Upinzani watangaza mapambano 2008

STATE DEPARTMENT Ndio wanaoshughulika na masuala yanayohusiana na makubaliano ya kisheria baina ya US na mataifa mengine pale inapokuja kwenye makubaliano ya ugaidi na Corruptions pamoja na money laundering!

Kwenye yale makubaliano aliyoyasaini Kikwete kuna sehemu imewekwa wazi kabisa kuwa haya makubaliano ni sheria!
 
Ulisoma kile alichosema balozi wa US kipindi kile issue ya Balali ikiwa moto kwenye media bongo? Marekani walikuwa tayari kusaidia kumleta Balali TZ lakini serikali ya CCM kama kawaida yao waka ...........

Kwanini asiwa organize watanzania wote hapa ili tuishinikize marekani watukabidhi mtuhumiwa as per agreement?
Ama ni kwasababu ameshapinga urafiki na Kikwete?
 
Zitto hakuwa bungeni wakati huo.... wabunge waliokuwa bungeni wa upinzani na wachache wa ccm walijaribu bila mafanikio kuunda kamati huru ya bunge kwenye hili.

Katika hili Zitto hawezi kujibu maswali yako maana hana power ya kutoa content ya kilichomo kwenye report mpaka aliyeunda tume/kamati atakapoitoa rasmi.

Kwa sasa Zitto atakachofanya ni kusubiria tu kama wewe na mimi kuona Kikwete atafanya nini na report ya kamati yake aliyoiunda kwa mbembwe nyingi.

Ok sasa baada ya kuyatema yaliyoitwa maslahi na kukubali suspension yake...Ni wazi kama si wasamaria wema na juhudi za upinzani kumchangia pesa hali yake ingekuwa mbaya!
Then Kikwete akamwambia njoo hapa kijana..This is the way it should be done?
 
Ukiwa mpinzani nadhani huwezi ukapinga kila kitu .Kuna maamuzi na utashi wa mtu.Zitto kama Watanzania wengine amekuwa akiamini kwamba JK can make changes , maana hata kuna wengine hapa piga ua wanasema CCM safi angalau yeye anasema JK can do something .Kuna usemi tata hapa .Kwamba JK ana nia njema na kaonyesha nia .Mimi naupinga muda wote .Zitto anaamini JK ana nia njema so anampa nafasi yake je ni ubaya kwa Zitto kumetetea mtu anaye weza kuamini kwamba anaweza kufanya jambo ? Uhuru huu jamani wa mtu .

Kama uamuzi wowote wa Kikwete hautahusisha kukamatwa kwa mafisadi...Then mimi na wao!
 
Tanzania’s Threshold Program will improve the ability of civil society to monitor the government’s progress in combating corruption; strengthen the rule of law so that corruption cases can be successfully tried and offenders convicted; establish a Financial Intelligence Unit to detect financial crime; and increase the transparency of public procurement. The U.S. Agency for International Development, assisted by the Departments of Treasury and Justice, will administer and oversee implementation of the program. Tanzania will move ahead to implement its Threshold Program following a period of Congressional notification and a signing ceremony, scheduled to take place in Washington, DC.
 
Mama Mkapa ni nee Maro,

Je Yona Maro wetu ana uhusiano naye? Isije kuwa kuna maslahi ya kifamilia.
 
Tanzania’s Threshold Program will improve the ability of civil society to monitor the government’s progress in combating corruption; strengthen the rule of law so that corruption cases can be successfully tried and offenders convicted; establish a Financial Intelligence Unit to detect financial crime; and increase the transparency of public procurement. The U.S. Agency for International Development, assisted by the Departments of Treasury and Justice, will administer and oversee implementation of the program. Tanzania will move ahead to implement its Threshold Program following a period of Congressional notification and a signing ceremony, scheduled to take place in Washington, DC.

Samahani Mwafrika wa Kike..Ni Departments of Treasury and justice.
 
Shy

Wewe ni mmoja kati ya watu wa hatari san wanaonitisha hapa Tanzania.

Nikiangalia namna unavyojibu hoja inaonekana kabisa kuwa una kichwa kizuri na kwa hiyo kwa kutumia resourses za Tanzania umeandaliwa vizuri. lakini unaonesha wazi kuwa umechagua kutumikia genge la mafisadi. Sikunyimi kuchagua kazi wala mwajiri. Lakini nakushauri usifanye kazi za fedheha kwako na kwa nchi yako.

