Upinzani watangaza mapambano 2008

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Posted Date::1/2/2008
Upinzani watangaza mapambano 2008
Salim Said, MUM na Muhibu Said
Mwananchi

VYAMA vya CUF, Chadema, NCCR-Mageuzi na TLP, vimesema vitautumia mwaka mpya wa 2008 kuendesha mapambano ya kudai katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi ili kujenga demokrasia ya kweli nchini.

Azma ya vyama hivyo vilivyomo kwenye ushirikiano wa kisiasa, ni miongoni mwa salamu na ujumbe wa mwaka mpya, uliosomwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kwa niaba ya wenyeviti wenzake wa vyama hivyo, walipozungumza na waandishi wa habari makao makuu ya CUF, jijini Dar es Salaam jana.

Akisoma salamu na ujumbe huo, Mbowe alisema mapambano hayo ambayo watayapa kipaumbele mwaka huu, yatatumia mbinu mbalimbali kuishinikiza serikali kuingiza ajenda hizo kwenye utendaji wake ndani ya mwaka huu. Tunautangaza mwaka mpya wa 2008 kuwa ni mwaka wa mapambano ya kudai katiba mpya na tume huru ya uchaguzi.

Tumekusudia kuongeza presha ya hali na mali kwa kuwashirikisha wadau wa ndani na nje ya siasa kuhakikisha katiba mpya inapatikana. Pia tunatambua umuhimu wa kuwapo tume huru ya uchaguzi, alisema Mbowe na kuongeza:

Tunayafanya mambo haya kama ndio ajenda yetu kuu kwa mwaka huu, kwa sababu kama itafika mwaka 2009 suala la madai ya katiba mpya na tume huru ya uchaguzi yatakuwa hayajaingizwa katika ajenda za utekelezaji wa serikali, basi itakuwa vigumu kutekelezwa, kwa kuwa mwaka 2009 hadi 2010 ni kipindi kifupi mno kudai mambo hayo.

Hata hivyo, alisema tayari wameshaandaa rasimu ya katiba ambayo wataipeleka kwa wananchi ili kuijadili na kutoa maoni yao juu ya katiba mpya.

Alisema suala la tume huru, si ushiriki wa wapinzani ndani yake, bali linatokana na mambo mengi, ukiwamo mfumo, sheria, muundo, mamlaka, majukumu na wajibu wake katika mustakbali na mchakato mzima wa kuandaa na kusimamia chaguzi mbalimbali nchini. �Hatuna mfano mzuri na cha kujifunza zaidi ya ni hali ya Kenya kwa sababu tume zinajiona kuwa ni sehemu ya serikali ndani ya nchi husika, alisema Mbowe.

Alisema hali ngumu ya maisha inayowakabili Watanzania ni matokeo ya jeuri za viongozi wa serikali kupuuza ushauri wa wananchi, sera mbovu, zisizokuwa endelevu zinazopangwa na serikali kwa kuwafanya wananchi kama mateka na kuwafanya wanavyotaka.

Hali hiyo ndugu zangu haitokani na kupanda kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia. Hivyo ni visingizio tu vya serikali kwani Kenya, Uganda na hata Msumbiji nao wananunua mafuta hayo hayo na kwenye soko hilo hilo, lakini hakuna mfumko wa bei ya bidhaa kama Tanzania, alisema Mbowe.

Alitoa pole kwa Wakenya walioathiriwa na vurugu za kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyomweka madarakani Rais wa nchi hiyo, Mwai Kibaki. Hata hivyo, alisema kitendo cha Rais Kibaki kutangazwa na kuapishwa kushika wadhifa huo haraka haraka ni kuonyesha matokeo ya uchaguzi huo hayakuwa sahihi.

Alisema kutangazwa na kuapishwa haraka haraka kwa Rais Kibaki, hakukufanywa kwa lengo la utendaji bali kumkabidhi madaraka na jeshi kama nyenzo ya kuwakandamiza aliowadhulumu haki zao kwenye uchaguzi.

Akizungumzia michezo, Mbowe alisema serikali imefanya sekta ya michezo kuwa ni jukwaa la propaganda za kisiasa, badala ya kuifanya kuwa sekta nzuri ya kutoa ajira kwa vijana.

