mibiki mitali
JF-Expert Member
- Feb 5, 2018
- 238
- 392
Hali ya ndani ya mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa ni shwari
Leo tumepita getini bila bugudha na hakuna polisi wa nje zaidi ya hawa maalum wa mahakama
Hakika Jambo la jana kupigania haki ya mahakama na kutaka isimame kama mhimili huru ni nzuri sana
Jopo la mawakili wetu wa utetezi (mawakili wa Freeman Mbowe na wenzake) kama kawaida yao, limefika on-time, Mapema sana ikiwa sifa yake kuu nidhamu, Ushirikiano, upendo na kwenda na muda, pia kusikiliza na kujali hisia na sauti za ndugu, jamaa, marafiki wa wateja wao (watuhumiwa)
Ndugu zangu mnaouliza kuhusu shahidi wa leo ni nani, hakika wasikilizaji hatuwezi kufahamu. Hiyo ni kazi ya Jamhuri kuwasilisha jina la shahidi wao mbele ya mahakama kati ya wale mashahidi 24 waliotajwa kwenye preliminary hearing...
Hivi sasa ni saa 4 asubuhi na dakika zake 19 kwa saa za Afrika ya mashariki, bado mheshimiwa Jaji na mawakili wa upande wa Jamhuri (serikali) hawajaingia ndani ya chumba cha mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa. Mahakama sasa imejaa TOP!
Pia, tunawashukuru jeshi la polisi kutoka moyoni kabisa, mmepungua ndani ya chumba cha mahakama, mbarikiwe.. Eeh! Mmeona watu wameingia wenyewe mahakamani, wamejipanga wenyewe na sasa wanasubiri mahakama ianze. SISI ni wastaarabu na tunahubiri ustaarabu kila siku #MboweSioGaidi
Hivi sasa ni saa 4 na dakika 25 saa za Afrika ya mashariki bado mawakili wa serikali na mheshimiwa Jaji hawajaingia ndani ya chumba cha mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa..
Pamoja na kwamba polisi leo sio wengi kama siku zote, lakini kuna mzozo umeibuka hapa Mahakamani. Wananchi wanasema wamekosa nafasi za kuketi, hivyo wanaomba askari polisi wapungue mahakamani, wakaimarishe ulinzi wa raia na mali zao, ili nafasi zipatikane nyingi. Bado wapo!
Askari mmoja hapa anahamaki na kusema polisi na usalama nao wanayo haki ya kusikiliza mwenendo wa kesi maana ni open court na wanahoji kwamba tunapata wapi haki ya kuipangia mahakama nani wa kuingia na kukaa ndani? Swali hilo ukiwauliza wao kwanini walituzia jana, hawana jibu?
Raia bado wanasisitiza askari wasimame na kupungua mahakamani ndani, walinde watu na mali zao, ili wananchi wapate nafasi ya kuketi. Wananchi wanawakazia macho na kuwatambua. Lakini tunawaeleza wananchi watulie, waache askari hao wafuatilie kesi. Wasipate sababu kwamba VURUGU..
Hivi sasa ni saa 4 na dakika 53 kwa saa za Afrika ya mashariki, bado kesi inayowahusu Freeman Mbowe na wenzake watatu haijaanza, tunamsubiria mheshimiwa Jaji na mawakili wa serikali waingie ndani ya chumba cha mahakama.
Hivi sasa ni saa 5 na dakika zake 6 saa za Afrika ya mashariki.
Hali ya eneo la mahakama ni shwari kabisa, ni kata ya Sinza, wilaya ya Ubungo, Mkoani Dar es Salaam
Hali ya hewa ni mawingu kiasi na nyuzi Joto 27.7 inayoruhusu kabisa shahidi kuendelea na kesi, bila visingizio!
Pamoja na mheshimiwa Jaji kusisitiza Jana kuwa kesi ianze leo saa 4 kamili Kufuatia ombi la mawakili wa serikali, Lakini mpaka sasa, ni 5 na dakika 15 kesi bado haijaanza, lakini hatuelewi, labda sababu zilizo nje ya uwezo wao. Tuendelee kuwa na subira, maana yavuta kheri..
Mstari wa pili kutoka mwisho, wameketi waandishi wa habari (leo tupo nao live), Wameingia Kwa wingi sana kuliko Siku zote (inspiration), Leo na wao wamenufaika na msimamo wa Jana. Wabarikiwe.
Mstari wa mwisho (Backbench) wameketi watu mchanganyanyiko wakiwepo Polisi na TISS.
Sema kwa sauti mbowe sio gaidi
Unpopular opinion: wewe unadhani kwa kuchelewa huku mawakili wa serikali kuingia ndani ya chumba cha mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa, Je, wanamshauri DPP aachane na hii kesi dhidi ya Freeman Mbowe na wenzake maana wanajua #MboweSioGaidi, namna gani?
Jopo la mawakili wa utetezi
1.Peter Kibatala
2.Jeremiah Mtobesya
3.Jonathan Mndeme
4.John Malya
5.Evaresta Kisanga
6.Hadija Aron
7.Maria Mushi
8.Gaston Garubindi
9.Seleman Matauka
10.Ferdinand Makore
11.Dickson Matata
12.Rita Ntagazwa
13.Alex Masaba
14.Michael Mwangasa
Habari njema sana, ule mtiti mdogo wa wananchi umesaidia benchi lilikuwa reserved kwa makarao, wameanza kukaa familia na ndugu wa watuhumiwa..
Ubishi na makavu yanasaidia sana.. Tusiache kuongea na kupiga kelele kuhusu haki zetu wakati wote ndugu zangu. Msiache kuongea.
Jopo la mawakili wa utetezi (wanaitwa mawakili wasomi, utake usitake), yaani mawakili wa Freeman Mbowe na wenzake wakijadiliana jambo la kitaalam.. Unaweza kuwapa jina, hebu pendekeza jina, hii timu yao inapaswa kupewa jina gani?
Pamoja na kwamba watuhumiwa wamefikishwa mapema (tangu saa 3 asubuhi) na mawakili wa utetezi kufika mapema ndani ya chumba cha mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi, bado mawakili wa serikali hawajafika. Hivi sasa ni saa 5 na dakika 29 saa za Afrika ya mashariki
Shukrani za pekee leo zimuendee Wakili Gabriel Fikirini ambaye kafika mahakamani kwa mara ya kwanza akisafiri kutokea Jijini Mwanza kwa ajili ya kuongeza nguvu kwenye kesi ya Freeman Mbowe na na wenzake..
Wakili Deogratius Mahinyila (@AdvMahinyila) aliyetoka Jijini Dodoma hadi Dar es Salaam kuongeza nguvu tangu wiki iliyopita.. Niliwapa simulizi yake kwa ufupi, niwape tena? Umri wake ni mdogo mara 3 ya umri wa Humphrey Polepole na mara 5 ya umri wa Mzee Kabudi.
Wakili Deogratius Mahinyila (@AdvMahinyila) atakumbukwa akiwa mgombea wa udiwani kupitia Chadema Dodoma, kata ya Berega, alishitakiwa kwa makosa uhujumu uchumi, akiwa gerezani, Isanga (gereza katili) akafanya mitihani ya uwakili na kufaulu kuwa wakili wa mahakama kuu.
Mambo vip mkuu.
How was the case chief
====
Jaji: Mimi nimepata nafasi ya kutafakari , nilianza kwenye hoja iliyoibuliwa na wakili wa serikali, kumbukumbu za mahakama zinaonyesha Kibatala alisema kwa niaba ya Mawakili wote na Kwa niaba ya Washitakiwa wote siku hiyo ya 15.09.2020 uwakilishi ilikuwa kwa mawakili wote na kwaNiaba ya washtakiwa wote.
hivyo utenganisho inaanza Leo
ni maamuzi yangu kuwa mahojiano yaliyofanywa na Wakili Kibatala na Wakili Mtobesya kwa niaba ya Mawakili wote na washtakiwa wote
hivyo basi sioni sababu ya kumuita tena shahidi wa kwanzaJaji: Hivyo naangiza kuendelea na shahidi wa pili aitwe sasa tuweze kuendelea....
Jaji: katika Mwenendo wa Mahakama nimeondoa kuwa Kibatala ni Wakili wa mshtakiwa wa 4 kwa siku ya tarehe hiyo ya 15.. Kibatala aliwakilisha washtakiwa wote kwa niaba ya mawakili wote..Jaji anamuita Shahidi
Shahidi anaingia anajikwaa
Jaji: pole sana
Shahidi: naitwa Inspector Mahita
Jaji: wewe ni dini gani?
Shahidi: ni Muislamu
Jaji: unaweza kuapa?
Shahidi: Wallah Wabillah nathibitishaWakili wa Serikali : Shahidi ieleze Mahakama wewe ni Mkazi wa wapi
shahidi: Mkazi wa Morogoro
wakili wa Serikali: Unafanya kazi gani
Shahidi: Polisi
wakili wa Serikali: kabla ya 2021 leo ulikuwa wapi?
shahidi: nilikuwa msaidizi Ofisi ya Upelelezi Arusha wakili wa Serikali umenza lini Kazi ya Upolisi
Shahidi: 2010
wakili wa Serikali: katika Idara ya upelelezi huko Polisi upo tangu lini?
shahidi: Takribani miaka 8
wakili wa Serikali: Ukiwa msaidizi wa upelelezi majukumu yako ni yapi?shahidi: upelelezi wa Makosa ya jinai, ukamataji wa watuhumiwa, Kusimamia Askari ambao wapo chini yangu, Kupokea maelekezo ya Viongozi wangu, kufanya Upekuzi, kufanya escort za watuhumiwa, lengo la msingi Kuzia na kupambana na uhalifuwakili wa Serikali: nitakuuliza Mnamo tarehe 04 Mwezi 08 2020 tarehe hiyo ulikuwa wapi?
shahidi: nilikuwa kituoni natekeleza Majukumu yangu kama kawaida
wakili wa Serikali: kituo gani?
Shahidi: kituo cha kati
wakili wa Serikali: ieleze Mahakama 04.8.2020 jioni ilikuwajeshahidi: nilipigiwa simu na afande wangu ACP Ramadhan Kingai
wakili wa Serikali: eleza alikupigia simu akisemaje
shahidi: aliniambia niende ofisini kwake
wakili wa Serikali: eleza ulivyo tekeleza
shahidi: nilifika ofisini kwake
wakili wa Serikali: alikupa malekezo gani?shahidi: kuna kazi na Askari nitaondoka nao, kuna kazi na suala la kufuatilia
wakili wa Serikali: kitu gani kingine alikueleza?
shahidi: aliniambia niandae Askari wengine
shahidi: tuliaanza safari tukiwa dereva wake Constable Azizi
wakili wa Serikali: mlisimama wapi?shahidi: Polisi Arumeru, wilaya ya Usa river
wakili wa Serikali: Mkaelekea wapi?
shahidi: tulikuwa tunaelekea Kilimanjaro tukasimamama kituo cha USA river wilaya ya Arumeru
Jaji: mwanzo umeongea tofauti, umechanganya?
wakili wa Serikali: rudia Vizuri
shahidiolice Usa riverwakili wa Serikali: Polisi Usa river kilitokea nini?
shahidi: tulishika wote tukiwa na Afande Kingai tukapata Briefing ya kazi
wakili wa Serikali: Briefing uliyopewa ilihusu kazi gani?
Shahidi: Briefing niliyopewa ni kwamba kuna Kikundi kina panga kufanya matukio ya kigaidi
Shahidi: maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Arusha, Kilimanjaro, Dar es Salaam na Mwanza na pia kikundi hicho kilikuwa na nia ya kumdhuru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya
wakili wa Serikali: Elezea sasa mkafanyeje?shahidi: kwa kuwa kikundi hicho kilikuwa Mkoa wa Kilimanjaro Wilaya ya Moshi Mjini kwenda Kuwamakata
wakili wa Serikali: baada ya briefing kitu gani kiliendelea?
shahidi: tuliendelea na safari na tulifika majira ya Saa 2 Usiku. tukaendelea na upelelezi kuwakamata watuhumiwawakili wa Serikali: mliendelea na upelelezi mpaka muda gani?
shahidi: ilipofika majira ya saa 6 tukiwa tumewakosa ikabidi tubreak..
wakili wa Serikali: ieleze mahakama sasa tarehe 05 Mwezi wa 8 2020 mlifanya nini!shahidi: ilikuwa muda wa asubuhi tuliendelea kusubiri taarifa ambazo afande alikuwa akizopokea na ilipofika Saa 6 akaniambia kuwa watuhumiwa tuliokuwa tunawatafuta wameonekana Maeneo ya RAU MOSHI..
wakili wa Serikali: Rau ipo Maeneo gani?
shahidi: ipo kama unaelekea Key Hotelwakili wa Serikali: ifahamishe mahakama hatua mlizo chukua ni zipi.
shahidi: kwanza tuliuliza afande hao tunaoenda kuwakamata muonekano wao ukoje? Afande akasema mmoja alikuwa amevaa Shati, Mmoja alikuwa amevaa kama Kitenge na Mtuhumiwa wa tatu alikuwa amevaa Jezi ya mpira..wakili wa Serikali: watu mliotakiwa kuwakamata ni wangapi?
shahidi: watu watatu kwa mujibu wa Afande
wakili wa Serikali: baada ya hapo?
