Upuuzi wa Kocha Pablo wa Simba SC unavyozidi kuisafishia Yanga SC njia ya kuwa Mabingwa wa NBC Premier League kwa 75% mpaka sasa

Tunapitia kipindi cha mpito tu, mashabiki acheni mihemuko na kulalama sana. Sio simba tu inatopitia nyakati ngumu kwasasa. Tp mazembe na barcelona piah wapo nyakati ngumu.

Ngoma ikivuma sana hupasuka.
Utetezi wa Kipumbavu sana huu Mkuu.
 
Hakuna timu isiyopoteza au ku draw acheni pressure kwa timu,ingawa ni kweli usajiri wa wafungaji ulikuwa muhimu
Kwahiyo kama Mwenyewe hapa Umeshakiri kuwa hatukusajili vyema Washambuliaji unadhani kuna mwanga wowote hasa katika Kushinda Mechi zetu kama hizi ( zile ) nyepesi mfano ile ya Mbeya City mbovu mbovu imetutoa Jasho na Kukojolewa nao Kimoko kile?
 
Yaani Kocha kabisa umeshapoteza Mechi Mbeya halafu Mechi muhimu ya leo Morogoro unakuja Kumjaribu Beki Mbovu Gadiel Michael wakati Mchezaji mahiri Mohammed Hussein Tshabalala unae na hujataka Kumuanzisha?

Yaani Kocha kabisa una Wachezaji very talented and creative kama Chama na Morrison unaacha Kuwaanzisha unawaingiza baadae kabisa?

Yaani kabisa Kocha Sisi Watu wa Mpira tumeshaona kuwa John Boko tayari 'Kwishnei' Kisoka halafu Wewe unamtetea huku ukiendelea Kumpanga Kikosini wakati una Vijana au Wachezaji wengine very Competent wa Kuisadia Timu?

Tayari Kocha uko na Kikosi na umeshaona ukitoa tu Meddie Kagere huna tena Mshambuliaji mwingine unaacha kuuambia Uongozi uachane na Chris Mugalu ili haraka tusajili 'Striker' mpya unabaki kudemadema tu utafikiri Ligi Kuu ya NBC ni ya Babu zako uliowaacha huko Kijijini Kwanu Hispania?

UKWELI MCHUNGU

GENTAMYCINE mpaka sasa nawapa 75% Yanga SC kuwa Mabingwa labda tu 'Complacency' iwagharimu na wasipouchukua Ubingwa nitawadharau kuliko Maelezo kwani Kiuhalisia na Kimazingira wana dalili zote za kuwa Mabingwa.

KWENU WANA SIMBA SC WENZANGU

Ili Yanga SC isiwe Bingwa inatakiwa ama ifungwe Mechi 3 au itoke Sare Mechi 4 je, tukiacha Unafiki na Ushabiki wetu mnadhani kwa Yanga SC hii ya sasa na walivyojipanga Kimkakati ndani na nje ya Uwanja hili litawezekana?

Na kumbukeni wakati huo tunaiombea mabaya haya Yanga SC na Sisi Simba SC tunatakiwa Kushinda tu Mechi zetu zote zilizobaki je, kwa Upuuzi na Ubovu wa Kocha Pablo mnadhani Simba SC yetu hii itaweza kulifanya hili wakati tuna Wachezaji dhaifu na wasio na Uchungu na Simba SC yetu?

LAWAMA KWA VIONGOZI WA SIMBA SC

Uongozi wa Simba SC wa sasa hauko serious na umewekeza zaidi katika Mapato na Biashara lakini siyo Ushindani wa Simba SC Uwanjani.

Wenzetu ( Watani ) zetu wanasajili Majembe ili Kujiimarisha zaidi Kiushindani Sisi kutwa tunahimizwa tu Kuchangia Ujenzi wa Uwanja wetu ili Ujengwe haraka kana kwamba TFF wametufukuza katika Viwanja vilivyopo.

NANI KASEMA HAJI MANARA KWENDA YANGA SC HAKUNA MADHARA YOYOTE KWA SIMBA SC YETU?