NInajiaminisha kuwa unafahamu fika kuwa umasikini wa Tanzania unatokana na ufisadi na sera mbaya sana za CCM za uwekezaji na kulinda waovu. Wewe unaonyesha wazi kufanya moja ya kazi muhimu sana wanayopewa vidampa wa CCM ya kuwalinda na kuwasafisha waovu a.k.a mafisadi. Kama nilivyokuahidi mwanzoni kuwa sitakupangia ajira ya kufanya, hata sasa sifanyi hivyo. Fanya kazi yoyote ili mradi mkono uende kinywani

Kwa kuwa umekuwa ukijiita RESEACHER. Ningekushauri ujitahidi sana kuweka jamvini hoja zinazodhihirisha kuwa wewe ni researcher. Vinginevyo kwa pumba unazoweka hapa jamvini ninakuona kama unadhalilisha fani. Wenye fani yao watakapokuibukia sijui utajificha wapi.

Watch out today's Tanzania is as bright. Your words can't be carried in our vessel brother.
 
Last edited:
Kwa sasa Zitto atakachofanya ni kusubiria tu kama wewe na mimi kuona Kikwete atafanya nini na report ya kamati yake aliyoiunda kwa mbembwe nyingi.
Hiyo ripoti ameshakabidhiwa rais. Kila mtu anasubiri rais aitangaze. Nilipokuwa Bongo nilipata nafasi ya kuzungumza na Mzee Mark Bomani. Kuna mambo mazito humo subirini tu. Tume imefanya kazi yake na rais ameshapewa.
 
Hiyo ripoti ameshakabidhiwa rais. Kila mtu anasubiri rais aitangaze. Nilipokuwa Bongo nilipata nafasi ya kuzungumza na Mzee Mark Bomani. Kuna mambo mazito humo subirini tu. Tume imefanya kazi yake na rais ameshapewa.


Mkuu Jasusi
Baada ya ripoti ile kuwekwa mezani kwake katika kuta za Ikulu nimenasa info kwamba hatayasema yote ambayo akina Zitto wameambiwa na wananchi .So tutegemee porojo na ngoma kuishia hapo .Yaliyomo ni mazito na yanaweza kweli kuimaliza CCM maana ndiyo wako madarakani .Nime bahatika kupata rough report si kamili .Mama yangu twafa .
 
Mkuu Jasusi
Baada ya ripoti ile kuwekwa mezani kwake katika kuta za Ikulu nimenasa info kwamba hatayasema yote ambayo akina Zitto wameambiwa na wananchi .So tutegemee porojo na ngoma kuishia hapo .Yaliyomo ni mazito na yanaweza kweli kuimaliza CCM maana ndiyo wako madarakani .Nime bahatika kupata rough report si kamili .Mama yangu twafa .

Lyunyungu,
Kijuu juu tu maana tunasubiri uhondo utoke Ikulu, Mzee Bomani anasema hii mikataba ya madini utafikiri waliyoisaini walikuwa wamenyweshwa pombe. Mtu mwenye akili zako timamu, tena mtaalamu wa sheria, usingekubali baadhi ya mikataba tuliyoisaini katika madini. Pia anasema kuna ushahidi kuwa kuna mikataba ililetwa imeshaandikwa na kuandaliwa na wawekezaji na kazi yetu ilikuwa ni kuweka tu mkono, bila hata kuhoji. Lakini tusubiri, tusimwondolee rais ile excitement ya breaking news.
 
Hiyo ripoti ameshakabidhiwa rais. Kila mtu anasubiri rais aitangaze. Nilipokuwa Bongo nilipata nafasi ya kuzungumza na Mzee Mark Bomani. Kuna mambo mazito humo subirini tu. Tume imefanya kazi yake na rais ameshapewa.

Jasusi unataka tukumbuke kumsubiri Mh Rais atoe ripoti halafu tumsahau nani?
 
Mkuu Jasusi
Baada ya ripoti ile kuwekwa mezani kwake katika kuta za Ikulu nimenasa info kwamba hatayasema yote ambayo akina Zitto wameambiwa na wananchi .So tutegemee porojo na ngoma kuishia hapo .Yaliyomo ni mazito na yanaweza kweli kuimaliza CCM maana ndiyo wako madarakani .Nime bahatika kupata rough report si kamili .Mama yangu twafa .

Hayawi hayawi....
Sasa baada ya hapo nani wa kulaumiwa if that happens to be the truth?
 
Jasusi unataka tukumbuke kumsubiri Mh Rais atoe ripoti halafu tumsahau nani?

kwi!kwi!kwi!
Labda tusahau ya Richmond, EPA na vijisenti. Yaani Tanzania yetu hii if it is not one thing it is the other.
 
Naona kuna watu wengi pamoja na mimi huwa hatukubaliani na maswala unayowakilisha.Leo naunga mkono ka-part...

Lakini hili jambo la upinzani kutokuwa na policy mpya kinanikera sana. Maana wao ukiangalia sana ni critic of the government of the day...hio ni wajibu wao lakini mbona hawatoi mbadala?