Badala ya kuichukulia michezo kama sekta nzuri ya kutoa ajira, serikali ya CCM inaichukulia sekta hiyo kama jukwaa la propaganda za kisiasa ambapo timu yetu ya taifa ikishinda huitwa JK eleven, lakini inaposhindwa huitwa Taifa Stars, alisema Mbowe.

Alisema pia katika mwaka mpya wa 2008, ushirikiano wa vyama vyao, utaendelea kujenga hoja za nguvu ili kuibana serikali na kuwatetea wananchi bila woga na kuwahamasisha Watanzania kuunga mkono upinzani. Vilevile alisema wataendelea kuboresha na kustawisha ushirikiano wa vyama vyao kwa kushughulikia kasoro zinazojitokeza na kujenga hali ya kuaminiana.

Tutaendelea kuufanya ushirikiano wa vyama vyetu usiwe wa viongozi wa juu tu bali uwe ushirikiano wa Watanzania wote walioshikama na kupambanma na mfumo wa chama dola unaowasababishia kuendelea kuogelea kwenye ujinga, maradhi, umaskini, ufisadi na dhuluma kwa miaka 46 ya uhuru bila sababu zozote za msingi, alisema Mbowe.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Juma Duni Haji alidai kuwa tatizo la serikali ya Rais Jakaya Kikwete ni kuweka mbele usanii kuliko utendaji na kudai kuwa kwa kawaida katika nchi zinazofuata mfumo wa utawala bora kunakuwa na uwajibikaji na uwajibishwaji lakini Tanzania hakuna mambo hayo.

Kwa mfano, katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) kulikuwa na mtu aliyetakiwa kupasuliwa mguu akapasuliwa kichwa na aliyetakiwa kupasuliwa kichwa akapasuliwa mguu. Ilitakiwa Waziri Mwakyusa (Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David) awajibike, lakini cha ajabu hakuna aliyewajibika au kuwajibishwa isipokuwa tume kuundiwa tume, alisema Haji.

Naye Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia aliwapa pole Watanzania kutokana na kuanza mwaka mpya kwa gharama kubwa za bei mpya ya umeme na kusema kuwa wasitarijie unafuu wowote wa maisha kwa sababu kupanda kwa umeme, kutasababisha kupanda kwa bei za kila kitu.

Nyota njema huonekana asubuhi, kama leo tunauanza mwaka mpya kwa kupandishiwa bei ya umeme, Watanzania tutarajie maisha magumu zaidi.. alisema Mbatia.

Wakati huo hu, Naibu Katibu Mkuu wa TLP, Benedict Mutungirehi alisema kupanda kwa gharama za umeme, kumefanywa ili kuwabana wananchi wafidie madeni ya Shirika la Umeme nchini na kampuni ya IPTL ambapo kila mwezi serikali hulipa zaidi ya Sh3 bilioni.
 
Niliwahi kuona tangazo katika mtandao wakati Fulani , mmoja wa wabunge wa upinzani Tanzania ameacha namba yake ya simu atakayotumia atakapofika marekani , kwa wale ambao hawako busy wanapenda kuonana nae na vijana wengine wengi wenye muelekeo wa kipinzani .

Sitaki kubisha inaonekana wapinzani wamewashika sana vijana wa kitanzania walio nchi za nje haswa marekani kiasi kwamba zitto anapokanyaga huko wanaona mwokozi wao kafika watu wanasongamana wanataka kumwona kupiga nae picha na vitu kama hivyo .

Pamoja na kuacha hizo namba za simu na watanzania kujitokeza kuonana nae , sera na mambo anayoongea katika mikutano hii ni zile zile , za ufisadi ambazo sasa hivi ni zilipendwa , yale yale ya epa na mambo mengine ambayo kwa hakika sio ya kujenga upinzani sio ya kujenga nchi ni ya kupasua hadhi ya nchi na watu wake nje ya mipaka yake .

Namheshimu Nyepesi na Wenzake wengi kama watanzania lakini siwezi kuheshimu na kuendelea kusikiliza watu wenye mawazo ya kuvuruga wananchi wakiwa nje ya mipaka yao huwa nashangaa kama hawana masuala mengine ya kuongea zaidi ya haya .

Hao ni chadema ndio wameshikilia Epa , Ufisadi na Usalama wa Taifa , ukirudi kwa upande wa baba zako chama cha wananchi CUF , ningekuwa mimi ni mwanachama wa CUF ningehoji kwanini hao viongozi wawili wa CUF wako pale walipo mpaka sasa hivi

Tangia upinzani umeanzishwa ni viongozi wale wale wa CUF wanaowashika masikio baadhi ya wanachama wao , ni viongozi wale wale wakorofi wako madarakani katika chama hicho mpaka sasa hivi , sijui CUF hawana viongozi wengine ni lazima wawe hawa hwaw ?

Mtihani wao wa kwanza wameshaushindwa wa kuleta maelewano huko visiwani , kwa sababu wameshashindwa jaribio hilo , sioni sababu ya kwanini wasiache nafasi hizo wazi waje watu wengine wenye utashi zaidi yao , watu wanaopenda kukaa mezani na kumaliza tofauti zao .

Niliangalia hata wakati wa maandamano ya CUF visiwani wiki iliyopita mmoja wa washairi aliposema kwamba anaweza kujilipua kama mambo yataendelea kuwa hivyo , wengine wakawaambia wenzao wasipeleka bidhaa katika kisiwa kingine wakipeleka basi wao ni halali yao .

Yote hayo yanasemwa viongozi wa CUF wamekaa katika viti wanasinzia wengine wanacheka na kufurahia kwa madaha kama vile ile ni halali yao kusema vile na hakuna chochote kile mbele yake .

Nilitegemea mmoja wa viongozi hawa au msemaji wa CUF aje mbele na kusema kile kilichosomwa na yule mshairi sio msimamo wa CUF lakini hakikutokea kitu kama hicho kwahiyo tuchukulie basi kuanzia sasa hivi na mpaka hapo viongozi wa CUF watakapoamua baadaye

Kwamba sera za CUF kuanzia sasa hivi ni KUJILIPUA , KUKATAZA BIASHARA NA UNGUJA NA KUPUNGUZA UNDUGU WAO kwa sababu hawa wengine sio wanachama wao , wao ni CCM.
 
Wewe kazi yako ya kujikombakomba kwa polisi na kufuatilia wana JF ni mbaya zaidi ya huyo mtenzi wa CUF ambaye hana uwezo wowote wa kufanya kile alichosema wakati wewe unashirikiana na polisi wanaowasakama wana JF.

Snitch mkubwa....
 
Hivi wewe shy unajipya??Au na wewe kimelea cha mafisadi??mm nawasiwasi na wewe ni kafisadi kwa maana unabeza wapinzani kuzungumzia ufisadi wewe unafikiri hapa chini vinywani mwa wananchi ni neno gani lilotawala mdomoni si UFISADI???sasa kwa nn wewe unabeza wapinzani wasizungumzie??Bila upinzani hawa jamaa ambao ni ndugu zako bila shaka wangefichuliwa hawa???wewe ulikuwa unajua baba ako MKAPA alikuwa anapiga bussiness pale whitehouse ulikuwa unajua weweee??Sasa nimejua wewe SHY ndo unataka kutuhadaa wananchi....Kama wapinzani wanazungumzia hayo nje ya nchi na wewe jenga hoja kuwatetea mafisadi mpambane na wananchi ndo watajua zipi pumba na upi mchele.
Binafsi nakuona wewe FISADI tu.
 
Mimi sio mwananchama wa CUF lakini naamini CUF sio wanafiki kama CCM walivyowanafiki, Naibu waziri kiongozi anasema neno kesho makamba ansema huo ni msimamo wake binafsi kwanini msikubali kuwa huo ni msimamo wa chama, mimi sioni tatizo kama mtu anadai haki yake hata kama hatajilipua maana kuna watu wanapata mateso wanaona bora wafe kuliko kuendelea kuishi.
 
Wakati ule wa chama kushika hatamu na zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa sisiem ulimalizika mwaka 1999.Huwezi kusema upinzani unahadaa jamii tukakubali kwa urahisi,Siku hizi kila mtu anajua mbivu na mbichi.Tunajua aliye nguo na asiye na nguo.
Amandla.............Ngawethu
 
Shy never gives up. I wanted to say something lakini mmeniwahi wote, Mwafrika wa Kike, Single D, Invisible. Thanks.
 