shahidi: tulifika maeneo ambayo walikwepo tukiwa na gari yetu yenye tinted, tuka Drop Section ya kwanza ambayo alioongoza Afande kingaiShahidi: section ya pili nili' drop mimi na Afande Francis na gari
timu ya kwanza ilikuwa inaelekea kwa watuhumiwa.
watuhumiwa walikuwa wameiona, watuhumiwa wawili walianza kutoka wakielekea nilipo mimi..
wakili wa Serikali: eleza uliwatambuaje.shahidi: section ya kwanza ya Afande Kingai ilivyotoka iliwafanya watake kukimbia, ilibidi kuwasimamisha kutaka kujiridhisha
wakili wa Serikali: ifahamishe Mahakama kwa namna gani uliwasimamisha
shahidi: nikawasimamisha kwa Sauti kali "Simama hapo chini ya ulinzi"wakili wa Serikali: baada ya response yako hiyo walifanya nini?
shahidi: walisimama, wakaamriwa kuweka mikono juu wakatii..
wakili wa Serikali: kitu gani kilifuata?
shahidi: nilijitambulisha, naitwa Inspector Mahita natokea Central Arusha nafanya kazi kwenye kikosi Maalumwakili wa Serikali: Baada ya kuwatambulisha?
shahidi: niliwaonya wakiwa wawili kuwa wanatuhumiwa kula njama za kutenda matendo ya ugaidi
wakili wa Serikali: wenzenu wakina Kingai wakati huo walikuwa wapi?
shahidi: walikuwa wanakuja, sababu walikuwa umbali mrefuShahidi: kingai akatoa order kwa Jumanne wapekuliwe
wakili wa Serikali: shahidi sasa ieleze Mahakama Jumanne alitekeleza vipi Maelekezo ya Kingai?
shahidi: alitekeleza, kuna mama mmoja alikuwa anashuhudia pale, aliwaambia wasogee karibu washuhudie anachokifanya..Shahidi: huyo mama alikuwa anauza supu..
wakili wa Serikali: ieleze Mahakama taratibu za Upekuzi.
shahidi: Mmoja ali amriwa asimame juu ambaye baadae nikaja kumtambua alikuwa anaitwa Adamoo Adama kasekwa
wakili wa Serikali: wakati huo ulikuwa unafanya nini?shahidi nilikuwa na afande Jumanne
shahidi: wakati afande anampekua upande wa kushoto wa suruali yake alikuta Luvern Pistol A5340
wakili wa Serikali: kitu gani kingine?
shahidi: aliendelea kumkagua mifukoni akamakuta na kete 58 ambazo baadae zilijulikana ni madawa ya kulevyawakili wa Serikali: kitu gani kingine?
Shahidi: alikuwa na simu yake
wakili wa Serikali: ieleze mahakama ndani ya Pistol palikuwa na kitu gani?
shahidi: ndani ya magazine palikuwa na risasi 3
wakili wa Serikali: baada ya upekuzi nini kilifuata?shahidi: Upekuzi uliofuatia ulikuwa wa Adam Ling'wenya. yeye wakati anapelekuliwa alikuwa na kete 25
wakili wa Serikali: mbali na kete ni kitu gani kingine?
shahidi: na simu yake
wakili wa Serikali kingine unachokumbuka
Shahidi: Hapana kwa sasa..wakili wa Serikali: mashahidi waliokwepo Unawakumbuka, ieleze mahakama majina yao..
Shahidi: nakumbuka majina yao ya kwanza ya Anita na Esther
wakili wa Serikali: baada ya Upekuzi nini kulifuata
shahidi: naona...
wakili Peter Kibatala: Objection aseme ni hear say au anakijuaJaji: mmeelewa?
wakili wa Serikali: ndiyo
shahidi: baada ya Upekuzi
shahidi: tulianza kujaza Certificate of Seizure
wakili wa Serikali: baada ya kusaini kilifuata nini?
wakili Peter Kibatala: Objection hajasema ilisainiwa
Jaji: ni kweli hajasema wakili wa Serikali?wakili wa Serikali: samahani mheshimiwa
shahidi: Baada ya kujaza Certificate of Seizure ilisainiwa na watuhumiwa
wakili wa Serikali mkaelekea wapi?
Shahidi: tukaelekea kituo cha kati Moshi
wakili wa Serikali: wakati mnaelekea Moshi Kitu gani kilifuata?shahidi: yalikuja magari 2 tukapanda
wakili wa Serikali: mkaelekea wapi?
shahidi: kituo cha kati Moshi
wakili wa Serikali: wakati mnaelekea Moshi kitu gani kilifuata?
Shahidi: Afande kingai aliwauliza kwa taarifa alizonazo walikuwa 3, je 3 Moses Lijenje yupo wapi?wakili wa Serikali: Majibu yao yalikuwa ni yapi? +
shahidi: walisema kweli walikuwa naye na wakakubali kutuonyesha alipokuwa, kwani walikuwa naye palepale wakati tunawakamata
shahidi: Afande kingai alitoa maelekezo Afande Francis aendelee kuwachukua maelezo..Shahidi: sisi tuliokuwa kwenye gari jeupe na Afande kingai pamoja na Jummane tukawa tumerudi RAU madukani kumtafuta mtuhumiwa mwingine Moses
wakili wa Serikali: nini sasa mlichofanya?
shahidi: baada ya kurudi tulimkosa..
Shahidi: lakini Adam na Ling'wenya wenyewe wakasema huyu kuna vijiwe vyake tulivyokuwa tunazunguka wote Moshi
wakili wa Serikali: baada ya kutoka Rau mkaelekea wapi?
Shahidi: tukawa tunazunguka maeneo mbalimbali. ndani ya Moshi Mjini, KCMC, Majengo yaani vijiwe vijiweShahidi: baadae tukaenda mpaka Boma Ng'ombe na Aishi..
Jaji: hebu rudia maeneo mliyozunguka ndani ya Moshi
shahidi anarudia.......
wakili wa Serikali: kwanini mlikuwa mnazunguka maeneo hayo?
shahidi: watuhumiwa wenyewe walikuwa wanatuongoza
wakili wa Serikali: ikawajeShahidi: tulimaliza saa nne au saa tano usiku
wakili wa Serikali: nini kilifanyika?
Shahidi: tulikaa pale Boma kwa sababu tulijua atapanda vibasi hadi saa 2 asubuhi. Tulikaa Boma Mg'ombe tukafanya kikao cha kipolisi asubuhi kwenye saa 2 mpaka saa 3. tukaelekea kituo cha katiwakili wa Serikali: mlielekea Kitio cha kati kufanya nini
shahidi: kuwaweka watuhumiwa mahabusu
wakili wa Serikali: siku inayofuata nini kilifanyika?
shahidi: saa 11 kuelekea saa 2 kwenda kuwafuata watuhumiwa mahabusu, kwa Afande alisema tuelekee Stand kuuShahidi: tulienda na watuhumiwa kwa sababu wao ndiyo wanamfahamu, na tulikaa Stand tukijua anaweza kuwa anataka kwenda kusafiri na kukaa stand bila mafanikio
wakili wa Serikali: nini kilifuata?
shahidi: tukielekea maeneo ya pale stand sisi na watuhumiwa tukaenda kupata chaiamejificha na baadae tukaeleka Sakina Arusha
wakili wa Serikali: ifahamishe kama Mlifika Arusha, Arusha mlipita maeneo gani?
shahidi: kwakuwa tulikuwa kwenye leading investigation moja kwa moja tulienda Sakina na hatukumkuta tukaona wanatupotezea mudawakili wa Serikali: baada ya kupata chai nini kilifuata?
shahidi: hoja iliibuka kwa watuhumiwa kuwa Moses ana dada yake Arusha
wakili wa serikali: baada ya hoja hiyo nini kilifuata?
shahidi: Afande Kingai alisema tupite kwanza kwenye vijiwe tulivyopata Jana anaweza kuwawakili wa Serikali: baada ya ya kuwakosa mlielekea wapi?
shahidi: tukielekea Moshi na Afande kingai akatoa malekezo kuwa kwakuwa kesi tunayoifuatilia imefunguliwa Dar es Salaam
wakili wa Serikali: unasema alitakiwa kuelekea Dar es Salaam kwa ajili ya nini?shahidi: kwa sababu Kesi ilifunguliwa Dar es Salaam tulitakiwa twende Dar es Salaam na kwa sababu matukio yalikuwa yafanyike sehemu mbalimbali ikabidi twende Dar es Salaam..
wakili wa Serikali: ieleze mahakama chakula cha mchana mlipata wapi?wakili Peter Kibatala: Objection anafundisha cha kuongea
Jaji: Objection izingatiwe
wakili wa Serikali: nimesikia Mheshimiwa Jaji
wakili wa Serikali: baada ya ya kuelekea Dar es Salaam nini kilifuata?shahidi: tukiwa njia panda Himo gari yetu ilipata Break Down, afande akaita gari nyingine na pale pana kuwa papo bize cha kula cha usiku ilibidi tupate pale.
wakili wa Serikali: kwa kuwa unasema mlipata Break Down ni majira gani mliondoka Pale?shahidi: tuliondoka majira ya saa 2 Usiku na Kufika Dar es Salaam Majira ya saa 11 Alfajiri siku ya tarehe 07
Jaji: Mlifika Dar es Salaam saa ngapi?
shahidi: saa 11 Alfajiri
wakili wa Serikali: nakurudisha nyuma mlipokuwa njia panda Himo unasema mlikula je ni akina nani hao?shahidi: sisi na Convoy yetu yote pamoja na watuhumiwa
wakili wa Serikali: baada ya kufika Central nini kilifuata hiyo saa 11?
shahidi: afande kingai alitupatia Break akatuambia Saa 1 turudi pale Central..
wakili wa Serikali: saa 1 kitu gani kilifanyika?shahidi: afande alitupa maelekezo tutoke kituoni pale Central na Goodluck na Asst. Inspector Swila kuendelea na upelelezi
Jaji: Mlipewa Maelekezo gani?
shahidi: Afande kingai alitupa maelekezo tutoke tuendelee kufanya upelelezi kuhusiana na watuhumiwa ambao bado hawajakamatwawakili wa Serikali: shahidi ieleze mahakama sasa muda wote mlipokuwa mnatoka na watuhumiwa, wakati huo walikuwa kwenye ulinzi wa nani?
shahidi: wakati huo mimi ndiyo nilikuwa nasimamia ulinzi
wakili Serikali: kwakuwa wewe ndiyo ulikuwa na watuhumiwa wakati wote ieleze Mahakamawalikuwa na hali gani?
shahidi: walikuwa na hali nzuri
wakili wa Serikali: sawawakili wa Serikali: Shahidi nakupeleka pia, kwamba Tarehe 7 mlikuwa Dar es Salaam na kwamba mlipewa maelezo kuendelea na upelelezi Je, ni lini tena uliitwa tena kushughukika na watuhumiwa??
shahidi anasita.. anasita tena hapa..
Namna gani pale..Jaji: anasema endeleeni wewe na anaekuongoza ni suala lenu
shahidi: niliitwa 08.8.2020 kituo cha Central na nilipofika nilikutana na Afande kingai na Jopo zima la timu na nilipewa malekezo kuwa watuhumiwa wale wote tuwatie Central pale lockup au tuwapeleke kituo cha MbweniShahidi baada ya kusitasita, sasa anaendelea hapa..
Anasema, kwa sababu ya msingi ni kwamba watuhumiwa kwa mafunzo waliyopitia inapaswa tuwapeleka kituo kingine
Jaji; rudia sababu ipi iliwafanya muwatoe Central police Dar es Salaam tafadhali ndugu shahidi..shahidi: afande Kingai alisema kutoka watuhumiwa wenyewe mafuno yao na Makomandoo, walikuwa ni Makomandoo wa JWTZ na kwamba Complexity ya upelelezi wenyewe sababu watuhumiwa wengine tulikuwa bado hatujawapata
kwamba tuwapeleke kituo cha Mbweni kwa a sababu Kuna Informationtulikuwa hatujazimalizia
wakili wa Serikali: kituo cha Mbweni kipo wapi?
shahidi: kipo Wilaya ya Kinondoni
wakili wa Serikali: mliowapeleka tofauti na wewe mlikuwa na akina nani?
Shahidi: ASP Jumanne, Asst. Inspector Swila, Detective Constable Goodluckwakili wa Serikali: unakumbuka Ilikuwa majira gani
shahidi: Saa nne kuelekea saa tano
Jaji: kama unaweza kufafanua ilikuwa ya Asubuhi au Jioni?
shahidi: ilikuwa Asubuhi?
wakili wa Serikali: Shaidi yapo malalamiko kuwa Watu hawa waliteswa!
shahidi: Hapana, hawakuteswawakili wa Serikali: walipata Treatment gani?
shahidi: walipata Treatment ya Dignity na Respect
wakili wa Serikali: ni hayo tu mheshimiwa Jaji
Jaji: Utetezi Je, mpo tayari kuendelea?
wakili Peter Kibatala: naomba kwanza tushauriane na wakili wa Mshtakiwa ili aanze..KIBWAGIZO..
Kwa hiyo askari polisi wa kikosi cha ACP Ramadhan Kingai walikunywa chai na magaidi, kiroho safi baada ya kupata breakdown eeh! Bado hawa magaidi rojo-rojo kweli, sio kama Osama Bin LADEN.. MAGAIDI??? Face with tears of joy
Tuendelee...Kimya kidogo, kisha anasimama wakili Nashon Nkungu..
Wakili Nashon Nkungu: nakumbuka tarehe 08 ulitoa maelezo Central police?
shahidi: sahihi kabisa
wakili Nashon Nkungu: anampelekea shahidi maelezo hayo..
Shahidi: anayakana kuwa siyo ya kwake sababu hajaya saini..Wakili Nashon: anamuomba sasa Jaji apewe rasmi maelezo hayo mahakamani ambayo shahidi wa pili aliyoyatoa kwa RCO Ilala..
wakili wa Serikali: anamuomba Jaji kuwa wakili aanze kwanza kusema anachotaka kabla ya maelezo..
Jaji: anauliza kwa tashwishwi, Maelezo yapo au hayapo?wakili wa Serikali wanakunali kuwa maelezo hayo yapo Mahakamani..
Jaji anamueleza wakili Nashon Nkungu kuwa Endelea kutengeneza msingi wako, na kisha uyatumie hayo maelezo...wakili Nashon: Shahidi Je, ni kweli maelezo uliyoyatoa katika statement yake ya RCO Ilala kuwa kulikuwa kuna kazi unaenda kufanya Moshi Baada ya kupigiwa na Afande kingai na kuwa ulikuwa hufahamu unaenda wapi tofauti na ulichosema kwenye statement yako?shahidi: ni kweli sikuwa najua mpaka nilipofika Arumeru
wakili Nashon: Je shahidi unaweza kueleza upande ambao mshtakiwa aliposachiwa alitolewa hiyo pistol kwa Demonstration?
shahidi anasimama anafanya kwa kitendowakili Nashon: kati yako na Kingai nani alikuwa na nafasi nzuri ya kuwaona watuhumiwa?
shahidi: wote
wakili Nashon: kwa hiyo ni sahihi nikisema kuwa alichokiona kingai ndicho ulichokiona wewe?
shahidi: kama nilivyosema mimi nilitokea kwa mbele..wakili Nashon: ieleze mahakama kuwa kati ya wewe na Kingai nani anaidanganya Mahakama, Sababu Kingai anasema mliwakamata wakati wanakunywa supu wewe unasema wakati wanatembea..
shahidi: Mimi sijui Kingai katoa ushahidi gani, maana sikuwepo..Nashon: Je shahidi unamfahamu BWIRE?
shahidi: siwezi kujibu
Jaji: Shahidi, unapswa kujibu
shahidi: sikuwa namfhamu kwa tarehe hiyo
Nashon: unaifahamu Police Notebook
shahidi: nafahamu
Nashon: unajua ulitakiwa kuna nayo mahakamani?
shahidi: taarifa ya siri mali ya polisiwakili Nashoni anakaa anamkaribisha wakili John Mallya
Malya: Shahidi ni sahihi Polisi wanapima Afya mara kwa mara?
shahidi: hiyo ni Jambo binafsi
Jaji: Shahidi Jibu tafadhali kama unafahamu au hujui
Mallya: umefanya kazi na Kingai kwa muda gani?
shahidi: kwa Miaka 3 au 2wakili Mallya: kwa hiyo nikisema Kingai ana matatizo ya kusahau au kupoteza kumbukumbu ni sahihi?
shahidi: siwezi kujibu
Jaji; toa JIBU
shahidi: sifahamu
Wakili Mallya: kwa hiyo nikisema Kingai ana kumbukumbu NZURI napatia.?
Shahidi: ndiyo!wakili Mallya: umeeleza katika msafara wemu mlianzia Moshi Je akija mtu akisema mlianzia Boma Ng'ombe atakuwa ni muongo?
Shahidi: Sifahamu.
wakili Mallya: unapswa ujue kwa sababu ulikwepo kwenye msafara..
shahidi: Ndiyo atakuwa anasema uongo..wakili Mallya: Umesema kuwa mliwapa chakula watuhumiwa ila hukutaja aina ya chakula wa kiasi cha chakula
shahidi: ndiyo
Wakili Mallya: Umezungumzia kuhusu kituo cha Polisi Central
shahidi: ndiyo
Wakili Mallya: Je ni Kwei pale kuna huduma zote ikiwemo mahabusu?
shahidi ndiyowakili Mallya: pale Central kuna polisi wengi kuliko Mbweni
shahidi: sahihi kabisa
Mallya: kuna Ofisi ya RPC ILALA?
shahidi: sahihi Kabisa
wakili Mallya: kuna ZCO?
shahidi: sahihi kabisa
Mallya: kuna Mkuu wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam?
shahidi: sahihi Kabisawakili Mallya: Je hawa polisi wote tuliowataja kule Mbweni Wapo?
shahidi: Mheshimiwa naomba arudie swali lake!
Jaji: Swali lake rahisi sana nitakusaidia kukuelewesha. umetaja Ofisi za ZCO, RPC Ilala Je Kule Mbweni Ofisi zipo au hazipo?
shahidi: Mh. naomba ni mjibu wakiliwakili Mallya: Jibu Ofisi zipo au hazipo?
shahidi: hazipo
Wakili Mallya: Sasa hilo ndipo jibu ndugu shahidi
Jaji anasema; kwa sababu ya Afya zetu nahairisha shauri hili kwa dakika 10 tu halafu tutarejea..Mahakama inarejea
Jaji ameingia
Kesi inatajwa tena
Mafaili yana pandishwa kwa jaji
Kila Mtu Yupo Kwenye eneo lake
Upande wa Utetezi na Upande wa Mashitaka
Shahidi inspector Mahita yupo palepale kizimbaniJaji anauliza kama Wakili Mallya amemamaliza
Jaji anauliza Wakili Dickson Matata Kama yupo Tayari Kuendelea
Wakili Dickson Matata nikumbushe Majina yako
shahidi Naitwa Inspector Mahita Omary Mahita
Matata nitakuwa sahihi nikisema wewe ni mtoto wa IGP mstaafu Omary Mahita?shahidi: Sahihi
wakili Matata Wakati Baba yako akiwa IGP wewe Ulikuwa wapi
shahidi: nilikuwa Chuo kikuu
wakili Matata: kwa hiyo wakati Baba yako alikuwa IGP ulikuwa na akili timamu?
shahidi: Ndiyowakili Matata: Unakumbuka kuhusu kauli ya Baba yako kuhusu kuwakuta CUF na visu kuhusu kuleta vurugu nchini?
wakili wa Serikali Objection
wakili Matata: naondoa Swali langu
wakili Matata Kituo cha kwanza Mwaka 2010 ulianzia Kazi wapi
Shahidi: Zanzibarwakili Matata: baada ya hapo ulikwenda wapi
shahidi: Arusha kuwa Msaidizi wa upelelezi wilaya ya Arusha
wakili Matata: nitakuwa sahihi nikisema unawajibika kupokea Maagizo yoyote kutoka kwa kiongozi wako?
shahidi: nawajibika kupokea Maelekezo yoyote kutoka kwa Kiongozi wanguwakili Matata: wakati mnawakamata watuhumiwa mlisema mlikuwa na kikosi Maalum?
shahidi: Kweli
wakili Matata: Kikosi hicho chote kimetokea Arusha?
wakili Matata: Na kikosi hicho kilikuwa chini ya RPC Kingai?
shahidi: Sahihi kabisaMatata: unakubaliana na mimi unapotoka kwenye eneo lako la kazi unapaswa kuwa na movement order?
shahidi: Kweli
Matata: na unapotoka Arusha Kwenda Moshi ni Mkoa Mwingine?
Shahidi: Kweli
wakili Matata: na unapofika mkoa mwingine unapswa uriporti kwanza kwa mamlaka ya Mkoa huo?Shahidi: ni kweli
wakili Matata: Katika maelezo yako hakuna uliposema umeripoti popote
shahidi: Lakini.........
Matata: Jibu ndiyo au siyo
wakili Matata: umeeeleza mahakama umeriport kwa nani?
shahidi: sikuileza Mahakamawakili Matata: kuna sehemu umetoa ushahidi kuwa Umeriport Moshi?
shahidi: Sijaja nao..
wakili Matata: Nyinyi mlipowakamata watuhumiwa ndiyo Mliwasafirisha Mpaka Dar es Salaam!
shahidi: Sahihi Kabisa
wakili Matata: Mallya kakuuliza kuhusu central sitaki kurudia hukoshahidi: nilishamjibu hilo wakili
wakili Matata: unapaswa unijibu mimi sasa hivi..
Jaji: anapswa anijibu mimi..
wakili Matata: Mheshimiwa Jaji, mimi ndiye ninayetaka Jibu lake
Jaji: nakuelewawakili Matata: katika Maelezo yako hakuna sehemu uliyozungumza kuwa Nyie baada ya Kufika Dar es Salaam mlifanya yote na kwenda kote huko hakuna ulipo zungumza kuwa umeongozana na Askari gani wa Dar es Salaam
shahidi: rudia Swali
Matata anarudia Swali lake hapa ndugu zangu..shahidi: nilieleza kuwa tarehe 8 ya Mwezi 8 kuwa nilipoitwa na ACP kingai tukakutana Central
wakili Matata: katika Maelezo yako umezungumzia kuhusu Watuhumiwa Kupelekwa Mbweni, je umewahi kusikia Pale Central Kuna Mtuhumiwa alishwahi Kutoroka?
shahidi: watuhumiwa wanatorokaJaji: Mbona swali rahisi sana shahidi, labda walishawahi kutoroka au hujui
Shahidi: Mimi sijui aisee
wakili Matata: kati ya Central Police Dar es Salaam na Mbweni Police Station wapi pana Usalama zaidi?shahidi: kama nilivyoeleza kuwa kutokana na viongozi kusema watuhumiwa wapelekwe Mbweni kwa usalama
wakili Matata: nakuuliza wewe siyo viongozi wako tafadhali
shahidi: Kama nilivyosema Mbweni ndiyo sehemu sahihi ya kuwapeleka watuhumiwa hao na pana usalama zaidiwakili Matata: utakubaliana nami wakati mnasema mlifika DSM haujasema mli' report kwa nani?
shahidi: Sahihi Kabisa
Matata: tutoke huko turudi kwenye ukamataji, ni sahihi hujjazungumza kuwa kabla ya kuwasachi watuhumiwa kuwa nyie mlisachiwa na nani kwa mujibu wa sheria?shahidi: ni kweli sijazungumza hilo
Matata: katika mazungumzo yako yote hujazungumza kuwa ni wakati gani walichukuliwa maelezo
shahidi: ni sahihi sijazungumza
Matata: Shahidi ulisema ulikuwa kwenye kikosi kazi na kuwasafirisha kutoka Dar es Salaam, Utakubaliana na mimi?kuwa wakati yanafanyika yote wewe ulikuwa sehemu ya Kikosi kazi?
shahidi: hauko sahihi mheshimiwa
Matata: usahihi ni upi?
shahidi: kuna wakati sisi tulikuwa tunaendelea na kazi zingine na nilishaeleza
shahidi: haupo sahihi..wakili Matata: umeeeleza kuwa watuhumiwa walikuwa ni makomandoo?
shahidi: kweli
wakili Matata: Makomandoo ni watu ambao wana mafunzo ya Kijeshi, utakubaliana na mimi wanahitaji security zaidi, ni kweli.?
shahidi: sahihiwakili Matata: wakati mnazungumzia kuwakamata haujazungumzia kuwafunga pingu
shahidi: si kweli
wakili Dickson Matata amemaliza anamshukuru Jaji anaenda kukaa..
Sasa ni zamu ya wakili Msomi, Peter Kibatala..wakili Kibatala: nauliza swali ninalouliza mara zote. je unafahamu kuwa kazi ninayoifanya siyo personal?
shahidi: kweli
wakili Kibatala: mwambie Mheshimiwa Jaji kilichokufanya ushindwe kuja jana ni kwasababu ulikuwa una process kibali cha kijeshi!wakili Kibatala: mwambie Mheshimiwa Jaji kilichokufanya ushindwe kuja jana ni kwa sababu ulikuwa una process kibali cha kijeshi..
shahidi si kweli, umepata wapi taarifa? nilipata Jana asubuhi..
Kibatala: wapi?
shahidi: kwa Afande Kingaiwakili Kibatala: ooohhh! Mwambie Jaji kuwa umewasiliana na Afande Kingai jana saa 3 Asubuhi
shahidi: lakiiiiiiiiiiniiiiiiiiii.......
wakili Peter Kibatala: jibu kulinda heshima yako tafadhali..
shahidi: ndiyo niliwasiliana na Afande KingaiKibatala: Je unafahamu kuwa Kingai alikuwa Shaidi kwenye kesi hii
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: uliona wapi?
shahidi: niliona kwenye mitandao ya kijamii
Kibatala: Kwenye mtandao gani?
shahidi: Twitter
Kibatala: umekana proceeding za maswali na majibu pia
shahidi: HapanaKibatala: nani kakwambia uje kuzungumzia suala ya Chakula Moshi na Himo?
shahidi: ni Jambo la wazi. ndiyo uhalisia.
Kibatala: Nani alikwambia uje kuzungumza masuala ya chakula mahakamani?
