Upepo wa Tundu Lissu ughaibuni umetulia sasa na watu wamerudi kufanya kazi

tatum

JF-Expert Member
Jan 16, 2018
5,786
4,490
Wiki kama mbili hivi kumekuwa na malumbano na mijadala mingi sana katika vyombo vya habari vya hapa Tanzania kuanzia kwenye tv,redio na mitandao ya kijamii kuhusu ziara ya Mhe Tundu Lissu huko Ulaya na Marekani akiwa anajaribu kueleza yale anayopna yeye kuwa ni mapungufu ya Serikali ya awamu ya tano katika utawala wake.

Baada ya mijadala na mahojiano yake huko majuu na kushikiliwa bango na watz wenye msimamo kama Tundu Lissu naona upepo huo sasa umetulia na watu wameanza kufanya kazi zao kama kawaida na kujadili mambo ya msingi sasa ya kuendeleza nchi na watu wake.

Tulijua tu kuwa upepo huu utatulia tu baada ya muda mfupi na ndiyo mara nyingi mambo ya kisiasa yalivyo.

Tusubiri atakapo ibuka tena kwenye kurudi kwake Tanzania kama kweli atarudi na kuitangazia dunia kuwa sasa anarudi Tanzania kama alivyojinasibu huko Marekani kuwa atarudi kwa kishindo kikuu hapa nchini.

Naona kwa maneno yake aliyokuwa anaiaminisha dunia kuwa nchi yetu ikoje huko majuu kiukweli ni ngumu sana kurudi hivi karibuni labda baada ya miaka 20 kuisha au asirudi kabisa.
 
Ukumsikiliza vizr kumbe, alisema tarehe 20 dakitari wake anamhitaji kwa oparation nyingine.....kwahiyo bwana mkubwa iko angalau kwasasa soon tutamuona TBC live....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We ndio uliacha kazi maana ulilazimishwa kuja kuitetea serikali hapa jukwaani na kuacha kazi zako. Tundu Lissu hajakimbia nchi bali yupo Ulaya kwa matibabu. Akiwa huko akajiongeza kwa kueleza dunia ukweli kwa kile alichofanyiwa na serikali hapa nchini.

Ni hivi, atarudi na mkitaka mfanye lolote, tena ikibidi mpigeni risasi safari hii hapo uwanja wa Taifa. Lissu ni mzalendo na hakusubiri madaraka ndio aonyeshe uzalendo wake.

Atarudi na atagombea urais sambamba na kuanzisha vuguvugu la katiba ya Warioba ipitishwe.
 
We ndio uliacha kazi maana ulilazimishwa kuja kuitetea serikali hapa jukwaani na kuacha kazi zako. Tundu Lissu hajakimbia nchi bali yupo Ulaya kwa matibabu. Akiwa huko akajiongeza kwa kueleza dunia ukweli kwa kile alichofanyiwa na serikali hapa nchini. Ni hivi, atarudi na mkitaka mfanye lolote, tena ikibidi mpigeni risasi safari hii hapo uwanja wa Taifa. Lissu ni mzalendo na hakusubiri madaraka ndio aonyeshe uzalendo wake. Atarudi na atagombea urais sambamba na kuanzisha vuguvugu la katiba ya Warioba ipitishwe.
Adui wa Taifa tunamjua na adhabu ya msaliti inajulikana
 
Hilo lijamaa limekata pumzi.
Endelea kujidanganya. Lissu yuko kwenye maandalizi ya upasuaji wa mwisho utaofanyika kesho

Sasa kama aliweza kuwafanya mzimie kwa presha kipindi hajamaliza upasuaji, saizi itakua mara 10 ya pale. Unazimia saizi unakuja kupata fahamu 2020 unakuta uliyekua unamponda kashikilia kiti kudadeki

Sent using unknown device
 
Back
Top Bottom