Upo uzembe mkubwa kwa Serikali kusimamia fursa katika miradi ya maendeleo tuliyokopa

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
Nimeenda mradi wa maji mmoja tunaoutekeleza hapa nchini kwetu kwa kutumia mkopo wa mabilioni kutoka "EUROPEAN INVESTMENT BANK" pamoja na AFD.

Mabilioni haya tuliyakopa tunatekeleza mradi huo kwa kutumia kampuni ya kichina.

Kampuni imeajiri wahandisi watanzania wanne na anayelipwa fedha nyingi ni milioni 3.5 lakini kampuni imeajiri wachina kibao ikiwemo wafungwa huko kwao. mfungwa wa kichina ambaye hata elimu yake hajafikia engineer analipwa milioni 6 anapofanya kazi kwenye mradi huu.

Bado mimi najiuliza inakuwaje tunaruhusu mgeni anakuja kwetu analipa mfungwa wa huko kwao kuliko mhandisi wa kwetu?

Halafu wahandisi hawa wameajiriwa wanafanya kazi ambazo si za saiti, kazi za saiti zote wanafanya wachina wenyewe.

Kwa maoni yangu tunalo jukumu kama taifa kuhakikisha tunapokopa, kuhakikisha tunaingiza wataalamu wa kutosha katika miradi miradi hii ambayo tumekopa na baadae tutalipa na kuhakikisha hata watu wetu wanalipwa fedha nzuri kwenye miradi hii.

Nakumbuka mwaka 213 serikali ilipitisha sheria ya wafanyakazi wote wanaofanya kazi kwenye construction kulipwa sio chini ya 10,000 kwa siku. Sheria hii ilileta mapinduzi makubwa kwa vibarua katika makampuni ya ujenzi kwani vibarua walikuwa wanalipwa mpaka elfu 3 kwa siku.

Sasa tunalo eneo jingine la kutazama jinsi gani wataalamu wetu tunaowasomesha wanaingizwa katika miradi hii tuliyokopea fedha kwanza kutengeneza ajira na pili kubakiza sehemu ya pesa hiyo katika jamii yetu.

Upo ubaguzi mkubwa sana katika makampuni mengi yanayotekeleza miradi hii baina ya wazawa na wageni kana kwamba nchi yetu bado hatujapata uhuru na tunayo matabaka bado ya wageni kuwa first class na wenyeji kuwa third class.

Usisahau kukomenti na kunipia kura ili tushirikiane kutokomeza ubaguzi katika jamii yetu ambao una sura ya ajira
 
Nimeenda mradi wa maji mmoja tunaoutekeleza hapa nchini kwetu kwa kutumia mkopo wa mabilioni kutoka "EUROPEAN INVESTMENT BANK" pamoja na AFD.

Mabilioni haya tuliyakopa tunatekeleza mradi huo kwa kutumia kampuni ya kichina.

Kampuni imeajiri wahandisi watanzania wanne na anayelipwa fedha nyingi ni milioni 3.5 lakini kampuni imeajiri wachina kibao ikiwemo wafungwa huko kwao. mfungwa wa kichina ambaye hata elimu yake hajafikia engineer analipwa milioni 6 anapofanya kazi kwenye mradi huu.

Bado mimi najiuliza inakuwaje tunaruhusu mgeni anakuja kwetu analipa mfungwa wa huko kwao kuliko mhandisi wa kwetu?

Halafu wahandisi hawa wameajiriwa wanafanya kazi ambazo si za saiti, kazi za saiti zote wanafanya wachina wenyewe.

Kwa maoni yangu tunalo jukumu kama taifa kuhakikisha tunapokopa, kuhakikisha tunaingiza wataalamu wa kutosha katika miradi miradi hii ambayo tumekopa na baadae tutalipa na kuhakikisha hata watu wetu wanalipwa fedha nzuri kwenye miradi hii.

Nakumbuka mwaka 213 serikali ilipitisha sheria ya wafanyakazi wote wanaofanya kazi kwenye construction kulipwa sio chini ya 10,000 kwa siku. Sheria hii ilileta mapinduzi makubwa kwa vibarua katika makampuni ya ujenzi kwani vibarua walikuwa wanalipwa mpaka elfu 3 kwa siku.

Sasa tunalo eneo jingine la kutazama jinsi gani wataalamu wetu tunaowasomesha wanaingizwa katika miradi hii tuliyokopea fedha kwanza kutengeneza ajira na pili kubakiza sehemu ya pesa hiyo katika jamii yetu.

Upo ubaguzi mkubwa sana katika makampuni mengi yanayotekeleza miradi hii baina ya wazawa na wageni kana kwamba nchi yetu bado hatujapata uhuru na tunayo matabaka bado ya wageni kuwa first class na wenyeji kuwa third class.

Usisahau kukomenti na kunipia kura ili tushirikiane kutokomeza ubaguzi katika jamii yetu ambao una sura ya ajira
mfano wa jinsi wenzetu wanavyobana malipo kwa watu wao

"Minimum Contractor Staff and Salaries (Technical Specification ITB 2011-023 – Lot # 1)
Beside labours and technicians, the minimum contractor’s staff should be as follows:
1. Project Manager 1
2. Site Engineer 1
3. Office boy 1

The minimum salaries of the contractor’s staff should be as follows:
1. Project Manager 25 US$
2. Site Engineer 20 US$
3. Office boy 12 US$
4. Technician 15 US$
5. Worker 12 US$"


unaweza kuona viwango hivyo angalau vinaweka minimum payment na havisemi kama mwajiriwa atakuwa mbongo alipwe kidogo na kama ni mweupe alipwe kufuru.

bado tunao ubaguzi wa rangi katika kazi zinazojumuisha wageni na wenyeji na tunapaswa kupambana na hilo.

nafasi za wazawa katika management lazima ziwekwe wazi kupitia mikataba au sheria za kazi
 
Back
Top Bottom