Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Mara nyingi sana nimesikia wanasiasa wakitoa ahadi za kuchimba visima kama njia ya kutatua tatizo la maji - iwe mjini au vijijini. Hebu angalia vichwa hivi vya habari kisha usome swali langu tena:
Wamarekani kuchimba visima 20 Dakawa
Watumia Sh400 mil kuchimba visima
Dewji achimba visima kwa milioni 500 Singida
Abood aingiza mitambo ya kuchimba visima
Mbunge aanza kuchimba visima 60 jimboni
Ujenzi visima vya maji Morogoro, wakazi pembezoni mwa mji kunufaika.
Sasa kuna vitu najiuliza:
a. Kwanini mara nyingi suluhisho la haraka linalochukuliwa kukabiliana na tatizo la maji ni kuchimba visima na hivyo kuwasababisha wananchi kuyafuata maji kutoka majumbani mwao badala ya kufikiria mfumo wa kuwaletea maji hayo (yanayopatikana kwenye visima hivyo) kwa wananchi?
b. Je, kuna uwezekano wa kubuni njia ya kuunganisha visima kadhaa kutengeneza mfumo wa maji wa mahali (local water supply system) badala ya kuwa na visima kimoja kimoja? Kwa mfano, visima 50 (au hata kimoja tu) vinajaza maji kwenye tanki la jumuiya na kutoka kwenye tanki (lililoko uphill) mabomba yanarudishwa wa wananchi? Kinachohitajika ni kutengeneza pump ya upepo kusukuma maji mlimani.
c. Ni kweli kuchimba visima vingi yaweza kuwa ni suluhisho la sasa "hivi" la maji lakini ni visima vingapi ambavyo vimebakia kutumika baada ya miaka na viko katika hali gani na je ndilo suluhisho bora zaidi? Kuna namna nyingine yoyote ya kuweza kutumia maji yaliyoko ardhini kutengeneza mfumo wa maji safi katika jamii mbalimbali?
Ninajua kuna wataalamu wa mambo mbalimbali hapa ambao wanaweza kutusaidia kujibu swali hili: Je inawezekana kutumia maji ya visimani kuweza kuyafikisha kwenye nyumba ya kila mwanakijiji badala ya kila mwanakijiji kulifuata bomba au kisima kilipo?
Wamarekani kuchimba visima 20 Dakawa
Watumia Sh400 mil kuchimba visima
Dewji achimba visima kwa milioni 500 Singida
Abood aingiza mitambo ya kuchimba visima
Mbunge aanza kuchimba visima 60 jimboni
Ujenzi visima vya maji Morogoro, wakazi pembezoni mwa mji kunufaika.
Sasa kuna vitu najiuliza:
a. Kwanini mara nyingi suluhisho la haraka linalochukuliwa kukabiliana na tatizo la maji ni kuchimba visima na hivyo kuwasababisha wananchi kuyafuata maji kutoka majumbani mwao badala ya kufikiria mfumo wa kuwaletea maji hayo (yanayopatikana kwenye visima hivyo) kwa wananchi?
b. Je, kuna uwezekano wa kubuni njia ya kuunganisha visima kadhaa kutengeneza mfumo wa maji wa mahali (local water supply system) badala ya kuwa na visima kimoja kimoja? Kwa mfano, visima 50 (au hata kimoja tu) vinajaza maji kwenye tanki la jumuiya na kutoka kwenye tanki (lililoko uphill) mabomba yanarudishwa wa wananchi? Kinachohitajika ni kutengeneza pump ya upepo kusukuma maji mlimani.
c. Ni kweli kuchimba visima vingi yaweza kuwa ni suluhisho la sasa "hivi" la maji lakini ni visima vingapi ambavyo vimebakia kutumika baada ya miaka na viko katika hali gani na je ndilo suluhisho bora zaidi? Kuna namna nyingine yoyote ya kuweza kutumia maji yaliyoko ardhini kutengeneza mfumo wa maji safi katika jamii mbalimbali?
Ninajua kuna wataalamu wa mambo mbalimbali hapa ambao wanaweza kutusaidia kujibu swali hili: Je inawezekana kutumia maji ya visimani kuweza kuyafikisha kwenye nyumba ya kila mwanakijiji badala ya kila mwanakijiji kulifuata bomba au kisima kilipo?