Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,398
- Thread starter
- #61
Mimi kabla ya 2015 nilikuwa mpinzani khasa tena wa aina ya Dr Slaa.Contents za uzi zinahusu uchaguzi mkuu wa 2020.
Na hapa ndio ulitakiwa uweke hizo mbinu mbadala acha ngonjera za 2006.
Tuliongoea sana humu na tukawa twamponda weee JK wa watu.
Chadema ilitakiwa kimyakimya inaanda majimbo hivyo kwanza kutafuta watu ambao watakuwa wagombea wao wa maana wa ubunge.
Pili, wabunge wa Chadema walipaswa kushiriki shughuli za maendeleo na sio kwenda majimboni wakati wa kampeni kama alivyofanya bwana Mbowe na alichokutana nacho nafikiri ulikisikia.
Hivyo ni kama nnavyosisitiza, kuwa kimkakati zaidi yaani strategic na kuwa objective.
Ukifanya hivyo hata siku ukiomba mdahalo utaonena unafaa kufanya mdahalo.
Ukiwa mshari sahau kila kitu.
Siasa ni sayansi.
Ndo maana CCM walikuwa wakiwaangalia mlipokuwa mkijimwambafwai majukwani na ukimsikiliza Polepole utaona namna anavyojibu hoja kisayansi na wananchi wanasikiliza na kuelewa.
Hata Bashiru nae taratibu akawaita mabalozi kuwaambia ukweli kwamba watulie na wakamwelewa.
Watanzania si wajinga ila hawapendi shari na vurugu.
Hata ile siku mabomu yalipolipuka kule Mtoni nilishuhudia jinsi watiu walivyoacha majumbani vitoto vichanga na vibibi kizee na kukimbilia kusikojulikana.
Ilikuwa ni baada ya utulivu ndipo watu walianza kuchungulia na kujitokeza uwanja wa Taifa kutafuta ndugu zao.
Narudia, siasa ni sayansi.