Troll JF
JF-Expert Member
- Feb 6, 2015
- 7,804
- 12,224
Polisi wameenda kupekua nyumbani kwa Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu , wakiongozana na mwanasheria huyo.
Tundu Lissu alikamatwa na Polisi akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na anakabiliwa na tuhuma za Uchochezi na Kumkashifu Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
UPDATE 1
Jeshi la Polisi limemaliza upekuzi waliokuwa wanafanya nyumbani kwa Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu wanaelekea Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.
Taarifa ya msemaji wa Chadema Tumaini Makene amesema Lissu anapelekwa polisi kwa ajili ya taratibu zingine za kisheria kuendelea ikiwa ni pamoja na dhamana yake ambayo kisheria iko wazi.
Amesema upekuzi uliofanyika ulihusu makosa mawili anayotuhumiwa nayo ya kumkashifu rais na Uchochezi kuhusu kushikiliwa ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 huko nchini Canada.
Tundu Lissu alikamatwa na Polisi akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na anakabiliwa na tuhuma za Uchochezi na Kumkashifu Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
UPDATE 1
Jeshi la Polisi limemaliza upekuzi waliokuwa wanafanya nyumbani kwa Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu wanaelekea Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.
Taarifa ya msemaji wa Chadema Tumaini Makene amesema Lissu anapelekwa polisi kwa ajili ya taratibu zingine za kisheria kuendelea ikiwa ni pamoja na dhamana yake ambayo kisheria iko wazi.
Amesema upekuzi uliofanyika ulihusu makosa mawili anayotuhumiwa nayo ya kumkashifu rais na Uchochezi kuhusu kushikiliwa ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 huko nchini Canada.