..........sera na mambo anayoongea katika mikutano hii ni zile zile , za ufisadi ambazo sasa hivi ni zilipendwa , yale yale ya epa na mambo mengine ambayo kwa hakika sio ya kujenga upinzani sio ya kujenga nchi ni ya kupasua hadhi ya nchi na watu wake nje ya mipaka yake.


Naona kuna watu wengi pamoja na mimi huwa hatukubaliani na maswala unayowakilisha.Leo naunga mkono ka-part...

Lakini hili jambo la upinzani kutokuwa na policy mpya kinanikera sana. Maana wao ukiangalia sana ni critic of the government of the day...hio ni wajibu wao lakini mbona hawatoi mbadala?

Uti wa mgongo wa Tanazania ni KILIMO lakini hakuna hata chama kiwe CCM au wapinzani ambao wana sera nzito ya kilimo na kuweza kutunyayua sisi wakulima into new century.
 
Nilikuwa najiuliza Lunyungu yuko wapi? Lahaula.. naona ametokea sasa..na amejitolea kuonana uso kwa macho na huyu mtoa vi-hoja.
 
Niliwahi kuona tangazo katika mtandao wakati Fulani , mmoja wa wabunge wa upinzani Tanzania ameacha namba yake ya simu atakayotumia atakapofika marekani , kwa wale ambao hawako busy wanapenda kuonana nae na vijana wengine wengi wenye muelekeo wa kipinzani .

Sitaki kubisha inaonekana wapinzani wamewashika sana vijana wa kitanzania walio nchi za nje haswa marekani kiasi kwamba zitto anapokanyaga huko wanaona mwokozi wao kafika watu wanasongamana wanataka kumwona kupiga nae picha na vitu kama hivyo .

Pamoja na kuacha hizo namba za simu na watanzania kujitokeza kuonana nae , sera na mambo anayoongea katika mikutano hii ni zile zile , za ufisadi ambazo sasa hivi ni zilipendwa , yale yale ya epa na mambo mengine ambayo kwa hakika sio ya kujenga upinzani sio ya kujenga nchi ni ya kupasua hadhi ya nchi na watu wake nje ya mipaka yake .

Namheshimu Nyepesi na Wenzake wengi kama watanzania lakini siwezi kuheshimu na kuendelea kusikiliza watu wenye mawazo ya kuvuruga wananchi wakiwa nje ya mipaka yao huwa nashangaa kama hawana masuala mengine ya kuongea zaidi ya haya .

Hao ni chadema ndio wameshikilia Epa , Ufisadi na Usalama wa Taifa , ukirudi kwa upande wa baba zako chama cha wananchi CUF , ningekuwa mimi ni mwanachama wa CUF ningehoji kwanini hao viongozi wawili wa CUF wako pale walipo mpaka sasa hivi

Tangia upinzani umeanzishwa ni viongozi wale wale wa CUF wanaowashika masikio baadhi ya wanachama wao , ni viongozi wale wale wakorofi wako madarakani katika chama hicho mpaka sasa hivi , sijui CUF hawana viongozi wengine ni lazima wawe hawa hwaw ?

Mtihani wao wa kwanza wameshaushindwa wa kuleta maelewano huko visiwani , kwa sababu wameshashindwa jaribio hilo , sioni sababu ya kwanini wasiache nafasi hizo wazi waje watu wengine wenye utashi zaidi yao , watu wanaopenda kukaa mezani na kumaliza tofauti zao .

Niliangalia hata wakati wa maandamano ya CUF visiwani wiki iliyopita mmoja wa washairi aliposema kwamba anaweza kujilipua kama mambo yataendelea kuwa hivyo , wengine wakawaambia wenzao wasipeleka bidhaa katika kisiwa kingine wakipeleka basi wao ni halali yao .

Yote hayo yanasemwa viongozi wa CUF wamekaa katika viti wanasinzia wengine wanacheka na kufurahia kwa madaha kama vile ile ni halali yao kusema vile na hakuna chochote kile mbele yake .

Nilitegemea mmoja wa viongozi hawa au msemaji wa CUF aje mbele na kusema kile kilichosomwa na yule mshairi sio msimamo wa CUF lakini hakikutokea kitu kama hicho kwahiyo tuchukulie basi kuanzia sasa hivi na mpaka hapo viongozi wa CUF watakapoamua baadaye

Kwamba sera za CUF kuanzia sasa hivi ni KUJILIPUA , KUKATAZA BIASHARA NA UNGUJA NA KUPUNGUZA UNDUGU WAO kwa sababu hawa wengine sio wanachama wao , wao ni CCM.

Nianze kwa kukupongeza ndugu yangu SHY kwa kweli umesema mabo ya kweli kabisa haiwezekeni hawa jamaa hasa CUF wamekuwa ni wafalme nafikiri toka vyama hivi vimeanzishwa viongozi ni hao hao ukiuliza unaonekana kwamba hufai maana demokirasia haiwezi kuwa kwa ccm tu hata huko CUF tunatarajia kuwe na mabadiliko au ndiyo ule usemi unaosema "CUF NI SEFU NA SEFU NI CUF" ni wa kweli ikiwa na maana kama sefu hayupo na CUF haipo
 
Ipole ukisha maliza uje na pale utueleze kwa nini wapemba wanakamatwa usiku wa manane wakiwa wamelala .Kisa ni barua pekee ama kuna kitu gani ?Chuki jamani chuki .Watu wana mtu wao wanampenda kama sisi tunavyo mpenda JK pamoja na kutofanya lolote .
 
Sidhani kama kuna umuhimu wa vyombo vya habari kutoa taarifa kuhusu watu hawa kama watu hao hao pia walishindwa kupeleka mapendekezo yao serikalini yaangaliwe ndio waanze kukurupuka , sasa wakaamua kukurupuka na kuanzisha historia nyingine katika zanzibar naamini CUF watalipia hili suala kwanjia yoyote ambayo ni halali wao kulipia

Haiwezekani watu wadogo kama hawa waendeshe watu namna hii kama vile wao ndio wamezaliwa na hivyo visiwa
 
Nianze kwa kukupongeza ndugu yangu SHY kwa kweli umesema mabo ya kweli kabisa haiwezekeni hawa jamaa hasa CUF wamekuwa ni wafalme nafikiri toka vyama hivi vimeanzishwa viongozi ni hao hao ukiuliza unaonekana kwamba hufai maana demokirasia haiwezi kuwa kwa ccm tu hata huko CUF tunatarajia kuwe na mabadiliko au ndiyo ule usemi unaosema "CUF NI SEFU NA SEFU NI CUF" ni wa kweli ikiwa na maana kama sefu hayupo na CUF haipo

AHSANTE IPOLE

WANACHAMA WA CHAMA HIKI WAMEKUWA KIMYA SANA SIJUI KWANINI HAWAJITOKEZI KUULIZA , KUHOJI AU KUDADISI CHOCHOTE KINACHOENDELEA YAANI HATA UKIANGALIA KATIKA OFFICE ZAO MAMBO NI YALE YALE HAWANA HATA MIRADI HAWANA NINI , NDIO WATU HAWA TUWAPE NCHI ? TUKAE KATIKA TV KUSIKILIZA HOTUBA ZAO HAWA AMBAO HATA MIFANO HAWANA
 
Niliwahi kuona tangazo katika mtandao wakati Fulani , mmoja wa wabunge wa upinzani Tanzania ameacha namba yake ya simu atakayotumia atakapofika marekani , kwa wale ambao hawako busy wanapenda kuonana nae na vijana wengine wengi wenye muelekeo wa kipinzani .

Sitaki kubisha inaonekana wapinzani wamewashika sana vijana wa kitanzania walio nchi za nje haswa marekani kiasi kwamba zitto anapokanyaga huko wanaona mwokozi wao kafika watu wanasongamana wanataka kumwona kupiga nae picha na vitu kama hivyo .

Pamoja na kuacha hizo namba za simu na watanzania kujitokeza kuonana nae , sera na mambo anayoongea katika mikutano hii ni zile zile , za ufisadi ambazo sasa hivi ni zilipendwa , yale yale ya epa na mambo mengine ambayo kwa hakika sio ya kujenga upinzani sio ya kujenga nchi ni ya kupasua hadhi ya nchi na watu wake nje ya mipaka yake .