Tena Kuondoka kwa Haji Manara Kumetuathiri pakubwa Simba SC kwani alichokifanya Manara ni kuwaambia wana Yanga SC ( Viongozi na Wadhamini ) Siri zote zilizoipa Ubingwa mara Nne ( 4 ) na Yanga SC sasa nao kupitia GSM na Pesa walizonazo wanapita mule mule alikokuwa akipita Simba SC ( hasa Tajiri Mo Dewji ) na kwa Kujidhatiti Kwao kubakia Kileleni mpaka Watangazwe Mabingwa.

MIUJIZA

Najua duniani kuna Maajabu ( Miujiza ) ya kwamba pamoja na Yanga SC kutamba hivi ila nao wanaweza Kuukosa Ubingwa huu na Simba SC akauchukua tena.

Kwa Uchezaji mbovu wa Simba SC wa sasa na Umakini wa Yanga SC ni Mwendawazimu tu pekee atakataa kuwa hadi sasa ( leo ) Yanga SC ana 75% za kuwa Mabingwa.

LAWAMA NA VISINGIZIO VYA KIPUMBAVU

Kuna Watu wanadai Simba SC inaonewa na kwamba Yanga SC wanapendelewa.

GENTAMYCINE nakataa isipokuwa ninachojua tu ni kwamba Yanga SC imesajili Wachezaji wa Matokeo na Simba SC tumesajili Wachezaji wa Maonyesho na 10% kwa baadhi ya Viongozi wa Simba SC.

Upuuzi mwingine ni huu baada ya Kufungwa na Mbeya City na Leo kutoa Suluhu na Mtibwa Sugar FC baadhi ya wana Simba SC wanadai Viwanja vilikuwa Kikwazo.

Nami nauliza kama Viwanja vya Sokoine ( Mbeya ) na Manungu ( Morogoro ) ni Vibovu na Kikwazo Kwetu Klabu yetu ya Simba SC imejenga wapi Uwanja wake?

Na kama Viwanja vilikuwa ni Vibovu vya Mbeya na Morogoro imekuwaje Wapinzani wetu wenye Miguu na Nguvu sawa na Sisi wao wameweza Kuvicheza na wala hawalalamiki au Kudeka kama Sisi?

NINI KIFANYIKE KWA SASA?

Tuache Kuiwazia Yanga SC 24/7 na Kucheza Mechi zao Kifitna ili Wafungwe au Watoke Sare tuweze Kuwakaribia bali tujitathmini wapi tumekosea kwa Msimu huu, tujisahahiihishe na tucheze Mechi zetu Kimkakati na tusiruhusu tena Kufungwa au hata kutoka Sare Mechi nyinginezo kuanzia sasa.

HITIMISHO

Wana Simba SC tukubali tu kuwa Kutesa ni kwa zamu na Watani zetu Yanga SC kwa Msimu huu wapo vyema na walijipanga vvema Kimkakati ( hasa Ndani na Nje ) ya Uwanja.

Viongozi wa Simba SC amkeni haraka!!

Cc: Daudi Mchambuzi
Hujui mpira kaa chini kitulize! Kiwanja kama Manungu kilivyo kibaya utaishia kumpa lawama Pablo, kwani huyo Tshabalala kule Mbeya hakucheza? Wewe jamaa hujui mpira na nipo tayari kwa matusi yako
 
Mtoto wa kiongozi tunayemshimu unatukana hovyo?
Mbona hata Yeye ukimzingua huwa anakupa tu Makavu Mkuu na ukizubaa hata Kibao utapigwa? au Umesahau pengine kwakuwa sasa ni Mzee na Kastaafu?
 
Hatushtuliwi na matusi. Endelea kubwabwaja, sisi tunakupa vidonge vinavyostahili.
Pamoja na huko Kuongea Kwake Ugoro hapa JamiiForums lakini Juha Wewe na huyo FORTALEZA Kutwa hamuachi Kumsoma na Kumfuatilia hapa JamiiForums je, nikiwaiteni Wapumbavu nitakuwa nawakosea / nakosea?
 
