Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Kutoka TZS 1.5T mpaka TZS 2.4T: Hazina Imeoza, Tunataka Uchunguzi wa kina
( Forensic Audit ).
Mambo Saba (7) Katika Ripoti ya CAG Juu ya Uhakiki wa TZS 1.5 Trilioni
Utangulizi:
Ndugu wanahabari,
Februari 1, 2019 Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliwasilisha Bungeni taarifa yake ya mwaka pamoja na taarifa ya Uhakiki wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) juu ya tofauti ya Shilingi 1.5 Trilioni zisizoonekana matumizi yake katika ripoti ya CAG ya hesabu za mwaka wa fedha wa 2016/17. Naomba nimpongeze CAG kwa kazi nzuri aliyoifanya.
Nilichangia bungeni juu ya mambo kadhaa yatokanayo na ripoti hiyo ya Uhakiki wa CAG juu ya TZS1.5 Trilioni, pamoja na ripoti ya PAC iliyoletwa Bungeni. Bahati mbaya bado Serikali imeshindwa kuleta majibu juu ya maswali yaliyoulizwa na CAG pamoja nasi wabunge juu ya namna inavyotumia fedha za umma, hasa baada ya uchunguzi wa CAG juu ya sakata la TZS 1.5 Trilioni kuibua madudu zaidi.
Hivyo basi, niko hapa kuzungumza na umma wa Watanzania, kupitia nyinyi Wanahabari, ili kuwajulisha juu ya hali ya Hazina pamoja na matumizi mabaya ya Fedha zao yanayofanywa na Serikali ya CCM, kwa kueleza mambo saba (7) mabaya ya Serikali kutoka kwenye ripoti ya hiyo ya CAG juu ya 1.5 Trilioni.
Mambo Saba (7) Mabaya Katika Ripoti ya CAG Juu ya 1.5 Trilioni
1. Serikali Imetoa Taarifa Nne Tofauti Juu ya Mapato ya Ziada (Overdraft) ya Shilingi Bilioni 290
Kwa mujibu wa ripoti ya Uhakiki wa CAG juu ya matumizi ya TZS 1.5 Trilioni, Serikali ilishindwa kuthibitisha kwake juu ya namna ilivyotumia fedha hizo. Katika Utetezi wake kwa CAG Serikali ilieleza kuwa katika Shilingi 1.5 Trilioni kulikuwa OVERDRAFT ya Shilingi 290.67 Bilioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) - na hivyo fedha hizo zilitumika kwenye miradi ya Maendeleo.
Hata hivyo, Serikali kupitia Hazina haikumpa CAG vielelezo ama uthibitisho wowote juu ya hiyo Overdraft wala kuthibitisha matumizi ya fedha hizo. Aidha, CAG alipoomba vielelezo vya Overdraft husika kutoka BOT, majibu ya BOT kupitia barua ya uthibitisho(CONFIRMATION LETTER ) ni kuwa kulikuwa na Akiba Sifuri (ZERO balance) wakati hazina inafunga hesabu zao juni 2017.
Lakini taarifa za Ukaguzi wa Hesabu za BOT zinazoishia Juni, 2017 zinaonyesha kulikuwa na akiba ya OVERDRAFT ya Serikali Kuu ya shilingi 1.5 trilioni, na Serikali ilitozwa riba ya shilingi 150 bilioni. Jambo baya zaidi ni kuwa taarifa ya Overdraft ya Serikali iliyopelekwa kwa CAG ni tofauti kabisa na taarifa ya Serikali hiyo hiyo iliyoitoa Bungeni Aprili 20, 2018 kupitia Naibu Waziri wa Fedha, ambapo Serikali ilisema kwenye Shilingi 1.5 Trilioni kuna Overdraft ya Shilingi 79.1 Bilioni. Hapa Serikali imetoa taarifa nne zinazotofautiana.
