Upoteaji wa majina ya asili ya Waafrika

Kweli kabisa
Mtu mweusi anaitwa
Peter John Jacob.
Antony Peter Petro.
Antonio John Mathias.
Elizabeth Eliah Michael.
Mariam Michael John
Esau John Peter...

Huku ni kuendeleza ukoloni...

Tulipaswa kuitwa..
Ulimwengu Tanzania Tabora.
Chamtuchake Dodo Achimwene.
Msambwanda Ndiowangu urithi.
Mboondefu Mkazuzu Meza.
Fungameza Muganyizi rweyemamu.
Rweyemamu kashaija nyaishozi.
Akiba haiozi wa lindi.
Masawe marandu

Majina yetu yaasili yangetusaidia sana kulinda asili yetu duniani na ingekuwa rahisi dunia kutambua watanzania...

Hapa ndio tunasema pia tumetawaliwa kiutamaduni....
 
Hayo majina ya asili yatatusaidia nini? au yataturejesha uchumi wa kati?
Jambo kama hili la majina linaweza lisionekane kama Jambo kubwa la kuhitaji kupewa umuhimu lakini siku zote mbuyu huanza kama mchicha. Na tabia yetu sisi watu wa rangi nyeusi ya kudharau mambo madogo ndio hutusababisha kuja kupata maafa makubwa baadae. Ningeweza kukuelezea Ni jinsi gani Jambo kama hili linavyoweza kuchangia kushika kwa uchumi lakini itahitaji niandike uzi mwinge kabisa. Lakini Nina uhakika ukichukua muda na ukiwa na hamu ya kujua zaidi na kufanya uchunguzi, utagundua kuwa hata Jambo dogo Kama hili lisipotatuliwa mapema litatuletea shida, na shida zingine zimeshaanza kujidhihirisha.
 
Watoto wangu nimewapa majina ya kiafrika tu. Na hapa niliamua kuwa mbabe kidogo. Wake zangu nimewakataza kuwapa watoto majina sijui za kikristu au kizungu.

Huwa nawapa wake zangu nafasi ya kuchagua majina ila kwa maelekezo na sharti moja tu, lazima majina yawe ya kiafrika la sivyo natumia turufu yangu kutoa jina na hakuna mjadala katika hilo.

Pia nimekataa, hakuna mwanangu kuniita sijui daddy, mimi ni baba. Full stop.

Lugha pia za asili na kiswahili ndo nawafundisha watoto. Kiingereza wanajifunzia shuleni.

Huu ni msimamo wangu kama binadamu ninayejitambua.
Uko sahihi
 
Hiki kizazi cha nyoka hakitauelewa huu uzi kwa sasa. Ila siku zaja ambapo wajukuu, vitukuu na vilembwe vyetu vitaitafuta asili yao (utamaduni na mila) maana watajikuta majina yao ni kama ya wazungu lakini asili yao ni tofauti na wazungu.
Umesema kwel, tusipofanya juhudi ya kutunza asili zetu watoto wetu hawatapata nafasi ya kujua wao Ni akina Nani, chimbuko lao. Na kwahilo itakuwa ngumu kwao kusimama na kuwa imara Kama hata hawajujui wao wametokea wapi.
 
Watoto wangu nimewapa majina ya kiafrika tu. Na hapa niliamua kuwa mbabe kidogo. Wake zangu nimewakataza kuwapa watoto majina sijui za kikristu au kizungu.

Huwa nawapa wake zangu nafasi ya kuchagua majina ila kwa maelekezo na sharti moja tu, lazima majina yawe ya kiafrika la sivyo natumia turufu yangu kutoa jina na hakuna mjadala katika hilo.

Pia nimekataa, hakuna mwanangu kuniita sijui daddy, mimi ni baba. Full stop.

Lugha pia za asili na kiswahili ndo nawafundisha watoto. Kiingereza wanajifunzia shuleni.

Huu ni msimamo wangu kama binadamu ninayejitambua.
Uko sahihi sana. Tunahutaji watu wenye msimamo Kama wewe, hongera.
 
hongera sana kwa uzi huu mzuri. Hili jambo huwa nalifikiria sana aisee. Yaani tumepoteza identity yetu kabisa. Na hili kwa kiasi kikubwa linachagizwa na dini za kigeni tulizoletewa. Mfano, Kwa wakristo wanakwambia kabisa mtoto wakati wa kubatizwa apewe jina la kikristo, hapa wanakuwa washakulimit kutumia jina lako la asili kwa kisingizio cha dini. Kwani tujiulize, huwezi kuwa mkristo au muislam na ukatumia jina lako la asili.? Je jina lako ndo tiketi ya kuiona pepo?
Mbona west africans ni waumini wa hizi dini tulizoletewa na wengi wao wanatumia majina yao ya asili?

Pili, haya majina yanachagizwa na ulimbukeni wa wazazi ambao wanadhani jina la kizungu ni superior kwa jina kiafrica. Wapo radhi kulikejeli na kulicheka jina la asili na kulitukuza jina la kigeni. Huu ni upotokaji wa kiwango kikubwa sana. Yaani mtu yuko proud kuitwa jina la muarabu au mzungu ila asiitwe jina ala asili yake!

Hivi wazungu/ waarabu tuliwa jiuliza huwa wanatufikiriaje wakisikia tunajiita majina yao?
Ni kweli kwamba dini zimechangia Sana katika kukuza tatizo hili. Lakini tukumbuke kuwa hizi dini zililetwa na hao wakoloni wakiwa na lengo lao walilotaka kulitimiza, dini sio mbaya lakini tusiwe walimbukeni wakutumia dini kama kisingizio au kitu Cha kutukandamiza hata maandiko yametuambia kuwa tutumie maarifa yetu tuliyopewa na Mungu (wanadamu wanaang'amia kwa kukosa maarifa). Inabidi tutumie maarifa ya kutambua kuwa hatuhitaji kuyakana majina yetu I'll twende mbinguni, Mungu mwenyewe alikuwa na sababu zake za kutufanya tuzaliwe Tanzania na kuwa na tamaduni hizi. Tulinde tamaduni zetu.
 
Back
Top Bottom