UPDATES Mgomo wa Madaktari: - INTERNS WOTE WARUDISHWA MUHIMBILI BILA MASHARTI

watanzania wavivu,wanatafuta sababu tu.kwanini hawakujua madai yao mpaka interns wafukuzwe
 
Poleni sana wandugu kwa hili sakata, Ila tuwe makini sana hii serikali this tyme imeshindwa kuongoza watu kwa usahihi na inajaribu kutafuta njia hapo ili ilete wat iz DIVIDE AND RULE, na kwa kuliona hili we should be very careful hapa watawachuja watu kimyakimya na kwa kuwaacha interns wanataka kupunguza nguvu ya wenye madai NI KAMA MPANGO WA KUPOOZA HALI ILIYOPO I CAN ASSURE TUSIPOKUWA MAKINI WATATAFUTA WATU especial wale organizers, then put under stress, wanaweza wapewe barua za onyo or anythig ushauri, WATEKELEZE MADAI YOTE VILEVILE IN THOSE Agreements WE SHOULD SEEK IMMUNITY ya kutoguswa baada ya hili suala pplz
 
Kwanza walionyesha dharau kwa mainterns kwa kutowalipa kilicho chao halali japo kiduchu
Pili walionyesha dharau kwa fani ya udaktari baada ya kuwalipa maitern kwa masimango na baadae kuwafukuzia mbali
Tatu walionyesha dharau kwa madaktari bingwa baada ya kukataa madai yao kwamba maintern warudishwe Muhimbili maana hapo ndipo walipopangiwa tangu awali.

Sasa serikali ilisubiri watu wafe ndo waone kuwa kiburi chao hakina tija kwa afya ya taifa
Je kuwarudisha maintern ni nia njema au ni kutapatapa
Je kuna uhalali wa huyu katibu mkuu wa afya, mganga mkuu wa serikali na waziri wa afya kuendelea na nyadhifa zao wakati madaktari tayari wameshakosa imani na viongozi hawa?
Mwisho, serikali ipo tayari kujifunza kutumia hela kidogo ilizo nazo kwa matumizi ya msingi kama afya a elimu kwa wananchi badala ya posho hewa na matanuzi ya kisiasa -- mfano kutumia bilioni 50 kwa uhuru wa kihistoria wakati CT scan muhimbiili ikiwa moja nayo ni mahututi?
 
Hebu rudia kujisoma kwanza halafu urudi utuambie hapa mpenda majungu ni yupi hapa?
Watanzania bwana. Ila ni kawaida kwa wapiga majungu sishangai. Hivi kumbe kuna watu wanataka suluhu kati ya madaktari na Serikali isiwepo ili waendeleea kupiga majungu, mara Serikali haisikilizi matatizo, mara Serikali inacheza na afya za wananchi wake. ili iweje sasa ina maana kweli hilo nalo limekuwa siasa kweli, Eti Chadema wanasema watatoa takwimu za vifo vilivyotokana na athari za mgomo wa madaktari, kisa eti kiongozi wao kafariki huko Muhimbili. Hizi si siasa? Kumbe kuna kila sababu ya kuamini kwamba mgomo huu ulikuwa na mkono wa baadhi ya wanasiasa. Angalia hata contribution mbalimbali za watu humu zinazohusiana na mgomo huo, ni ushabiki tu, watu wanathamani mgomo uendelee ili wafurahi ili ionekane kwmba Serikali imeshindwa.
Serikali iendeleze mazungumzo na Madaktari nao wakubaliane na Serikali badala ya kusikiliza maneno ya uchochezi. wapo watu ambao kwa makusukdi tu hawaitakii mema Nchi yetu. Wengine walishatamka kwamba Serikali haitatawalika na kwa maana hiyo wanafikiri kauli zao zisipotimia basi wataonekana kama ni manabii wa uongo na kuanzisha vituko vya kushawishi watu kugoma , kufanya fujo n.k. Kamwe kwa akili zangu siwezi kuwaona wanasiasa wa aina hiyo kama watetea wanyonge. Ni wachochezi/wabinafsi/wenye chuki/husuda n.k. Tuwaepuke hao. Tuache Serikali ifikie muafaka na Wafanyakazi wake ili chi isonge mbele. Kama kuna watu wana damu ya kupenda shari waende somalia, na kwingineko.
 
Sababu ya Matatizo yote haya ni Kiburi cha Brandina S.J Nyoni. Yeye priority zake ni kununua ving'amuzi vya magari manne kwa Shilingi 1.3 Billions na kulipa madeni hewa ya matibabu nje ya nchi badala ya kulipa hawa ndugu zetu Intern Doctors.
 
hii nchi tatizo ni kua na uongozi unaofanya kazi kwa kishikaji hakuna m2 aliye serius na majukumu aliyonayo. hili suala halikupaswa kufika hapa, ilihitajika busara kutoka kwa viongozi wa wizara toka kipindi ile cha interns hapa walipofikia wametaka wenyewe na ukizingatia wabunge wanatak laki 200/day nadhani madaktari wapewe chao na watumishi wengine kma walimu na polisi wapewe arrears zao pamoja na kuboreshwa allowance zao. enough is enough
 
Katika kuhaha kwa serkali kujaribu kutafuta suluhu ya mgomo wa madaktari leo serikali imekwenda kuonana na madaktari wakiwa katika vikao vyao visivyo na kikomo (extended meetings) pale starlight hotel. Delegation ilikuwa na wajumbe wafuatao: Waziri wa Utumishi - Hawa Ghasia, Waziri wa Afya - Haji Mponda, Katibu Mkuu Wizara ya Afya - Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa serikali - Deo Mtasiwa

Ujumbe wa serikali ambao kimsingi walisema wametumwa na Waziri Mkuu ulikuja kwa ajili ya kusikiliza madai ya madaktari na wao kujaribu kutoa utatuzi kwa yale yaliyo ndani ya uwezo wao.

Hata hivyo madai ya madaktari kwa mara nyingine tena waliambiwa na wao kupewa nafasi ya kutoa majibu ambayo walisema mengi kati ya hayo yanazungumzika na kwamba suala la interns (madaktari waliopo katika mafunzo katika vitendo) serikali imekubali kuwarudisha Muhimbili bila masharti yeyote. Suala la nyumba, risk allowance na mengineyo wamekubali kukaa na madaktari kupitia viongozi wao ili kujaribu kupata suluhu.

Hata hivyo madaktari wameazimia kuendela na vikao vyoa visivyo na kikomo mpaka hapo madai yao yatakapopatiwa ufumbuzi na kwambwa wajumbe waliambiwa wamfikishie waziri mkuu madai yao

Nawasilisha
Mod tunaomba uunganisha hz POST PLZ!
 
aibu yao itawaumbua na kuwagarimu wengi. Kilaza Mponda ndo atajua kukurupukia madaraka sio......
 
Back
Top Bottom