Hatushtuliwi na matusi. Endelea kubwabwaja, sisi tunakupa vidonge vinavyostahili.
Unanipa Vidonge ila Wewe kile Kidonge chako cha Ugonjwa wako wa Akili ulionao kwa muda mrefu umekumbuka Kunywa leo?
 
Hichi ndicho kinachofanyika sasa 🤔🤔🤔

"Tuache Kuiwazia Yanga SC 24/7 na Kucheza Mechi zao Kifitna ili Wafungwe au Watoke Sare tuweze Kuwakaribia bali tujitathmini wapi tumekosea kwa Msimu huu, tujisahahiihishe na tucheze Mechi zetu Kimkakati na tusiruhusu tena Kufungwa au hata kutoka Sare Mechi nyinginezo kuanzia sasa."
 
Kwamba Manara ana siri za Simba kumzidi Senzo aliyehamia upande wa pili? Hilo nakataa,Manara hana impact yoyote kwa Simba kupata matokeo haya maana ni kawaida timu kama Simba kufungwa maana misimu karibu yote Simba amepoteza mechi na kusuluhu lakini bado akachukua ubingwa.

Yanga misimu yote minne ambayo simba amechukua ubingwa wamekuwa wakiongoza ligi tena bila kufungwa hadi mzunguko wa kwanza kwisha.

Msimu ulioisha simba tulipoteza mechi mbili za awali kabisa huku yanga wakiendeleza ushindi lakini mwisho wa msimu ubingwa msimbazi.
Acha uongo mkuu.

Ni msimu uliopita tu Yanga ndiyo aliongoza ligi tena kwasababu Simba alikuwa na viporo lukuki....
 
Mechi ipi simba aliyobebwa..

Pia sema ipi alifanyiwa fitina
ukweli mchungu kama huu ndo unaweza kutuvusha na sio kudanganyana eti vyura wanabebwa, ukiitazama league tangu ianze kiuanamichezo utagundua simba tumebebwa mechi nyingi na uto wamebebwa mechi 1 tu ile ya namungo.

kama kweli viongozi na wapenzi wa simba tunataka kurejea ktk makali yetu ni lazima kuufanyia kazi ukweli mchungu ulioletwa na mtoa mada kwenye chapisho hili.

NB:ubingwa bado hauna mwenyewe ikiwa tutasolve matatizo yetu haraka.
 
Siku zote Mwerevu ( GENTAMYCINE ) lazima awe Chukizo na Kero kwa AUTHENTIC MORONS kama Wewe na Van pebles hivyo wala sishangai badala yake nasomga mbele tu.

Na kinachonishangaza na mpaka nawadharau na kuwaona hamna tofauti na Takataka Ngumu zilizoko Vyooni ni kwamba Kutwa ( 24/7 ) mkiwa hapa mnasema kuwa hamnipendi, najisikia na sina Akili hata kuniita Mwehu ila nyie nyie ndiyo mnaongoza Kunisoma na Kunifuatilia kila ninachoandika hapa.

Msiache Kunichukia tena zidisheni Ok?
Kwani MWEHU hafatiliwi?Mbna hoja nyepesi hii?Unaweza kumfatilia MWEHU ili ucheke tu kwa vitendo nyake vya kichizi,au pengine ujue tabia za wehu zinakuwaje pindi wakiwa na furaha au hasira.Nawapenda sana WEHU WALIPO NIPO.
 
Kwani MWEHU hafatiliwi?Mbna hoja nyepesi hii?Unaweza kumfatilia MWEHU ili ucheke tu kwa vitendo nyake vya kichizi,au pengine ujue tabia za wehu zinakuwaje pindi wakiwa na furaha au hasira.Nawapenda sana WEHU WALIPO NIPO.
Na huwezi kumjua Mwehu kama nawe siyo Mwehu hivyo nichukue tu nafasi hii kukujua Wewe Mwehu Mwenzangu.
 
Back
Top Bottom