UPDP: Uzinduzi wa kampeni katika picha

Lukansola

JF-Expert Member
Sep 5, 2010
5,435
1,597
Nimesoma thread humu ndani kuhusu mgombea ubunge wa UPDP, kwa bahati nzuri nilifanikiwa kupata picha zake baada ya kufukuzia msafara wake kwa baiskeli, ulinipita nikiwa katika baa ya Kibo nikipata msosi. Alipofika aliuliza hapa ndio stendi yenu akajibiwa ndio, akauliza maliwatoni ni wapi, akaelekea huko akidai anakwenda kukagua, lakini nadhani alikwenda kuchimba dawa maana alikuwa chicha mbaya.

Nimewaletea picha hizo ili wale ambao kwa sababu moja ama nyingine hamkuweza kuziona msipitwe.






Msafara 1.jpg

Msafara wa Ali Kabaka, mgombea Ubunge kwa tiketi ya UPDP ukielekea kwenye viwanja vya kampeni eneo la stendi mjini Igunga tarehe 25/09/2011. Gari inayoonekana nyuma sio sehemu ya msafara huo.
 

Attachments

  • High Table.jpg
    High Table.jpg
    107.2 KB · Views: 235
  • Umati uliompokea 2.jpg
    Umati uliompokea 2.jpg
    154.7 KB · Views: 521
Nimesoma thread humu ndani kuhusu mgombea ubunge wa UPDP, kwa bahati nzuri nilifanikiwa kupata picha zake baada ya kufukuzia msafara wake kwa baiskeli, ulinipita nikiwa katika baa ya Kibo nikipata msosi. Alipofika aliuliza hapa ndio stendi yenu akajibiwa ndio, akauliza maliwatoni ni wapi, akaelekea huko akidai anakwenda kukagua, lakini nadhani alikwenda kuchimba dawa maana alikuwa chicha mbaya.

Nimewaletea picha hizo ili wale ambao kwa sababu moja ama nyingine hamkuweza kuziona msipitwe.






View attachment 37882

Msafara wa Ali Kabaka, mgombea Ubunge kwa tiketi ya UPDP ukielekea kwenye viwanja vya kampeni eneo la stendi mjini Igunga tarehe 25/09/2011. Gari inayoonekana nyuma sio sehemu ya msafara huo.

Kwa kweli niliona habari ya Mh.Ali Kabaka mgombea wa UDDP ilirushwa TBC a.k.a TV ya chama, jamaa alikua anaongea kwa sauti ya kilevi na alikua anaulizwa maswali na baadhi ya wapambe wake alikua nao kwenye msafara wake. Alizidi kudhihirisha kuwa amelewa pale aliposema kuwa atawawezesha vijana wawe wanalipwa 'dollar pound'ambapo sikuelewa anamaanisha nini. Akazidi kuwaambia kuwa anajua vijana wanateseka kwa kukaa vijiweni na kuchomwa na jua kama solar pannel na atawawezesha wawe na maisha mazuri na kuacha kukaa vijiweni kupigwa na jua kutwa nzima kama solar pannel. Pia alitanngaza sera yake ya kilimo kwa kusema yeye ataanzisha programme itakayoitwa ardhi kwanza na kilimo baadae.Mgombea alikua anongea kwa nmana ya kilevi na kihuni na kushangiliwa na kundi la watu walioonekana wamelewa chakari.Katikati ya mkutano MC alitangaza kuwa hou ni mkutano wa kipekee kwa kuwa kuna vinywaji na wahudhuriaji wanakaribishwa ila wanunue kwa hela yao na akasema zipo bia, soda na chips Kwa kweli UDDP wametia aibu ni kama mgombea wao alikua anaigiaza FUTUHI
 
attachment.php


kuna haja ya ku-redefine maana ya msafara! huu ndo msafara?
na kweli hii ni futuhi,hata kama ni comedi,the std was a bit too low for my liking!
afu mbona mikono wamefanya kama kunguru, ama ndo wanaashiria kuparua ccm?
jamaa hajui hata kama power tiller zimefail kabisa kwenye market,anasema hakuna mwananfunzi kwenda na jembe shuleni,atanunua for every skul!
 
