Upepo wa Halima Mdee na wenzake utapita kama ulivyopita wa ICC na Rais Magufuli

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,974
Siasa za Tanzania ni za aina yake ambazo zinaweza kukupa matumaini ambayo hayapo kama huzijui vizuri. Siasa za Tanzania ni kama upepo unaopita ambao hauna madhara yoyote kwa wanaozijua vizuri siasa za Tanzania!

Baada ya Uchaguzi Mkuu 2020, hoja zilizojaa kwenye mitandao ya kijamii kwa wiki tatu zilikuwa ni Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) na Rais Magufuli!

Wasiozijua vizuri siasa za Tanzania wakaambiwa wakusanye vielelezo na vidhibiti ili wahalifu nchini wakashitakiwe kwenye mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC). Wasiozijua vizuri siasa nchini wakakusanya na kukabidhi ''vielelezo'' na ''vidhibiti'' kwa waliowaagiza!

Watanzania tukaaambiwa ''tukae mkao wa kula'' kwa sababu ''vielelezo'' na ''vidhibiti'' vimewasilishwa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC). Maelezo haya yaliwafanya wasiozijua vizuri siasa za Tanzania kuanza kushangilia huku wengine wakitumaini wako mbioni kushuhudia Uchaguzi Mkuu mwingine kwa sababu watawala wa sasa wakiongozwa na Rais Magufuli wanapelekwa gerezani, Uholanzi!

Wanaozijua siasa za Tanzania vizuri wakasema, hizi ni porojo za kisiasa za kipoza uongo (political placebo) ambazo baada ya muda ukweli utazisambaratisha!

Kwa sasa huwezi kusikia tena suala la Rais Magufuli kupelekwa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) likijadiliwa na wale waliolianzisha kwenye mitandao ya kijamii! Wanajua UPEPO UMEPITA!

Hata yule aliyekuwa anajiita ''Mwanasheria'' wa Tundu Lissu, Robert Amsterdam huwezi kumsikia tena akipiga kelele kuhusu Rais Magufuli na ICC! UPEPO UMEPITA! Nasikia amehamia kwenye siasa za Uganda!

Upepo uliopo kwa sasa ni upepo wa Halima Mdee na wenzake! Hata huu upepo baada ya muda utapita bila kuleta madhara yoyote kwa wale wanaozijua vizuri siasa nchini! Hata Halima Mdee wakati akiongea na vyombo vya habari alisema huu ni upepo tu ''usio na madhara'' ambao utapita!

Walewale waliokuwa mstari wa mbele kwenye upepo wa Rais Magufuli na ICC kwa sasa tena wamekuwa mstari wa mbele kwenye upepo wa Halima Mdee na wenzake!

Baada ya huu upepo wa Halima Mdee na wenzake kupita, wabunge wa viti maalum wa CHADEMA wataenda bungeni na CHADEMA wataendelea kupokea ruzuku zitokanazo na Uchaguzi Mkuu ambao viongozi wa CHADEMA wanatuambia ''hawautambui''!

ACT-Wazalendo pia watajiunga na serikali ya mapinduzi Zanzibar AKA SUK kuunda serikali na maisha yataendelea!

Hii ndio Tanzania ambayo kama huzijui vizuri siasa zake unaweza kujipa matumaini ambayo kiuhalisia hayapo bali unachohangaika nacho ni siasa za kipoza uongo (political placebo)!
 
1607062900660.jpeg
 
Hili ni hitimisho lako lakini ukweli unabaki kuwa siasa za Tanzania ni kama upepo ambao hauna madhara kwa wanaozijua vizuri!

Acha tu boss hii nchi ni kichekesho cha karne. Kuna mtendaji mmoja huko vijijini ninakokwenda alikuwa anawaongolesha wananchi kwa vitisho eti iwapo hiyo 50m@kijiji ikifika wasionane wabaya. Nikamwambia una uhakika na hiyo hela maana rais huyu sio mtu mkweli, akaniapia kwa Miungu yake, na akasema siku hela ikiingia nitameza matapishi yangu. Sasa hivi tukionana huko kijijini hataki hata kunipungia mkono.

