Upinzani Ivory Coast wakataa mabadiliko ya Tume ya Uchaguzi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,007
9,873
Ivory Coast


Wafuasi wa upinzani wamekuwa wakipinga hatua ya rais ya kugombea kwa mara ya tatu. Upinzani huko Ivory Coast umekataa mpango wa serikali wa kufanya mabadiliko katika tume ya uchaguzi kabla ya uchaguzi utakaofanyika wiki ijayo na kusisitiza kwamba utasusia uchaguzi huo.

Rais Alassane Ouattara anatafuta kuchaguliwa katika muhula wa tatu hatua iliyozua utata. Kugombea kwake kumesababisha maandamano kote nchini humo.

Umoja wa Mataifa umeonesha wasiwasi wake kuhusu ghasia zinazoendelea ambazo zimesababisha vifo vya watu karibu saba huku zaidi ya 40 wakijeruhiwa, kwa mujibu wa serikali.

"Wagombea wa upinzani wanasisitiza kuwa wataendelea kuasi dhidi ya utekelezaji wa sheria na kusema wanataka taasisi za kimataifa kuingilia kati," Maurice Kakou Guikahue, msemaji wa upinzani, alizungumza na wanahabari Alhamisi.

Wagombea wawili wa upinzani – aliyekuwa rais, Henri Konan Bédié, na aliyekuwa waziri mkuu, Pascal Affi N'Guessan – walitangaza kususia uchaguzi mapema mwezi huu.
 
Huyu aliingia madarakani kwa mtutu wa bunduki nadhani njia hiyo hiyo itumike kumtoa madarakani.
 
Afrika ina laana mbaya sana, huyu Ouattara aliingia madarakani baada ya aliyekuwa rais Bw. Gbagbo kuiba kura na kufurumishwa kutoka ikulu kwa msaada wa majeshi ya Ufaransa.

Leo jinamizi la kiafrika tayari limeshamng'anga'ania naye anakatalia madarakani, kuna kila dalili huenda yale yaliyomkuta Gbagbo yakamkuta na yeye.
 
Na bado kuna watu wanafikiri madaraka yanaachiwa kwa kipande cha karatasi ......Africa
 
Back
Top Bottom