Upotoshwaji / Uongo huu uliojaa unafiki uliopitiliza haufai kuungwa mkono na tunaojielewa upstairs

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,359
108,391
Kuna Kampeni moja ambayo naweza kusema ni ya Kipuuzi / Kiupupu inayoendelea katika Shule ambayo ni ya kuwasaidia Wadogo zetu wa Kike kwa kuwapa Taulo zao za Kike ( Sanitary Pads / Sanitary Towels ) Uswahili tunaziita Pedi / Mkate wa Wanawake.

Yawezekana kabisa walioanzisha hii Kampeni wakawa na Hoja mahala fulani ila Mimi leo najitoa mhanga kupingana nao hasa kwa Uwongo wao ambao kutwa wanajitahidi kuueneza kuwa Watoto zetu hawa Kike / Wadogo zetu wanafeli huko Shuleni kwakuwa wanakosa hizi Taulo zao za Kujisitiri hasa wawapo Hedhini / katika Siku zao za mzunguko wa mwezi za Kike.

Hivi leo unaposema kuwa mnawasaidia hawa Mabinti / Dada zetu hizi Taulo zao ili muwasaidie katika ufaulu wao ambao mnadai kuwa kutwa unashuka mnamaanisha nini? Hivi miaka ya huko nyuma ( zamani zile ) Mama na Dada zetu ambao wengi wao walikuwa Vipanga / Werevu Shuleni nao walikuwa wanatumia hizi Taulo zenu? Mbona ufaulu wao ulikuwa ni mkubwa / wa juu mno japo walikuwa na mazingira magumu na ya shida?

Nitakuwa wa mwisho kuukubali huu Upotoshwaji tunaolazimishwa kuuamini kuwa moja ya sababu kubwa ambayo inawafanya hawa Wadogo / Dada zetu kufeli Masomo yao huko Shuleni ni kutopata hizi Taulo zao za Hedhi ila mkiniambia kuwa wanafeli kutokana na UPOPOMA / UPUMBAVU wao uliowatukuka na ambao pengine wengi wao wameurithi kutoka Kwetu sisi Wazazi wao nitakubaliana nanyi tena kwa 100% kabisa.

Enyi Waandaji wa hii Kampeni tafadhalini sana siku nyingine mnapojua kuwa mnakuja na vitu hivi vya hovyo hovyo / kijinga kijinga jueni kwamba Tanzania ya leo kuna Vipanga kibao ambao wanaweza kufikiri na kutafakari mambo kwa marefu na mapana yake na msirudie tena kuja na aina yenu hii ya Upupu / Upuuzi kwa Umma / Jamii.

Zipo sababu nyingi ambazo zinawafanya hawa Mabinti wafeli na yawezekana hii sababu yenu moja ambayo kutwa mnaikazania huku ikiwapatieni tu umaarufu wa KIPOPOMA ikawa ina 0.5% kati ya sababu kadhaa ambazo ndizo zina umuhimu.

Katika vitu ambavyo GENTAMYCINE huwa nachukia na sivipendi ni Kudanganywa kwa hoja nyepesi kabisa wakati mwenyewe najielewa. Halafu na cha kusikitisha kabisa hadi Wazazi nao wameshaambukizwa huu UPOPOMA nao wameamini 100% kuwa Mabinti zao wanafeli Shuleni kwa kukosa Taulo za Kike / Pedi.

Nimemaliza na Sindano ya GENTAMYCINE leo iwaingieni vilivyo. Mijitu mizima kabisa na yenye akili zao inasimama huku ikiwa imevaa Tai na kuanza kuongea tena kwa kusisitiza kuwa Wanafunzi wa Kike wanafeli Shuleni kwa kukosa Pedi. Miaka ya 30's, 40's hadi 80's Pedi zilikuwepo? Mbona ufaulu wa Dada na Mama zetu ulikuwa ni wa juu mno?
 
Swali nililokuwa nimebaki nalo ni je Huduma hii itatolewa hata baada ya kamera????? Kwa niwajuavyo wauza sura hiyo ndio nitolee... Well said Genta..

Akhsante kwa kunielewa Mkuu. Nachukia mno kudanganywa na Watu ambao wanadhani wako makini kumbe ni hopeless kabisa. Hivi kweli siku 3 au 4 au 5 za mwezi zinaweza kumfanya Mtoto wa Kike akafeli Shuleni? Hao Waandaaji wa hizi Kampeni wajitahidi kuacha huu ukengeukaji wao uliotukuka.
 