Namheshimu Nyepesi na Wenzake wengi kama watanzania lakini siwezi kuheshimu na kuendelea kusikiliza watu wenye mawazo ya kuvuruga wananchi wakiwa nje ya mipaka yao huwa nashangaa kama hawana masuala mengine ya kuongea zaidi ya haya .

Hao ni chadema ndio wameshikilia Epa , Ufisadi na Usalama wa Taifa , ukirudi kwa upande wa baba zako chama cha wananchi CUF , ningekuwa mimi ni mwanachama wa CUF ningehoji kwanini hao viongozi wawili wa CUF wako pale walipo mpaka sasa hivi

Tangia upinzani umeanzishwa ni viongozi wale wale wa CUF wanaowashika masikio baadhi ya wanachama wao , ni viongozi wale wale wakorofi wako madarakani katika chama hicho mpaka sasa hivi , sijui CUF hawana viongozi wengine ni lazima wawe hawa hwaw ?

Mtihani wao wa kwanza wameshaushindwa wa kuleta maelewano huko visiwani , kwa sababu wameshashindwa jaribio hilo , sioni sababu ya kwanini wasiache nafasi hizo wazi waje watu wengine wenye utashi zaidi yao , watu wanaopenda kukaa mezani na kumaliza tofauti zao .

Niliangalia hata wakati wa maandamano ya CUF visiwani wiki iliyopita mmoja wa washairi aliposema kwamba anaweza kujilipua kama mambo yataendelea kuwa hivyo , wengine wakawaambia wenzao wasipeleka bidhaa katika kisiwa kingine wakipeleka basi wao ni halali yao .

Yote hayo yanasemwa viongozi wa CUF wamekaa katika viti wanasinzia wengine wanacheka na kufurahia kwa madaha kama vile ile ni halali yao kusema vile na hakuna chochote kile mbele yake .

Nilitegemea mmoja wa viongozi hawa au msemaji wa CUF aje mbele na kusema kile kilichosomwa na yule mshairi sio msimamo wa CUF lakini hakikutokea kitu kama hicho kwahiyo tuchukulie basi kuanzia sasa hivi na mpaka hapo viongozi wa CUF watakapoamua baadaye

Kwamba sera za CUF kuanzia sasa hivi ni KUJILIPUA , KUKATAZA BIASHARA NA UNGUJA NA KUPUNGUZA UNDUGU WAO kwa sababu hawa wengine sio wanachama wao , wao ni CCM.

Wivu unanukia hapa!
Kinachokukera wewe ninini kama hao vijana wa marekani wakimkaribisha kwa vishindo?

Kila mtu anajua cheupe na cheusi

Penginepo mambo ya UFISADI yamewaamsha macho watanzania waishio marekani.

Labda kinachokukera shy nikwamba hakuna kiongozi RAIS aliyeongoza katika kipindi kigumu kama Kikwete.
Na anajua dhahiri kwamba pamoja kwamba wanasema wapinzani hawana sera lakini sera za CCM zimebainika na wananchi hawataichagua tena.
 
Sera Zimebainika Kwamba Ni Nzuri Na Bora Zinaweza Kumkomboa Mtu Yeyote Ambaye Anaamua Kwa Nia Na Dhamira Moja Kupigania Maisha Yake Mpaka Mwisho

Yaani Watanzania Mmpaka Leo Wako Pale Wanacheza Bao Wanategemea Ccm Iwaletee Ubwabwa , Wali Na Maharage ? Katika Dunia Ya Ngapi Hiyo ? Hakuna Wa Kukuletea

Kila Mbuzi Atakula Kwa Urefu Wa Kamba Yako , Sasa Kama Kambo Yako Ni Fupi Usiseme Ccm Ndio Imechukuwa Hayo Majani Yako Ni Kwa Sababu Ya Kamba Yako Wewe Mwenyewe , Ni Wewe Mwenyewe Ujitoe Hicho Kitanzi Ukapigane
 
Mwanatanu,
Ushasoma manifesto ya CHADEMA? Hawa wana sera nzuri kuhusu kilimo na kumwezesha Mtanzania katika umiliki wa maliasili zake. Sizo hizo za CCM za kuwagawia Makaburu na Wamarekani madini yetu kwa bei ya chee. Au tumwite Mnyika hapa akupe tuisheni ya chap chap?
 
Back
Top Bottom