Kuna wengine niliwaambia mradi wa bomba la mafuta ya Uganda ni utapeli kama utapeli mwingine, kada mmoja wa mboga mboga akawa ananiambia lazima huo mradi ukamilike kufika hii 2020, na serikali ichukue hela za ajabu. Leo hii ni mwisho wa 2020 hakuna hata kipande cha bomba bovu hapa nchini la hilo bomba la tapeli Museveni, zaidi ya juzi kuja kwenye kampeni za kuhalalisha wizi wa kura kwenye maonyesho ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
 
Acha tu boss hii nchi ni kichekesho cha karne. Kuna mtendaji mmoja huko vijijini ninakokwenda alikuwa anawaongolesha wananchi kwa vitisho eti iwapo hiyo 50m@kijiji ikifika wasionane wabaya. Nikamwambia una uhakika na hiyo hela maana rais huyu sio mtu mkweli, akaniapia kwa Miungu yake, na akasema siku hela ikiingia nitameza matapishi yangu. Sasa hivi tukionana huko kijijini hataki hata kunipungia mkono.

Kuna wengine niliwaambia mradi wa bomba la mafuta ya Uganda ni utapeli kama utapeli mwingine, kada mmoja wa mboga mboga akawa ananiambia lazima huo mradi ukamilike kufika hii 2020, na serikali ichukue hela za ajabu. Leo hii ni mwisho wa 2020 hakuna hata kipande cha bomba bovu hapa nchini la hilo bomba la tapeli Museveni, zaidi ya juzi kuja kwenye kampeni za kuhalalisha wizi wa kura kwenye maonyesho ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
Nadhani kuhusu bomba la Mafuta, Wafaransa wanasubiri kwanza uchaguzi upite nchini Uganda!

Kuhusu milioni 50 kila kijiji, nakubali CCM walihadaa umma kwenye Ilani ya Uchaguzi 2015 na walipaswa kuwaomba wananchi msamaha! Tatizo wana siasa wetu ni wagumu sana kuomba msamaha!
 
Nadhan umeandika hivi lengo lako unataka kujua nini kinaendelea huko ICC right? Hof yako nn na nyinyi hamjauwa watu?
 
Nadhani kuhusu bomba la Mafuta, Wafaransa wanasubiri kwanza uchaguzi upite nchini Uganda! Kuhusu milioni 50 kila kijiji, nakubali CCM walihadaa umma kwenye Ilani ya Uchaguzi 2015 na walipaswa kuwaomba wananchi msamaha! Tatizo wana siasa wetu ni wagumu sana kuomba msamaha!
Nadhani kuhusu bomba la Mafuta, Wafaransa wanasubiri kwanza uchaguzi upite nchini Uganda! Kuhusu milioni 50 kila kijiji, nakubali CCM walihadaa umma kwenye Ilani ya Uchaguzi 2015 na walipaswa kuwaomba wananchi msamaha! Tatizo wana siasa wetu ni wagumu sana kuomba msamaha!
Nadhani kuhusu bomba la Mafuta, Wafaransa wanasubiri kwanza uchaguzi upite nchini Uganda! Kuhusu milioni 50 kila kijiji, nakubali CCM walihadaa umma kwenye Ilani ya Uchaguzi 2015 na walipaswa kuwaomba wananchi msamaha! Tatizo wana siasa wetu ni wagumu sana kuomba msamaha!
Bomba la mafuta lilikuwa likamilike 2020, hukumbuki uzinduzi wake huko Chongoleani Tanga mbele ya Magufuli, Museveni na hao wafaransa. Mpaka siku hiyo wakapatanishwa Makonda na Ruge RIP?

Hapo bado sijazungumzia zile porojo za uchumi wa gas kabla ya 2015. Unakumbuka tulivyokuwa tunaimbishwa uchumi wa gas kama wendawazimu, na tukaambiwa bomba la gas likifika Dar tutazalisha umeme wa 5,000mg na kuuza nchi jirani? Mara kaingia rais huyu mapambio ya gas yameisha, sasa hivi ni 2,115mg umeme wa maji! Sasa unajiuliza 5,000mg ni wapi wapi na 2,115mg. Usishangae akiingia rais mwingine akasema umeme wa makaa ya nawe ndio sawa. Na hadithi ikabadilika.
 
Suala la kina Mdee halihusiani na upepo kabisa, hilo linawahusisha wanachama, kama patakuwepo na makubaliano kati yao ( Mdee na wenzake na Chadema) lazima wanachama watajulishwa.

Suala la ICC nalo bado mpaka hiyo mahakama itakapotoa taarifa yake.

Mambo ya upepo peleka kwenye ahadi zenu za CCM, nje ya hapo hakuna upepo.

Usipende kuishi kwa mazoea, hii dunia imebadilika.
 
18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom