Upinzani umeufyata, wamachinga bado kujitambua lakini silaha hii KAMWE hawatakwepa!

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Upinzani ni aibu tupu kwa kusalimu amri kwa dola na kufumbia macho katiba kusiginwa hususani haki za kidemokrasia na uhuru wa kutoa maoni. Udhaifu wao ni ufisadi wao. Ni wanafiki wakubwa hawana chembe ya tofauti na mahasimu wao....

Waathirika wakubwa wa kusiginwa hizi haki za kiutu kabisa ni machinga lakini bado wako usingizini kudai stahiki zao: Hawajui nguvu waliyonayo!

Lakini, msikate tamaa kwani Mwenyezi Mungu yu hai. Hatakubali KAMWE adhihakiwe na maovu.

Watawala na wapiga fimbili za Hemelini kawatupia laana ya ulafi hawali wakashiba. Huvimbiwa lakini njaa na kiu inawachachamalia hadi aidha watubu na kufanya malipizi au waangamizwe kwa laana ya ulafi.

Ulafi wao lazima uwatokee puani kwani wanakula hata visivyoliwa!

Matokeo yake hadi tufike 2020, wengi hawatafurukuta. Aidha watakuwa wanauguza majeraha ya "viherere vyao" au watakuwa wametulizwa tuli kwenye makaburi yao.

UKIMWI ndiyo dili hivi sasa. Wataibatiza kisukari kubwa, au maini au figo au saratani lakini mzee huyu wa masharubu mwenyewe ni "HAPA KAZI TU." hamwachi mlafi salama bila kumpiga ngwala.

Jina la Bwana lihidimiwe milele!

Amina.
 
Upinzani ni aibu tupu kwa kusalimu amri kwa dola na kufumbia macho katiba kusiginwa hususani haki za kidemokrasia na uhuru wa kutoa maoni. Udhaifu wao ni ufisadi wao. Ni wanafiki wakubwa hawana chembe ya tofauti na mahasimu wao....

lakini mzee huyu wa masharubu mwenyewe ni "HAPA KAZI TU." hamwachi mlafi salama bila kumpiga ngwala.
Sijakuelewa hapo..????????
 
Upinzani ni aibu tupu kwa kusalimu amri kwa dola na kufumbia macho katiba kusiginwa hususani haki za kidemokrasia na uhuru wa kutoa maoni. Udhaifu wao ni ufisadi wao. Ni wanafiki wakubwa hawana chembe ya tofauti na mahasimu wao....

Waathirika wakubwa wa kusiginwa hizi haki za kiutu kabisa ni machinga lakini bado wako usingizini kudai stahiki zao: Hawajui nguvu waliyonayo!

Lakini, msikate tamaa kwani Mwenyezi Mungu yu hai. Hatakubali KAMWE adhihakiwe na maovu.

Watawala na wapiga fimbili za Hemelini kawatupia laana ya ulafi hawali wakashiba. Huvimbiwa lakini njaa na kiu inawachachamalia hadi aidha watubu na kufanya malipizi au waangamizwe kwa laana ya ulafi.

Ulafi wao lazima uwatokee puani kwani wanakula hata visivyoliwa!

Matokeo yake hadi tufike 2020, wengi hawatafurukuta. Aidha watakuwa wanauguza majeraha ya "viherere vyao" au watakuwa wametulizwa tuli kwenye makaburi yao.

UKIMWI ndiyo dili hivi sasa. Wataibatiza kisukari kubwa, au maini au figo au saratani lakini mzee huyu wa masharubu mwenyewe ni "HAPA KAZI TU." hamwachi mlafi salama bila kumpiga ngwala.

Jina la Bwana lihidimiwe milele!

Amina.
Kina Shaka/Sadifa & Co LTD ndiyo nyie
 
Upinzani ni aibu tupu kwa kusalimu amri kwa dola na kufumbia macho katiba kusiginwa hususani haki za kidemokrasia na uhuru wa kutoa maoni. Udhaifu wao ni ufisadi wao. Ni wanafiki wakubwa hawana chembe ya tofauti na mahasimu wao....