Shahidi: Hakuna, ni mambo ya kawaida kwa mwana damu kulaKibatala: unafahamu leo umekuja kwa ajili ya kesi Ndogo, na mojawapo ya MAHAKAMA inachokiangalia ni MAMBO mliyowatendea watuhumiwa ya kuwatesa?
shahidi: hilo nafahamu
Sauti ya Adhana inasikika KIBATALA anamuomba Jaji kupisha Adhana
Jaji anaruhusu zoezi Kusimama kidogoKibatala: Kazi ya Kingai ilikuwa ni nini?
shahidi: ni Mkuu wa Msafara
Kibatala: Adamo pale Boma Ng'ombe alikula Chakula gani?
shahidi: woteeeeee
Kibatala Sitaki wote jibu, Adamoo
shahidi: alikuwa Nyama Choma na MO ENERGY
Kibatala: Nani alilipa?Kibatala: nani alilipia hicho Chakula
shahidi: Afande Kingai
Kibatala' bila shaka baada ya Kutumia aliomba kurejeshewe Pesa zake za kulipia watuhumiwa chakula?
shahidi: siwezi kumjibia
Kibatala: Ulishawahi kushiriki zoezi la retirement za pesa za Kingai alizotumia?Kibatala: Kuna sehemu Umeongelea kumkabidhi Afande Kingai risiti za matumizi yake aweze kurejesha alipopewa pesa
Kibatala: Moshi kuna kambi ndogo ya Jeshi
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo pale Moshi Central walikaa siku mbili?
Shahidi: sahihiKibatala: na wakati mnawaweka Moshi Central police walikuwa wana mafunzo ya Kikomandoo?
shahidi: Ndiyo!
Kibatala: kwa hiyo sababu zipi special zipo Mbweni na hazipo Central zilizopelekea Kupeleka watuhumiwa Mbweni?
shahidi Kituo cha Mbweni ni Class A na Kituo Cha Mbweni hako a Watu wengi tukaamua Kuwatenganisha kutoka Central kuwapeleka Mbweni sababu ya Complexity ga Nature yao
Kibatala: Mwambie Jaji kama ulizungumza chochote Kuhusu two Separates Cells Moshi
Shahidi: sikuongeleaKibatala: Mwambie Jaji kama umezungumza popote kuwa hujasema kuwa vituo vingine kama Salenda havina hadhi ya kuwapeleka
Shahidi: sikusema
Kibatala Unajua Goodluck alikuwa Mbweni
Shahidi: ndiyo nafahamuKibatala: unafahamu details za uchukuliwaji wa maelezo?
shahidi: sifahamu, Sikuwepo
Kibatala: Umeulizwa kuhusu kuandika STATEMENT
shahidi:Sahihi
Kibatala: katika maelezo yako uliyarekodi kama shahidi kuna sehemu umezungumzia washtakiwa walisimama ili walewakili Peter Kibatala: katika maelezo ya maandishi yako kuna sehemu umezungumzia washtakiwa kuwa walishawahi kupelekwa Mbweni...
Shahidi: Hapana..Kibatala sawa ngoja nimepelekee
Shahidi: Mheshimiwa Jaji ananionyesha kitu kingine
JAJI: Muonyeshe taratibu MTAKUWA MMESHA MCHANGANYA shahidi.
wakili Peter Kibatala anasoma PGO 236 (3) ix
Shahidi anarudia kila neno.
Jaji anamwambia atulie sasa kidogoKibatala anamaliza kusoma..
shahidi sasa ametulia baada mchanganyiko pale
Kibatala: Unajua ulipokuwa unafanya arrest ulikuwa unafanya arrest nje ya Kituo chako cha kazi?
shahidi: sahihi kabisa
Kibatala Mwambie Jaji kama leo umetamka haya maneno kama ulimwambia Adamooshahidi: Mheshimiwa wakili anasoma nukuu tofauti kwenye PGO
Jaji: shahidi hebu TULIA jibu unachoulizwa tafadhali, Mnafikiri na mimi sisomi hiyo PGO?
Kibatala: Je, ulisema kama ilivyoandikwa katika PGO?
shahidi: Hapana sikusema kama ilivyoandikwa katika PGOKibatala: nasoma PGO 236(3) sehemu ya 10, Kwamba inataka kurekodi jibu la Adamoo katika Notebook yako
shahidi: Mheshimiwa Jaji anataka kumsaidia Wakili Kibatala PGO 272
Jaji: HIYO SIYO KAZI YAKO
Kibatala: sasa soma hapa kwenye PGO
SHAHIDI anasoma PGO ya 26Kibatala: ni sahihi au siyo sahihi kuwa misingi yote inayoainishwa katika UKAMATAJI LAZIMA IFUATWE KAMA RULA?
shahidi: Sahihi
Kibatala: Unafahamu Notebook kuwa ni kifaakazi katika ukamataji?
shahidi: kama nilivyoeleza kuwa nikifaa changu binafsiKibatala: unafahamu kuwa unakuja kutoa ushahidi kuhusu Statement ya Adam kasekwa?
shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mwambie Jaji hujui kuwa ulikuja kutoa ushahidi kuhusu kesi ndogo katika kesi kubwa kuhusu malekezo ya Adamoo
Shahidi: hilo sifahamu..Jaji: kama amabavyo tunazungumzia ukamataji na mambo ya utu kuzingatia naomba na hapa mahakamani tuzingatie mambo ya utu ya kumtendea mtu..
wakili Peter Kibatala: Naomba unisomee hapa katika PGO kuhusu Notebook..shahidi: iasema kuhusiana na kuwa na Notebook lakini silazimishwi kama nakumbuka kila kitu mahakamani
wakili Peter Kibatala: sihitaji tafsiri yako
Jaji: anaingilia kati naona MMECHOKA..
wakili Peter Kibatala: anataka irudiwe kusomwa sehemu ya 7Baada ua mvutano Jaji anatoa dakika kadhaa mawakili wapumzishe vichwa vyao kuhusu mabishano ya shahidi kusoma PGO...
mawakili wa Serikali wanataka Tafsiri ya PGO isitolewe hapa isomwe tafsiri iachiwe mahakama...kesi inatajwa tena
Kibatala: Shahidi unavyofahamu lile eneo ambalo Adamoo alikamatwa ni RAO au RAU?
shahidi: kwa ufahamu wangu ni RAU
Jaji: unaweza Ku' spell
shahidi: R. A. U
Kibatala: unalifahamu kuhusiana na kesi hii kwa sababu ndipo ulipomkamatia Mshtakiwa?shahidi: Ndiyo
wakili Peter Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama unafahamu sehemu inaitwa RAO
shahidi: inategemea na MATAMSHI
wakili Peter Kibatala: Miye nataka wewe
shahidi: HAPANA, sifahamuKibatala: Mwambie hakimu kama mlipofila Dar es Salaam alfajiri kama mliwapa Chakula Watuhumiwa, uliongelea hilo
shahidi Hapana sijaongelea..
wakili Peter Kibatala: na unafahamu kuwa chakula ni moja ya haki za binadamu? Nani alimkabidhi mtuhumiwa Central?
shahidi Afande Jumannewakili Peter Kibatala: unazifahamu details za makabidhiano ya watuhumiwa?
Shahidi: sifahamu
Kibatala: nilisikia ulichukua maelezo ya Onyo kwa Mshitakiwa Adamoo Kuhusiana na Kosa la Kula Njama kutenda Matendo ya Kigaidi. Je unalifahamu hilo shtaka?
Shahidi: Hapanawakili Peter Kibatala: wewe shahidi ni mwanasheria?
shahidi: Hapana
wakili Peter Kibatala: ilikuwa muda gani baada ya kuwakamata ukasema kwa fact hizi kosa lao ni kula njama za KUTENDA MATENDO ya KIGAIDI
shahidi: Muda tukiwa Arumeru..Kibatala: kwa hiyo ni wewe ndiye ulifahamu hilo kosa au uliambiwa na Afande Kingai hawa wanatakiwa washitakiwe kwa makosa yapi?
shahidi: Afande kingai alituambia kesi ilifunguliwa DSM
Kibatala: kwa hiyo wewe ufahamu Details za shtaka lenyewe?
Shahidi: sifahamuKibatala: Nasikia, kuna mtu mlikamata wakati wa KUKAMATA?
Shahidi: NDIYO
Kibatala: Mwambie Jaji kwamba ni lini ulisadiki kuwa yale ni madawa ya kulevya
Shahidi: tukiona tunajua hiki ni kitu fulani, Tulitumia uzoefu wetu tu..
wakili Peter Kibatala: Mwambie Jaji kuwa mpaka leo unafahamu kuna report iliyotoka kwa mkemia yale ni madawa ya KULEVYA..
shahidi: sifahamu kwa sababu mimi siyo Mpelelezi..wakili Peter Kibatala: Unafahamu kwa mujibu PGO kuwa mtu yoyote anayepatikana na madawa ya kulevya anatakiwa afikishwe mbele ya Hakimu kwa haraka iwezekanavyo?
Shahidi: ndiyo nafahamu..
wakili Peter Kibatala: ulielezea ni siku gani mliwakamata watuhumiwa?
shahidi: Hapana, sikuzungumzia...
wakili Peter Kibatala: Ulizungumza ni lini mlitoka Moshi?
shahidi: Mimi sikuzungumzia..wakili Peter Kibatala: Je kwa ufahamu wako kosa la kula njama linahisiana na madawa ya kulevya?
Shahidi: inategemea
wakili Peter Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji iwapo unafahamu connections kati ya kesi iliyopo na madawa ya kulevya
wakili Peter Kibatala: Twende kwenye BundukiKibatala: je ni sahihi kwa mujibu wa PGO Pistol imekuwa Classified kama Property?
shahidi: nafahamu
wakili Peter Kibatala: unafahamu kwa sheria ya UGAIDI Pistol siyo Property?
Shahidi: sifahamuKibatala: Je unafahamu Pistol kama Property hasa kama haijulikani mmiliki wake ni nani kwa mujibu PGO 236 na 272?
shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Property ambayo Pistol haijulikani mmiliki wake ni nani, Utaratibu wake unakuwaje?
Shahidi: upelelezi ufanyikeKibatala: unafahamu chochote kuwa kuna upelelezi umefanyika mpaka mnawapeleka Mbweni kuwa Mmiliki wake ni nani?
shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Unakubaliana na mimi mtuhumiwa wa madawa ya Kulevya anatakiwa kupelekwa Mahakamani ili upelelezi ufanyike?
Shahidi: sifahamuwakili Peter Kibatala: Umezungumzia kuzunguka Moshi na Machame na Aishi Hotel, mliingia au hamkuingia?
shahidi: kama TIMU hatukuingia..
wakili Peter Kibatala: kama angekuwa NDANI usingejua?
shahidi: Kama timu tungejua baada ya kupata taarifa..shahidi: Kama timu tungejua baada ya Kupata taarifa
wakili Peter Kibatala: mimi nipo specific kuhusiana na Aishi Hotel, kuhusu taarifa za intelijensia mtuhumiwa mliambiwa kuwa yupo ndani au lah?
Shahidi: Mimi sijui...Kibatala: Mlipotola Arusha mlifanya Briefing Arumeru, Mwambie Jaji Taarifa zenu Adamoo, Lingwenya na Moses Lijenje kama waliishi Aishi Aishi Machame
shahidi: Nilikuwa sina
Niliambiwa Kuna waharifu tunaemda kuwakamata, Mimi sikuwa na taarifa kama watuhumiwa wanaishi Aishi Hotel
wakili Peter Kibatala: Shahidi Je, toka Mnafanya Briefing mpaka Mnazumguka nao kuna mahala popote ulikuwa unafahamu kama watuhumiwa wote watatu waliwahi kufanya mkutano Aishi Machame?
Shahidi: Hapana, sifahamu..shahidi: Hapana sifahamu
wakili Peter Kibatala: Mliwafanyia interview washtakiwa wakati mnazunguka nao
shahidi: Afande kingai alikuwa anaripoti kwenye Notebook yake..
wakili Peter Kibatala: Ukiiona utaikumbuka?
Shahidi: Hapana..wakili Peter Kibatala: Umeonyeshwa hapa MAHAKAMANI hiyo NOTEBOOK leo.?
shahidi; Hapana
Jaji anaingilia kati hapa.
Jaji anasema wakili Kibatala aendelee Jumatatu sababu ya muda..
Jaji natamani Kesi iwe inaisha Saa 11 Jioni
Jaji anaomba serikali iwahishe watuhumiwa..Jaji anasema anatamani kuona kesi ikiisha saa 11.
wakili wa serikali: Naomba kesi ihiarishwe mpaka Jumatatu..
Jaji anamuuliza Wakili Kibatala..
Kibatala: naridhia ihairishwe hadi hiyo Jumatatu..jaji anashukuru tena mawakili wa pande zote mbili kuendelea kuvumiliana hata pale hoja zilikuwa ngumu ngumu..
Jaji anasema, namna hii ndiyo tunaweza kufika mwisho vizuri.... Nahairisha shauri hili hadi Jumatatu, saa 4:00 Asubuhi kwa ajili ya kumalizia hoja za majumuisho..jaji ninawatakia Kheri wote hadi hiyo Jumatatu, ahsante sana, Jaji anasimama, polisi anapiga kelele zile za KOOOOOOOORRRRTIIIIII na wote tunasimama..