Akhsante kwa kunielewa Mkuu. Nachukia mno kudanganywa na Watu ambao wanadhani wako makini kumbe ni hopeless kabisa. Hivi kweli siku 3 au 4 au 5 za mwezi zinaweza kumfanya Mtoto wa Kike akafeli Shuleni? Hao Waandaaji wa hizi Kampeni wajitahidi kuacha huu ukengeukaji wao uliotukuka.
Wangegusa matatizo sugu kama motisha kwa waalimu, vitendea kazi hasa vitabu vinavyobadilika kila kukicha, ufundishaji unaokidhi mahitaji ya sasa... Kumbuka wakati ule tuna shule za ufundi, kilimo na biashara... vijana walitoka na ujuzi dira na hivyo hata walioshindwa kuendelea na masomo walikuwa valuable kwenye jamii... Hivi sasa ni mambo ya kiki tuuuuuuuuuuuuu
 
eti wanafeli kisa nini? Mbona watu wanaendekeza ujinga hivi? Ndio pedi ina umuhimu wake ila sioni kama kukosekana kwake kunamuathiri mtu kiasi hicho... Kuna watu hadi leo wanatumia vitambaa na wanadunda tu njiani...
 
Ndio viongozi wetu wanavyotaka tuwe kama makasuku tu kuimbishwa kila ujinga wanaokuja nao. Wajinga kabisa tena warudi darasani wakaanze kujifunza hata maana ya mantiki.
 
~~>>>Mambo ya siri wameweka bayana na ya bayana yamekuwa ni siri........ Haya mambo ya pedi yalikuwa ni mambo ya siri leo hii imekuwa tofauti ..
 
Naomba kila atakayerusha maneno hapa angalau kwanza aeleze yeye mara yake ya kwanza alipata hedhi lini na alijisikiaje. Ikiwa hujawahi kupata hedhi pengine kwa kuwa jinsi yako ni kama ya
Mwana Mtoka Pabaya , basi tuheshimu mawazo ya wanaofahamu hedhi kwa vitendo.

Mimi kwa maoni yangu, watoto wa kike wanaathirika kimasomo kwani wana uhakika wa kukosa madarasa kwa siku kadhaa kila mwezi ikiwa na pamoja na athari za kisaikolojia kwa kuchekwa, kuzomewa na kutetwa na wenzio. Ieleweke kuwa faragha ni haki ya kila mtu. Inapokuwa bayana kuwa leo Angela ana kidoa chekundu kwa kuwa tu kimevujia kwenye nguo, basi upo uwezekano Angela akaanza kuwaepuka wenzake kwa aibu hata baada ya siku zake kupita.
 
Hawa si ndio wale wale wanaosema watoto wa siku hizi wanafeli sababu ya ukosefu wa vitabu na madawati sijui wanaumia migongo kwa kukaa chini.....wakati mimi naanza darasa la kwanza nimesoma kwa kukaa kwenye mabetri ya gari na matofali.....na vitabu sikuwa navyo na mwisho wa siku nikatoboa azaboy
 
Ingependeza sana kama ungemalizia maelezo yako na kutuelezea uzoefu wako binafsi (personal experience) ukiwa kwenye siku zako za hedhi alaf utuonyeshe jinsi ambavyo sio kikwazo/sababu ya wewe kutokufanya vizuri kazi zako za kila siku..
 
Nakubaliana na wewe, hakuna kitu kibaya kama kuchekwa, kuzomewa na kuwa bullied na wanafunzi wenzako kwa sababu yoyote ile. Mwanafunzi wa kiume au wa kike (teenager) anakuwa katika wakati mgumu sana pale anapojua yeye ndio topic of the day shuleni. Hawa wamefanya utafiti wakagundua wasichana wengi hasa wa familia maskini wanakosa shule wakiwa kwenye siku zao na wameona hii ndio solution for now. As long as haileti madhara sioni sababu ya wao kupingwa.

Naomba kila atakayerusha maneno hapa angalau kwanza aeleze yeye mara yake ya kwanza alipata hedhi lini na alijisikiaje. Ikiwa hujawahi kupata hedhi pengine kwa kuwa jinsi yako ni kama ya
Mwana Mtoka Pabaya , basi tuheshimu mawazo ya wanaofahamu hedhi kwa vitendo.

