Upendeleo kwenye kugawa rasilimali za Taifa ukiendelea, tutaanza kuchaguana kiuzawa

Tigershark

JF-Expert Member
Oct 9, 2018
7,051
12,560
Hatari mojawapo kubwa ninayoiona iwapo tabia hii ya kupendelea Chato kunakofanywa na serikali ni kwamba tutaanza kuchagua kiongozi kutokana na uzawa!

Mfano mimi ni wa Kusini, akigombea Rais wa kutoka kusini basi nitamchagua nikiamini atafanya upendeleo na kuelekeza miradi mingi kusini kuliko maeneo mengine! Hivyo kigezo cha kwanza itakuwa kabila na vingine ndio vitafuata!

Kinachofanywa na serikali ya JPM cha kuelekeza miradi mingi Chato ni cha kupigiwa kelele na kila Mtanzania kwa mustakabali wa umoja wa taifa letu!

Sio kwamba waliomtangulia hawakutamani kupeleka maendeleo walikozaliwa ila miiko na maadili ya kazi zao iliwasuta! Kodi tunalipa wote hivyo vipaumbele vipangwe kwa haki.
 
Ni jambo baya tulikemee.
Sasa kuna watu nawashangaa wanakuja na hoja nyepesi kuwa hata Chato ni Tanzania! Mimi nilitegemea mtu aniambie hata Rais asingekuwa JPM basi miradi kama hiyo ingefanyika Chato kutokana na potential iliyoko huko kiuchumi!

Mtu akinishawishi kuwa Miradi inayoendelea Chato haina uhusiano na Rais kuwa mzawa wa Chato, nitamwelewa!
 
Kinachofanyika sasa Chato, ni aibu kubwa kwa Rais, CCM, Serikali na kwa Taifa letu. Lazima uwe mwendawazimu hasa kuunga mkono uchafu huu unaoendelea sasa:

1) Bohari kuu ya madawa ya kanda MSD Chato

2) Hospitali ya ya Rufaa ya Kanda Chato

3) Uwanja wa ndege wa kimataifa Chato

4) Uwanja wa mpira Chato

5) Mbuga ya wanyama ya kutengenezwa Chato

6) Kivuko cha kisasa Chato

7) Taa za kuongozea magari Chato

8) Chuo cha VETA Chato

9) Bandari Chato

Jamani, hivi huyu aliutaka Urais kwaajili ya kuijenga Tanzania au kuijenga Chato? Huyu ni Rais wa Tanzania au Rais wa Chato.

Huko CCM, hakuna japo mmoja tu aliyesalia wa kuweza kukemea huu uchafu wa upendeleo unaoendelea huko Chato?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kuna watu nawashangaa wanakuja na hoja nyepesi kuwa hata Chato ni Tanzania!Mimi nilitegemea mtu aniambie hata Rais asingekuwa JPM basi miradi kama hiyo ingefanyika Chato kutokana na potential iliyoko huko kiuchumi!
Mtu akinishawishi kuwa Miradi inayoendelea Chato haina uhusiano na Rais kuwa mzawa wa Chato,nitamwelewa!
Hoja yako imekaa kama mtu mwenye upeo na uwezo wa kujenga hoja.

Ni upumbavu wa hali juu kutetea huo uchafu unaoendelea huko Chato kwa hoja eti Chato nako ni Tanzania. Nina uhakika hoja ya namna hiii inatolewa na watu waliopungukiwa kichwani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hoja yako imekaa kama mtu mwenye upeo na uwezo wa kujenga hoja.

Ni upumbavu wa hali juu kutetea huo uchafu unaoendelea huko Chato kwa hoja eti Chato nako ni Tanzania. Nina uhakika hoja ya namna hiii inatolewa na watu waliopungukiwa kichwani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeongea ukweli mtupu japo hao jamaa wataweka pamba masikioni!
 
Kinachofanyika sasa Chato, ni aibu kubwa kwa Rais, CCM, Serikali na kwa Taifa letu. Lazima uwe mwendawazimu hasa kuonga mkono uchafu huu unaoendelea sasa:

1) Bohari kuu ya madawa ya kanda MSD Chato

2) Hospitali ya ya Rilufaa ya Kanda Chato

3) Uwanja wa ndege wa kimataifa Chato

4) Uwanja wa mpira Chato

5) Mbuga ya wanyama ya kutengenezwa Chato

6) Kivuko cha kisasa Chato

7) Taa za kuongozea magari Chato

Sent using Jamii Forums mobile app
Bandari kubwa inakaribia kukamilika Chato!
 
Jukumu la uongozi ni kuunganisha watu alisema Nyerere.

Tatizo kasema usinipangie
 
Kwakweli ni jambo baya sana. Hivi kila Rais afanye kwao kwa upendeleo hiyo nchi itakuwaje. Yafuatayo kwake

1. Uwanja wa ndege wa kimataifa
2. Hosptali kubwa ya Rufaa
3.uwanja mkubwa wa mpira
4. Daraja kubwa la busis Trilion 4
5. Chuo kikubwa ca Veta
6. Mbuga kubwa ya wanyama burigi
7. Mataa ya kuongoza magari
8. Kiwanda cha minofu ya samak
9. Majengo makubw CRDB,NMB, TRAA
10. Mkoa wa Chato, wakat wowote

Hayo yote wenzake waliomtangulia hawakufanya, maake Azimio la Arusha lilisema " CHEO NI DHAMANA, SITATUMIA CHEO CHANGU KWA MANUFAA BINAFSI" Waliogopa maadili, leo tunaona Chato imekuwa IKULU ya kupokelea mpk Maraisi, TUPAZE SAUTI, viningevyo atapeleka mpk Reli kwake. Tuamke
 
Kwakweli no jambo baya sana. Hivi kila Rais afanye kwao kwa upendeleo hiyo nchi itakuwaje. Yafuatayo kwake
1. Uwanja wa ndege wa kimataifa
2. Hosptali kubwa ya Rufaa
3.uwanja mkubwa wa mpira
4. Daraja kubwa la busis Trilion 4
5. Chuo kikubwa ca Veta
6. Mbuga kubwa ya wanyama burigi
7. Mataa ya kuongoza magari
8. Kiwanda cha minofu ya samak
9. Majengo makubw CRDB,NMB, TRAA
10. Mkoa wa Chato, wakat wowote

Hayo yote wenzake waliomtangulia hawakufanya, maake Azimio la Arusha lilisema " CHEO NI DHAMANA, SITATUMIA CHEO CHANGU KWA MANUFAA BINAFSI" Waliogopa maadili, leo tunaona Chato imekuwa IKULU ya kupokelea mpk Maraisi, TUPAZE SAUTI , viningevyo atapeleka mpk Reli kwake. Tuamuke
Bohari kubwa ya madawa MSD Chato, bandari nayo inakaribia kukamilika!
 
Hatari mojawapo kubwa ninayoiona iwapo tabia hii ya kupendelea Chato kunakofanywa na serikali, ni kwamba tutaanza kuchagua kiongozi kutokana na uzawa!

Mfano mimi ni wa Kusini, akigombea Rais wa kutoka kusini basi nitamchagua nikiamini atafanya upendeleo na kuelekeza miradi mingi kusini kuliko maeneo mengine! Hivyo kigezo cha kwanza itakuwa kabila na vingine ndio vitafuata!

Kinachofanywa na serikali ya JPM cha kuelekeza miradi mingi Chato ni cha kupigiwa kelele na kila Mtanzania kwa mustakabali wa umoja wa taifa letu!

Sio kwamba waliomtangulia hawakutamani kupeleka maendeleo walikozaliwa ila miiko na maadili ya kazi zao iliwasuta! Kodi tunalipa wote hivyo vipaumbele vipangwe kwa haki.

Mkuu hii mbegu aliyoipanda Magufuli tayari imeshamea. Yeye ndio amehujumu upinzani ili usiwepo nchini. Niliwahi kusema, watu wenye uelewa finyu ndio wanaona Magufuli anafanya sawa kuhujumu upinzani kwa kutumia madaraka yake, bila kujua akihujumu upinzani usiwepo, atasababisha upinzani sahihi wa sera na itikadi kuondoka, ila atatengeneza upinzani hatari kwa nchi wa ukabila na ukanda.

Mimi sio mtabiri, ila kwakuwa Magufuli ndio msimu wake wa mwisho madarakani, iwapo atakubali kishingo upande kutoka madarakani, basi ushindani utakaokuwepo ni wa kikabila na kikanda, na lengo litakuwa ni kuhakikisha anayeingia anapendelea kanda yao kimaendeleo. Nashangaa usalama wa taifa kutokuliona hili. Utawala huu rasmi umekuja kuligawa taifa hili. Muda ni mwalimu mzuri wa hili.
 
Back
Top Bottom