Mimi pia nawatakia jioni njema, na wapenda na tuendelee kusomana hapa, don't touch the dial. Same time same place. #MboweSioGaidi
Zaidi soma: Thread 'Kesi ya Mbowe na Wenzake: Shahidi ACP Ramadhani Kingai afunguka upande wa Jamhuri' Kesi ya Mbowe na Wenzake: Shahidi ACP Ramadhani Kingai afunguka upande wa Jamhuri
Leo tumepita getini bila bugudha na hakuna polisi wa nje zaidi ya hawa maalum wa mahakama
Hakika Jambo la jana kupigania haki ya mahakama na kutaka isimame kama mhimili huru ni nzuri sana
Jopo la mawakili wetu wa utetezi (mawakili wa Freeman Mbowe na wenzake) kama kawaida yao, limefika on-time, Mapema sana ikiwa sifa yake kuu nidhamu, Ushirikiano, upendo na kwenda na muda, pia kusikiliza na kujali hisia na sauti za ndugu, jamaa, marafiki wa wateja wao (watuhumiwa)
Ndugu zangu mnaouliza kuhusu shahidi wa leo ni nani, hakika wasikilizaji hatuwezi kufahamu. Hiyo ni kazi ya Jamhuri kuwasilisha jina la shahidi wao mbele ya mahakama kati ya wale mashahidi 24 waliotajwa kwenye preliminary hearing...
Hivi sasa ni saa 4 asubuhi na dakika zake 19 kwa saa za Afrika ya mashariki, bado mheshimiwa Jaji na mawakili wa upande wa Jamhuri (serikali) hawajaingia ndani ya chumba cha mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa. Mahakama sasa imejaa TOP!
Pia, tunawashukuru jeshi la polisi kutoka moyoni kabisa, mmepungua ndani ya chumba cha mahakama, mbarikiwe.. Eeh! Mmeona watu wameingia wenyewe mahakamani, wamejipanga wenyewe na sasa wanasubiri mahakama ianze. SISI ni wastaarabu na tunahubiri ustaarabu kila siku #MboweSioGaidi
Hivi sasa ni saa 4 na dakika 25 saa za Afrika ya mashariki bado mawakili wa serikali na mheshimiwa Jaji hawajaingia ndani ya chumba cha mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa..
Pamoja na kwamba polisi leo sio wengi kama siku zote, lakini kuna mzozo umeibuka hapa Mahakamani. Wananchi wanasema wamekosa nafasi za kuketi, hivyo wanaomba askari polisi wapungue mahakamani, wakaimarishe ulinzi wa raia na mali zao, ili nafasi zipatikane nyingi. Bado wapo!
Askari mmoja hapa anahamaki na kusema polisi na usalama nao wanayo haki ya kusikiliza mwenendo wa kesi maana ni open court na wanahoji kwamba tunapata wapi haki ya kuipangia mahakama nani wa kuingia na kukaa ndani? Swali hilo ukiwauliza wao kwanini walituzia jana, hawana jibu?
Raia bado wanasisitiza askari wasimame na kupungua mahakamani ndani, walinde watu na mali zao, ili wananchi wapate nafasi ya kuketi. Wananchi wanawakazia macho na kuwatambua. Lakini tunawaeleza wananchi watulie, waache askari hao wafuatilie kesi. Wasipate sababu kwamba VURUGU..
Hivi sasa ni saa 4 na dakika 53 kwa saa za Afrika ya mashariki, bado kesi inayowahusu Freeman Mbowe na wenzake watatu haijaanza, tunamsubiria mheshimiwa Jaji na mawakili wa serikali waingie ndani ya chumba cha mahakama.
Hivi sasa ni saa 5 na dakika zake 6 saa za Afrika ya mashariki.
Hali ya eneo la mahakama ni shwari kabisa, ni kata ya Sinza, wilaya ya Ubungo, Mkoani Dar es Salaam
Hali ya hewa ni mawingu kiasi na nyuzi Joto 27.7 inayoruhusu kabisa shahidi kuendelea na kesi, bila visingizio!
Pamoja na mheshimiwa Jaji kusisitiza Jana kuwa kesi ianze leo saa 4 kamili Kufuatia ombi la mawakili wa serikali, Lakini mpaka sasa, ni 5 na dakika 15 kesi bado haijaanza, lakini hatuelewi, labda sababu zilizo nje ya uwezo wao. Tuendelee kuwa na subira, maana yavuta kheri..
Mstari wa pili kutoka mwisho, wameketi waandishi wa habari (leo tupo nao live), Wameingia Kwa wingi sana kuliko Siku zote (inspiration), Leo na wao wamenufaika na msimamo wa Jana. Wabarikiwe.
Mstari wa mwisho (Backbench) wameketi watu mchanganyanyiko wakiwepo Polisi na TISS.
Sema kwa sauti mbowe sio gaidi
Unpopular opinion: wewe unadhani kwa kuchelewa huku mawakili wa serikali kuingia ndani ya chumba cha mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa, Je, wanamshauri DPP aachane na hii kesi dhidi ya Freeman Mbowe na wenzake maana wanajua #MboweSioGaidi, namna gani?
Jopo la mawakili wa utetezi
1.Peter Kibatala
2.Jeremiah Mtobesya
3.Jonathan Mndeme
4.John Malya
5.Evaresta Kisanga
6.Hadija Aron
7.Maria Mushi
8.Gaston Garubindi
9.Seleman Matauka
10.Ferdinand Makore
11.Dickson Matata
12.Rita Ntagazwa
13.Alex Masaba
14.Michael Mwangasa
Habari njema sana, ule mtiti mdogo wa wananchi umesaidia benchi lilikuwa reserved kwa makarao, wameanza kukaa familia na ndugu wa watuhumiwa..
Ubishi na makavu yanasaidia sana.. Tusiache kuongea na kupiga kelele kuhusu haki zetu wakati wote ndugu zangu. Msiache kuongea.
Jopo la mawakili wa utetezi (wanaitwa mawakili wasomi, utake usitake), yaani mawakili wa Freeman Mbowe na wenzake wakijadiliana jambo la kitaalam.. Unaweza kuwapa jina, hebu pendekeza jina, hii timu yao inapaswa kupewa jina gani?
Pamoja na kwamba watuhumiwa wamefikishwa mapema (tangu saa 3 asubuhi) na mawakili wa utetezi kufika mapema ndani ya chumba cha mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi, bado mawakili wa serikali hawajafika. Hivi sasa ni saa 5 na dakika 29 saa za Afrika ya mashariki
Shukrani za pekee leo zimuendee Wakili Gabriel Fikirini ambaye kafika mahakamani kwa mara ya kwanza akisafiri kutokea Jijini Mwanza kwa ajili ya kuongeza nguvu kwenye kesi ya Freeman Mbowe na na wenzake..
Wakili Deogratius Mahinyila (@AdvMahinyila) aliyetoka Jijini Dodoma hadi Dar es Salaam kuongeza nguvu tangu wiki iliyopita.. Niliwapa simulizi yake kwa ufupi, niwape tena? Umri wake ni mdogo mara 3 ya umri wa Humphrey Polepole na mara 5 ya umri wa Mzee Kabudi.
Wakili Deogratius Mahinyila (@AdvMahinyila) atakumbukwa akiwa mgombea wa udiwani kupitia Chadema Dodoma, kata ya Berega, alishitakiwa kwa makosa uhujumu uchumi, akiwa gerezani, Isanga (gereza katili) akafanya mitihani ya uwakili na kufaulu kuwa wakili wa mahakama kuu.
Mambo vip mkuu.
How was the case chief
====
Jaji: Mimi nimepata nafasi ya kutafakari , nilianza kwenye hoja iliyoibuliwa na wakili wa serikali, kumbukumbu za mahakama zinaonyesha Kibatala alisema kwa niaba ya Mawakili wote na Kwa niaba ya Washitakiwa wote siku hiyo ya 15.09.2020 uwakilishi ilikuwa kwa mawakili wote na kwaNiaba ya washtakiwa wote.
hivyo utenganisho inaanza Leo
ni maamuzi yangu kuwa mahojiano yaliyofanywa na Wakili Kibatala na Wakili Mtobesya kwa niaba ya Mawakili wote na washtakiwa wote
hivyo basi sioni sababu ya kumuita tena shahidi wa kwanzaJaji: Hivyo naangiza kuendelea na shahidi wa pili aitwe sasa tuweze kuendelea....
Jaji: katika Mwenendo wa Mahakama nimeondoa kuwa Kibatala ni Wakili wa mshtakiwa wa 4 kwa siku ya tarehe hiyo ya 15.. Kibatala aliwakilisha washtakiwa wote kwa niaba ya mawakili wote..Jaji anamuita Shahidi
Shahidi anaingia anajikwaa
Jaji: pole sana
Shahidi: naitwa Inspector Mahita
Jaji: wewe ni dini gani?
Shahidi: ni Muislamu
Jaji: unaweza kuapa?
Shahidi: Wallah Wabillah nathibitishaWakili wa Serikali : Shahidi ieleze Mahakama wewe ni Mkazi wa wapi
shahidi: Mkazi wa Morogoro
wakili wa Serikali: Unafanya kazi gani
Shahidi: Polisi
wakili wa Serikali: kabla ya 2021 leo ulikuwa wapi?
shahidi: nilikuwa msaidizi Ofisi ya Upelelezi Arusha wakili wa Serikali umenza lini Kazi ya Upolisi
Shahidi: 2010
wakili wa Serikali: katika Idara ya upelelezi huko Polisi upo tangu lini?
shahidi: Takribani miaka 8
wakili wa Serikali: Ukiwa msaidizi wa upelelezi majukumu yako ni yapi?shahidi: upelelezi wa Makosa ya jinai, ukamataji wa watuhumiwa, Kusimamia Askari ambao wapo chini yangu, Kupokea maelekezo ya Viongozi wangu, kufanya Upekuzi, kufanya escort za watuhumiwa, lengo la msingi Kuzia na kupambana na uhalifuwakili wa Serikali: nitakuuliza Mnamo tarehe 04 Mwezi 08 2020 tarehe hiyo ulikuwa wapi?
shahidi: nilikuwa kituoni natekeleza Majukumu yangu kama kawaida
wakili wa Serikali: kituo gani?
Shahidi: kituo cha kati
wakili wa Serikali: ieleze Mahakama 04.8.2020 jioni ilikuwajeshahidi: nilipigiwa simu na afande wangu ACP Ramadhan Kingai
wakili wa Serikali: eleza alikupigia simu akisemaje
shahidi: aliniambia niende ofisini kwake
wakili wa Serikali: eleza ulivyo tekeleza
shahidi: nilifika ofisini kwake
wakili wa Serikali: alikupa malekezo gani?shahidi: kuna kazi na Askari nitaondoka nao, kuna kazi na suala la kufuatilia
wakili wa Serikali: kitu gani kingine alikueleza?
shahidi: aliniambia niandae Askari wengine
shahidi: tuliaanza safari tukiwa dereva wake Constable Azizi
wakili wa Serikali: mlisimama wapi?shahidi: Polisi Arumeru, wilaya ya Usa river
wakili wa Serikali: Mkaelekea wapi?
shahidi: tulikuwa tunaelekea Kilimanjaro tukasimamama kituo cha USA river wilaya ya Arumeru
Jaji: mwanzo umeongea tofauti, umechanganya?
wakili wa Serikali: rudia Vizuri
shahidiolice Usa riverwakili wa Serikali: Polisi Usa river kilitokea nini?
shahidi: tulishika wote tukiwa na Afande Kingai tukapata Briefing ya kazi
wakili wa Serikali: Briefing uliyopewa ilihusu kazi gani?
Shahidi: Briefing niliyopewa ni kwamba kuna Kikundi kina panga kufanya matukio ya kigaidi
Shahidi: maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Arusha, Kilimanjaro, Dar es Salaam na Mwanza na pia kikundi hicho kilikuwa na nia ya kumdhuru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya
wakili wa Serikali: Elezea sasa mkafanyeje?shahidi: kwa kuwa kikundi hicho kilikuwa Mkoa wa Kilimanjaro Wilaya ya Moshi Mjini kwenda Kuwamakata
wakili wa Serikali: baada ya briefing kitu gani kiliendelea?
shahidi: tuliendelea na safari na tulifika majira ya Saa 2 Usiku. tukaendelea na upelelezi kuwakamata watuhumiwawakili wa Serikali: mliendelea na upelelezi mpaka muda gani?
shahidi: ilipofika majira ya saa 6 tukiwa tumewakosa ikabidi tubreak..
wakili wa Serikali: ieleze mahakama sasa tarehe 05 Mwezi wa 8 2020 mlifanya nini!shahidi: ilikuwa muda wa asubuhi tuliendelea kusubiri taarifa ambazo afande alikuwa akizopokea na ilipofika Saa 6 akaniambia kuwa watuhumiwa tuliokuwa tunawatafuta wameonekana Maeneo ya RAU MOSHI..
wakili wa Serikali: Rau ipo Maeneo gani?
shahidi: ipo kama unaelekea Key Hotelwakili wa Serikali: ifahamishe mahakama hatua mlizo chukua ni zipi.
shahidi: kwanza tuliuliza afande hao tunaoenda kuwakamata muonekano wao ukoje? Afande akasema mmoja alikuwa amevaa Shati, Mmoja alikuwa amevaa kama Kitenge na Mtuhumiwa wa tatu alikuwa amevaa Jezi ya mpira..wakili wa Serikali: watu mliotakiwa kuwakamata ni wangapi?
shahidi: watu watatu kwa mujibu wa Afande
wakili wa Serikali: baada ya hapo?
