Upotoshaji wa dhana ya uhuru ndani ya upinzani

Oct 6, 2020
27
50
Katika siasa za ushindani kama ilivyo ushindani holela wa soko huria kumeibuka upotoshwaji mkubwa wa kutumia fikra za Mwalimu Nyerere nyingi na hapa nitajikita katika dhana ya “UHURU”.

Kwa makusudi katika mchakato wa kuwa makuhadi wa soko huria, na pengine pia wapinzani kutokuwa na falsafa , inayoongoza itakidi na baadaye kutengeneza miongozo kama vile ilivyokuwa kwa Azimio la Arusha na sera. Wapinzani kwa kuendekeza tamaa binafsi za kulinganisha juhudi za sasa za kujikomboa kiuchumi wamekuwa wasaliti kwa kukosa uzalendo wa kulinda matakwa ya wanyonge ambao ndio kwa muda mrefu wamekuwa wahanga wa ukoloni mamboleo unajivika gwanda la “Uhuru” wa mawazo.

Upinzani huu umeendeleza propaganda ucharwa za kulinganisha juhudi za sasa za kujenga uchumi wa kitaifa na jumuishi unamlenga mtu mnyonge kama vile ni sawa na mapambano ya kumng’oa ukoloni ulio kuwa na nia ovu ya kinyonyaji kwa manufaa ya chi za kipebari.

Dhana ya Mwalimu Nyerere juu ya Uhuru ilikuwa bayana ni Uhuru wa kitabaka ukimlenga mtu wa tabaka la wanyonge kuondokana na mfumo wa kibeberu uliondoa utu kwa minajiri ya kulimbikiza mali kwa njia unyonyaji wa nguvu kazi na rasilimali za nchi na kusafirishwa nchi za Magharibi.

Hata neno “mabeberu” ndio dhana kuu iliyotawala maono na mapambano ya Mwalimu ambayo kwa sasa wapinzani hawataki kuhisikia maana inawachoma na kubomoa genge lao la ukwapuaji na kunadi sera za kinyonjaji zinazopiginia Uhuru wa uliberali mambo leo wenye nia ile ile ya historia ya ukoloni iliyokuwa na lengo kubwa la kulimbikiza mali kwa kupitia ulaghai. Na ulaghai huu unachochochewa na askari hawa kukodi wanaosambaza dhana ya ukombozi wa kweli wa kujenga Uhuru wa kiuchumi na fikra zinazopiginia wanyonge.

Dhana ya Uhuru ya wapinzani inashadadia mgawanyiko wa kijamii unachochea mfalakano, lakini pia kutia dhana ya Uhuru mamboleo inafifisha juhudi za pamoja za taifa la kizalendo la wanyonge kukata minyororo ya unyonyaji.

Inasukuma kubomoa nguvu ya demokrasia ya umma; maana mabeberu wanaogopa nguvu ya umma wa wanyonge na dhana ya kiliberali ya kujenga Uhuru uliojikita kwa mtu mmoja ni mkakati wa kuua nguvu ya tabaka kupigania kubomoa mfumo wa kibepari unaokosa utu na haki kwa maslahi ya watu wachache wenye mitaji(mabepari).

Mwalimu Nyerere alipata msukosuko kutoka chi za Magharibi alipokuwa anapinga waziwazi kupitia hatua zake za kukemea na kuweka sera thabiti za kuwathibiti mabeberu. Kwa Mwalimu ubepari ndio ulikuwa adui wa Uhuru wa kweli. Kwa wapinzani neno kama “mabeberu, ubepari; matabaka nk. yenye fikra za kimapinduzi unafunikwa kapuni.