Waathirika wakubwa wa kusiginwa hizi haki za kiutu kabisa ni machinga lakini bado wako usingizini kudai stahiki zao: Hawajui nguvu waliyonayo!

Lakini, msikate tamaa kwani Mwenyezi Mungu yu hai. Hatakubali KAMWE adhihakiwe na maovu.

Watawala na wapiga fimbili za Hemelini kawatupia laana ya ulafi hawali wakashiba. Huvimbiwa lakini njaa na kiu inawachachamalia hadi aidha watubu na kufanya malipizi au waangamizwe kwa laana ya ulafi.

Ulafi wao lazima uwatokee puani kwani wanakula hata visivyoliwa!

Matokeo yake hadi tufike 2020, wengi hawatafurukuta. Aidha watakuwa wanauguza majeraha ya "viherere vyao" au watakuwa wametulizwa tuli kwenye makaburi yao.

UKIMWI ndiyo dili hivi sasa. Wataibatiza kisukari kubwa, au maini au figo au saratani lakini mzee huyu wa masharubu mwenyewe ni "HAPA KAZI TU." hamwachi mlafi salama bila kumpiga ngwala.

Jina la Bwana lihidimiwe milele!

Amina.


Na bado, dadadeki!
 
Kuna watu mtaabika sana kutetea upinzani huu mbovu na wa kilaghai
 
Upinzani ni aibu tupu kwa kusalimu amri kwa dola na kufumbia macho katiba kusiginwa hususani haki za kidemokrasia na uhuru wa kutoa maoni. Udhaifu wao ni ufisadi wao. Ni wanafiki wakubwa hawana chembe ya tofauti na mahasimu wao....

Waathirika wakubwa wa kusiginwa hizi haki za kiutu kabisa ni machinga lakini bado wako usingizini kudai stahiki zao: Hawajui nguvu waliyonayo!

Lakini, msikate tamaa kwani Mwenyezi Mungu yu hai. Hatakubali KAMWE adhihakiwe na maovu.

Watawala na wapiga fimbili za Hemelini kawatupia laana ya ulafi hawali wakashiba. Huvimbiwa lakini njaa na kiu inawachachamalia hadi aidha watubu na kufanya malipizi au waangamizwe kwa laana ya ulafi.

Ulafi wao lazima uwatokee puani kwani wanakula hata visivyoliwa!

Matokeo yake hadi tufike 2020, wengi hawatafurukuta. Aidha watakuwa wanauguza majeraha ya "viherere vyao" au watakuwa wametulizwa tuli kwenye makaburi yao.

UKIMWI ndiyo dili hivi sasa. Wataibatiza kisukari kubwa, au maini au figo au saratani lakini mzee huyu wa masharubu mwenyewe ni "HAPA KAZI TU." hamwachi mlafi salama bila kumpiga ngwala.

Jina la Bwana lihidimiwe milele!

Amina.
Inanishangaza kufikiri wanaoathirika na kuvunjwa huku kwa haki za binadamu na kuminywa uhuru ni tatizo la so called wapinzani! Je wewe kama mwananchi wa kawaida ambaye hauna chama chochote au huko katika chama ikiwemo na chama tawala, je unafaidika na hali hiyo ya uvunjifu na ukiukwaji wa sheria na haki zako? Kama siyo ni kwa nini basi uwalaumu hao wapinzani badala ya kuchukua hatua...au ndiyo mwendelezo wa unafiki?
 