shahidi: tulifika maeneo ambayo walikwepo tukiwa na gari yetu yenye tinted, tuka Drop Section ya kwanza ambayo alioongoza Afande kingaiShahidi: section ya pili nili' drop mimi na Afande Francis na gari
timu ya kwanza ilikuwa inaelekea kwa watuhumiwa.
watuhumiwa walikuwa wameiona, watuhumiwa wawili walianza kutoka wakielekea nilipo mimi..
wakili wa Serikali: eleza uliwatambuaje.shahidi: section ya kwanza ya Afande Kingai ilivyotoka iliwafanya watake kukimbia, ilibidi kuwasimamisha kutaka kujiridhisha
wakili wa Serikali: ifahamishe Mahakama kwa namna gani uliwasimamisha
shahidi: nikawasimamisha kwa Sauti kali "Simama hapo chini ya ulinzi"wakili wa Serikali: baada ya response yako hiyo walifanya nini?
shahidi: walisimama, wakaamriwa kuweka mikono juu wakatii..
wakili wa Serikali: kitu gani kilifuata?
shahidi: nilijitambulisha, naitwa Inspector Mahita natokea Central Arusha nafanya kazi kwenye kikosi Maalumwakili wa Serikali: Baada ya kuwatambulisha?
shahidi: niliwaonya wakiwa wawili kuwa wanatuhumiwa kula njama za kutenda matendo ya ugaidi
wakili wa Serikali: wenzenu wakina Kingai wakati huo walikuwa wapi?
shahidi: walikuwa wanakuja, sababu walikuwa umbali mrefuShahidi: kingai akatoa order kwa Jumanne wapekuliwe
wakili wa Serikali: shahidi sasa ieleze Mahakama Jumanne alitekeleza vipi Maelekezo ya Kingai?
shahidi: alitekeleza, kuna mama mmoja alikuwa anashuhudia pale, aliwaambia wasogee karibu washuhudie anachokifanya..Shahidi: huyo mama alikuwa anauza supu..
wakili wa Serikali: ieleze Mahakama taratibu za Upekuzi.
shahidi: Mmoja ali amriwa asimame juu ambaye baadae nikaja kumtambua alikuwa anaitwa Adamoo Adama kasekwa
wakili wa Serikali: wakati huo ulikuwa unafanya nini?shahidi nilikuwa na afande Jumanne
shahidi: wakati afande anampekua upande wa kushoto wa suruali yake alikuta Luvern Pistol A5340
wakili wa Serikali: kitu gani kingine?
shahidi: aliendelea kumkagua mifukoni akamakuta na kete 58 ambazo baadae zilijulikana ni madawa ya kulevyawakili wa Serikali: kitu gani kingine?
Shahidi: alikuwa na simu yake
wakili wa Serikali: ieleze mahakama ndani ya Pistol palikuwa na kitu gani?
shahidi: ndani ya magazine palikuwa na risasi 3
wakili wa Serikali: baada ya upekuzi nini kilifuata?shahidi: Upekuzi uliofuatia ulikuwa wa Adam Ling'wenya. yeye wakati anapelekuliwa alikuwa na kete 25
wakili wa Serikali: mbali na kete ni kitu gani kingine?
shahidi: na simu yake
wakili wa Serikali kingine unachokumbuka
Shahidi: Hapana kwa sasa..wakili wa Serikali: mashahidi waliokwepo Unawakumbuka, ieleze mahakama majina yao..
Shahidi: nakumbuka majina yao ya kwanza ya Anita na Esther
wakili wa Serikali: baada ya Upekuzi nini kulifuata
shahidi: naona...
wakili Peter Kibatala: Objection aseme ni hear say au anakijuaJaji: mmeelewa?
wakili wa Serikali: ndiyo
shahidi: baada ya Upekuzi
shahidi: tulianza kujaza Certificate of Seizure
wakili wa Serikali: baada ya kusaini kilifuata nini?
wakili Peter Kibatala: Objection hajasema ilisainiwa
Jaji: ni kweli hajasema wakili wa Serikali?wakili wa Serikali: samahani mheshimiwa
shahidi: Baada ya kujaza Certificate of Seizure ilisainiwa na watuhumiwa
wakili wa Serikali mkaelekea wapi?
Shahidi: tukaelekea kituo cha kati Moshi
wakili wa Serikali: wakati mnaelekea Moshi Kitu gani kilifuata?shahidi: yalikuja magari 2 tukapanda
wakili wa Serikali: mkaelekea wapi?
shahidi: kituo cha kati Moshi
wakili wa Serikali: wakati mnaelekea Moshi kitu gani kilifuata?
Shahidi: Afande kingai aliwauliza kwa taarifa alizonazo walikuwa 3, je 3 Moses Lijenje yupo wapi?wakili wa Serikali: Majibu yao yalikuwa ni yapi? +
shahidi: walisema kweli walikuwa naye na wakakubali kutuonyesha alipokuwa, kwani walikuwa naye palepale wakati tunawakamata
shahidi: Afande kingai alitoa maelekezo Afande Francis aendelee kuwachukua maelezo..Shahidi: sisi tuliokuwa kwenye gari jeupe na Afande kingai pamoja na Jummane tukawa tumerudi RAU madukani kumtafuta mtuhumiwa mwingine Moses
wakili wa Serikali: nini sasa mlichofanya?
shahidi: baada ya kurudi tulimkosa..
Shahidi: lakini Adam na Ling'wenya wenyewe wakasema huyu kuna vijiwe vyake tulivyokuwa tunazunguka wote Moshi
wakili wa Serikali: baada ya kutoka Rau mkaelekea wapi?
Shahidi: tukawa tunazunguka maeneo mbalimbali. ndani ya Moshi Mjini, KCMC, Majengo yaani vijiwe vijiweShahidi: baadae tukaenda mpaka Boma Ng'ombe na Aishi..
Jaji: hebu rudia maeneo mliyozunguka ndani ya Moshi
shahidi anarudia.......
wakili wa Serikali: kwanini mlikuwa mnazunguka maeneo hayo?
shahidi: watuhumiwa wenyewe walikuwa wanatuongoza
wakili wa Serikali: ikawajeShahidi: tulimaliza saa nne au saa tano usiku
wakili wa Serikali: nini kilifanyika?
Shahidi: tulikaa pale Boma kwa sababu tulijua atapanda vibasi hadi saa 2 asubuhi. Tulikaa Boma Mg'ombe tukafanya kikao cha kipolisi asubuhi kwenye saa 2 mpaka saa 3. tukaelekea kituo cha katiwakili wa Serikali: mlielekea Kitio cha kati kufanya nini
shahidi: kuwaweka watuhumiwa mahabusu
wakili wa Serikali: siku inayofuata nini kilifanyika?
shahidi: saa 11 kuelekea saa 2 kwenda kuwafuata watuhumiwa mahabusu, kwa Afande alisema tuelekee Stand kuuShahidi: tulienda na watuhumiwa kwa sababu wao ndiyo wanamfahamu, na tulikaa Stand tukijua anaweza kuwa anataka kwenda kusafiri na kukaa stand bila mafanikio
wakili wa Serikali: nini kilifuata?
shahidi: tukielekea maeneo ya pale stand sisi na watuhumiwa tukaenda kupata chaiamejificha na baadae tukaeleka Sakina Arusha
wakili wa Serikali: ifahamishe kama Mlifika Arusha, Arusha mlipita maeneo gani?
shahidi: kwakuwa tulikuwa kwenye leading investigation moja kwa moja tulienda Sakina na hatukumkuta tukaona wanatupotezea mudawakili wa Serikali: baada ya kupata chai nini kilifuata?
shahidi: hoja iliibuka kwa watuhumiwa kuwa Moses ana dada yake Arusha
wakili wa serikali: baada ya hoja hiyo nini kilifuata?
shahidi: Afande Kingai alisema tupite kwanza kwenye vijiwe tulivyopata Jana anaweza kuwawakili wa Serikali: baada ya ya kuwakosa mlielekea wapi?
shahidi: tukielekea Moshi na Afande kingai akatoa malekezo kuwa kwakuwa kesi tunayoifuatilia imefunguliwa Dar es Salaam
wakili wa Serikali: unasema alitakiwa kuelekea Dar es Salaam kwa ajili ya nini?shahidi: kwa sababu Kesi ilifunguliwa Dar es Salaam tulitakiwa twende Dar es Salaam na kwa sababu matukio yalikuwa yafanyike sehemu mbalimbali ikabidi twende Dar es Salaam..
wakili wa Serikali: ieleze mahakama chakula cha mchana mlipata wapi?wakili Peter Kibatala: Objection anafundisha cha kuongea
Jaji: Objection izingatiwe
wakili wa Serikali: nimesikia Mheshimiwa Jaji
wakili wa Serikali: baada ya ya kuelekea Dar es Salaam nini kilifuata?shahidi: tukiwa njia panda Himo gari yetu ilipata Break Down, afande akaita gari nyingine na pale pana kuwa papo bize cha kula cha usiku ilibidi tupate pale.
wakili wa Serikali: kwa kuwa unasema mlipata Break Down ni majira gani mliondoka Pale?shahidi: tuliondoka majira ya saa 2 Usiku na Kufika Dar es Salaam Majira ya saa 11 Alfajiri siku ya tarehe 07
Jaji: Mlifika Dar es Salaam saa ngapi?
shahidi: saa 11 Alfajiri
wakili wa Serikali: nakurudisha nyuma mlipokuwa njia panda Himo unasema mlikula je ni akina nani hao?shahidi: sisi na Convoy yetu yote pamoja na watuhumiwa
wakili wa Serikali: baada ya kufika Central nini kilifuata hiyo saa 11?
shahidi: afande kingai alitupatia Break akatuambia Saa 1 turudi pale Central..
wakili wa Serikali: saa 1 kitu gani kilifanyika?shahidi: afande alitupa maelekezo tutoke kituoni pale Central na Goodluck na Asst. Inspector Swila kuendelea na upelelezi
Jaji: Mlipewa Maelekezo gani?
shahidi: Afande kingai alitupa maelekezo tutoke tuendelee kufanya upelelezi kuhusiana na watuhumiwa ambao bado hawajakamatwawakili wa Serikali: shahidi ieleze mahakama sasa muda wote mlipokuwa mnatoka na watuhumiwa, wakati huo walikuwa kwenye ulinzi wa nani?
shahidi: wakati huo mimi ndiyo nilikuwa nasimamia ulinzi
wakili Serikali: kwakuwa wewe ndiyo ulikuwa na watuhumiwa wakati wote ieleze Mahakamawalikuwa na hali gani?
shahidi: walikuwa na hali nzuri
wakili wa Serikali: sawawakili wa Serikali: Shahidi nakupeleka pia, kwamba Tarehe 7 mlikuwa Dar es Salaam na kwamba mlipewa maelezo kuendelea na upelelezi Je, ni lini tena uliitwa tena kushughukika na watuhumiwa??
shahidi anasita.. anasita tena hapa..
Namna gani pale..Jaji: anasema endeleeni wewe na anaekuongoza ni suala lenu
shahidi: niliitwa 08.8.2020 kituo cha Central na nilipofika nilikutana na Afande kingai na Jopo zima la timu na nilipewa malekezo kuwa watuhumiwa wale wote tuwatie Central pale lockup au tuwapeleke kituo cha MbweniShahidi baada ya kusitasita, sasa anaendelea hapa..
Anasema, kwa sababu ya msingi ni kwamba watuhumiwa kwa mafunzo waliyopitia inapaswa tuwapeleka kituo kingine
Jaji; rudia sababu ipi iliwafanya muwatoe Central police Dar es Salaam tafadhali ndugu shahidi..shahidi: afande Kingai alisema kutoka watuhumiwa wenyewe mafuno yao na Makomandoo, walikuwa ni Makomandoo wa JWTZ na kwamba Complexity ya upelelezi wenyewe sababu watuhumiwa wengine tulikuwa bado hatujawapata
kwamba tuwapeleke kituo cha Mbweni kwa a sababu Kuna Informationtulikuwa hatujazimalizia
wakili wa Serikali: kituo cha Mbweni kipo wapi?
shahidi: kipo Wilaya ya Kinondoni
wakili wa Serikali: mliowapeleka tofauti na wewe mlikuwa na akina nani?
Shahidi: ASP Jumanne, Asst. Inspector Swila, Detective Constable Goodluckwakili wa Serikali: unakumbuka Ilikuwa majira gani
shahidi: Saa nne kuelekea saa tano
Jaji: kama unaweza kufafanua ilikuwa ya Asubuhi au Jioni?
shahidi: ilikuwa Asubuhi?
wakili wa Serikali: Shaidi yapo malalamiko kuwa Watu hawa waliteswa!
shahidi: Hapana, hawakuteswawakili wa Serikali: walipata Treatment gani?
shahidi: walipata Treatment ya Dignity na Respect
wakili wa Serikali: ni hayo tu mheshimiwa Jaji
Jaji: Utetezi Je, mpo tayari kuendelea?
wakili Peter Kibatala: naomba kwanza tushauriane na wakili wa Mshtakiwa ili aanze..KIBWAGIZO..
Kwa hiyo askari polisi wa kikosi cha ACP Ramadhan Kingai walikunywa chai na magaidi, kiroho safi baada ya kupata breakdown eeh! Bado hawa magaidi rojo-rojo kweli, sio kama Osama Bin LADEN.. MAGAIDI??? Face with tears of joy
Tuendelee...Kimya kidogo, kisha anasimama wakili Nashon Nkungu..
