Upinzani huko Tanzania mjilaumu wenyewe, mliingia kichinjioni mkiona

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,757
48,407
Upinzani wa Tanzania mjilaumu wenyewe tu, maana chaguzi za serikali za mitaa mligomea na kuona kilichotendeka, CCM walizoa kila kitu bila kupepesa macho, maana kwamba walikua tayari kuwafuta kwenye historia ya nchi, walikua tayari kufanya chochote na lolote bila aibu.

Sasa mmekuwa mkilaumu kwamba tume ya uchaguzi ina upendeleo, kwamba sio huru, kwamba inafuata maagizo ya CCM, licha ya yote mkadiriki kuhusika kwenye uchaguzi chini ya hiyo hiyo tume, mkafanya kampeni iliyokua inahudhuriwa na nyomi kubwa iliyoonyesha kweli mamilioni ya Watanzania walikua wanawapenda, mkafanya CCM wapanic zaidi, ndio hayo matokeo yake, wamekumbakumba kila kitu kiasi kwamba hata wafuasi wa CCM wengi wameonyesha kufedheheshwa na kilichotokea, japo kunao wanajipa ujoto humu kwenye mitandao lakini mioyoni inawauma.

Kwa umoja wa taifa mkubali kusonga mbele hamna kikubwa mnachoweza kukifanya, imeisha hiyo, mlijipeleka kichinjioni huku mkilalamika na ndio hayo matokeo yake. Bunge lote ni kijani kwa kwenda mbele.

Akina Kagame na Museveni popote walipo wanachekelea tu. Afrika tamu sana hili bara.
 
Sasa soma kuhusu kushindwa kwa mchakato wa katiba mpya baada ya maccm kuona kwamba wasingeshinda tena chaguzi kwa njia haramu.

 

Kabisa Mkuu wahuni wa maccm wamegundua hawana nguvu ya hoja ya kuwavutia Watanzania wengi wawapigie kura ukilinganisha na wapinzani. Pamoja na JIWE kudai ataishughulikia Katiba mpya ili kuifikisha Tanzania mahali pazuri baadaye akang’aka kwa kujua inaweza kuwa kaburi lake na hivyo kuwa Rais wa awamu moja tu. Hivyo utaona hawa wahuni wa maccm maslahi yao binafsi na chama chao cha wahuni wanayapa priority kubwa sana kuliko yale ya Tanzania na Watanzania. Ikibidi hata kuua wanaua ili kubaka demokrasi.
Hapa kupitisha mswaada ni mambo na exclamation tuu, hamna haja ya kura. Yaani kiranja wa wengi bungeni hatakuwa na ugumu wowote wa kufanya whipping. Akikohoa tuu mswaada ndio huooo, kishaa pita!.. 🤣🤣
 
Upinzani using wingi a katika uchaguzi mkuu huu, haya matatizo yasingeonekana na kamwe yasingepatiwa suluhu. 2025 hali ingekua hii hii.
 
Ebu na wewe pambana na Corona yako.
Ya Tanzania tuachie wenyewe.
Unawalaumu kwa kipi?
Kwa hyo unahalalisha dhulma ya CCM?
Wangesusia uchaguzi ili iweje?
 
Wewe hujaijua CCM.

Ni dubu na shetani mwenye kiu kubwa.

Watu washajitahidi sana kutafuta njia kwa njia ya haki.

Rejea: Bob Chacha Wangwe kukata rufaa Mahakama ya Afrika kuhusu wakurugenzi kusimamia uchaguzi

Kitu unachoshindwa kuelewa ni kuwa, huku vyama vya upinzani havipambani na CCM.

Bali katika vita na Dola. Tena kuna rundo la watu wa usalama, JWTZ,Polisi, Magereza, Zimamoto.

Mwaka huu CCM wameingiza mtaani mpaka Migambo.

Hakuna mchakato wowote uliofsnyika kwa Uhuru: Kuanzia utoaji wa fomu, wagombea wa upinzani kuenguliwa, kampeni mpaka utangazaji wa matokeo huwa ni vurugu tu.

Mwaka , baada 2015 vyama vya upinzani kuungana CCM wakatunga sheria ya kuzuia hilo tena.

Hivyo unaweza kunionea mwenyewe hali ilivyo.

