Mzalendo Uchwara
JF-Expert Member
- Jan 26, 2020
- 3,712
- 11,687
Benard Membe ameweka wazi kuwa ikiwa vyama vya upinzani vitaungana na kumkubalia agombee ,basi yuko tayari kupeperusha bendera.
Hili litakua kosa kubwa, usaliti wa hali ya juu na dhambi isiyo sameheka kwa sababu zifuatazo.
1. Kama ilivyokuwa kwa Lowasa, Benard Membe atakua amejiunga na upinzani kwa maslahi yake binafsi. Sio kwamba anakubaliana na sera na falsafa za vyama vya upinzani, na wala sio kwamba anavipenda na kuvitakia mema vyama vya upinzani, hapana! Anataka kwenda huko ili tu atimize ndoto yake ya kugombea urais. Angependa zaidi kuitimiza akiwa kwenye chama anachokipenda cha CCM, lakini huko wamemtimua.
2. Kutenda kosa sio kosa bali kurudia kosa ni kosa kubwa, vyama vya upinzani vikiongozwa na CHADEMA vilifanya kosa la namna hii mwaka 2015, litakua jambo la ajabu kama watakua hawajifunza kutokana na maamuzi yale ya hovyo na yanayo kigharimu chama hadi leo hii.
3. Ni usaliti mkubwa kwa wafia chama na wananchi. Jaribu kufikiri mtu kama Tundu Lissu na wengine, wamekipigania chama usiku na mchana kwa jasho na damu, wengine wameuawa, wengine wamepata ulemavu wa kudumu na wengine wamepoteza mali zao, alafu leo hii unapowadia wakati muhimu kama huu, chama kinawaacha hawa wote na kuamua kumpa nafasi 'outsider' ili atimize ndoto zake binafsi! Ni usaliti usio sameheka. Dr. Slaa hawezi kuwasamehe CDM kwa kile walichokifanya 2015, na iwapo watakirudia tena basi kundi kubwa zaidi litajitenga nao na kuunga mkono juhudi, kuwanini ujitese wakati unao wahangaikia hawauoni umuhimu wako?
4. CCM wanaweza kuwa wanapanga hizi drama za Membe na chama chake, kama anavyojitapa yeye mwenyewe kuwa alikua mtumishi kwenye ile idara nyeti, basi tukae tukijua uzandiki na hujuma ni sehemu tu ya umahiri wake. Chama chake pendwa kinaweza kuwa kinamtumia kwa wakati huu ili kuuweka uchaguzi mkuu 'under control', akigombea mtu wao kama Membe hata akishindwa basi wana uhakika wa kumpa maelekezo awatulize wafuasi wake kuwa mambo yanashughulikiwa kwenye vyombo vya kisheria.
Lakini akigombea mtu radical wa upinzani, wanahofu kuwa anaweza kukataa matokeo na kuhamasisha wananchi wayakatae matokea kwa nguvu zote. Mwisho wa siku nchi inaweza kutumbukia kwenye sintofahamu itakayo hatarisha utawala wa CCM (au usalama wa taifa kwa mujibu wa viongozi wa CCM).
Hili litakua kosa kubwa, usaliti wa hali ya juu na dhambi isiyo sameheka kwa sababu zifuatazo.
1. Kama ilivyokuwa kwa Lowasa, Benard Membe atakua amejiunga na upinzani kwa maslahi yake binafsi. Sio kwamba anakubaliana na sera na falsafa za vyama vya upinzani, na wala sio kwamba anavipenda na kuvitakia mema vyama vya upinzani, hapana! Anataka kwenda huko ili tu atimize ndoto yake ya kugombea urais. Angependa zaidi kuitimiza akiwa kwenye chama anachokipenda cha CCM, lakini huko wamemtimua.
2. Kutenda kosa sio kosa bali kurudia kosa ni kosa kubwa, vyama vya upinzani vikiongozwa na CHADEMA vilifanya kosa la namna hii mwaka 2015, litakua jambo la ajabu kama watakua hawajifunza kutokana na maamuzi yale ya hovyo na yanayo kigharimu chama hadi leo hii.
3. Ni usaliti mkubwa kwa wafia chama na wananchi. Jaribu kufikiri mtu kama Tundu Lissu na wengine, wamekipigania chama usiku na mchana kwa jasho na damu, wengine wameuawa, wengine wamepata ulemavu wa kudumu na wengine wamepoteza mali zao, alafu leo hii unapowadia wakati muhimu kama huu, chama kinawaacha hawa wote na kuamua kumpa nafasi 'outsider' ili atimize ndoto zake binafsi! Ni usaliti usio sameheka. Dr. Slaa hawezi kuwasamehe CDM kwa kile walichokifanya 2015, na iwapo watakirudia tena basi kundi kubwa zaidi litajitenga nao na kuunga mkono juhudi, kuwanini ujitese wakati unao wahangaikia hawauoni umuhimu wako?
4. CCM wanaweza kuwa wanapanga hizi drama za Membe na chama chake, kama anavyojitapa yeye mwenyewe kuwa alikua mtumishi kwenye ile idara nyeti, basi tukae tukijua uzandiki na hujuma ni sehemu tu ya umahiri wake. Chama chake pendwa kinaweza kuwa kinamtumia kwa wakati huu ili kuuweka uchaguzi mkuu 'under control', akigombea mtu wao kama Membe hata akishindwa basi wana uhakika wa kumpa maelekezo awatulize wafuasi wake kuwa mambo yanashughulikiwa kwenye vyombo vya kisheria.
Lakini akigombea mtu radical wa upinzani, wanahofu kuwa anaweza kukataa matokeo na kuhamasisha wananchi wayakatae matokea kwa nguvu zote. Mwisho wa siku nchi inaweza kutumbukia kwenye sintofahamu itakayo hatarisha utawala wa CCM (au usalama wa taifa kwa mujibu wa viongozi wa CCM).