Wakili Nashon Nkungu: nakumbuka tarehe 08 ulitoa maelezo Central police?
shahidi: sahihi kabisa
wakili Nashon Nkungu: anampelekea shahidi maelezo hayo..
Shahidi: anayakana kuwa siyo ya kwake sababu hajaya saini..Wakili Nashon: anamuomba sasa Jaji apewe rasmi maelezo hayo mahakamani ambayo shahidi wa pili aliyoyatoa kwa RCO Ilala..
wakili wa Serikali: anamuomba Jaji kuwa wakili aanze kwanza kusema anachotaka kabla ya maelezo..
Jaji: anauliza kwa tashwishwi, Maelezo yapo au hayapo?wakili wa Serikali wanakunali kuwa maelezo hayo yapo Mahakamani..
Jaji anamueleza wakili Nashon Nkungu kuwa Endelea kutengeneza msingi wako, na kisha uyatumie hayo maelezo...wakili Nashon: Shahidi Je, ni kweli maelezo uliyoyatoa katika statement yake ya RCO Ilala kuwa kulikuwa kuna kazi unaenda kufanya Moshi Baada ya kupigiwa na Afande kingai na kuwa ulikuwa hufahamu unaenda wapi tofauti na ulichosema kwenye statement yako?shahidi: ni kweli sikuwa najua mpaka nilipofika Arumeru
wakili Nashon: Je shahidi unaweza kueleza upande ambao mshtakiwa aliposachiwa alitolewa hiyo pistol kwa Demonstration?
shahidi anasimama anafanya kwa kitendowakili Nashon: kati yako na Kingai nani alikuwa na nafasi nzuri ya kuwaona watuhumiwa?
shahidi: wote
wakili Nashon: kwa hiyo ni sahihi nikisema kuwa alichokiona kingai ndicho ulichokiona wewe?
shahidi: kama nilivyosema mimi nilitokea kwa mbele..wakili Nashon: ieleze mahakama kuwa kati ya wewe na Kingai nani anaidanganya Mahakama, Sababu Kingai anasema mliwakamata wakati wanakunywa supu wewe unasema wakati wanatembea..
shahidi: Mimi sijui Kingai katoa ushahidi gani, maana sikuwepo..Nashon: Je shahidi unamfahamu BWIRE?
shahidi: siwezi kujibu
Jaji: Shahidi, unapswa kujibu
shahidi: sikuwa namfhamu kwa tarehe hiyo
Nashon: unaifahamu Police Notebook
shahidi: nafahamu
Nashon: unajua ulitakiwa kuna nayo mahakamani?
shahidi: taarifa ya siri mali ya polisiwakili Nashoni anakaa anamkaribisha wakili John Mallya
Malya: Shahidi ni sahihi Polisi wanapima Afya mara kwa mara?
shahidi: hiyo ni Jambo binafsi
Jaji: Shahidi Jibu tafadhali kama unafahamu au hujui
Mallya: umefanya kazi na Kingai kwa muda gani?
shahidi: kwa Miaka 3 au 2wakili Mallya: kwa hiyo nikisema Kingai ana matatizo ya kusahau au kupoteza kumbukumbu ni sahihi?
shahidi: siwezi kujibu
Jaji; toa JIBU
shahidi: sifahamu
Wakili Mallya: kwa hiyo nikisema Kingai ana kumbukumbu NZURI napatia.?
Shahidi: ndiyo!wakili Mallya: umeeleza katika msafara wemu mlianzia Moshi Je akija mtu akisema mlianzia Boma Ng'ombe atakuwa ni muongo?
Shahidi: Sifahamu.
wakili Mallya: unapswa ujue kwa sababu ulikwepo kwenye msafara..
shahidi: Ndiyo atakuwa anasema uongo..wakili Mallya: Umesema kuwa mliwapa chakula watuhumiwa ila hukutaja aina ya chakula wa kiasi cha chakula
shahidi: ndiyo
Wakili Mallya: Umezungumzia kuhusu kituo cha Polisi Central
shahidi: ndiyo
Wakili Mallya: Je ni Kwei pale kuna huduma zote ikiwemo mahabusu?
shahidi ndiyowakili Mallya: pale Central kuna polisi wengi kuliko Mbweni
shahidi: sahihi kabisa
Mallya: kuna Ofisi ya RPC ILALA?
shahidi: sahihi Kabisa
wakili Mallya: kuna ZCO?
shahidi: sahihi kabisa
Mallya: kuna Mkuu wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam?
shahidi: sahihi Kabisawakili Mallya: Je hawa polisi wote tuliowataja kule Mbweni Wapo?
shahidi: Mheshimiwa naomba arudie swali lake!
Jaji: Swali lake rahisi sana nitakusaidia kukuelewesha. umetaja Ofisi za ZCO, RPC Ilala Je Kule Mbweni Ofisi zipo au hazipo?
shahidi: Mh. naomba ni mjibu wakiliwakili Mallya: Jibu Ofisi zipo au hazipo?
shahidi: hazipo
Wakili Mallya: Sasa hilo ndipo jibu ndugu shahidi
Jaji anasema; kwa sababu ya Afya zetu nahairisha shauri hili kwa dakika 10 tu halafu tutarejea..Mahakama inarejea
Jaji ameingia
Kesi inatajwa tena
Mafaili yana pandishwa kwa jaji
Kila Mtu Yupo Kwenye eneo lake
Upande wa Utetezi na Upande wa Mashitaka
Shahidi inspector Mahita yupo palepale kizimbaniJaji anauliza kama Wakili Mallya amemamaliza
Jaji anauliza Wakili Dickson Matata Kama yupo Tayari Kuendelea
Wakili Dickson Matata nikumbushe Majina yako
shahidi Naitwa Inspector Mahita Omary Mahita
Matata nitakuwa sahihi nikisema wewe ni mtoto wa IGP mstaafu Omary Mahita?shahidi: Sahihi
wakili Matata Wakati Baba yako akiwa IGP wewe Ulikuwa wapi
shahidi: nilikuwa Chuo kikuu
wakili Matata: kwa hiyo wakati Baba yako alikuwa IGP ulikuwa na akili timamu?
shahidi: Ndiyowakili Matata: Unakumbuka kuhusu kauli ya Baba yako kuhusu kuwakuta CUF na visu kuhusu kuleta vurugu nchini?
wakili wa Serikali Objection
wakili Matata: naondoa Swali langu
wakili Matata Kituo cha kwanza Mwaka 2010 ulianzia Kazi wapi
Shahidi: Zanzibarwakili Matata: baada ya hapo ulikwenda wapi
shahidi: Arusha kuwa Msaidizi wa upelelezi wilaya ya Arusha
wakili Matata: nitakuwa sahihi nikisema unawajibika kupokea Maagizo yoyote kutoka kwa kiongozi wako?
shahidi: nawajibika kupokea Maelekezo yoyote kutoka kwa Kiongozi wanguwakili Matata: wakati mnawakamata watuhumiwa mlisema mlikuwa na kikosi Maalum?
shahidi: Kweli
wakili Matata: Kikosi hicho chote kimetokea Arusha?
wakili Matata: Na kikosi hicho kilikuwa chini ya RPC Kingai?
shahidi: Sahihi kabisaMatata: unakubaliana na mimi unapotoka kwenye eneo lako la kazi unapaswa kuwa na movement order?
shahidi: Kweli
Matata: na unapotoka Arusha Kwenda Moshi ni Mkoa Mwingine?
Shahidi: Kweli
wakili Matata: na unapofika mkoa mwingine unapswa uriporti kwanza kwa mamlaka ya Mkoa huo?Shahidi: ni kweli
wakili Matata: Katika maelezo yako hakuna uliposema umeripoti popote
shahidi: Lakini.........
Matata: Jibu ndiyo au siyo
wakili Matata: umeeeleza mahakama umeriport kwa nani?
shahidi: sikuileza Mahakamawakili Matata: kuna sehemu umetoa ushahidi kuwa Umeriport Moshi?
shahidi: Sijaja nao..
wakili Matata: Nyinyi mlipowakamata watuhumiwa ndiyo Mliwasafirisha Mpaka Dar es Salaam!
shahidi: Sahihi Kabisa
wakili Matata: Mallya kakuuliza kuhusu central sitaki kurudia hukoshahidi: nilishamjibu hilo wakili
wakili Matata: unapaswa unijibu mimi sasa hivi..
Jaji: anapswa anijibu mimi..
wakili Matata: Mheshimiwa Jaji, mimi ndiye ninayetaka Jibu lake
Jaji: nakuelewawakili Matata: katika Maelezo yako hakuna sehemu uliyozungumza kuwa Nyie baada ya Kufika Dar es Salaam mlifanya yote na kwenda kote huko hakuna ulipo zungumza kuwa umeongozana na Askari gani wa Dar es Salaam
shahidi: rudia Swali
Matata anarudia Swali lake hapa ndugu zangu..shahidi: nilieleza kuwa tarehe 8 ya Mwezi 8 kuwa nilipoitwa na ACP kingai tukakutana Central
wakili Matata: katika Maelezo yako umezungumzia kuhusu Watuhumiwa Kupelekwa Mbweni, je umewahi kusikia Pale Central Kuna Mtuhumiwa alishwahi Kutoroka?
shahidi: watuhumiwa wanatorokaJaji: Mbona swali rahisi sana shahidi, labda walishawahi kutoroka au hujui
Shahidi: Mimi sijui aisee
wakili Matata: kati ya Central Police Dar es Salaam na Mbweni Police Station wapi pana Usalama zaidi?shahidi: kama nilivyoeleza kuwa kutokana na viongozi kusema watuhumiwa wapelekwe Mbweni kwa usalama
wakili Matata: nakuuliza wewe siyo viongozi wako tafadhali
shahidi: Kama nilivyosema Mbweni ndiyo sehemu sahihi ya kuwapeleka watuhumiwa hao na pana usalama zaidiwakili Matata: utakubaliana nami wakati mnasema mlifika DSM haujasema mli' report kwa nani?
shahidi: Sahihi Kabisa
Matata: tutoke huko turudi kwenye ukamataji, ni sahihi hujjazungumza kuwa kabla ya kuwasachi watuhumiwa kuwa nyie mlisachiwa na nani kwa mujibu wa sheria?shahidi: ni kweli sijazungumza hilo
Matata: katika mazungumzo yako yote hujazungumza kuwa ni wakati gani walichukuliwa maelezo
shahidi: ni sahihi sijazungumza
Matata: Shahidi ulisema ulikuwa kwenye kikosi kazi na kuwasafirisha kutoka Dar es Salaam, Utakubaliana na mimi?kuwa wakati yanafanyika yote wewe ulikuwa sehemu ya Kikosi kazi?
shahidi: hauko sahihi mheshimiwa
Matata: usahihi ni upi?
shahidi: kuna wakati sisi tulikuwa tunaendelea na kazi zingine na nilishaeleza
shahidi: haupo sahihi..wakili Matata: umeeeleza kuwa watuhumiwa walikuwa ni makomandoo?
shahidi: kweli
wakili Matata: Makomandoo ni watu ambao wana mafunzo ya Kijeshi, utakubaliana na mimi wanahitaji security zaidi, ni kweli.?
shahidi: sahihiwakili Matata: wakati mnazungumzia kuwakamata haujazungumzia kuwafunga pingu
shahidi: si kweli
wakili Dickson Matata amemaliza anamshukuru Jaji anaenda kukaa..
Sasa ni zamu ya wakili Msomi, Peter Kibatala..wakili Kibatala: nauliza swali ninalouliza mara zote. je unafahamu kuwa kazi ninayoifanya siyo personal?
shahidi: kweli
wakili Kibatala: mwambie Mheshimiwa Jaji kilichokufanya ushindwe kuja jana ni kwasababu ulikuwa una process kibali cha kijeshi!wakili Kibatala: mwambie Mheshimiwa Jaji kilichokufanya ushindwe kuja jana ni kwa sababu ulikuwa una process kibali cha kijeshi..
shahidi si kweli, umepata wapi taarifa? nilipata Jana asubuhi..
Kibatala: wapi?
shahidi: kwa Afande Kingaiwakili Kibatala: ooohhh! Mwambie Jaji kuwa umewasiliana na Afande Kingai jana saa 3 Asubuhi
shahidi: lakiiiiiiiiiiniiiiiiiiii.......
wakili Peter Kibatala: jibu kulinda heshima yako tafadhali..
shahidi: ndiyo niliwasiliana na Afande KingaiKibatala: Je unafahamu kuwa Kingai alikuwa Shaidi kwenye kesi hii
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: uliona wapi?
shahidi: niliona kwenye mitandao ya kijamii
Kibatala: Kwenye mtandao gani?
shahidi: Twitter
Kibatala: umekana proceeding za maswali na majibu pia
shahidi: HapanaKibatala: nani kakwambia uje kuzungumzia suala ya Chakula Moshi na Himo?
shahidi: ni Jambo la wazi. ndiyo uhalisia.
Kibatala: Nani alikwambia uje kuzungumza masuala ya chakula mahakamani?
Shahidi: Hakuna, ni mambo ya kawaida kwa mwana damu kulaKibatala: unafahamu leo umekuja kwa ajili ya kesi Ndogo, na mojawapo ya MAHAKAMA inachokiangalia ni MAMBO mliyowatendea watuhumiwa ya kuwatesa?
shahidi: hilo nafahamu
Sauti ya Adhana inasikika KIBATALA anamuomba Jaji kupisha Adhana
Jaji anaruhusu zoezi Kusimama kidogoKibatala: Kazi ya Kingai ilikuwa ni nini?
shahidi: ni Mkuu wa Msafara
Kibatala: Adamo pale Boma Ng'ombe alikula Chakula gani?
shahidi: woteeeeee
Kibatala Sitaki wote jibu, Adamoo
shahidi: alikuwa Nyama Choma na MO ENERGY
Kibatala: Nani alilipa?Kibatala: nani alilipia hicho Chakula
shahidi: Afande Kingai
Kibatala' bila shaka baada ya Kutumia aliomba kurejeshewe Pesa zake za kulipia watuhumiwa chakula?
shahidi: siwezi kumjibia
Kibatala: Ulishawahi kushiriki zoezi la retirement za pesa za Kingai alizotumia?Kibatala: Kuna sehemu Umeongelea kumkabidhi Afande Kingai risiti za matumizi yake aweze kurejesha alipopewa pesa
Kibatala: Moshi kuna kambi ndogo ya Jeshi
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo pale Moshi Central walikaa siku mbili?
Shahidi: sahihiKibatala: na wakati mnawaweka Moshi Central police walikuwa wana mafunzo ya Kikomandoo?
shahidi: Ndiyo!
Kibatala: kwa hiyo sababu zipi special zipo Mbweni na hazipo Central zilizopelekea Kupeleka watuhumiwa Mbweni?
shahidi Kituo cha Mbweni ni Class A na Kituo Cha Mbweni hako a Watu wengi tukaamua Kuwatenganisha kutoka Central kuwapeleka Mbweni sababu ya Complexity ga Nature yao
Kibatala: Mwambie Jaji kama ulizungumza chochote Kuhusu two Separates Cells Moshi
Shahidi: sikuongeleaKibatala: Mwambie Jaji kama umezungumza popote kuwa hujasema kuwa vituo vingine kama Salenda havina hadhi ya kuwapeleka
Shahidi: sikusema
Kibatala Unajua Goodluck alikuwa Mbweni
Shahidi: ndiyo nafahamuKibatala: unafahamu details za uchukuliwaji wa maelezo?
shahidi: sifahamu, Sikuwepo
Kibatala: Umeulizwa kuhusu kuandika STATEMENT
shahidi:Sahihi
Kibatala: katika maelezo yako uliyarekodi kama shahidi kuna sehemu umezungumzia washtakiwa walisimama ili walewakili Peter Kibatala: katika maelezo ya maandishi yako kuna sehemu umezungumzia washtakiwa kuwa walishawahi kupelekwa Mbweni...
Shahidi: Hapana..Kibatala sawa ngoja nimepelekee
Shahidi: Mheshimiwa Jaji ananionyesha kitu kingine
JAJI: Muonyeshe taratibu MTAKUWA MMESHA MCHANGANYA shahidi.
wakili Peter Kibatala anasoma PGO 236 (3) ix
Shahidi anarudia kila neno.
Jaji anamwambia atulie sasa kidogoKibatala anamaliza kusoma..
shahidi sasa ametulia baada mchanganyiko pale
Kibatala: Unajua ulipokuwa unafanya arrest ulikuwa unafanya arrest nje ya Kituo chako cha kazi?
shahidi: sahihi kabisa
Kibatala Mwambie Jaji kama leo umetamka haya maneno kama ulimwambia Adamooshahidi: Mheshimiwa wakili anasoma nukuu tofauti kwenye PGO
Jaji: shahidi hebu TULIA jibu unachoulizwa tafadhali, Mnafikiri na mimi sisomi hiyo PGO?
Kibatala: Je, ulisema kama ilivyoandikwa katika PGO?
shahidi: Hapana sikusema kama ilivyoandikwa katika PGOKibatala: nasoma PGO 236(3) sehemu ya 10, Kwamba inataka kurekodi jibu la Adamoo katika Notebook yako
shahidi: Mheshimiwa Jaji anataka kumsaidia Wakili Kibatala PGO 272
Jaji: HIYO SIYO KAZI YAKO
Kibatala: sasa soma hapa kwenye PGO
SHAHIDI anasoma PGO ya 26Kibatala: ni sahihi au siyo sahihi kuwa misingi yote inayoainishwa katika UKAMATAJI LAZIMA IFUATWE KAMA RULA?
shahidi: Sahihi
Kibatala: Unafahamu Notebook kuwa ni kifaakazi katika ukamataji?
shahidi: kama nilivyoeleza kuwa nikifaa changu binafsiKibatala: unafahamu kuwa unakuja kutoa ushahidi kuhusu Statement ya Adam kasekwa?
shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mwambie Jaji hujui kuwa ulikuja kutoa ushahidi kuhusu kesi ndogo katika kesi kubwa kuhusu malekezo ya Adamoo
Shahidi: hilo sifahamu..Jaji: kama amabavyo tunazungumzia ukamataji na mambo ya utu kuzingatia naomba na hapa mahakamani tuzingatie mambo ya utu ya kumtendea mtu..
wakili Peter Kibatala: Naomba unisomee hapa katika PGO kuhusu Notebook..shahidi: iasema kuhusiana na kuwa na Notebook lakini silazimishwi kama nakumbuka kila kitu mahakamani
wakili Peter Kibatala: sihitaji tafsiri yako
Jaji: anaingilia kati naona MMECHOKA..
wakili Peter Kibatala: anataka irudiwe kusomwa sehemu ya 7Baada ua mvutano Jaji anatoa dakika kadhaa mawakili wapumzishe vichwa vyao kuhusu mabishano ya shahidi kusoma PGO...
mawakili wa Serikali wanataka Tafsiri ya PGO isitolewe hapa isomwe tafsiri iachiwe mahakama...kesi inatajwa tena
Kibatala: Shahidi unavyofahamu lile eneo ambalo Adamoo alikamatwa ni RAO au RAU?
shahidi: kwa ufahamu wangu ni RAU
Jaji: unaweza Ku' spell
shahidi: R. A. U
Kibatala: unalifahamu kuhusiana na kesi hii kwa sababu ndipo ulipomkamatia Mshtakiwa?shahidi: Ndiyo
wakili Peter Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama unafahamu sehemu inaitwa RAO
shahidi: inategemea na MATAMSHI
wakili Peter Kibatala: Miye nataka wewe
shahidi: HAPANA, sifahamuKibatala: Mwambie hakimu kama mlipofila Dar es Salaam alfajiri kama mliwapa Chakula Watuhumiwa, uliongelea hilo
shahidi Hapana sijaongelea..
wakili Peter Kibatala: na unafahamu kuwa chakula ni moja ya haki za binadamu? Nani alimkabidhi mtuhumiwa Central?
shahidi Afande Jumannewakili Peter Kibatala: unazifahamu details za makabidhiano ya watuhumiwa?
Shahidi: sifahamu
Kibatala: nilisikia ulichukua maelezo ya Onyo kwa Mshitakiwa Adamoo Kuhusiana na Kosa la Kula Njama kutenda Matendo ya Kigaidi. Je unalifahamu hilo shtaka?
Shahidi: Hapanawakili Peter Kibatala: wewe shahidi ni mwanasheria?
shahidi: Hapana
wakili Peter Kibatala: ilikuwa muda gani baada ya kuwakamata ukasema kwa fact hizi kosa lao ni kula njama za KUTENDA MATENDO ya KIGAIDI
shahidi: Muda tukiwa Arumeru..Kibatala: kwa hiyo ni wewe ndiye ulifahamu hilo kosa au uliambiwa na Afande Kingai hawa wanatakiwa washitakiwe kwa makosa yapi?
shahidi: Afande kingai alituambia kesi ilifunguliwa DSM
Kibatala: kwa hiyo wewe ufahamu Details za shtaka lenyewe?
Shahidi: sifahamuKibatala: Nasikia, kuna mtu mlikamata wakati wa KUKAMATA?
Shahidi: NDIYO
Kibatala: Mwambie Jaji kwamba ni lini ulisadiki kuwa yale ni madawa ya kulevya
Shahidi: tukiona tunajua hiki ni kitu fulani, Tulitumia uzoefu wetu tu..
wakili Peter Kibatala: Mwambie Jaji kuwa mpaka leo unafahamu kuna report iliyotoka kwa mkemia yale ni madawa ya KULEVYA..
shahidi: sifahamu kwa sababu mimi siyo Mpelelezi..wakili Peter Kibatala: Unafahamu kwa mujibu PGO kuwa mtu yoyote anayepatikana na madawa ya kulevya anatakiwa afikishwe mbele ya Hakimu kwa haraka iwezekanavyo?
Shahidi: ndiyo nafahamu..
wakili Peter Kibatala: ulielezea ni siku gani mliwakamata watuhumiwa?
shahidi: Hapana, sikuzungumzia...
wakili Peter Kibatala: Ulizungumza ni lini mlitoka Moshi?
shahidi: Mimi sikuzungumzia..wakili Peter Kibatala: Je kwa ufahamu wako kosa la kula njama linahisiana na madawa ya kulevya?
Shahidi: inategemea
wakili Peter Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji iwapo unafahamu connections kati ya kesi iliyopo na madawa ya kulevya
wakili Peter Kibatala: Twende kwenye BundukiKibatala: je ni sahihi kwa mujibu wa PGO Pistol imekuwa Classified kama Property?
shahidi: nafahamu
wakili Peter Kibatala: unafahamu kwa sheria ya UGAIDI Pistol siyo Property?
Shahidi: sifahamuKibatala: Je unafahamu Pistol kama Property hasa kama haijulikani mmiliki wake ni nani kwa mujibu PGO 236 na 272?
shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Property ambayo Pistol haijulikani mmiliki wake ni nani, Utaratibu wake unakuwaje?
Shahidi: upelelezi ufanyikeKibatala: unafahamu chochote kuwa kuna upelelezi umefanyika mpaka mnawapeleka Mbweni kuwa Mmiliki wake ni nani?
shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Unakubaliana na mimi mtuhumiwa wa madawa ya Kulevya anatakiwa kupelekwa Mahakamani ili upelelezi ufanyike?
Shahidi: sifahamuwakili Peter Kibatala: Umezungumzia kuzunguka Moshi na Machame na Aishi Hotel, mliingia au hamkuingia?
shahidi: kama TIMU hatukuingia..
wakili Peter Kibatala: kama angekuwa NDANI usingejua?
shahidi: Kama timu tungejua baada ya kupata taarifa..shahidi: Kama timu tungejua baada ya Kupata taarifa
wakili Peter Kibatala: mimi nipo specific kuhusiana na Aishi Hotel, kuhusu taarifa za intelijensia mtuhumiwa mliambiwa kuwa yupo ndani au lah?
Shahidi: Mimi sijui...Kibatala: Mlipotola Arusha mlifanya Briefing Arumeru, Mwambie Jaji Taarifa zenu Adamoo, Lingwenya na Moses Lijenje kama waliishi Aishi Aishi Machame
shahidi: Nilikuwa sina
Niliambiwa Kuna waharifu tunaemda kuwakamata, Mimi sikuwa na taarifa kama watuhumiwa wanaishi Aishi Hotel
wakili Peter Kibatala: Shahidi Je, toka Mnafanya Briefing mpaka Mnazumguka nao kuna mahala popote ulikuwa unafahamu kama watuhumiwa wote watatu waliwahi kufanya mkutano Aishi Machame?
Shahidi: Hapana, sifahamu..shahidi: Hapana sifahamu
wakili Peter Kibatala: Mliwafanyia interview washtakiwa wakati mnazunguka nao
shahidi: Afande kingai alikuwa anaripoti kwenye Notebook yake..
wakili Peter Kibatala: Ukiiona utaikumbuka?
Shahidi: Hapana..wakili Peter Kibatala: Umeonyeshwa hapa MAHAKAMANI hiyo NOTEBOOK leo.?
shahidi; Hapana
Jaji anaingilia kati hapa.
Jaji anasema wakili Kibatala aendelee Jumatatu sababu ya muda..
Jaji natamani Kesi iwe inaisha Saa 11 Jioni
Jaji anaomba serikali iwahishe watuhumiwa..Jaji anasema anatamani kuona kesi ikiisha saa 11.
wakili wa serikali: Naomba kesi ihiarishwe mpaka Jumatatu..
Jaji anamuuliza Wakili Kibatala..
Kibatala: naridhia ihairishwe hadi hiyo Jumatatu..jaji anashukuru tena mawakili wa pande zote mbili kuendelea kuvumiliana hata pale hoja zilikuwa ngumu ngumu..
Jaji anasema, namna hii ndiyo tunaweza kufika mwisho vizuri.... Nahairisha shauri hili hadi Jumatatu, saa 4:00 Asubuhi kwa ajili ya kumalizia hoja za majumuisho..jaji ninawatakia Kheri wote hadi hiyo Jumatatu, ahsante sana, Jaji anasimama, polisi anapiga kelele zile za KOOOOOOOORRRRTIIIIII na wote tunasimama..
Mimi pia nawatakia jioni njema, na wapenda na tuendelee kusomana hapa, don't touch the dial. Same time same place. #MboweSioGaidi
Zaidi soma: Thread 'Kesi ya Mbowe na Wenzake: Shahidi ACP Ramadhani Kingai afunguka upande wa Jamhuri' Kesi ya Mbowe na Wenzake: Shahidi ACP Ramadhani Kingai afunguka upande wa Jamhuri