upendeleo kwa wanawake ni njia sahihi ya kuleta usawa na wanaume?

Majaribio ni kitu kizuri lakini kuna vitu havihitaji majaribio kama uongozi wa nchi. Tukiamuwa kuwapa uongozi kundi fulani eti kubadili mindset nahofu tutakuwa nyuma siku zote. Uwezo wa mwanamke au mtu mwengine yeyote hauji kwa kupewa upendeleo kwani upendeleo ni kuonyesha kasoro ya anaependelewa. Wanawake wetu wa Tanzania hawahitaji kupendelewa bali ni kupewa fursa sawa na wenzao wanaume. Tumeshuhudia huko nyuma wanawake ambao walionyesha uwezo wao si kwa upendeleo. Tulikuwa na wanawake kama Bi tit, Julie Manning na wengineo na kwa wa karibuni ni wanawake kama Mongella.
Okay na tutowe upendeleo kama sera yetu, sasa kwanini katila Baraza la Mawaziri wako wachache? Ni kiini macho kujidai kuwa tuwe sawa huku tukidharau hilo kwenye nafasi zilizo nyeti kama uwaziri, na vyombo vikuu vya utawala.
kweli tuwape fursa na sio upendeleo
 
huu ni ujinga na upungufu wa akili, hii awamu ya nne kweli ni ya wanwake( au ya kike) kama alivotabiri sheikh yahya, tunajaza madudu tu katika system itakuja kutucost kama vile kuungoa ukoloni, jamani hata vitabu vitakatifu havikulivalia njuga hili jambo, why twampa Mwenyezi Mungu masahihisho? Mwanamke kazi zake zipo wazi, kutokana na nyakati basi kama anaweza apambane, so muhimu ni kujitahidi kuchange mindset za watu na si kumzuia mwanaume mwenye uwezo asipande ili mwanamke apande, at the end of the day mwnamke hata kama ana uwezo zaidi ya mwanamme wake, mme ndo provider siku zote, its nature! lazma ukojoe, ule, uwe na love feeling, upige chafya hizi ni nature tulivoumbwa!si issues za siasa na kutafuta ujiko kwa mademu, viongozi wetu pambaf kabisa!!

Duu,you must be kidding!
 
mi siamini km kuna kitu mfume dume, nadhani ni fikra ambazo zimepandikizwa vichwani mwa watu, km hii hali ilikuwepo toka mwanzo basi niamini kuwa wanawake wamejiletea wenyewe kwani walionyesha kutokuwa na uwezo toka mwanzo, pointi ni kuwa kama ni ubunge au uwaziri basi mwanamke ni lazima aupate kwa njia sawa na mwanamme sio kupewa tu, hyo nadhani ndio itakuwa njia sahihi ya kuwaempower...
 
Back
Top Bottom