2. Bilioni 976.96 Zimetumika Ikulu Bila kupitishwa na Bunge na Kuidhinishwa na CAG
Baada ya Serikali kushindwa kuonyesha zilivyotumika Shilingi 1.5 Trilioni iliamua kujilinda kwa kuitumia Ikulu kwa kuwa inajua CAG hatakagua Ikulu. Hivyo CAG alielezwa kuwa shilingi 976.96 bilioni zilihamishwa kutoka kwenye mafungu mbalimbali ya Kibajeti ya Serikali (Reallocation) na kupelekwa Fungu namba 20 (Ikulu).
Bunge halikupitisha shilingi 976.96 zitumike na Ikulu, na hata hiyo huo uhamishaji (Reallocation) haukuidhinishwa na CAG kama Sheria inavyotaka, na hata baada ya kutumia bado Serikali haikumpa CAG vielelezo wala uthibitisho wowote wa matumizi hayo.
Serikali imeshindwa kuthibitisha imetumiaje Shilingi 1.5 Trilioni, Maelezo kuwa zimetumika na Ofisi ya Rais Ikulu yametolewa kwa makusudi kwa sababu Serikali inajua kuwa CAG hakagui Ofisi ya Rais Ikulu, hivyo ni kichaka cha matumizi mabaya ya fedha za Umma. Jambo baya zaidi ni kuwa Kamati ya Bunge ya PAC ililikalia kimya jambo hili kwenye ripoti yake iliyoletwa bungeni.
3. Serikali na CCM Wamedanganya Juu ya Magazijuto ya Mapato tarajiwa (RECEIVABLES), Hati Fungani Pamoja na Fedha za Zanzibar
Aprili 20,2018 Serikali ilitoa kauli bungeni, kupitia Naibu Waziri wa Fedha juu ya shilingi 1.5 trilioni. Katika majibu hayo, Serikali ilisema kuwa shilingi 203.9 bilioni zilipelekwa Zanzibar ( transfer to Zanzibar), Mapato tarajiwa (Receivables) yalikuwa Shilingi 687 bilioni, Malipo ya Dhamana na Hati Fungani zilizoiva yalikuwa shilingi 698 bilioni, na matumizi ya ziada (Overdraft) kutoka Benki Kuu yalikuwa shilingi 79 bilioni. Serikali ilieleza kuwa changamoto za mfumo wa mahesabu wa IPSAS ACCRUAL ilisababisha kuchelewesha CAG kuona hayo mapato tarajiwa (Receivables). Maelezo kama haya pia yalitolewa na Mwenezi wa CCM wakati akifanya Magazijuto yake.
CAG amewaumbua CCM na Serikali yake kwa uongo huo, kwenye taarifa ya Uhakiki wa tofauti ya TZS 1.5 Trilioni hakuna sehemu yoyote inayosema kuhusiana na jambo la RECEIVABLES. Tukumbuke kwamba katika Mfuko Mkuu wa Hazina fedha zinazoingia ni TASLIMU tu.
Kuhusu Dhamana za Serikali na Hati Fungani, Serikali ilipotakiwa na CAG ipeleke vielelezo na uthibitisho wa shilingi 698 bilioni, ilishindwa kufanya hivyo. Imeishia kupeleka tu nyaraka ya Excel (Excel Spread Sheets) ambayo mtu yoyote anaweza kuweka namba na takwimu zozote anazotaka ili kutimiza matakwa yake. Kuonyesha kuwa Serikali haiko makini, hata kwenye hizo nyaraka za Excel ilizopeleka, bado jumla ya Malipo ya Dhamana na Hati Fungani zilizoandikwa unapata shilingi 853 bilioni na si shilingi 697 bilioni.
Njia rahisi ya uthibitisho ilikuwa ni Serikali kusema tu hizo Hati Fungani ni za lini, ziliiva lini, ni za kiasi gani na zililipwa lini ili CAG apate uthibitisho wake kutoka Benki Kuu (BOT). Lakini Serikali ilishindwa kufanya hivyo.
4. Hazina ni Ofisi Dhaifu Kiutendaji, Imetumia Nyaraka za Excel Ambazo CAG Amezishuku ( unreliable and not credible )
Ukiacha suala la takwimu za Hatifungani na dhamana za Serikali ambazo vielelezo vyake vingepaswa vitokane na taarifa ya Benki Kuu (BOT) na badala yake Serikali ilipeleka kwa CAG nyaraka za Excel, kwa ujumla CAG ameonyesha kuwa Hazina ni Ofisi dhaifu kiutendaji kwa kuwa haileti vielelezo wala uthibitisho wa kihasibu, bali hutumia tu nyaraka za Excel (Excel Spread Sheets).
Mfumo huo wa Excel haupaswi kutumika kwenye uandaaji wa taarifa za kihasibu kwa kuwa ni mfumo unaoweza kutumika na mtu yeyote yule kufuta, kuongeza au kuweka takwimu zozote zile ili kutimiza matakwa yake. Ni mfumo unaotoa urahisi kwa mtu kuiba au kufanya udanganyifu kwa urahisi tu. Ndio sababu mfumo huo CAG ameukataa na amewataka Hazina kuacha kuchakata hesabu za kihasibu kupitia Excel na kisha kupeleka kwake kama vielelezo.
5. Hazina Walitumia Fedha za Wahisani ( TZS 190bn kutoka Umoja wa Ulaya), Kinyume na Utaratibu, na Bila Idhini ya CAG
Uhakiki wa CAG juu ya shilingi 1.5 trilioni unaonyesha kuwa kuna fedha shilingi 189.9 bilioni ambazo ziliingizwa kimakosa kwenye akaunti ya Hazina (Mfuko Mkuu wa Hazina). Lakini Katiba Mkuu wa Hazina aliamua kuzitumia, na hivyo kuvunja Sheria ya Fedha ya mwaka 2001 kifungu cha 16(2c) inayomtaka kutotumia fedha yoyote inayoingia kwenye akaunti ya hazina hadi apate idhini kutoka kwa CAG, jambo ambalo Katibu wa Hazina hakufanya. Fedha hizi zilitolewa na Umoja wa Ulaya kwa ajili ya miradi mbalibali nchini. Mpaka CAG alipomaliza uhakiki wake, Hazina ilishindwa kutoa vielelezo vya matumizi ya fedha hizo. Inashangaza sana Serikali inafanya matumizi mabaya hata ya fedha za wafadhili, jambo la hatari litakaloipa shida nchi yetu.
6. CAG Ameonyesha hoja za ukaguzi zenye thamani ya TZS 2.4 Trilioni
Ripoti ya CAG ya uhakiki wa TZS 1.5 trilioni, imeonyesha kuwa fedha za umma zisizo na uthibitisho wa matumizi sio Shilingi 1.5 trilioni tena, bali ni shilingi 2.4 Trilioni. Bungeni nilihojiwa nimepata wapi kiasi hicho jambo ambalo lilimfanya Naibu Spika kufuata mchango wangu Bungeni kinyume na Kanuni baada ya kuombwa na Mnadhimu wa Wabunge wa CCM Mheshimiwa Jenista Mhagama. Naibu Spika hakunipa nafasi ya kujieleza. Nimeandika barua kwa Spika wa Bunge kulalamikia jambo hilo na nimemshtaki Naibu Spika kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge. Naomba niwaeleza Watanzania kuhusu hizo TZS 2.4T nilizipataje.
Mchanganuo wake ni kama ifuatavyo:
• TZS 290.67 bilioni ambayo ni Overdraft yenye utata.
• TZS 976.96 bilioni iliyotumika Ikulu (Reallocation) bila kupitishwa na Bunge, bila idhini ya CAG na haikukaguliwa matumizi yake.
• TZS 656.6 bilioni ambayo ilikuwatofauti (Mis-match) kati ya Fedha zilizoidhnishwa kutoka akaunti ya mapato (exchequer issue warrants) na ripoti ya fedha iliyotolewa ( exchequer release report )
• TZS 3.45 bilioni ambayo ilikuwa exchequer issues warrant ambayo ilifutwa bila sababu za msingi
• TZS 3.3 bilioni ambayo exchequer issue warrant ambayo haikuwa na vielelezo
• TZS 234.12 bilioni ni fedha ambazo hazikuingizwa kwenye exchequer account na hakukuwa na vielelezo
• TZS 189.99 bilioni hizi zilitumiwa na Katibu Mkuu Hazina bila kupata kibali cha CAG na kinyume na sharia ya Fedha
Jumla ya hoja zote hizo ni Shilingi 2.4 trilioni
7. PAC haikueleza ukweli wote kwa Umma Juu ya Hoja ya Kutoonekana kwa Shilingi 1.5 Trilioni
Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwa makusudi imeupotosha umma, kwa kutangaza kuwa CAG amesema kuwa “Hakuna Shilingi 1.5 Trilioni zilizoibiwa”. Jambo ambalo ni dhahiri kuwa SI KWELI kutokana na masuala hayo sita mabaya kwenye ripoti ya CAG. Narudia nilichosema Bungeni kuwa sio Kazi ya CAG kusema kama kuna wizi au la, isipokuwa yeye alifanya uhakiki na uhakiki huo umeonyesha maeneo ambayo nimeeleza. Hoja zote nilizoeleza Bungeni kama Mtaalamu wa Uhasibu hazikupata majibu isipokuwa viroja kutoka kwa Wabunge wa CCM. Hivyo, ninapendekeza kuwa Uchunguzi wa kina (forensic audit ) ufanyike ili kupata ukweli wa matumizi haya makubwa ya fedha za Umma zikiwemo fedha za Wafadhili. CAG ana mamlaka hayo kwa mujibu wa sheria ya Ukaguzi wa Taifa (Public Audit Act 2008). Ninaamini CAG atafanyia kazi pendekezo langu hili.
Catherine Nyakao Ruge
Mbunge, Viti Maalum Mkoa wa Mara
Februari 5, 2019
Dodoma
( Forensic Audit ).
Mambo Saba (7) Katika Ripoti ya CAG Juu ya Uhakiki wa TZS 1.5 Trilioni
Utangulizi:
Ndugu wanahabari,
Februari 1, 2019 Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliwasilisha Bungeni taarifa yake ya mwaka pamoja na taarifa ya Uhakiki wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) juu ya tofauti ya Shilingi 1.5 Trilioni zisizoonekana matumizi yake katika ripoti ya CAG ya hesabu za mwaka wa fedha wa 2016/17. Naomba nimpongeze CAG kwa kazi nzuri aliyoifanya.
Nilichangia bungeni juu ya mambo kadhaa yatokanayo na ripoti hiyo ya Uhakiki wa CAG juu ya TZS1.5 Trilioni, pamoja na ripoti ya PAC iliyoletwa Bungeni. Bahati mbaya bado Serikali imeshindwa kuleta majibu juu ya maswali yaliyoulizwa na CAG pamoja nasi wabunge juu ya namna inavyotumia fedha za umma, hasa baada ya uchunguzi wa CAG juu ya sakata la TZS 1.5 Trilioni kuibua madudu zaidi.
Hivyo basi, niko hapa kuzungumza na umma wa Watanzania, kupitia nyinyi Wanahabari, ili kuwajulisha juu ya hali ya Hazina pamoja na matumizi mabaya ya Fedha zao yanayofanywa na Serikali ya CCM, kwa kueleza mambo saba (7) mabaya ya Serikali kutoka kwenye ripoti ya hiyo ya CAG juu ya 1.5 Trilioni.
Mambo Saba (7) Mabaya Katika Ripoti ya CAG Juu ya 1.5 Trilioni
1. Serikali Imetoa Taarifa Nne Tofauti Juu ya Mapato ya Ziada (Overdraft) ya Shilingi Bilioni 290
Kwa mujibu wa ripoti ya Uhakiki wa CAG juu ya matumizi ya TZS 1.5 Trilioni, Serikali ilishindwa kuthibitisha kwake juu ya namna ilivyotumia fedha hizo. Katika Utetezi wake kwa CAG Serikali ilieleza kuwa katika Shilingi 1.5 Trilioni kulikuwa OVERDRAFT ya Shilingi 290.67 Bilioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) - na hivyo fedha hizo zilitumika kwenye miradi ya Maendeleo.
Hata hivyo, Serikali kupitia Hazina haikumpa CAG vielelezo ama uthibitisho wowote juu ya hiyo Overdraft wala kuthibitisha matumizi ya fedha hizo. Aidha, CAG alipoomba vielelezo vya Overdraft husika kutoka BOT, majibu ya BOT kupitia barua ya uthibitisho(CONFIRMATION LETTER ) ni kuwa kulikuwa na Akiba Sifuri (ZERO balance) wakati hazina inafunga hesabu zao juni 2017.
Lakini taarifa za Ukaguzi wa Hesabu za BOT zinazoishia Juni, 2017 zinaonyesha kulikuwa na akiba ya OVERDRAFT ya Serikali Kuu ya shilingi 1.5 trilioni, na Serikali ilitozwa riba ya shilingi 150 bilioni. Jambo baya zaidi ni kuwa taarifa ya Overdraft ya Serikali iliyopelekwa kwa CAG ni tofauti kabisa na taarifa ya Serikali hiyo hiyo iliyoitoa Bungeni Aprili 20, 2018 kupitia Naibu Waziri wa Fedha, ambapo Serikali ilisema kwenye Shilingi 1.5 Trilioni kuna Overdraft ya Shilingi 79.1 Bilioni. Hapa Serikali imetoa taarifa nne zinazotofautiana.
2. Bilioni 976.96 Zimetumika Ikulu Bila kupitishwa na Bunge na Kuidhinishwa na CAG
Baada ya Serikali kushindwa kuonyesha zilivyotumika Shilingi 1.5 Trilioni iliamua kujilinda kwa kuitumia Ikulu kwa kuwa inajua CAG hatakagua Ikulu. Hivyo CAG alielezwa kuwa shilingi 976.96 bilioni zilihamishwa kutoka kwenye mafungu mbalimbali ya Kibajeti ya Serikali (Reallocation) na kupelekwa Fungu namba 20 (Ikulu).
Bunge halikupitisha shilingi 976.96 zitumike na Ikulu, na hata hiyo huo uhamishaji (Reallocation) haukuidhinishwa na CAG kama Sheria inavyotaka, na hata baada ya kutumia bado Serikali haikumpa CAG vielelezo wala uthibitisho wowote wa matumizi hayo.
Serikali imeshindwa kuthibitisha imetumiaje Shilingi 1.5 Trilioni, Maelezo kuwa zimetumika na Ofisi ya Rais Ikulu yametolewa kwa makusudi kwa sababu Serikali inajua kuwa CAG hakagui Ofisi ya Rais Ikulu, hivyo ni kichaka cha matumizi mabaya ya fedha za Umma. Jambo baya zaidi ni kuwa Kamati ya Bunge ya PAC ililikalia kimya jambo hili kwenye ripoti yake iliyoletwa bungeni.
3. Serikali na CCM Wamedanganya Juu ya Magazijuto ya Mapato tarajiwa (RECEIVABLES), Hati Fungani Pamoja na Fedha za Zanzibar
Aprili 20,2018 Serikali ilitoa kauli bungeni, kupitia Naibu Waziri wa Fedha juu ya shilingi 1.5 trilioni. Katika majibu hayo, Serikali ilisema kuwa shilingi 203.9 bilioni zilipelekwa Zanzibar ( transfer to Zanzibar), Mapato tarajiwa (Receivables) yalikuwa Shilingi 687 bilioni, Malipo ya Dhamana na Hati Fungani zilizoiva yalikuwa shilingi 698 bilioni, na matumizi ya ziada (Overdraft) kutoka Benki Kuu yalikuwa shilingi 79 bilioni. Serikali ilieleza kuwa changamoto za mfumo wa mahesabu wa IPSAS ACCRUAL ilisababisha kuchelewesha CAG kuona hayo mapato tarajiwa (Receivables). Maelezo kama haya pia yalitolewa na Mwenezi wa CCM wakati akifanya Magazijuto yake.
CAG amewaumbua CCM na Serikali yake kwa uongo huo, kwenye taarifa ya Uhakiki wa tofauti ya TZS 1.5 Trilioni hakuna sehemu yoyote inayosema kuhusiana na jambo la RECEIVABLES. Tukumbuke kwamba katika Mfuko Mkuu wa Hazina fedha zinazoingia ni TASLIMU tu.
Kuhusu Dhamana za Serikali na Hati Fungani, Serikali ilipotakiwa na CAG ipeleke vielelezo na uthibitisho wa shilingi 698 bilioni, ilishindwa kufanya hivyo. Imeishia kupeleka tu nyaraka ya Excel (Excel Spread Sheets) ambayo mtu yoyote anaweza kuweka namba na takwimu zozote anazotaka ili kutimiza matakwa yake. Kuonyesha kuwa Serikali haiko makini, hata kwenye hizo nyaraka za Excel ilizopeleka, bado jumla ya Malipo ya Dhamana na Hati Fungani zilizoandikwa unapata shilingi 853 bilioni na si shilingi 697 bilioni.
Njia rahisi ya uthibitisho ilikuwa ni Serikali kusema tu hizo Hati Fungani ni za lini, ziliiva lini, ni za kiasi gani na zililipwa lini ili CAG apate uthibitisho wake kutoka Benki Kuu (BOT). Lakini Serikali ilishindwa kufanya hivyo.
4. Hazina ni Ofisi Dhaifu Kiutendaji, Imetumia Nyaraka za Excel Ambazo CAG Amezishuku ( unreliable and not credible )
Ukiacha suala la takwimu za Hatifungani na dhamana za Serikali ambazo vielelezo vyake vingepaswa vitokane na taarifa ya Benki Kuu (BOT) na badala yake Serikali ilipeleka kwa CAG nyaraka za Excel, kwa ujumla CAG ameonyesha kuwa Hazina ni Ofisi dhaifu kiutendaji kwa kuwa haileti vielelezo wala uthibitisho wa kihasibu, bali hutumia tu nyaraka za Excel (Excel Spread Sheets).
Mfumo huo wa Excel haupaswi kutumika kwenye uandaaji wa taarifa za kihasibu kwa kuwa ni mfumo unaoweza kutumika na mtu yeyote yule kufuta, kuongeza au kuweka takwimu zozote zile ili kutimiza matakwa yake. Ni mfumo unaotoa urahisi kwa mtu kuiba au kufanya udanganyifu kwa urahisi tu. Ndio sababu mfumo huo CAG ameukataa na amewataka Hazina kuacha kuchakata hesabu za kihasibu kupitia Excel na kisha kupeleka kwake kama vielelezo.
5. Hazina Walitumia Fedha za Wahisani ( TZS 190bn kutoka Umoja wa Ulaya), Kinyume na Utaratibu, na Bila Idhini ya CAG
Uhakiki wa CAG juu ya shilingi 1.5 trilioni unaonyesha kuwa kuna fedha shilingi 189.9 bilioni ambazo ziliingizwa kimakosa kwenye akaunti ya Hazina (Mfuko Mkuu wa Hazina). Lakini Katiba Mkuu wa Hazina aliamua kuzitumia, na hivyo kuvunja Sheria ya Fedha ya mwaka 2001 kifungu cha 16(2c) inayomtaka kutotumia fedha yoyote inayoingia kwenye akaunti ya hazina hadi apate idhini kutoka kwa CAG, jambo ambalo Katibu wa Hazina hakufanya. Fedha hizi zilitolewa na Umoja wa Ulaya kwa ajili ya miradi mbalibali nchini. Mpaka CAG alipomaliza uhakiki wake, Hazina ilishindwa kutoa vielelezo vya matumizi ya fedha hizo. Inashangaza sana Serikali inafanya matumizi mabaya hata ya fedha za wafadhili, jambo la hatari litakaloipa shida nchi yetu.
6. CAG Ameonyesha hoja za ukaguzi zenye thamani ya TZS 2.4 Trilioni
Ripoti ya CAG ya uhakiki wa TZS 1.5 trilioni, imeonyesha kuwa fedha za umma zisizo na uthibitisho wa matumizi sio Shilingi 1.5 trilioni tena, bali ni shilingi 2.4 Trilioni. Bungeni nilihojiwa nimepata wapi kiasi hicho jambo ambalo lilimfanya Naibu Spika kufuata mchango wangu Bungeni kinyume na Kanuni baada ya kuombwa na Mnadhimu wa Wabunge wa CCM Mheshimiwa Jenista Mhagama. Naibu Spika hakunipa nafasi ya kujieleza. Nimeandika barua kwa Spika wa Bunge kulalamikia jambo hilo na nimemshtaki Naibu Spika kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge. Naomba niwaeleza Watanzania kuhusu hizo TZS 2.4T nilizipataje.
Mchanganuo wake ni kama ifuatavyo:
• TZS 290.67 bilioni ambayo ni Overdraft yenye utata.
• TZS 976.96 bilioni iliyotumika Ikulu (Reallocation) bila kupitishwa na Bunge, bila idhini ya CAG na haikukaguliwa matumizi yake.
• TZS 656.6 bilioni ambayo ilikuwatofauti (Mis-match) kati ya Fedha zilizoidhnishwa kutoka akaunti ya mapato (exchequer issue warrants) na ripoti ya fedha iliyotolewa ( exchequer release report )
• TZS 3.45 bilioni ambayo ilikuwa exchequer issues warrant ambayo ilifutwa bila sababu za msingi
• TZS 3.3 bilioni ambayo exchequer issue warrant ambayo haikuwa na vielelezo
• TZS 234.12 bilioni ni fedha ambazo hazikuingizwa kwenye exchequer account na hakukuwa na vielelezo
• TZS 189.99 bilioni hizi zilitumiwa na Katibu Mkuu Hazina bila kupata kibali cha CAG na kinyume na sharia ya Fedha
Jumla ya hoja zote hizo ni Shilingi 2.4 trilioni
7. PAC haikueleza ukweli wote kwa Umma Juu ya Hoja ya Kutoonekana kwa Shilingi 1.5 Trilioni
Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwa makusudi imeupotosha umma, kwa kutangaza kuwa CAG amesema kuwa “Hakuna Shilingi 1.5 Trilioni zilizoibiwa”. Jambo ambalo ni dhahiri kuwa SI KWELI kutokana na masuala hayo sita mabaya kwenye ripoti ya CAG. Narudia nilichosema Bungeni kuwa sio Kazi ya CAG kusema kama kuna wizi au la, isipokuwa yeye alifanya uhakiki na uhakiki huo umeonyesha maeneo ambayo nimeeleza. Hoja zote nilizoeleza Bungeni kama Mtaalamu wa Uhasibu hazikupata majibu isipokuwa viroja kutoka kwa Wabunge wa CCM. Hivyo, ninapendekeza kuwa Uchunguzi wa kina (forensic audit ) ufanyike ili kupata ukweli wa matumizi haya makubwa ya fedha za Umma zikiwemo fedha za Wafadhili. CAG ana mamlaka hayo kwa mujibu wa sheria ya Ukaguzi wa Taifa (Public Audit Act 2008). Ninaamini CAG atafanyia kazi pendekezo langu hili.
Catherine Nyakao Ruge
Mbunge, Viti Maalum Mkoa wa Mara
Februari 5, 2019
Dodoma