Uti wa mgongo wa Tanazania ni KILIMO lakini hakuna hata chama kiwe CCM au wapinzani ambao wana sera nzito ya kilimo na kuweza kutunyayua sisi wakulima into new century.
kwenda zako huzijui sera za vyama hivyo na wala hujazisoma manifesto zao mf. za 2005 ndio maana unakimbilia kusema havina sera nzuri za kilimo, wewe na shy sawasawa tu
 
Mi nakumbuka tulipiga kelele sana hapa JF kuhusu Mh Zitto kuingia kamatini ama la!
Kwamba kama uamuzi wake huo utakuwa na manufaa yoyote yale kwa wananchi!
Kwamba uamuzi wake huo hautambana kuweza kufanya kazi yake ya kuwatumikia wananchi vyema!
Kwamba.... Kwani hakuwa na taarifa kuwa kuna kamati nyingi tu ambazo zilishafanya kazi zake na kuwasilisha ripoti lakini all got blown to the wind! Bado zimekaliwa na watu wesha kula mafao yao?!
Na hakuna hata mwanakamati mmoja ambaye anajishughulisha kumbana Rais atoe Ripoti! Whether ni hii ya kina Zitto ama nyinginezo zilizopita!
Wao wanaplay on his game kwasababu Election year ni kama mwaka tu na ushee and the propaganda ni kuendelea kusubiri kama tulivyokuwa tukisubiri ripoti za kamati zote zilizopita going back to Mkapa's reign!
TUMESHASAHAU!
 
Nadhani lilikuwa wazo zuri kwa Zitto kuwemo kwenye hiyo kamati. Hii ilikuwa ni kamati ya kitaalamu na wala siyo ya kisanii kwa hiyo kuwa na watu kutoka pande mbalimbali lilikuwa wazo zuri. Alinichekesha Mzee Bomani kwamba aliulizwa na watu mbalimbali kuwa na "wewe mzee umekubalije kuingia kwenye hii tume ya wasanii?" Yaani hata kabla ya kazi kumalizika kuna watu walishaiona hiyo tume kuwa ni gelesha tu. Lakini nadhani wamefanya kazi nzuri. Ngoja tusubiri tuione ripoti yenyewe, na kama wasemavyo Wamarekani the proof will be in the pudding.
 
Shy, ukweli ni kwamba unachemsha sana na unatakiwa kuona "shy" kwa Watanzania. Pesa zilizoibiwa ni zaidi ya pesa zote alizotoa Bush za barabara na wanaofaidika ni wachache walioaminika na jamii. Watanzanhia tulioko nje tunauchungu kwani sisi huku wenzenu tunafanyakazi kwa bidii na hatuishi kwa kuibia watu kama nyie wa bongo, sisi hapa si wafisadi. Watanzania walio nje wametuma zaidi ya $400M mwaka jana tu kusaidia ndugu na jamaa, pesa hii ni ya jasho na kazi za usiku kucha lakini kinachouma ni kwamba Watanzania wenzetu badala ya kusaidia hawa Wananchi masikini kwa kujenga barabara, hospitali,mashule na umeme unajilimbikizia pesa za misaada kwenye account za nje na kufanya ufisadi.Hakuna jambo ambalo litafanyika kama wafisadi ndio wanaongoza nchi labda mabadiliko mengine yafanyike. Hivyo ningekushauri kama Shy kweli unapenda nchi yetu basi kemea wafisadi na wapinzani wanahaki zote za kupongeza na kuongelea ufisadi kwani ni jambo kubwa sana. Mikataba mingi imesainiwa vibaya kwasababu ya rushwa na mipango ya maendeleo gani yatuzuia waziri kuiba zaidi ya sheria!, je ni nani amefungwa kutokana na wizi wa pesa ya wananchi, je kunampango gani wakukomesha mafisadi kutoka kwa CCM. Mafisadi wanatakiwa kuelewa kwamba miaka 20 ijayo wananchi hawatavumilia 2% ya Watanzania wawe na uwezo halafu 98% wawe masikini italeta mitafaruku mikubwa na huku nje hiyo pesa itaisha tu. Shy sisi wa nje ni lazima uelewe si wanasiasa lakini tuna uchungu na nchi yetu na wengi wetu tutakuwa na maisha mazuri tu lakini tunasikitika kuona Watanzania wenzetu wanakula pesa ya uma ya vizazi vijavyo. Zitto kwa upande mwingine anaonekana kuwa na upeo mkubwa kuliko viongozi wengi wazee!!
 
Ukweli ni kwamba upinzani hawana nyimbo kabisaaa wala game plan ya maana.

Halafu Mwanakijiji unaumwa au? Naona umebonyeza thanks mfululizo humu, sasa sijui kibao cha mall kimekufanya trigger happy?
 
nzoka.. hizi asante ni kwa sababu nimesoma posts zao zote na zimekuwa "useful" katika kuandaa jibu langu.
 
Back
Top Bottom