Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa JamiiForums.
Ndugu zangu Watanzania;
Upi ni uamuzi sahihi wa kufanywa na abiria pindi gari (hususan daladala) inapoanza kurudi nyuma baada ya kushindwa kupanda mlima?
Je, ulishawahi kujikuta katika hali hii na ulifanya nini?
Nimeamua kuomba ushauri hapa kwa maana kwamba siku ya tarehe 13 October 2020, ambapo mvua kubwa sana ilinyesha sana, nilipokuwa ninatoka Kitunda huku Dar sasa ninarudi Kivule nikiwa katika bodaboda maeneo ya sehemu moja wanaitwa kwa Mwailafu nilishihudia gari ya abiria almaarufu kama daladala ikirudi "reverse" baada ya kushindwa kupamba mlima mdogo kutokana na udongo wake kuwa unatereza kwa kiingereza wanasema "treacherous"
Katika harakati za kutaka kuokoa maisha yao kuna abiria wawili ambao ni wakaka wao wakaruka nje lakini abiria wengine wote wakabaki ndani ya daladala ile huku wakipiga mayowe wasijue nini la kufanya.
Mungu si Athumani, dereva wa ile gari alikuwa jasiri na shupavu alifanikiwa kuigonesha ile gari pembezoni mwa ukingo wa barabara hivyo kuzuia gari ile isiingie katika daraja kubwa ambalo bado linaendelea na ujenzi.
NB: Picha hapo juu haina uhusiano wowote na hicho kisa nilichosimulia.
Kuna baadhi ya watu wanadai kuruka wakati daladala/gari ime-fail brake mlimani sio uamuzi sahihi ila kuna baadhi wanadai kuwa ndio jambo jema la kufanya wakati wa janga la namna ile
Upi ni uamuzi sahihi wa kufanywa na abiria? Je, ulishawahi kujikuta katika hali hii na ulifanya nini?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Ndugu zangu Watanzania;
Upi ni uamuzi sahihi wa kufanywa na abiria pindi gari (hususan daladala) inapoanza kurudi nyuma baada ya kushindwa kupanda mlima?
Je, ulishawahi kujikuta katika hali hii na ulifanya nini?
Nimeamua kuomba ushauri hapa kwa maana kwamba siku ya tarehe 13 October 2020, ambapo mvua kubwa sana ilinyesha sana, nilipokuwa ninatoka Kitunda huku Dar sasa ninarudi Kivule nikiwa katika bodaboda maeneo ya sehemu moja wanaitwa kwa Mwailafu nilishihudia gari ya abiria almaarufu kama daladala ikirudi "reverse" baada ya kushindwa kupamba mlima mdogo kutokana na udongo wake kuwa unatereza kwa kiingereza wanasema "treacherous"
Katika harakati za kutaka kuokoa maisha yao kuna abiria wawili ambao ni wakaka wao wakaruka nje lakini abiria wengine wote wakabaki ndani ya daladala ile huku wakipiga mayowe wasijue nini la kufanya.
Mungu si Athumani, dereva wa ile gari alikuwa jasiri na shupavu alifanikiwa kuigonesha ile gari pembezoni mwa ukingo wa barabara hivyo kuzuia gari ile isiingie katika daraja kubwa ambalo bado linaendelea na ujenzi.
NB: Picha hapo juu haina uhusiano wowote na hicho kisa nilichosimulia.
Kuna baadhi ya watu wanadai kuruka wakati daladala/gari ime-fail brake mlimani sio uamuzi sahihi ila kuna baadhi wanadai kuwa ndio jambo jema la kufanya wakati wa janga la namna ile
Upi ni uamuzi sahihi wa kufanywa na abiria? Je, ulishawahi kujikuta katika hali hii na ulifanya nini?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.