasoma shule ya wavulana miaka ile, nilikua na rafiki yangu tuliekua twasoma shule moja. Mara kadhaa wakati wa kurejea hom tulikua tukifatana nae, kwetu mimi palikua karibu na shule, na mwenzangu kwao palikua mbali , (kwa mujibu wa maelezo yake.)
Hivyo mara nyingi ilikua tukitoka skuli tunafika nae kwetu kama kuna karizki tunafinya nae, siku nyingine anapitiliza n.k. Ikatokea wakati rafiki yangu akawa mgonjwa na hakuweza kufika shule. Na hadi kufikia kuumwa mi sikua nikipajua kwao.
Siku moja Mama yangu akaniuliza "Mbona yule mwenzio kitambo haonekani ?"
nikamjibu kua anaumwa.
Mama akaniuliza "Umeshawahi kwenda kumjua hali ?"
nikamjibu mama kua kwao sipajui.
Maa akaniambia "Basi huo urafiki wenu ni wa kinafiki"
nikamuuliza maa kwa vipi ?
Akanijibu "Kawaida urafiki wa kuishia barabarani, si urafiki wa ukweli, je? Ukisikia amekufa ndiyo ukapatafute kwao siku ya msiba?"
Sikua na majibu ya kumpa maa.
Hapa Jf members wengi ni marafiki, bt majority wao ni urafiki unaoishia majukwaani.
Hivi mimi Judgement leo nimekufa hapa mtajuaje? Hata zile R.I.P zenu nitazipataje ?
Mf. mdogo hapa kuna members kitambo hawaonekani kama,
> Nitonye
>Maprsoo
> Figaniga
> F. Foxy
> AshaDii - afadhali kidogo Ashadii twaweza pata habari zake kwa Bro. Kaizer je? Hao wengine ? Nani ana data zao?
Aidha hao Members niliowatanya hapo ni baadhi tu, bt wako kibao. Mimi sipendezwi sana na urafiki wa kihivi. Napenda nikisikia member flani anaumwa nikamuone, ana shida nimsaidie, nami nna tatizo tunasaidiana hata kwa mawazo. Basi si mbaya mkaacha kujuana Members mnaoishi mikoa mbalimbali. Lakini unakuta mko mkoa mmoja hamjuani. Member anakufa si ajabu pengine mnaishi jirani , lakini hutomzika coz hamjuani, lakini Jf mlikua marafiki mnachart mnafurahi n.k Hii inaskitisha sana.
Naomba kutoa hoja.
Judgement.
Nikiwa nasoma shule ya wavulana miaka ile, nilikua na rafiki yangu tuliekua twasoma shule moja. Mara kadhaa wakati wa kurejea hom tulikua tukifatana nae, kwetu mimi palikua karibu na shule, na mwenzangu kwao palikua mbali , (kwa mujibu wa maelezo yake.)
Hivyo mara nyingi ilikua tukitoka skuli tunafika nae kwetu kama kuna karizki tunafinya nae, siku nyingine anapitiliza n.k. Ikatokea wakati rafiki yangu akawa mgonjwa na hakuweza kufika shule. Na hadi kufikia kuumwa mi sikua nikipajua kwao.
Siku moja Mama yangu akaniuliza "Mbona yule mwenzio kitambo haonekani ?"
nikamjibu kua anaumwa.
Mama akaniuliza "Umeshawahi kwenda kumjua hali ?"
nikamjibu mama kua kwao sipajui.
Maa akaniambia "Basi huo urafiki wenu ni wa kinafiki"
nikamuuliza maa kwa vipi ?
Akanijibu "Kawaida urafiki wa kuishia barabarani, si urafiki wa ukweli, je? Ukisikia amekufa ndiyo ukapatafute kwao siku ya msiba?"
Sikua na majibu ya kumpa maa.
Hapa Jf members wengi ni marafiki, bt majority wao ni urafiki unaoishia majukwaani.
Hivi mimi Judgement leo nimekufa hapa mtajuaje? Hata zile R.I.P zenu nitazipataje ?
Mf. mdogo hapa kuna members kitambo hawaonekani kama,
> Nitonye
>Maprsoo
> Figaniga
> F. Foxy
> AshaDii - afadhali kidogo Ashadii twaweza pata habari zake kwa Bro. Kaizer je? Hao wengine ? Nani ana data zao?
Aidha hao Members niliowatanya hapo ni baadhi tu, bt wako kibao. Mimi sipendezwi sana na urafiki wa kihivi. Napenda nikisikia member flani anaumwa nikamuone, ana shida nimsaidie, nami nna tatizo tunasaidiana hata kwa mawazo. Basi si mbaya mkaacha kujuana Members mnaoishi mikoa mbalimbali. Lakini unakuta mko mkoa mmoja hamjuani. Member anakufa si ajabu pengine mnaishi jirani , lakini hutomzika coz hamjuani, lakini Jf mlikua marafiki mnachart mnafurahi n.k Hii inaskitisha sana.
Naomba kutoa hoja.
Judgement.