uporwaji mwingine huu hapa,Mhe Prof Tibaijuka unajua

kimboka one

JF-Expert Member
Jan 23, 2010
734
85
jamani Tanzania ilipata uhuru mwaka 1961,wananchi tunaheshimiana na kupendana na hasa wananchi tunaupendo mkubwa na jeshi letu la wananchi,hiki wanachokifanya waporaji wachache wanataka kuondoa uhusiano nzuri uliopo kati yetu,nasema hapa maana tumejaribu sana kuwasiliana na wahusika lakini hakuna majibu labda hapa JF naweza kupata msaana.WAKAZI WA ENEO LA AMANI GOMVU KIGAMBONI WAMEPORWA MASHAMBA YAO kwa kinachodaiwa eti mashamba hayo yamechukuliwa na jeshi,hapa sipingani hata kidogo kama kweli ni jeshi linataka mashamba hayo ni vema lakini wanatakiwa kufuata taratibu walau ata taarifa tu juu ya mpango huo kwa viongozi wa mtaa au kata ambao mpaka sasa hakuna mwenye taarifa ila wamekuta jiwe linaloonesha mashamba yaha ni ya jeshi.mi ninasema huu ni uporaji wa haki za wananchi na tena wamefika mbali pale walipoamua kuvunja ujenzi katika mashamba hayo hivi ujasiri huu wanatoa wapi?,mhe waziri wa aridhi kunanini? hapa.na kunatetesi kwa wananchi kwamba huu ni mpango wa wakubwa kutumia jina la jeshi ili wajimilikishe aridhi hiyo kiulaini,nami nimefanya ka utafiti nikapata ramani ya pale ambayo ina kichwa cha habari kingine lakini kimefutwa na kuandikwa kwa mkono eneo la jeshi hata ukienda pale ofisi za aridhi temeke utakuta wamebandika ukutani,na kila mtu utakaye muuliza anatoa maelezo ya kujikanyaga wakionesha kuwa mpango huu si rasmi,wadau tusaidie na mama wa aridhi kama utaipata hii ifanyie kazi,mnataka twende wapi? kama ta huku vijiji mnatutoa bila ata fidia au taarifa,itafika mahali nasi tutakuja huko masaki.
 
Back
Top Bottom