Hicho kidemocracy, kimebaki na term limits tu na yenyewe iko shakani
 
Kabisa Mkuu wahuni wa maccm wamegundua hawana nguvu ya hoja ya kuwavutia Watanzania wengi wawapigie kura ukilinganisha na wapinzani. Pamoja na JIWE kudai ataishughulikia Katiba mpya ili kuifikisha Tanzania mahali pazuri baadaye akang’aka kwa kujua inaweza kuwa kaburi lake na hivyo kuwa Rais wa awamu moja tu. Hivyo utaona hawa wahuni wa maccm maslahi yao binafsi na chama chao cha wahuni wanayapa priority kubwa sana kuliko yale ya Tanzania na Watanzania. Ikibidi hata kuua wanaua ili kubaka demokrasi.
Hizi Ngonjera Ungeenda Kumuagia Mamluki wenu Wakati anarudi Kwa mabwana Wake. Unapoteza Nguvu tu

Tanzania Haina Upinzani kuna Wasaka Tonge na Wasaliti

Tulisha sema Upinzani wa Tanzania utakuja Letwa na Watoto wetu sio nyie Vibendera fuata upepo

HATUWEZI KURUKA MKOJO NA KUKANYAGA KINYESI
 
Sasa soma kuhusu kushindwa kwa mchakato wa katiba mpya baada ya maccm kuona kwamba wasingeshinda tena chaguzi kwa njia haramu.

Upinzani mngekubali ile Katiba ya kikwete angalau ilikua na mambo mazuri..Mengine mngedai baadae...kwa katiba hii tukiyonayo japo hata yenyewe haifuatwi upuuzi huu hautaisha..Inabidi mbadili mbinu ila kwenye hii Nec na Polisi hawa hawa Milele zote hamtakaa mpate kitu.
 
Wewe hujaijua CCM.

Ni dubu na shetani mwenye kiu kubwa.

Watu washajitahidi sana kutafuta njia kwa njia ya haki.

Rejea: Bob Chacha Wangwe kukata rufaa Mahakama ya Afrika kuhusu wakurugenzi kusimamia uchaguzi

Kitu unachoshindwa kuelewa ni kuwa, huku vyama vya upinzani havipambani na CCM.

Bali katika vita na Dola. Tena kuna rundo la watu wa usalama, JWTZ,Polisi, Magereza, Zimamoto.

Mwaka huu CCM wameingiza mtaani mpaka Migambo.

Hakuna mchakato wowote uliofsnyika kwa Uhuru: Kuanzia utoaji wa fomu, wagombea wa upinzani kuenguliwa, kampeni mpaka utangazaji wa matokeo huwa ni vurugu tu.

Mwaka , baada 2015 vyama vya upinzani kuungana CCM wakatunga sheria ya kuzuia hilo tena.

Hivyo unaweza kunionea mwenyewe hali ilivyo.

Hicho kidemocracy, kimebaki na term limits tu na yenyewe iko shakani

Sasa kama unavyosema ni kweli basi hapo msingeingia kwenye uchaguzi, upinzani mngesusia maana kilichofanyika ni kukipa chama cha CCM uhalali wa kujiaminisha wameshinda, yaani wewe uingie uwanjani kushindana na timu ambayo unaona wasimamizi wote wakiwemo marefaa wamejiandaa kuhakikisha unashindwa, wote wameswagwa wahakikishe hilo la sivyo ikule kwao, hivyo wanaishia kusindika bila aibu.

Kilichosalia ni nyote kumuabudu mkulu, mumuangukie miguuni na kumuomba moyo wake umsute kiasi cha kuwa tayari kurekebisha katiba na mengineyo, bahati nzuri yeye yuko kwenye hatamu yake ya mwisho, hivyo anayo uhuru wa kuiacha nchi ikiwa bora zaidi ya alivyoikuta.
 
Sasa kama unavyosema ni kweli basi hapo msingeingia kwenye uchaguzi, upinzani mngesusia maana kilichofanyika ni kukipa chama cha CCM uhalali wa kujiaminisha wameshinda, yaani wewe uingie uwanjani kushindana na timu ambayo unaona wasimamizi wote wakiwemo marefaa wamejiandaa kuhakikisha unashindwa, wote wameswagwa wahakikishe hilo la sivyo ikule kwao, hivyo wanaishia kusindika bila aibu.

Kilichosalia ni nyote kumuabudu mkulu, mumuangukie miguuni na kumuomba moyo wake umsute kiasi cha kuwa tayari kurekebisha katiba na mengineyo, bahati nzuri yeye yuko kwenye hatamu yake ya mwisho, hivyo anayo uhuru wa kuiacha nchi ikiwa bora zaidi ya alivyoikuta.
Rais Magufuli anateua na kutumbua zaidi ya asilimia 99% ya watumishi nchi hii. Ndio maana unaona watu wanajitoa akili ili kujipendekeza kwake wapate chochote.

Upinzani kuna vyama zaidi ya 18 na kama unavyoona kwenye msafara wa mamba na kenge wapo, siyo kila mtu aliye chama cha upinzani anapenda mageuzi, kuna wengine wanatafuta fursa tu.

