Updates za Corona Tanzania

Inahitajika roho ngumu mno kumwamini mwanasiasa
IMG-20200325-WA0042.jpeg


Jr
 
Kuna kitu cha ajabu nimekiona leo na ni muhimu kukiweka hapa.
Kama tujuavyo shule na vyuo vimefungwa kuepusha uenezwaji wa corona.. Ni hatua nzuri ya hadhari.. Lakini hatua hii ikitumika vibaya tutamalizana
Huku Pwani kuna minada na magulio.. Na natambua ni nchi nzima. Japo sehemu zingine ni magulio tu bila minada inayoambatana na karamu za vilevi na nyama choma
Leo ilikuwa ni zamu ya Loliondo Kibaha na machinjioni pia Kibaha
Loliondo ni gulio na machinjioni ni karamu...
Maeneo haya mawili hukusanya watu wengi kwa wakati mmoja wanaotoka nje na ndani ya Kibaha.. Kuanzia wauzaji, wanunuzi, wapataji, wapashaji mpaka watoa huduma wengine
Kwa siku nzima kumekuwa na pilika za ingia toka kwenye hayo maeneo mawili
Watu wote hawa muda huu wamesharejea makwao kukutana na familia zao na kesho baadhi wataenda nyumba za ibada kusali

Najaribu kuwaza umakini wa serikali kwenye kuzuia mikusanyiko kipindi hiki.. Kama leo hii kuna wenye maambukizi kwenye hayo maeneo mawili niliyotaja.. Tutarajie maafa baada ya wiki mbili zinazokuja
Rai yangu ni moja... Kuna magulio na minada kila siku ya wiki.. Bado hatujachelewa sana.. Serikali iweke zuio la muda.. Tutaokoa wengi

Jr
 
*Kwa wale tunaofikiri wagonjwa 19 wa Covid 19 kwa Tanzania bado SIO SERIOUS!! Hebu tuangalie wenzengu wa nchi nyingine walikotoka wiki tatu zilizopita*

Italy
February 21 2020 - 21 cases
March 27 2020 - 86,498 cases

United States
February 21 2020 - 16 cases
March 27 2020 - 100,037 cases

France
February 26 2020 - 18 cases
March 27 2020 - 32,964 cases

Germany
February 25 2020 - 18 cases
March 27 2020 - 50,178 cases

Spain
February 27 2020 - 25 cases
March 27, 2020 - 64,059 cases

Iran
February 19 2020 - 5 cases
March 27 2020 - 32,332 cases

South Africa
March 1 2020 - 1 case
March 27 2020 - 1,170 cases

*Tupo pale wenzetu walipokuwepo wiki mbili tatu zilizopita.*
*Kama hatutajitahidi kujikinga nasi tutafika huko*.

*Watanzania wenzangu tujitahidi kuzuia muendelezo wa maambukizi ya Covid 19 kwa kuzingatia njia tunazoelekezwa na wizara.* .

*Ni jukumu lako wewe na mimi! Tuzingatie*

Jr
 
Hii ni kutufahamisha sisi kuwa pH ya virusi vya corona inatofautiana kutoka 5.5 hadi 8.5.

Wote tunahitaji kufanya, kupinga virusi vya corona, tunahitaji kuchukua zaidi ya vyakula vya alkali ambavyo viko juu ya kiwango cha juu cha pH cha Virusi.

Ambavyo ni:

* Limao- 9.9pH *
* Chenza- 8.2pH *
* Parachichi- 15.6pH *
* Vitunguu - 13.2pH *
* Maembe - 8.7pH *
* Tangerine - 8.5pH *
* Mananasi - 12.7pH *
* Dandelion - 22.7pH *
* chungwa - 9.2pH *

Unajuaje kuwa una coronavirus?
1. * Kuwashwa kwenye koo
2. * kukauka koo
3. * Kikohozi kikavu. *
4. Joto kubwa
5. kupumua kwa tabu

kwa hivyo unapoona vitu hivi haraka chukua maji ya moto kiasi weka limao kisha kunywa

Usibakie na habari hii peke yako. Sambaza kwa familia yako yote na marafiki. Mungu akubariki.