Ni jukumu la watanzania wenye nia njema kuendelea kuibua propaganda hizi ambazo zinaenezwa kwa kasi ili kufifisha nia ya kuleta ukombozi wa kweli wa kiuchumi na kifikra unajenga demokrasia ya kweli inayosimamia ugawanyaji wa rasilimali za Taifa kwa wote pasipo kutoa mwanya maslahi ya wachache ya wanyonyaji kututia upofu kwa maneno yaliyokolezwa na kulebwa “Uhuru wa mawazo”. Tujenga Uhuru wa mawazo unapinga unyonyaji na uzalendo wa kulinda masilahi mapana ya wanyonge.

Tukatae ulaghai wa walio uza utu wao na kupiginia ukoloni mamboleo kwa kisingizio cha kudai Uhuru!
 
Katika siasa za ushindani kama ilivyo ushindani holela wa soko huria kumeibuka upotoshwaji mkubwa wa kutumia fikra za Mwalimu Nyerere nyingi na hapa nitajikita katika dhana ya “UHURU”.

Kwa makusudi katika mchakato wa kuwa makuhadi wa soko huria, na pengine pia wapinzani kutokuwa na falsafa , inayoongoza itakidi na baadaye kutengeneza miongozo kama vile ilivyokuwa kwa Azimio la Arusha na sera. Wapinzani kwa kuendekeza tamaa binafsi za kulinganisha juhudi za sasa za kujikomboa kiuchumi wamekuwa wasaliti kwa kukosa uzalendo wa kulinda matakwa ya wanyonge ambao ndio kwa muda mrefu wamekuwa wahanga wa ukoloni mamboleo unajivika gwanda la “Uhuru” wa mawazo.

Upinzani huu umeendeleza propaganda ucharwa za kulinganisha juhudi za sasa za kujenga uchumi wa kitaifa na jumuishi unamlenga mtu mnyonge kama vile ni sawa na mapambano ya kumng’oa ukoloni ulio kuwa na nia ovu ya kinyonyaji kwa manufaa ya chi za kipebari.

Dhana ya Mwalimu Nyerere juu ya Uhuru ilikuwa bayana ni Uhuru wa kitabaka ukimlenga mtu wa tabaka la wanyonge kuondokana na mfumo wa kibeberu uliondoa utu kwa minajiri ya kulimbikiza mali kwa njia unyonyaji wa nguvu kazi na rasilimali za nchi na kusafirishwa nchi za Magharibi.

Hata neno “mabeberu” ndio dhana kuu iliyotawala maono na mapambano ya Mwalimu ambayo kwa sasa wapinzani hawataki kuhisikia maana inawachoma na kubomoa genge lao la ukwapuaji na kunadi sera za kinyonjaji zinazopiginia Uhuru wa uliberali mambo leo wenye nia ile ile ya historia ya ukoloni iliyokuwa na lengo kubwa la kulimbikiza mali kwa kupitia ulaghai. Na ulaghai huu unachochochewa na askari hawa kukodi wanaosambaza dhana ya ukombozi wa kweli wa kujenga Uhuru wa kiuchumi na fikra zinazopiginia wanyonge.

Dhana ya Uhuru ya wapinzani inashadadia mgawanyiko wa kijamii unachochea mfalakano, lakini pia kutia dhana ya Uhuru mamboleo inafifisha juhudi za pamoja za taifa la kizalendo la wanyonge kukata minyororo ya unyonyaji.

Inasukuma kubomoa nguvu ya demokrasia ya umma; maana mabeberu wanaogopa nguvu ya umma wa wanyonge na dhana ya kiliberali ya kujenga Uhuru uliojikita kwa mtu mmoja ni mkakati wa kuua nguvu ya tabaka kupigania kubomoa mfumo wa kibepari unaokosa utu na haki kwa maslahi ya watu wachache wenye mitaji(mabepari).

Mwalimu Nyerere alipata msukosuko kutoka chi za Magharibi alipokuwa anapinga waziwazi kupitia hatua zake za kukemea na kuweka sera thabiti za kuwathibiti mabeberu. Kwa Mwalimu ubepari ndio ulikuwa adui wa Uhuru wa kweli. Kwa wapinzani neno kama “mabeberu, ubepari; matabaka nk. yenye fikra za kimapinduzi unafunikwa kapuni.

