Upelelezi wakamilika kesi ya Aveva na Kaburu ya kutakatisha dola 300,000

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
AVEVA 2018.jpg


Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jana iliambiwa kesi ya Aliyekuwa Rais wa Simba, Evans Aveva na makamu wake Godfrey Nyange maarufu kama Kaburu ya kutakatisha dola za Kimarekani 300,000 umekamilika

Hata hivyo, Aveva alishindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake hiyo kwa kuwa bado amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Madai hayo yalitolewa na upande wa Jamhuri jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Alidai kuwa mshtakiwa wa kwanza bado mgonjwa akiendelea na matibabu Muhimbili.

Hakimu alisema kesi hiyo itasikilizwa maelezo ya awali Aprili 5, mwaka huu.

Katika kesi ya msingi, vigogo hao wa Simba wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha dola za Marekani 300,000 (Sh. milioni 674.8 kwa kiwango cha ubadilishaji fedha cha jana).

Katika shtaka la kwanza ilidaiwa mahakamani hapo walipopanda kizimbani kwa mara ya kwanza Juni 29, mwaka jana kuwa Machi 15, 2016 washtakiwa wote kwa pamoja walighushi fomu ya kuhamisha fedha ya tarehe hiyo wakionyesha kwamba klabu ya Simba inalipa deni la dola za Marekani 300,000 kwa rais wake Aveva.

HAMISHA FEDHAKatika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa Machi 15, 2016 katika benki ya CRDB tawi la Azikiwe lililopo Ilala, jijini Dar es Salaam, Aveva aliwasilisha fomu ya kuhamisha fedha zilizoghushiwa ya terehe hiyo akinyesha kwamba Klabu ya Simba imemlipa dola za Marekani 300,000 huku akijua sio kweli.

Msigwa alidai katika shtaka la tatu, kati ya Machi 15 na Julai 29, 2016, washtakiwa wote wawili walikula njama ya kutakatisha fedha hizo huku wakijua zimetokana na nyaraka za kughushi.

Upande wa Jamhuri ulidai katika shtaka la nne, Machi 15, 2016 katika benki ya Barclays Tanzania Limited, tawi la Mikocheni, Wilaya ya Kinondoni Aveva alihamisha dola za Marekani 300,000.

Shtaka la tano, ilidaiwa kuwa Machi 15, mwaka 2016 katika benki ya Baclays tawi la Mikocheni, Kaburu alimsaidia Aveva kupata dola za Marekani 300,000 wakati akijua zimetokana na zao la uhalifu.

Washtakiwa wote walikana mashtaka yao lakini kwa kuwa mashtaka ya kutakatisha fedha hayana dhamana kwa mujibu wa sheria, walinyimwa.


Chanzo: Nipashe
 
Hivi Hans Pope aliponaje kwenye hili saga la kutakatisha pesa?

Hiyo kesi ni rahisi tu. Aveva akiri kosa alipe milioni 200 aachiwe huru.

Awe kama Ndama Mtoto Ya Ng'ombe. Maana hiyo kesi haina dhamana. Otherwise watatumia muda mrefu mahabusu.
 
Hivi Hans Pope aliponaje kwenye hili saga la kutakatisha pesa?

Hiyo kesi ni rahisi tu. Aveva akiri kosa alipe milioni 200 aachiwe huru.

Awe kama Ndama Mtoto Ya Ng'ombe. Maana hiyo kesi haina dhamana. Otherwise watatumia muda mrefu mahabusu.
Hans Pope usimchukulie poa.........labda umzungumzie yule wa vibali vya sugar!
 
Hivi Hans Pope aliponaje kwenye hili saga la kutakatisha pesa?

Hiyo kesi ni rahisi tu. Aveva akiri kosa alipe milioni 200 aachiwe huru.

Awe kama Ndama Mtoto Ya Ng'ombe. Maana hiyo kesi haina dhamana. Otherwise watatumia muda mrefu mahabusu.
Unajuwa Hans pope aliwai kuhukumiwa kifungo cha maisha kweny kipind cha Nyerere kuwa eti anataka kuipundua serikal ya Nyerere ...alikaa jela miaka 15 akaja kutolewa na Mwinyi....kizuri nikuwa Familiya yake ninzuri kiuchumi ...na Mwinyi alimpa back up kubwa baada yakutoka kifungoni...kwaiyo sahv anaishi kwa kimakini sana ...Jela alikaa sana.

Kwaiyo iyo kesi yakina Aveva awez kuwemo
 
Back
Top Bottom