Upoteaji wa majina ya asili ya Waafrika

Ni kweli kama ni maharifaa sina, nielekeze yanapatikana wapi, Lakini kama ni maarifa ninayo na nazidi kuwa nayo, day after day
Acha ubishi wa kitoto wenzako tumeona mengi Dunia hii usichukulie vitu simple simple au nikupigie usiku huu twende ukajue mambo ya asili 😂😂😂😂 jokes
 
Tunaogopa kuwapa watoto majina ya asili kwa sababu wenye majina hawapo, wamekufa wengine tushagombana n koo z afamilia kwa kushikana uchawi, wengine tangu tuondoke uko vijijini tangu tuondoke hatujarudi tunaogopa kulogwa sasa nani atawafanyia mambo ya asili endapo jambo likitokea usicheze na mambo ya asili kama ujui utajuta

Mnasema watoto wenu hawana akili darasani, mabinti mnalalamika hamzai wengine hamuolewi unazani shida inaanzia wapi shida ni hayo majina hayo mtoto unamwita kinjekitile, mkwawa, kashindye ujui mila na matambiko
Hayo ya kizungu wenye hayo majina bado wapo hai? Kuna shule wanangu wanasoma Nadhani ni wanangu tu ndo wana majina ya kilughaNdo wamekuwa ikon huko ... unakuja farasi lina Jayden 4!!!
 
Kuna jamaa yangu ana watoto 8 na watoto 7 wana majina ya asili sasa hawa watoto wote hakuna aliyemzima ni mwendo wa kuumwa kila wakati hebu tazama kuna kipindi watoto 3 walilazwa kwa pamoja kuna aliyekuwa bugando, Sekwao Toure (Seketule) na Mhimbili na wengine nyumbani baadhi wanalipuka mapepo n.k ila huyu mwingine 1 asiye na hayo majina hana shida yoyote akaja gundua baba yake na mama yake dada zake shangazi zake wengi ni wachawi wa kutupwa hivyo wanachezea watoto tangu nilipoona hili tukio la huyu bwana tena kwa macho yangu na wala si kusimuliwa HAKUNA MWANANGU ATAITWA HAYO MAJINA

Tatizo africa ktk koo zetu kuna mambo machafu na ya ajabu ila hatupendi hata kuyajadili unaweza jikuta unateseka ktk maisha yako yoote ya hapa duniani kisa majina ambayo kwa hakika hatujui hao wahenga wetu walikuaje. Mfano kuna jamaa alimaliza form 6 1992 PCB kutoka shule kubwa flani hapa nchini alipata division 1.5 yaani alikuwa BBA kabla ya kujiunga na MUHAS aliumwa miaka 3 yupo home na baadae akajiunga MUHAS akaumwa tena mwisho akaambiwa ili apone inabidi awe mganga wa kienyeji na kweli alipokubali akapona sasa hivi anatibu watu huko kijijini ana manywele mareefu kama jini lililofufuka hana mbele wala nyuma.
Mfano Lucy, Good luck kimasai kuna majina yake yenye maaha hii hii
Mimi sio mmasai ila wanangu nimewaita Namunyak na Esupat means Bahati / Good luck na Mwena respectively.

Nikipata mwingine namwita Nailejileji means Comfort kimasai
 
24 Reactions
Reply
Back
Top Bottom