Inanishangaza kufikiri wanaoathirika na kuvunjwa huku kwa haki za binadamu na kuminywa uhuru ni tatizo la so called wapinzani! Je wewe kama mwananchi wa kawaida ambaye hauna chama chochote au huko katika chama ikiwemo na chama tawala, je unafaidika na hali hiyo ya uvunjigu na ukiukwaji wa sheria na haki zako? Kama siyo ni kwa nini basi uwalaumu hso wapinzani badala ya kuchukua hatua...au ndiyo mwendelezo wa unafiki?
Unapoamua kuchukua jembe ulimwe hupaswi kugeuka jiwe
 
Wapaswa kubuni mbinu mpya

Mkuu mleta uzi, naona umeongea maneno ya mafumbo mafumbo kiasi wengi hawajakulewa, naona mpaka sasa uzi wako hausogei kwaajili ya huo mkanganyiko ulioleta. Sasa ili tukuelewe vizuri, hebu toa ushauri ni kipi wapinzani wanapaswa kufanya kwenye hizo mbinu mpya. Maana sasa kila mtu anasema wapinzani wabadili mbinu mara sijui mbinu mpya, lakini ukiuliza ni mbinu gani watumie wanakaa kimya. Hebu wewe tegua kitendawili, nakupa mji wa Chato.
 
Hahahaha baada ya Kuwapitisha Mtulia na Molel naona mmekuja na hoja mfu
 
Upinzani ni aibu tupu kwa kusalimu amri kwa dola na kufumbia macho katiba kusiginwa hususani haki za kidemokrasia na uhuru wa kutoa maoni. Udhaifu wao ni ufisadi wao. Ni wanafiki wakubwa hawana chembe ya tofauti na mahasimu wao....

Waathirika wakubwa wa kusiginwa hizi haki za kiutu kabisa ni machinga lakini bado wako usingizini kudai stahiki zao: Hawajui nguvu waliyonayo!

Lakini, msikate tamaa kwani Mwenyezi Mungu yu hai. Hatakubali KAMWE adhihakiwe na maovu.

Watawala na wapiga fimbili za Hemelini kawatupia laana ya ulafi hawali wakashiba. Huvimbiwa lakini njaa na kiu inawachachamalia hadi aidha watubu na kufanya malipizi au waangamizwe kwa laana ya ulafi.

Ulafi wao lazima uwatokee puani kwani wanakula hata visivyoliwa!

Matokeo yake hadi tufike 2020, wengi hawatafurukuta. Aidha watakuwa wanauguza majeraha ya "viherere vyao" au watakuwa wametulizwa tuli kwenye makaburi yao.

UKIMWI ndiyo dili hivi sasa. Wataibatiza kisukari kubwa, au maini au figo au saratani lakini mzee huyu wa masharubu mwenyewe ni "HAPA KAZI TU." hamwachi mlafi salama bila kumpiga ngwala.

Jina la Bwana lihidimiwe milele!

Amina.
Ukombozi wa nchi hii ni mimi, wewe na yule kama wajibu wetu wala siyo vyama vya siasa pekee vinavyoweza kuleta usawa kwa jamii

Tunapokubali kutawaliwa kwa mabavu kifkra na watawala eti sababu wapo viongozi wa kisiasa watatutetea huku wewe umelala usingizi wa pono ni kujidanganya tu na tutabaki hivi hivi kulalamika kila siku.

Vuguvugu la ukombozi wa fikra haliwezi kubebwa na wana siasa pekee huku sisi tumejificha kusikojilikana huku tukitegemea kuvuna matunda kibwerere bwere tu kwa kuhangaika wengine hatutoweza kujikomboa kamwe.

Tunapaswa tupaze sauti zetu kwa makundi yote ya kijamii kuanzia viongozi wa dini, viongozi wa asasi za kiraia, viongozi wa kisiasa na kila mwanaharakati wa kupigania haki za kiraia na hapo ndipo tutafanikiwa kukomboka kutoka kwenye mikono ya hawa waliojivika ukoloni mweusi.

Yaani wewe upo kivulini unataka kuona wengine wakimwagwa damu zao, kupoteza maisha, kubaki virema na yatima kwa ajili yako uje uvune matunda bila jasho?!
 
Back
Top Bottom