Upinzani waruhusiwa kukagua mitambo ya tume ya uchaguzi Kenya

Francis12

JF-Expert Member
Sep 30, 2016
7,533
22,276
Mahakama ya Juu nchini Kenya imeukubalia muungano wa upinzani nchini humo National Super Alliance (Nasa) kupekua sava zilizotumiwa na tume ya uchaguzi nchini humo wakati wa uchaguzi uliofanyika tarehe 8 Agosti.

Mahakama hiyo imesema muungano huo utaweza kusoma data kwenye sava hizo chini ya uangalizi kuhakikisha usalama wa mitambo ya IEBC hauhujumiwi.

Mgombea wa Nasa Raila Odinga amewasilisha kesi mahakamani kupinga ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee.

Mawakili wa Bw Odinga wameruhusiwa na mahakama kunakili data kutoka kwenye sava hizo kwa ajili ya kufanya uchunguzi kuhusu uchaguzi huo.

==>>Upinzani waruhusiwa kukagua mitambo ya tume ya uchaguzi Kenya - BBC Swahili
 
Huku kwenu hata kucompare tu data zenu za vituoni na zile anazotuma DED kwenda NEC ni "uchochezi":D. Kenya wametuacha mbali sana.
kwani si mawakala wote wapo na data wanakuwaga nazo.....labda useme tuu teknolojia yao ya kuwasilisha matokeo ipo juu zaidi yetu and this inaenda stage by stage haukurupuki tuu hata wao wametoka huku tulipo japo sipingani na wewe wametuacha but not to that extent
 
kwani si mawakala wote wapo na data wanakuwaga nazo.....labda useme tuu teknolojia yao ya kuwasilisha matokeo ipo juu zaidi yetu and this inaenda stage by stage haukurupuki tuu hata wao wametoka huku tulipo japo sipingani na wewe wametuacha but not to that extent

Tuace unafiki wametuacha mbali sana na katika mengi. Mahakama na mfumo wake iko huru kuliko kwetu. Katiba yao ni shirikishi kuliko yetu na zaidi tume yao iko huru zaidi kuliko yetu. Uchumi wametuzidi sana tu sisi mhata tukichanga nchi zote zilizosalia EA ndio tunawafikia. Wao wana viwanda sisi tuna Vi wonder.
 
.....kwa ukabila na ukanda !
Ukabila na ukanda hayo ni matatizo yao kama wa kenya hiyo ndo tamaduni yao...na ukabila na ukanda is not one of the criteria of democracy...yaan hatu determine democracy kwa kuangalia wanavoishi wao kama tamaduni ila transparency, gov accountability,rule of law, freedom of expression and good governance,...........hayo ya ukabila ni mambo yao ya ndani wala haya athiri hizo sifa apo juu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Demokrasia gani sasa hiyo?

Hiyo demokrasia ni not to that extent aisee mpaka wanakagua mitambo?

Sisi ndo tuna demokrasia hata zile karatasi za mawala zikipishana na RC haturuhusu kuzihoji sisi ndo wana demokrasia
 
Kenya wametuzidi sana kwenye Demokrasia na Utawala bora...Japo hili wako watu watabisha lakini hiyo ndo hali halisi. .Jamaa zetu wako vizuri sana na Mihimili yote 3 inajisimamia na inafanyakazi bila "shinikizo" lolote toka juu wala "kunipendekeza" kwa Mkulu wao..
Kwenye hili inabidi nchi nyingi za Kiafrika ziige, na hasa za Jumuiya ya Afrika Mashariki..

-Domhome-
 
haifai kuwepo !wenzetu wasomi weng sana na wameamka sasa sisi huku eti mtu msomi ni [HASHTAG]#POLEPOLE[/HASHTAG]!!!!!!!!!!!!!!!kilaza tu

wakina TL wangepatikana 500 atleast tungewaza kuwa na democrasia
lol
 
Back
Top Bottom