Upo uwezekano mkubwa Rais Magufuli hatoivusha Tanzania salama

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,874
Kwa jinsi mambo yanavyoenda na huko tulipotoka, naamini kuwa upo uwezekano mkubwa wa Rais Magufuli kutokuivusha Tanzania salama.

Nimeona vihashiria kuwa sasa wananchi wanaonyesha kuchoshwa kweli na mwenendo wa siasa za kibabe za nchi yetu. Hili ni jambo la hatari.

Ni kweli kuwa kwa muda wa miaka minne na nusu iliyopita, Tanzania imepitia majaribu makubwa na naamini sasa kwenye majaribu hayo ndiyo tuanelekea zaidi kwenye makali.

Unaweza usinielewe kwa sasa kutokana na mtazamo ulio nao, ila inahitaji maombi ya "kufa mtu" ili kuivusha nchi salama na hili wimbi. Inavyoonekana ni kama tumeamua wenyewe kujipeleka huko kutokana na kiburi chetu na kujisahau kuwa sisi tupo duniani na tumezungukwa na ardhi, siyo maji.

Kila kona sasa ni vurugu mechi, mambo ya kuzuia moto kwa nguo wala hayana maana. Kufunika pembe la ng'ombe kwa kiganja huku ukiamini kuwa umelizuia kuchomoza, ni ujinga. Kama nchi tunaelekea kufumbwa macho ili mengine yatokee!

Nani atamfunga paka kengele?
 
Mku mbona hujaeleweka sijui unaogopa nini?" ili kuivusha nchi salama na hili wimbi" Hilo wimbi ndo nini?
 
Ukisoma mitandaoni habari za siasa za Tanzania unaweza kuishi kwa hofu kubwa au kwa kujipa matumaini kuliko uhalisia wa mambo.

Ni kama vile wakati wa COVID-19 imepamba moto duniani ilikuwa ukienda mitandaoni hasa twitter unaweza kusema kila siku kwenye kila mtaa kuna mtu mmoja anakufa kwa huo ugonjwa hapa Tanzania.

Ukweli Lissu kapigwa pini mbaya sana kwenye media, kama kungekuwa hakuna viashiria vya 'bad motive ya wale wa nje' ningewaomba wenye dhamana wapunguze hii censorship ya media inapunguza hali na mushawasha wa uchaguzi mkuu.

Tatizo jombaa nae analipuka sana kinoma noma anachafua taswira ya nchi nzima, hata kama ni kumwaga mboga hii imezidi haina faida sana kwa nchi yake, kashikia bango COVID-19 sivyo kabisa.

Aliyeteseka na vikwazo dhidi ya Zimbabwe si Mugabe na familia yake ni wananchi na ndugu za wapinzani.
 
Jifunze kusoma kwanza kisha ulete hoja.
Hakuna kitu kinaitwa vihashilia.
Acha kukurupuka au unakimbizwa?
 
Kwa jinsi mambo yanavyoenda na huko tulipotoka, naamini kuwa upo uwezekano mkubwa wa Rais Magufuli kutokuivusha Tanzania salama.

Nimeona vihashiria kuwa sasa wananchi wanaonyesha kuchoshwa kweli na mwenendo wa siasa za kibabe za nchi yetu. Hili ni jambo la hatari.

Ni kweli kuwa kwa muda wa miaka minne na nusu iliyopita, Tanzania imepitia majaribu makubwa na naamini sasa kwenye majaribu hayo ndiyo tuanelekea zaidi kwenye makali.

Unaweza usinielewe kwa sasa kutokana na mtazamo ulio nao, ila inahitaji maombi ya "kufa mtu" ili kuivusha nchi salama na hili wimbi. Inavyoonekana ni kama tumeamua wenyewe kujipeleka huko kutokana na kiburi chetu na kujisahau kuwa sisi tupo duniani na tumezungukwa na ardhi, siyo maji.

Kila kona sasa ni vurugu mechi, mambo ya kuzuia moto kwa nguo wala hayana maana. Kufunika pembe la ng'ombe kwa kiganja huku ukiamini kuwa umelizuia kuchomoza, ni ujinga. Kama nchi tunaelekea kufumbwa macho ili mengine yatokee!

Nani atamfunga paka kengele?
TUKIRUDIA KOSA TENA TUMEKWISHA ATAVURUNDA ZAIDI MAANA ATOHITAJI TENA KURA ZETU NAFASI PEKEE NI OCTOBER ZAIDI YA HAPO TUMEKWIISHA
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom