Habari za kazi pia poleni na majukumu wapendwa,
Itakumbukwa katika kampeni za uchaguzi jimbo la kawe, mgombea wa Chama cha mapinduzi ambaye ndiye mbunge wa sasa wa Kawe mh Askofu Gwajima, alituhaidi vijana wa kawe kwenda mji wa Birmingham na Vijana wa Birmingham kuja huku kawe,
Kumekua na ukimya hapo katikati juu ya safari hii lakini leo naomba kuwafahamisha juu ya kinachoendelea
mpaka sasa baadhi ya vijana wa kawe tumeisha jipanga na wiki ijayo tunatarajia kwenda ofisi ya mbunge atupe utaratibu wa jinsi ya kupata paspoti za kusafilia ili isije ikaleta sintofahamu,
Tutakwenda pia kupata tarehe Rasmi ya kuelekea Birmingham, kwani tunaamini Askofu ni Mcha Mungu hawezi kutoa ahadi za uongo mbele ya kadamnasi,
Tunashukuru sana kwani haikua rahisi sisi kufika Mji wa Birmingham jimbo la Michigan USA tunamshukuru sana Askofu pamoja na Chama cha mapinduzi kwa ujumla,
Tunaomba muendelee kuwa na subira tutawafahamisha kila kinachoendelea pia tunaiomba serikali Isiweke ugumu kwenye upatikanaji wa paspoti kwani safari hii itajumuisha watu wengi sana
vile vile tunaomba mamlaka husika wawe waangalifi sana ili wasije wakajichanganya na vijana ambao sio wa Kawe,
tunaomba na wabunge wengine muige mfano huu mzuri wa mbunge wa kawe kwani italeta manufaa kwa watanzania wengi, tutakaapofika Birmingham tutajifuza mengi kwa faida ya vizazi vijavyo
update zinaendelea kuja......