Jr
 
“Basi angalieni, siku zinakuja, asema BWANA, ambazo katika siku hizo halitaitwa tena Tofethi, wala Bonde la mwana wa Hinomu bali litaitwa, Bonde la Machinjo; maana watazika watu katika Tofethi, hata hapatakuwapo mahali pa kuzika tena."

'Yeremia 7:32'
IMG-20200401-WA0086.jpeg


Jr
 
Kuna muda nikikaa na kutafakari hizi takwimu. Nakosa tumaini la kesho kwa sisi Afrika ambapo tumeambiwa baada ya wiki tatu nasi tutapata kushuhudia kilele Cha Covid-19. Giants Kama Italy, UK, USA, Spain kwa siku wanaffariko watu sio chini ya 800+ kwa umahiri wao. Mungu atusimamie.

Sijui tukimbilie wapi.

Jirani zetu Kenya nao, naona Mambo yamewakalia vibaya. Pamoja na lockdown lakini new cases zinazidi kukuwa.
20200401-202539.jpeg
20200401-202559.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inahitajika roho ngumu mno kumwamini mwanasiasa View attachment 1398765

Jr
Hii ndiyo mfano wa deficity and insufficience ya sheria tunazotunga zinakuwa rules and siyo sheria. Sheria lazima iwe ama iangalie exceptions. Magonjwa ya milipuko siyo magonjwa ya kufedhehesha wala kubeza na hivyo kutangaza ilipasa kwa kuwa inaweza kuponya kuanzia familia yake, jiarani yake, wafanyakazi wenzake ama watu wengine tu. Hii sheria inafanya kuwe na deficity ya benefit ya sheria yenyewe katika circumstance ya magonjwa ya milipuko. Magonjwa ya milipuko yana pattern mbaya sana na hayajali na mtu yeyote ni susceptible. Tumeona duniani jinsi hadi wataalamu wa afya wamekwenda tena waliobobea katika virology specifically huyu CORONA wamekwenda. Sasa tunaficha kwa faida ya kuzuia maambukizi au kwa faida ya wizara ya afya au kwa faida ya mgonjwa dhidi ya umati wa wananchi wote? From layman point of view hili haliko sawa hasa katika magonjwa ya milipuko...hii rule irekebishwe iwe sheria including exceptions hizi. Sheria without exception is a blind sheria na hivyo haiwezi kuona haki, ikiwa kipofu atatakiwa kuona dunia itapita na vitu vyake vyote. Sheria inakuwa sheria ikiwa na makali yake, considerate, covering exceptions ili iweze kutoa haki. Hapa kwenye magonjwa ya mlipuko ... hii sheria imetunyima haki watanzania .. hata hii ya kujua tu .. ili kuchukua tahadhari. Tahadhari ni pana na kwanza inahitaji habari kamili na sahihi.. mfano sasa tunaangalia sana na kusema mkuu umetoka nchi zenye mlipuko .. tukupime na tunakushuku kwa hali ya juu zaidi. Sasa hii ni habari inavyoweza kusaidia dhidi ya tahadhari.. pamoja na mambo mengine mfano umri, magonjwa mengine (pre-existing disease conditions) na habari zote zinazopasa kujumuishwa katika tahadhari. Hii ndiyo habari kamili na sahihi. Vinginevyo umri wa mgonjwa pia ni habari ila si kamili, jinale nani, kabila gani, anaishi wapi anafanya nini, amepataje uambukizo, alitembelea maeneo gani kabla na baada ya uambukizo. Nadhani hili lipitiwe upya na waziri mwenye dhamana na awatendee watanzania haki kupitia bunge tukufu?.

Tuendelee na tahadhari, usafi, usafi, usafi, social distancing, stay alert and vigilant, tule milo kamili, tufanye mazoezi, tupumzike vya kutosha, tuwe na muda wa furaha kupunguza stress pia inapunguza kinga ya mwili,

ANGALIZO: Tusiwanyanyapae wale wanaopata maambukizo kwa kuwa siyo self infliction disease na nchi iendelee na mipango yake bora tunayoiona kila kukicha - usiku na mchana

Nawasilisha
 
Natambua umahiri wetu wa kuvifanya vitu serious kuwa mizaha. Natambua ujuzi wetu wa kuyageuza majanga kuwa manufaa ya kisiasa.

