BABA NI CCM
Member
- Nov 24, 2018
- 86
- 98
Kidumu Chama Cha Mapinduzi
Leo niwape msaada ndugu zangu wa vyama vya upinzani. Ndiyo niwape msaada kwani CCM tunaamini bila hivi vyama vya upinzani hatutakuwa na sababu ya kuwa na vyama vingi. Naam kwa maana nyingine ni kuwa tunaviitaji hivi vyama.
Licha ya serikali kufanya jitihada nyingi kukuza demokrasia nchini vipo vyama na watu mmoja mmoja ambao wanafanya kila juhudi kukwamisha jambo hili. Wapo wanaovunja kwa maksudi sheria za nchi, taratibu na miongozo.
Muda wa siasa za majukwaa ulikwisha malizika, lakini kwa makusudi tunawaona ndugu zetu kutoka baadhi ya vyama vya upinzani wakitoa hoja kinzani kama vile hoja ya kuminywa demokrasia eti kisa tu muda wa kampeni za majukwaa umeisha, hivi mlitaka tukimbizane majukwaani miaka tano? ni lini tutafanya kazi kama kila uchwao tupo majukwaani hilo hapa Tanzania HAPANA.
Upinzani jijengeni hawa chadema wanajifia kwa kasi sasa wanatafuta wakufa nao. Cuf, Act wazalendo, Nld, Nccr mageuzi na vyama vingine jitathimini vyema msije kuwa misukule wasindikizaji. Epusheni viongozi wenu na mikwaruzo ya kisheria, epusheni wanachama wenu na utovu wa sheria, jiepusheni na maandamano na kuunga mkono hoja zenye lengo la kuikwamisha serikali. Hakika mtakuwa mmejijienga na mtakuwa. Msisite kukosoa ila msiache kushauri na mpuuze kupotosha.
Hayo ni yangu machache kwenu
#TwendeMaktabaTukasome
Wasalimu Lumumba
Ni mimi Mtoto wa Baba.
Leo niwape msaada ndugu zangu wa vyama vya upinzani. Ndiyo niwape msaada kwani CCM tunaamini bila hivi vyama vya upinzani hatutakuwa na sababu ya kuwa na vyama vingi. Naam kwa maana nyingine ni kuwa tunaviitaji hivi vyama.
Licha ya serikali kufanya jitihada nyingi kukuza demokrasia nchini vipo vyama na watu mmoja mmoja ambao wanafanya kila juhudi kukwamisha jambo hili. Wapo wanaovunja kwa maksudi sheria za nchi, taratibu na miongozo.
Muda wa siasa za majukwaa ulikwisha malizika, lakini kwa makusudi tunawaona ndugu zetu kutoka baadhi ya vyama vya upinzani wakitoa hoja kinzani kama vile hoja ya kuminywa demokrasia eti kisa tu muda wa kampeni za majukwaa umeisha, hivi mlitaka tukimbizane majukwaani miaka tano? ni lini tutafanya kazi kama kila uchwao tupo majukwaani hilo hapa Tanzania HAPANA.
Upinzani jijengeni hawa chadema wanajifia kwa kasi sasa wanatafuta wakufa nao. Cuf, Act wazalendo, Nld, Nccr mageuzi na vyama vingine jitathimini vyema msije kuwa misukule wasindikizaji. Epusheni viongozi wenu na mikwaruzo ya kisheria, epusheni wanachama wenu na utovu wa sheria, jiepusheni na maandamano na kuunga mkono hoja zenye lengo la kuikwamisha serikali. Hakika mtakuwa mmejijienga na mtakuwa. Msisite kukosoa ila msiache kushauri na mpuuze kupotosha.
Hayo ni yangu machache kwenu
#TwendeMaktabaTukasome
Wasalimu Lumumba
Ni mimi Mtoto wa Baba.