Ndio maana kuna watu hawakupata nafasi CCM ila baada kujenga jina kupitia vyama vya upinzani CCM imewachukua na kuwahonga vyeo.

Upinzani wakususa yatatokea ya serikali za mitaa au Zanzibar, hawana sibu kabisa. Kwao hata katiba ni takataka tu.

Wakitaka wanasajiri tu vyama bandia vinashiriki uchaguzi basi itaonekana vyama vyama upinzani vilikuwepo. Ni kama ilivyotokea wakati Tundu Lissu anafungiwa kufanya kampeni wiki nzima, kuna vyama vyao CCM vilishiriki kikao na kubariki hilo.

So, kususia uchaguzi ndicho hada CCM wanapenda, hata kabla ya Uchaguzi Magufuli alijua watasusa akawa ameshaandaa chama chake NCCR Mageuzi. Na baadhi ya wabunge waliokuwa upinzani akawanunua na kuwaahidi vyeo tayari walikuwa washahamia huko.

Tanzania tuko kstika hali ngumu sana, too bad ni kwamba jumuiya za kimataifa hazijaweka mkazo kuhusu kinachoendelea hapa.

JWTZ, TISS, MGAMBO, FEED FORCE, wanaua watu tu huko Pemba ili kumsimika mgombea wao.

- Hakuna internet

- Hakuna mawasiliano ya simu

- No body in, no body out

Unfortunately 😔☹️ hakuna media yenye uwezo wa kuripoti chochote huko. Magaidi wamekuja Mtwara wameteka kijiji kizima hakuna media inasema, media za msumbibi ndio zinaripoti.

We're all in a cage. Hatujui itakuaje

Hata Tundu Lissu kajitahidi mnoo maana kwasasa Magufuli kila mtu anamwogopa ameshaua watu mnoooo, tena anaua hadharani kabisa. Huyo Lissu slipigwa risasi 36 mchana kweupee
 
Rais Magufuli anateua na kutumbua zaidi ya asilimia 99% ya watumishi nchi hii. Ndio maana unaona watu wanajitoa akili ili kujipendekeza kwake wapate chochote.

Upinzani kuna vyama zaidi ya 18 na kama unavyoona kwenye msafara wa mamba na kenge wapo, siyo kila mtu aliye chama cha upinzani anapenda mageuzi, kuna wengine wanatafuta fursa tu.

Ndio maana kuna watu hawakupata nafasi CCM ila baada kujenga jina kupitia vyama vya upinzani CCM imewachukua na kuwahonga vyeo.

Upinzani wakususa yatatokea ya serikali za mitaa au Zanzibar, hawana sibu kabisa. Kwao hata katiba ni takataka tu.

Wakitaka wanasajiri tu vyama bandia vinashiriki uchaguzi basi itaonekana vyama vyama upinzani vilikuwepo. Ni kama ilivyotokea wakati Tundu Lissu anafungiwa kufanya kampeni wiki nzima, kuna vyama vyao CCM vilishiriki kikao na kubariki hilo.

So, kususia uchaguzi ndicho hada CCM wanapenda, hata kabla ya Uchaguzi Magufuli alijua watasusa akawa ameshaandaa chama chake NCCR Mageuzi. Na baadhi ya wabunge waliokuwa upinzani akawanunua na kuwaahidi vyeo tayari walikuwa washahamia huko.

Tanzania tuko kstika hali ngumu sana, too bad ni kwamba jumuiya za kimataifa hazijaweka mkazo kuhusu kinachoendelea hapa.

JWTZ, TISS, MGAMBO, FEED FORCE, wanaua watu tu huko Pemba ili kumsimika mgombea wao.

- Hakuna internet

- Hakuna mawasiliano ya simu

- No body in, no body out

Unfortunately 😔☹️ hakuna media yenye uwezo wa kuripoti chochote huko. Magaidi wamekuja Mtwara wameteka kijiji kizima hakuna media inasema, media za msumbibi ndio zinaripoti.

We're all in a cage. Hatujui itakuaje

Hata Tundu Lissu kajitahidi mnoo maana kwasasa Magufuli kila mtu anamwogopa ameshaua watu mnoooo, tena anaua hadharani kabisa. Huyo Lissu slipigwa risasi 36 mchana kweupee
Chunga sana na matamshi yako unapokuja hapa jukwaani kwani unaweza kupotezwa kwenye uso wa dunia jinsi alivyopotezwa marehemu Ben Saa8. In the meantime, tuendelee kusherehekea ushindi mkubwa aliopata JPM.
 
Rais Magufuli anateua na kutumbua zaidi ya asilimia 99% ya watumishi nchi hii. Ndio maana unaona watu wanajitoa akili ili kujipendekeza kwake wapate chochote.

