Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,808
- 11,973
Chama cha Akiba na Mikopo cha Jeshi la Polisi Tanzania, URA SACCOS kimekabidhi vifaa tiba pamoja na kompyuta kwa vikosi vya Jeshi la Polisi Tanzania.
Vifaa hivyo ni pamoja na vifaa tiba kwa ajili ya Hospitali ya Jeshi hilo iliyopo Kunduchi, Simiyu na Kumpyuta kwa ajili ya Kikosi cha Ufundi na kikosi cha Bohari Kuu ya Jeshi la Polisi.
Akikabidhi katika hafla fupi iliyofanyika katika ofisi hizo jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya URA SACCOS, Festo Christopher Mwikuni amesema vifaa hivyo vinathamani ya Tsh. 40,361,000 ikiwa ni kutimiza takwa la kisheria la kurudisha faida kwa jamii inayowazunguka.
Awali, Mkuu wa Kikosi cha Afya, Kamishna Saidizi wa Polisi, Hussen Yahaya na Mkuu wa Kikosi cha Ujenzi Kamishna Msaidizi Fadhili Ishekazoba pamoja na Mkuu wa Kikosi cha Bohari Kamishna Msaidizi Moses Mziray kwa pamoja wamekishukuru Chama hicho kwa msaada huo kwani umekuja wakati muafaka.