Nisaidieni jamani mgombea ni yupi hapa????mwenye suti, mwenye kofia, mwenye tai au mwenye nguo ya kijani???
 
mbona meza yenyewe ya kijani?lakini dhamila ya kuzindui kampeni imefanikiwa.tumpongeze kwa kuzindua kampeni salama bila kuzungumzia watu.amefanya kampeni za kisitalaabu.mia
 
Hi ni aibu kubwa kabisa kwa Taifa letu kama wagombea ndio hawa hatuwezi kabisa kuleta mabadiliko yoyote,hii ni sawa na comedy ya akina masanja tena hii haina kiwango
 
Najaribu kutafakari Sir name ya huyo mgombea eti KABAKA! sipati picha!
 
Kwa kweli niliona habari ya Mh.Ali Kabaka mgombea wa UDDP ilirushwa TBC a.k.a TV ya chama, jamaa alikua anaongea kwa sauti ya kilevi na alikua anaulizwa maswali na baadhi ya wapambe wake alikua nao kwenye msafara wake. Alizidi kudhihirisha kuwa amelewa pale aliposema kuwa atawawezesha vijana wawe wanalipwa 'dollar pound'ambapo sikuelewa anamaanisha nini. Akazidi kuwaambia kuwa anajua vijana wanateseka kwa kukaa vijiweni na kuchomwa na jua kama solar pannel na atawawezesha wawe na maisha mazuri na kuacha kukaa vijiweni kupigwa na jua kutwa nzima kama solar pannel. Pia alitanngaza sera yake ya kilimo kwa kusema yeye ataanzisha programme itakayoitwa ardhi kwanza na kilimo baadae.Mgombea alikua anongea kwa nmana ya kilevi na kihuni na kushangiliwa na kundi la watu walioonekana wamelewa chakari.Katikati ya mkutano MC alitangaza kuwa hou ni mkutano wa kipekee kwa kuwa kuna vinywaji na wahudhuriaji wanakaribishwa ila wanunue kwa hela yao na akasema zipo bia, soda na chips Kwa kweli UDDP wametia aibu ni kama mgombea wao alikua anaigiaza FUTUHI

Wamepewa ruzuku ya kampeni?
Wanachezea muda na rasilimali nyingine za nchi....
 
Kwa nilivowaona jana ktk tbc hata mgombea alikua kalewa chakari,napia hata mwenyekiti wa wilaya wa updp alikua chicha vibaya,watapa kura kidogo za walevi wenzao,ni kichekesho kitupu na tutaona mengi ktk wiki hii ya mwisho ya kampeni igunga.
 
Mgombea ni huyo mwenye koti na suruali isiyo na mkanda, pamoja yote, maneno na ahadi zake zisitafsiriwe kirahisi, lipo tatizo la ajira na serikali inapaswa kuondoa matatizo ya wananchi na kama ikishindikana basi yeye ni mtu sahihi wa kuondoa shida hizo (maji nk), kaongelea kuhusu malipo ya dollar-pound kwa vijana watakaoajiriwa kupiga kupe ng'ombe, hapa cha muhimu ni upuuzi tunaoendelea kuushabikia wa kufanya manunuzi kwa pesa za kigeni na kuidharau shilingi yetu, chukulia mfano wa chuo cha imtu kinachotoza ada kwa $, yapo baadhi ya maduka leo unakuta bidhaa inauzwa kwa dola wakati wao kodi wanatozwa kwa shilingi, huu ni upuuzi na kama tukishindwa basi mgombea wa UPDP anaweza kuuondoa
 
Watu wa hivyo ndio CCM inawataka sana ndio maana TBC1 walifanya coverage ya nguvu. Upuuzi kama huu ni matusi kwa Watanzania wapenda mabadiliko.
 
Nadhanin ndiyo demokrasia hata kama ni unafiki au kutumwa lakini si umeonekana kwenye luninga?
 
Hi ni aibu kubwa kabisa kwa Taifa letu kama wagombea ndio hawa hatuwezi kabisa kuleta mabadiliko yoyote,hii ni sawa na comedy ya akina masanja tena hii haina kiwango

Kosa ni la wafadhili, wangetunyima kwanza zile pesa wanazoipa serikari kufanyia upuuzi huu basi kusingekuwapo na Comedy za hivi
 
Back
Top Bottom