Mimi kwa maoni yangu, watoto wa kike wanaathirika kimasomo kwani wana uhakika wa kukosa madarasa kwa siku kadhaa kila mwezi ikiwa na pamoja na athari za kisaikolojia kwa kuchekwa, kuzomewa na kutetwa na wenzio. Ieleweke kuwa faragha ni haki ya kila mtu. Inapokuwa bayana kuwa leo Angela ana kidoa chekundu kwa kuwa tu kimevujia kwenye nguo, basi upo uwezekano Angela akaanza kuwaepuka wenzake kwa aibu hata baada ya siku zake kupita.
 
Naomba kila atakayerusha maneno hapa angalau kwanza aeleze yeye mara yake ya kwanza alipata hedhi lini na alijisikiaje. Ikiwa hujawahi kupata hedhi pengine kwa kuwa jinsi yako ni kama ya
Mwana Mtoka Pabaya , basi tuheshimu mawazo ya wanaofahamu hedhi kwa vitendo.

Mimi kwa maoni yangu, watoto wa kike wanaathirika kimasomo kwani wana uhakika wa kukosa madarasa kwa siku kadhaa kila mwezi ikiwa na pamoja na athari za kisaikolojia kwa kuchekwa, kuzomewa na kutetwa na wenzio. Ieleweke kuwa faragha ni haki ya kila mtu. Inapokuwa bayana kuwa leo Angela ana kidoa chekundu kwa kuwa tu kimevujia kwenye nguo, basi upo uwezekano Angela akaanza kuwaepuka wenzake kwa aibu hata baada ya siku zake kupita.
kama ndivyo je watakuwa wakiwapatia hizo pedi kwamuda wa miaka mingapi ili wasiwe wanakosa masomo? ACHENI UZUSHI HAO WALIOKUWA WAKIFAULU ZAMANI WALIWAHI KUWA WANAPELEKEWA PEDI NA NANI!!!!? WANAO KWAMA KWENDA SHULE NI WALE MLIO WALEA KAMA YAI, KIASI HATA KUFUA NGUO ZO ZA NDANI HAWAWEZI!!!!
 
HAYO MADUDE WAKAYAGAWE HUKO MAJUMBANI NA SI MASHULENI.KAMA KWELI WANAHITAJI WATOTO WAFAULU.WATAZAME CHANGAMOTO NYINGINE KWA MFANO KUNA SHULE YA SEKONDARI MOJA MKOA WA DODOMA WILAYA YA MPWAPWA KUNA MABWENI HAKUNA VITANDA HATA KIMOJA NA WALA GODORO WATOTO WANALALA CHINI NA HAKUNA UMEME INGAWA UMEME UMEPITA ENEO HILO KAMA KWELI WANA NIA NJEMA WAKAWASAIDIE HAO ILI KUONGEZA UFAULU WAACHE POROJO!
 
kama ndivyo je watakuwa wakiwapatia hizo pedi kwamuda wa miaka mingapi ili wasiwe wanakosa masomo? ACHENI UZUSHI HAO WALIOKUWA WAKIFAULU ZAMANI WALIWAHI KUWA WANAPELEKEWA PEDI NA NANI!!!!? WANAO KWAMA KWENDA SHULE NI WALE MLIO WALEA KAMA YAI, KIASI HATA KUFUA NGUO ZO ZA NDANI HAWAWEZI!!!!
Tujadili hoja tukiwa tumefahamiana, mimi ni ME. Wewe mwenzangu ni wa jinsi gani?
 
kama ndivyo je watakuwa wakiwapatia hizo pedi kwamuda wa miaka mingapi ili wasiwe wanakosa masomo? ACHENI UZUSHI HAO WALIOKUWA WAKIFAULU ZAMANI WALIWAHI KUWA WANAPELEKEWA PEDI NA NANI!!!!? WANAO KWAMA KWENDA SHULE NI WALE MLIO WALEA KAMA YAI, KIASI HATA KUFUA NGUO ZO ZA NDANI HAWAWEZI!!!!


Wewe hedhi yako ya mwezi huu imekuja na changamoto gani kwako? Tupe uzoefu wako kwanza
 
Back
Top Bottom