Ni jukumu la watanzania wenye nia njema kuendelea kuibua propaganda hizi ambazo zinaenezwa kwa kasi ili kufifisha nia ya kuleta ukombozi wa kweli wa kiuchumi na kifikra unajenga demokrasia ya kweli inayosimamia ugawanyaji wa rasilimali za Taifa kwa wote pasipo kutoa mwanya maslahi ya wachache ya wanyonyaji kututia upofu kwa maneno yaliyokolezwa na kulebwa “Uhuru wa mawazo”. Tujenga Uhuru wa mawazo unapinga unyonyaji na uzalendo wa kulinda masilahi mapana ya wanyonge.

Tukatae ulaghai wa walio uza utu wao na kupiginia ukoloni mamboleo kwa kisingizio cha kudai Uhuru!
Nchi yetu imekombolewa na kupata uhuru tangu 1961 na Mwalimu, binafsi nashangaa sana hii agenda ya uhuru wapinzani wametoka nayo wapi tena, ni mambo ya ajabu.
 
Wewe ni ingizo jipya kwenye chupa ya zamaniii! Lakini huna jipya lolote unaloleta zaidi ya kubadilisha mwandiko tu.
 
Mkuu kwanza usishangae hali hiyo kutokea, sababu kubwa ni mfumo ulioundwa ndani ya nchi hii hautowi nafasi hata siku moja kwa namna yeyote ile upinzani kushinda uchaguzi labda uchaguzi huo CCM awe amejitowa.

Kwa hiyo upinzani ni kuku aliye katwa kichwa na ameachwa anapaparika. Chochote upinzani ukishika unachukulia utapata ukombozi.

CCM imehodhi kila kitu, Intellect, pesa,zana za kazi, uongozi na tricks of trade,ushauri pia. Mtegemee hivi hivi hata fujo ambazo haziwezi kubadili kitu lakini zinaweza kutokea kwa kuwa upinzani ukijitambua utagundua hauna pa kwenda.

Juzi nilikuwa naongea na kiongozi mmoja wa upinzani ambao wengi wetu tunamuona mwerevu na nika mwambia hebu niwasaidie kutengeza critical path na tufanye critical path analysis ya jinsi ya kufanya kampeni kwa siku zilizo baki.

Kwanza hajui hichoni nini, pili kwa kuishi na hofu anaingiza mambo binafsi - mnamaliza. Mnapokuja kumaliza kazi ya utayarishaji unakuja kugundua hata ku operationalise written formular hawa wezi. Sasa sijui ndio urudi kuvaa magwanda ili watoto wako choo kipatikane kwa taabu?

Kumbuka wenzetu CCM wako Scientific sababu wanazo all arsenals, mtuu yeyote wa taaluma wanayo ihitaji wanamwita na kuitumia hata ikibidi wakulipe, na hawana taabu na hilo. Hata ukiwa mgumu pesa, vitisho na ushawishi utalainishwa tuu.

Kwa hiyo hapa CCM ni tatizo sana, Mpaka mtoe uhuru wa mambo mengi ndio ushindani wa kisiasa wa kweli uweze kupatikana.
 
Katika siasa za ushindani kama ilivyo ushindani holela wa soko huria kumeibuka upotoshwaji mkubwa wa kutumia fikra za Mwalimu Nyerere nyingi na hapa nitajikita katika dhana ya “UHURU”.

Kwa makusudi katika mchakato wa kuwa makuhadi wa soko huria, na pengine pia wapinzani kutokuwa na falsafa , inayoongoza itakidi na baadaye kutengeneza miongozo kama vile ilivyokuwa kwa Azimio la Arusha na sera. Wapinzani kwa kuendekeza tamaa binafsi za kulinganisha juhudi za sasa za kujikomboa kiuchumi wamekuwa wasaliti kwa kukosa uzalendo wa kulinda matakwa ya wanyonge ambao ndio kwa muda mrefu wamekuwa wahanga wa ukoloni mamboleo unajivika gwanda la “Uhuru” wa mawazo.