Hivi ni kipi kikubwa tumekifanya kama taifa cha serious kujikinga na hili gonjwa linalotaka kuwa janga la dunia?

Nimemsikia Waziri wa Afya akikutangazia umuhimu wa kutoshikana mikono wala kukumbatiana wakati wa kusalimiana kama ilivyo jadi yetu. Wanasiasa wakalibeba hili mzobe mzobe. Mengine yote sidhani kama yamepewa kipaumbele.

Waziri katangaza kila mkoa utenge maeneo maalum ya kuchunguza wenye dalili na viashiria vya huu ugonjwa.

Je, hili limetekelezwa?
Je, kuna vifaa ya kutosha kwenye hili?
Je, bajeti imetoka wapi?
Je, kuna wahudumu wa dharura wenye uelewa na huu ugonjwa wameandaliwa?
Je, sahihi ni kutenga vituo kila mkoa ama kila wilaya?
Je, mpaka sasa ni mikoa mingapi imelitekeleza hili?
Je, kuna changamoto yoyote?
Je, kuna kipindi maalum kwenye vyombo vya habari kutoa mapya ya kila siku kuhusiana na huu ugonjwa?

Hakika maswali ni mengi sana. Lakini nilichokiona kwenye huu ugonjwa ni mizaha na kukosa umakini. Hatuna takwimu rasmi zozote mpaka sasa za chochote kuhusiana na huu ugonjwa. Hatujaona umakini wowote kwenye maandalizi ya dharura. Chukulia mfano mkoa wa Pwani kutoka Mkuranga mpaka Bagamoyo utenge kituo kimoja tu cha ukaguzi wa corona, inawezekana kweli!?

Kinachopigiwa chepuo sasa ni kusalimiana bila kushikana mikono, eti kugongesha miguu. Mmh! Tumeiona kwa viongozi, lakini nyie msioshikana mikono sasa si mlikaa chumba kimoja kwa madakika mengi tu? Je, mlitumia viziba midomo na pua?

Hivi kwani corona ni ugonjwa wa ngozi? Iweje wachezaji uwanjani wazuiwe kusalimiana kwa kushikana mikono eti ni mojawapo ya kampeni ya kupambana na corona wakati huo huo wachezaji haohao watakuwa pamoja uwanjani kwa dakika 90+ wakishikana, wakivutana, wakiangukiana wakipumuliana? Vipi na wale mashabiki watazamani kwa maelfu walio majukwaani? Tuna abiria kwa maelfu wanasongana kwenye vyombo vya usafiri. Kwenye masoko. Kila mahali.

Bado hatuko serious na mizaha ndio imetawala kupitia siasa. Mungu pekee ndio anatubeba. Kitengo cha dharura kitaifa hakijasema chochote. Kipo kimya kabisa. Vyombo vyetu vya habari ni siasa na wanasiasa mwanzo mwisho. Viziba pua na midomo vimepanda bei maradufu. Box lilikokuwa linauzwa elfu 10 piece 50 sasa hivi linauzwa elfu 40 na hapo ugonjwa haujachanganya. Ukithibitika upo nchini na tukatakiwa kutumia hivyo vifaa tutafanyaje?


Jr
Common sense is not common anymore. Politics politics politics politics kwenye kilaaa jambo.

Kama mkuu mwenyewe amesema ni pepo usiriaz WA kulitatua hili tutaupata wapi?

Kunawa mikono ndio imekuwa mbiu...kunawa mikono kunawa mikono.. Lakini je nchi kama nchi tumejiaandaaje na hili janga?

Europe yote wanalia, America yote wanalia, Asia yote wanalia...

Sawa tukishanawa mikono ndo basi tena? Vipi mikusanyiko kwenye nyumba za ibada? Mipaka yetu? Japo kwenye suala LA Mipaka tumechelewa.

Elimu bado inahitajika kutolewa kwa raia, wapo wengi bado hawajachukulia usiriaz WA hii pandemic.

Mungu ibariki Tanzania. Mungu nibariki mimi na family yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom