LUSAJO L.M.
JF-Expert Member
- Aug 21, 2007
- 270
- 126
Nilipokuwa mdogo nilikuwa naona kila kitu ni rahisi maana kitu pekee nilichohitajika kusema ni mama naomba hiki; mama nataka kile na mama sitaki hiki. Kama mfalme yote nilitimiziwa. Leo nimebahatika kuwa mtu mzima na kuweza kuyafahamu maisha kwa jinsi yalivyo; ni kitu kimoja ambacho kila siku huwa nakiongea katika sala zangu na katika maongezi ya kawaida: Namshukuru Mama yangu kwa upendo wa kweli na kwa kujitolea kwake kutulea sisi. Leo tumekuwa watu wazima na katika umri alio nao ni faraja sana kwetu kwa kuwa tumekuwa na uwezo wa kumwangalia na kumtunza.
Shukurani kwa Mama nimekulia katika malezi bora na mema nikimjua Mungu na kufahamu thamani ya utu. Nampenda.
Shukurani kwa Mama nimekulia katika malezi bora na mema nikimjua Mungu na kufahamu thamani ya utu. Nampenda.