Upinzani huu umeendeleza propaganda ucharwa za kulinganisha juhudi za sasa za kujenga uchumi wa kitaifa na jumuishi unamlenga mtu mnyonge kama vile ni sawa na mapambano ya kumng’oa ukoloni ulio kuwa na nia ovu ya kinyonyaji kwa manufaa ya chi za kipebari.

Dhana ya Mwalimu Nyerere juu ya Uhuru ilikuwa bayana ni Uhuru wa kitabaka ukimlenga mtu wa tabaka la wanyonge kuondokana na mfumo wa kibeberu uliondoa utu kwa minajiri ya kulimbikiza mali kwa njia unyonyaji wa nguvu kazi na rasilimali za nchi na kusafirishwa nchi za Magharibi.

Hata neno “mabeberu” ndio dhana kuu iliyotawala maono na mapambano ya Mwalimu ambayo kwa sasa wapinzani hawataki kuhisikia maana inawachoma na kubomoa genge lao la ukwapuaji na kunadi sera za kinyonjaji zinazopiginia Uhuru wa uliberali mambo leo wenye nia ile ile ya historia ya ukoloni iliyokuwa na lengo kubwa la kulimbikiza mali kwa kupitia ulaghai. Na ulaghai huu unachochochewa na askari hawa kukodi wanaosambaza dhana ya ukombozi wa kweli wa kujenga Uhuru wa kiuchumi na fikra zinazopiginia wanyonge.

Dhana ya Uhuru ya wapinzani inashadadia mgawanyiko wa kijamii unachochea mfalakano, lakini pia kutia dhana ya Uhuru mamboleo inafifisha juhudi za pamoja za taifa la kizalendo la wanyonge kukata minyororo ya unyonyaji.

Inasukuma kubomoa nguvu ya demokrasia ya umma; maana mabeberu wanaogopa nguvu ya umma wa wanyonge na dhana ya kiliberali ya kujenga Uhuru uliojikita kwa mtu mmoja ni mkakati wa kuua nguvu ya tabaka kupigania kubomoa mfumo wa kibepari unaokosa utu na haki kwa maslahi ya watu wachache wenye mitaji(mabepari).

Mwalimu Nyerere alipata msukosuko kutoka chi za Magharibi alipokuwa anapinga waziwazi kupitia hatua zake za kukemea na kuweka sera thabiti za kuwathibiti mabeberu. Kwa Mwalimu ubepari ndio ulikuwa adui wa Uhuru wa kweli. Kwa wapinzani neno kama “mabeberu, ubepari; matabaka nk. yenye fikra za kimapinduzi unafunikwa kapuni.

Ni jukumu la watanzania wenye nia njema kuendelea kuibua propaganda hizi ambazo zinaenezwa kwa kasi ili kufifisha nia ya kuleta ukombozi wa kweli wa kiuchumi na kifikra unajenga demokrasia ya kweli inayosimamia ugawanyaji wa rasilimali za Taifa kwa wote pasipo kutoa mwanya maslahi ya wachache ya wanyonyaji kututia upofu kwa maneno yaliyokolezwa na kulebwa “Uhuru wa mawazo”. Tujenga Uhuru wa mawazo unapinga unyonyaji na uzalendo wa kulinda masilahi mapana ya wanyonge.

Tukatae ulaghai wa walio uza utu wao na kupiginia ukoloni mamboleo kwa kisingizio cha kudai Uhuru!
Umezungumza vyema saana ndugu Mwandishi...
Kumekua na Upotoshwaji Mkubwa sana na Wapinzani juu ya swala zima la Uhuru.
Jambo hili wanalitumia kwa namna mbaya ya kuleta Mafarakano kwa wananchi w Tanzania.
Watanzania hatupo tayari kutumika kisiasa na Wapinzani Uchwara.
 
Back
Top Bottom