Kwanza, ninawasalimu wakuu
Kwa muda mrefu nimekuwa nikitupia jicho jf. Nimejionea mengi. Nimejifunza mengi.
Wakati uchaguzi unakaribia nimeona jf ilipata wanachama wengi. lakini vilevile nimeona mada zinazowasilishwa zinalenga ushabiki zaidi wa kivyama. Tetesi pia zimeongezeka. Udini umeanza kupigiwa tarumbeta. Tunakwenda wapi?
Jambo moja lililonihuzunisha sana mimi kama M-tan-zan-ia ni kuona vyama vinavyojiita vya upinzani vinapigana vijembe, vinahujumiana, vinadharauliana. Hali hii inaonesha kuwa ukomavu wa kisiasa na ushawishi wa kisiasa bado ni mdogo katika vyama hivi. Hali hii inainufaisha CCM na inawaacha njia panda Watanzania ambao wanategemea vyama vya upinzani viwe vipaza sauti vyao, lakini pia watanzania wanategemea kuwa vyama hivi viwe mbadala siku CCM watakaposalimu amri.
Tuna vyama vikuu vya upinzani viwili CHADEMA na CUF, aidha vipo NCCR, TLP, UDP.
Baada ya uchaguzi kumalizika ni wazi CHADEMA na CUF ndivyo vyama vikuu vinavyoonekana kuwa ni changamoto kwa CCM.Lakini inaonekana kuanzia viongozi wa vyama hivi, wanachama wao na wapenzi wao wameingia katika malumbano ambayo kwa kifupi tunaweza kuyafupisha na kuyaita "VITA VYA PANZI".
Sote tunaelewa kuwa kuendelea na vita hii ni kuwa tunawatowa mhanga Watanzania wanaotaka mageuzi ya kweli na "KUNGURU" anachekelea hili. Ni kuwa CCM wataendelea kutawala kwa miongo kadha.
Tusitegemee kuwa hata kama CHADEMA na CUF watashirikiana kuwa hakutakuwa na tofauti lakini viongozi wa vyama hivi wanaweza kuwa na "common tone" na hapo ndiyo itaonekana kuwa wapo hapo kuwakilisha watanzania na siyo matakwa yao kichama au binafsi.
Tanzania ni kubwa kuliko chama chochote na kuidondosha CCM kuunda serikali Tanzania kunataka kazi. Kazi kweli kweli.
Kwanza bila ya Katiba Mpya itakayoshirikisha wigo mkubwa, umma wa watanzania katika kuiandika basi upinzani usahau kuingia madarakani kwa amani.Watanzania tusisahau jina kamili la CCM. MAPINDUZI ndio msisitizo. Katiba mpya najuwa ni agenda ambayo CHADEMA na CUF wanakubaliana.
CHADEMA na CUF wana sera ya Serikali Tatu.
Kuna sababu gani ya msingi inayowafanya wasikae pamoja kushirikiana katika kusukuma mbele agenda hizi? Katiba mpya ndani ya miaka miwili, tume huru za uchaguzi, Serikali tatu kwa Tanzania.
UMOJA ni NGUVU na Utengano ni udhaifu.
Kama ni milioni 200 au 100 za kuongoza upinzani, mnashindwa kuona mbali. mkiingia madarakani kuna mabilioni.
Kama tatizo ni kuwa CUF wamefanya muafaka na CCM basi CHADEMA hasa viongozi walipaswa kukaa na wenzao wa CUF kuwadadisi, kujifunza na kubadilishana nao mawazo kuona vipi wamefikia kushirikiana na CCM katika kuunda Serikali kule Zanzibar. Nani hajuwi kuwa Zanzibar kwa miongo kadhaa imekuwa na hali tete? Nani hajuwi kuwa CCM wanaposhindwa katika uchaguzi kupitia kisanduku cha kura huwa wana-back up plan?
Hekima, uwazi, kuaminiana na kuheshimiana kwa viongozi wa vyama vya upinzani inaonekana viko katika kiwango cha chini. Mnaweza kupingana bila ya kupigana. Pinganisheni hoja, changianeni mawazo kuona vipi mtawaletea watanzania afueni ya maisha...sizungumzii "maisha bora au maendeleo". Hayo yatawezekana tu pale Serikali Zetu Tatu zitakaposimikwa/ zitakapoundwa kupitia katiba mpya, tume huru za uchaguzi, nakuwepo mfumo mzuri wa mgawanyo wa madaraka wa mihimili ya dola.
Otherwise, Itakuwa ni kuganga njaa tu.
CHADEMA na CUF hamna haja ya kutoleana aibu zenu, kejeli au name calling kwenye viriri au vyombo vya habari. Watanzania hawatunufaika kwa hili isipokuwa wapenda mipasho na kuongeza furaha ya "KUNGURU". Kaeni chini, mjadiliane..mtakapotoka kwenye vikao vyenu muje na kauli za matumaini kwa Watanzania siyo kuendeleza kuwakatisha watu tamaa ya maisha. Kwa hilo CCM hawataki wala hawahitaji msaidizi. Si tumeona ndege ya uchumi inapaa na maisha bora kwa kila Mdanganyika? Wenyewe wanajuwa Watanzania ni kama kichwa cha mwendawazimu.Wanatubadilishia wimbo (kauli mbiu(, sisi tunaendelea kutimkwa!!! Tunacheza mdundiko!! Wao wanachana life!!!
Let us bring change!
Nawasilisha wakuu.
Kwa muda mrefu nimekuwa nikitupia jicho jf. Nimejionea mengi. Nimejifunza mengi.
Wakati uchaguzi unakaribia nimeona jf ilipata wanachama wengi. lakini vilevile nimeona mada zinazowasilishwa zinalenga ushabiki zaidi wa kivyama. Tetesi pia zimeongezeka. Udini umeanza kupigiwa tarumbeta. Tunakwenda wapi?
Jambo moja lililonihuzunisha sana mimi kama M-tan-zan-ia ni kuona vyama vinavyojiita vya upinzani vinapigana vijembe, vinahujumiana, vinadharauliana. Hali hii inaonesha kuwa ukomavu wa kisiasa na ushawishi wa kisiasa bado ni mdogo katika vyama hivi. Hali hii inainufaisha CCM na inawaacha njia panda Watanzania ambao wanategemea vyama vya upinzani viwe vipaza sauti vyao, lakini pia watanzania wanategemea kuwa vyama hivi viwe mbadala siku CCM watakaposalimu amri.
Tuna vyama vikuu vya upinzani viwili CHADEMA na CUF, aidha vipo NCCR, TLP, UDP.
Baada ya uchaguzi kumalizika ni wazi CHADEMA na CUF ndivyo vyama vikuu vinavyoonekana kuwa ni changamoto kwa CCM.Lakini inaonekana kuanzia viongozi wa vyama hivi, wanachama wao na wapenzi wao wameingia katika malumbano ambayo kwa kifupi tunaweza kuyafupisha na kuyaita "VITA VYA PANZI".
Sote tunaelewa kuwa kuendelea na vita hii ni kuwa tunawatowa mhanga Watanzania wanaotaka mageuzi ya kweli na "KUNGURU" anachekelea hili. Ni kuwa CCM wataendelea kutawala kwa miongo kadha.
Tusitegemee kuwa hata kama CHADEMA na CUF watashirikiana kuwa hakutakuwa na tofauti lakini viongozi wa vyama hivi wanaweza kuwa na "common tone" na hapo ndiyo itaonekana kuwa wapo hapo kuwakilisha watanzania na siyo matakwa yao kichama au binafsi.
Tanzania ni kubwa kuliko chama chochote na kuidondosha CCM kuunda serikali Tanzania kunataka kazi. Kazi kweli kweli.
Kwanza bila ya Katiba Mpya itakayoshirikisha wigo mkubwa, umma wa watanzania katika kuiandika basi upinzani usahau kuingia madarakani kwa amani.Watanzania tusisahau jina kamili la CCM. MAPINDUZI ndio msisitizo. Katiba mpya najuwa ni agenda ambayo CHADEMA na CUF wanakubaliana.
CHADEMA na CUF wana sera ya Serikali Tatu.
Kuna sababu gani ya msingi inayowafanya wasikae pamoja kushirikiana katika kusukuma mbele agenda hizi? Katiba mpya ndani ya miaka miwili, tume huru za uchaguzi, Serikali tatu kwa Tanzania.
UMOJA ni NGUVU na Utengano ni udhaifu.
Kama ni milioni 200 au 100 za kuongoza upinzani, mnashindwa kuona mbali. mkiingia madarakani kuna mabilioni.
Kama tatizo ni kuwa CUF wamefanya muafaka na CCM basi CHADEMA hasa viongozi walipaswa kukaa na wenzao wa CUF kuwadadisi, kujifunza na kubadilishana nao mawazo kuona vipi wamefikia kushirikiana na CCM katika kuunda Serikali kule Zanzibar. Nani hajuwi kuwa Zanzibar kwa miongo kadhaa imekuwa na hali tete? Nani hajuwi kuwa CCM wanaposhindwa katika uchaguzi kupitia kisanduku cha kura huwa wana-back up plan?
Hekima, uwazi, kuaminiana na kuheshimiana kwa viongozi wa vyama vya upinzani inaonekana viko katika kiwango cha chini. Mnaweza kupingana bila ya kupigana. Pinganisheni hoja, changianeni mawazo kuona vipi mtawaletea watanzania afueni ya maisha...sizungumzii "maisha bora au maendeleo". Hayo yatawezekana tu pale Serikali Zetu Tatu zitakaposimikwa/ zitakapoundwa kupitia katiba mpya, tume huru za uchaguzi, nakuwepo mfumo mzuri wa mgawanyo wa madaraka wa mihimili ya dola.
Otherwise, Itakuwa ni kuganga njaa tu.
CHADEMA na CUF hamna haja ya kutoleana aibu zenu, kejeli au name calling kwenye viriri au vyombo vya habari. Watanzania hawatunufaika kwa hili isipokuwa wapenda mipasho na kuongeza furaha ya "KUNGURU". Kaeni chini, mjadiliane..mtakapotoka kwenye vikao vyenu muje na kauli za matumaini kwa Watanzania siyo kuendeleza kuwakatisha watu tamaa ya maisha. Kwa hilo CCM hawataki wala hawahitaji msaidizi. Si tumeona ndege ya uchumi inapaa na maisha bora kwa kila Mdanganyika? Wenyewe wanajuwa Watanzania ni kama kichwa cha mwendawazimu.Wanatubadilishia wimbo (kauli mbiu(, sisi tunaendelea kutimkwa!!! Tunacheza mdundiko!! Wao wanachana life!!!
Let us bring change!
Nawasilisha wakuu.