Upinzani kuna vyama zaidi ya 18 na kama unavyoona kwenye msafara wa mamba na kenge wapo, siyo kila mtu aliye chama cha upinzani anapenda mageuzi, kuna wengine wanatafuta fursa tu.

Ndio maana kuna watu hawakupata nafasi CCM ila baada kujenga jina kupitia vyama vya upinzani CCM imewachukua na kuwahonga vyeo.

Upinzani wakususa yatatokea ya serikali za mitaa au Zanzibar, hawana sibu kabisa. Kwao hata katiba ni takataka tu.

Wakitaka wanasajiri tu vyama bandia vinashiriki uchaguzi basi itaonekana vyama vyama upinzani vilikuwepo. Ni kama ilivyotokea wakati Tundu Lissu anafungiwa kufanya kampeni wiki nzima, kuna vyama vyao CCM vilishiriki kikao na kubariki hilo.

So, kususia uchaguzi ndicho hada CCM wanapenda, hata kabla ya Uchaguzi Magufuli alijua watasusa akawa ameshaandaa chama chake NCCR Mageuzi. Na baadhi ya wabunge waliokuwa upinzani akawanunua na kuwaahidi vyeo tayari walikuwa washahamia huko.

Tanzania tuko kstika hali ngumu sana, too bad ni kwamba jumuiya za kimataifa hazijaweka mkazo kuhusu kinachoendelea hapa.

JWTZ, TISS, MGAMBO, FEED FORCE, wanaua watu tu huko Pemba ili kumsimika mgombea wao.

- Hakuna internet

- Hakuna mawasiliano ya simu

- No body in, no body out

Unfortunately 😔☹️ hakuna media yenye uwezo wa kuripoti chochote huko. Magaidi wamekuja Mtwara wameteka kijiji kizima hakuna media inasema, media za msumbibi ndio zinaripoti.

We're all in a cage. Hatujui itakuaje

Hata Tundu Lissu kajitahidi mnoo maana kwasasa Magufuli kila mtu anamwogopa ameshaua watu mnoooo, tena anaua hadharani kabisa. Huyo Lissu slipigwa risasi 36 mchana kweupee

Dah! Kwa kweli sikuwa nawaza hilo la vyama vya kununuliwa, kha hiyo balaa, yaani hapo ni ile huwa tunasema "you're damned if you do and damned if you don't"
 
Hapa Kazi Tu!
1604044021499.png
 
Dah! Kwa kweli sikuwa nawaza hilo la vyama vya kununuliwa, kha hiyo balaa, yaani hapo ni ile huwa tunasema "you're damned if you do and damned if you don't"
Yaani kwasasa kilichobaki ni kila mtu aisome namba ili tuongee lugha moja.

Kwasasa kuna watu wanadhani kina Mbowe, Zitto au Maalim Seif ndio wenye shida na kama ujuavyo chuki hupofusha.

Mfano mdogo tu: Hii ni payslip ya mwalimu (Degree holder) kwa shule za serkali: Hawa watu waliingia mkataba na Bodi ya mikopo kuwa wakipata ajira watakuwa wakikatwa 8% ya mshahara, alivyowekwa Magu kawapandishia makato mpaka 15% na hakuna hata chama cha wafanyakazi kinachoguna guna, tena wanasifia tu.

Na kama hilo halitoshi, hajaongeza annual increments ambazo zipo kisheria miaka yote mitano.

Picha ni huo mshahara, Netpsy ni kama Ksh 22,000 na kwa hilo deni halitaisha mpaka afe maana hata pension hatapata.
 

Attachments

  • IMG_20200921_190239.jpg
    IMG_20200921_190239.jpg
    25.6 KB · Views: 1
Wewe hujui chochote kuhusu Tz ,labda nikusaidie tu upinzani wamevuna walichokipanda hayo ndio yale matunda ya kupinga kila kitu hata kama cha maendeleo sasa watu kama hao wanafaida gani Kwa wananchi wazidi kuwakumbatia?

Haiwezekani ununuzi wa ndege wamepinga , barabara za juu Dar wamepinga, ujenzi wa reli wamepinga, ujenzi wa barabara kumi na ngapi cjui zike wamesema za kazi gani, ujenzi wa bwawa la umeme rufiji wamepinga wamesema tunayo kidatu , kuzuia mchanga wa madini wamepinga, kubadilisha mikataba ya madini wamepinga, yani hamna hata moja walilokubali sasa watu kama hao kuna haja gani ya kuwarudisha bungeni na Kwa manufaa ya nani?

Watanzania sio wajinga ukituzingua tunakuzingua ndio kanuni iliyotumika, sasa kama ulitaka watu warudi bungeni kwasababu tu ulizoea kuwaona nikukumbushe huu uchaguzi Kwa maslahi ya TZ na sio Kenya.
 
Back
Top Bottom