Upotofu juu ya matumizi ya ARV na HIV/ AIDS

KITAULO

JF-Expert Member
Apr 27, 2018
1,926
2,777
Wadau,
Ni jambo la kusikitisha kuona baadhi ya member/ wadau wakipotosha wenzentu (wanaoshi na VVU) kuhusiana na matumizi ya ARV au kwa jina lingine dawa za kufubaisha makali ya virusi vya Ukimwi. Kumekuwa na utaratibu wa kuanzisha mada ali maarufu kwa nyuzi ambazo kiuhalisia ni potofu au za kuhadaa kuwaasa au kushauri waathirika kuepuka/kupuuzia matumizi ya ARV.

Ukweli ni kwamba hizi dawa zimekuwa msaada mkubwa kwa wenzetu wenye maambukizi. Hebu tujaribu kuvuta kumbukumbu hali ilivyokuwa kwa kipindi kile cha miaka ya tisini (1990s) hali ilivyokuwa mbaya. Tulipoteza ndugu jamaa na marafiki wengi mno kwa vifo vya kudhalilika. Watu walikuwa wanaisha na kubaki mifupa mitupu, vidonda mwili mzima, kupungua uzito kupita maelezo.

Serikali kushirikia na wahisani wamekuja na suluhisho la kuokoa nguvu kazi kwa kugawa dawa za kusaidia watu waweze kufikia malengo yao hali kanakwamba wanamaambukizi na tumekuwa mashahidi kwa kuona watu wanaishi hata kwa zaidi ya miaka 35 baada ya kupata maambukizi na hata mwisho wa safari zao za maisha wakifa kifo chema kwa maana ya kutokuteseka ama kudhalilika kama hapo mwanzo, kama Ukimwi ungekuwa ni habari za kusadikika mpaka leo tungekuwa na msanii maarufu wa kundi la QUEEN BAND..FREDDIE MERCURY. Nadhani kwa wachache tumewahi kusikia habari za huyu nguli aliyefariki mwaka 1991 kutokana na Ukimwi akiwa ameishi miaka 6 tu tangu agundulike ni muathirika mwaka 1985. Huyu angekuwepo mapaka leo pengine kama ARV zingekuwepo.

Nakumbuka vizuri nikiwa kijana mdogo mwaka 1995 mama yangu aligundulika ni mwathirika hii ilitokana na baba baada ya kugundua kupoteza tumaini kabisa kilichopelekea kuchukua uhai wake kwa kunywa madawa mengi mwaka 1996. Mama aliikubali hali yake na kupambana mpaka mwaka 1998 safari yake ilipokomea ikiwa ni miaka mitatu tu baada ya kugundulika, Mama aliteseka sana na alikuwa kifo cha mateso na kudhalilika mno. Naamini kama hizi ARV zingekuwepo pengine mpaka leo tungekuwa naye. Sasa mtu anaponiambia ARV ni sumu simuelewi kabisa.

Mfano mwingine dada yangu (twin wangu) anaishi na VVU kwa karibu miaka 16 sasa tangu agundulike mwaka 2004,na hii ilitokana na kukubali hali yake na kuanza matibabu ya ARV punde alivyotakiwa kufanya hivyo na wataalamu wa afya. Mpaka leo anadunda na afya yake ipo sawa kabisa na mtu wala hauwezi kudhani kama ni mwathirika.

NB: Ndugu zangu naomba mpuuzie udhalimu na upotofu wa hawa ndugu zetu wanaowalaghai muache matumizi ya arv. Serikali na wataalamu wa afya wanajua umuhimu wa hizi dawa na kweli zinasaidia mno

Ukimwi upo na unaua kinga kwanza mengine baadae.
 
Ni kweli ARV zimesaidia sana jamani, nakumbuka rafiki yangu aliekufa kwa HIV miaka ya 90, alikonda akaisha kabisa, alikuwa anaharisha nonstop, ikafikia akatokea aina ya majipu yaliokuwa yanatoka usaha mzito almost mwili mzima, jamani tusipotoshane, ukitumia ukaishi hata miaka 20 ni bora kuliko kufa kwa mateso.
 
Tatizo la hizi dawa ukitumia sana figo zinaanza kuchoka, nasikia sababu ya sumu kali sana pia wanaotumia hua wanakufa ghafla sana...
 
Tatizo la hizi dawa ukitumia sana figo zinaanza kuchoka, nasikia sababu ya sumu kali sana pia wanaotumia hua wanakufa ghafla sana...
Kama upo Dar watafute wauza majeneza toka miaka ya 90 wakueleze biashara ya majeneza ilivyokuwa nzuri nyakati hizo kwa sababu ya vifo vingi vya wagonjwa wa Ukimwi.
 
Watu wanapotoshwa sana, ingekua ukimwi haupo bas vipimo visingeonyesha +ve na -ve kwa watu tofauti, vingeonyesha majibu sawa kwa wote. ARV ni muhimu pamoja na lishe bora kwa mtu aliyeathirika.
 
Hivi Wandugu zangu ni kweli hawa jamaa wamekosa dawa kweli? au wekausha tu waendelee kupiga hela? basi ata ajitokeze snitch mmoja kati yao afanye kweli kuikomboa dunia aiachie dunia historia ya kipekee hawa jamaa wana tesa sana ulimwengu..
 
Ni kweli kabisa....hizi dawa zimesaidia sana....miaka ya nyuma ulikuwa ukitoka kumuona mgonjwa...kama unaahadi ya kufanya ngono siku hiyo unaahirisha kabisa...Lakini je kwenye maambukizi mapya ikoje?

Hhasa kama utasex na hawa wanaotumia hizi dawa....kama huyo Dada yako isijeikawa watu wanapiga tu wanajua mzima...turudi kwenye imani...ukimwi ni pepo...la sivyo hali ingekuwa mbaya zaidi.
 
Ukimwi bado una utata, kuna ndugu yangu mke wake alifariki kwa ukimwi, yeye kupima yuko safi anadunda mpaka leo mwaka wa 10, kama mwili wako unakinga nzur hata utembee na mwenye HIV hupati,
Kwa hiyo dawa ya Ukimwi ni kuwa na kinga nzuri? Hebu elezea vizuri kisayansi hii kinga inafanyaje kazi
 
Kuna kipindi mnaona biashara haziendi basi ina bidi mtumie mbinu mbadala kujaza watu uwoga

Iko siku mbona mambo yatakuwa wazi tuu sema naona imehamia homa ya ini
 
Ni kweli kabisa....hizi dawa zimesaidia sana....miaka ya nyuma ulikuwa ukitoka kumuona mgonjwa...kama unaahadi ya kufanya ngono siku hiyo unaahirisha kabisa...Lakini je kwenye maambukizi mapya ikoje? hasa kama utasex na hawa wanaotumia hizi dawa....kama huyo Dada yako isijeikawa watu wanapiga tu wanajua mzima...turudi kwenye imani...ukimwi ni pepo...la sivyo hali ingekuwa mbaya zaidi.
kusex ni maisha yake binafsi ..jambo la msing kila mtu achukue tahadhari ..kutumia kinga ama kupima kabla ya kuanza kwichi kwichi...

naamini naye ni binadamu na atakuwa na mahusiano..so tuwe macho na wakweli tukijua hali zetu
 
Take it from me,
ARV ni muhimu SI kwa afya ya muathirika tu but pia kwa mwenzi wako na huzuia maambukizi mapya. Kama ukitumia ARV kwa ufasaha there is 80% that you can have sexual intercourse with your partner without affecting her/his health.

Hii hutokea pale umetumia pills vzr to the point of no viral load in your bloodstream
 
Na kuna tetesi kwamba ukitumia ARV na kufuata masharti yake kama kula vizuri, mazoezi na nk. wengine wakirudi kupima huwa mashine hazioni virus.

NB:

Nenda kapime kwanza.
 
Back
Top Bottom