Updates: Kukamatwa kwa Wanachama wa CHADEMA Kanisani Mwanza

Hata sikuelewi
Nimekuuliza wapi uliona raisi kavaa kijani kanisani
Unaniletea habari za wajinga,

Ccm wakifanya upumbavu na nyie mnaiga upumbavu huo.

Nacho pinga ni siasa (haijalishi ni chama gani) ndani ya kanisa (bilakujali ni kanisa/zehebu gani).

..hata asipovaa kila mtu anajua ni ccm na anazungumza kwa niaba ya ccm.

..sasa kama miaka na miaka ni nyinyi tu anaohutubia makanisani na misikitini kwanini mnafura chadema au chama kingine wakionekana ktk nyumba za ibada?
 
..hata asipovaa kila mtu anajua ni ccm na anazungumza kwa niaba ya ccm.

..sasa kama miaka na miaka ni nyinyi tu anaohutubia makanisani na misikitini kwanini mnafura chadema au chama kingine wakionekana ktk nyumba za ibada?
Mkuu!
Mapinduzi ni gharama
Ya uhai, muda na pesa
Upinzani mmejianda kwa gharama ipi.

Potelea mbali siasa za kiafrika ni unafiki tu.
 
Wakuu, nimepata hii updates ila kwa kweli hata kama Polisi wetu wanatumwa basi at least watumie hata akili. Why wanalazimisha kujenga chuki isiyomithilika kwenye jamii?? Was it necessary?

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi na baadhi ya Askari Wanyama pori wanaozea gerezani kwa kufanya mauwaji Kanisani. anyways wacha niwape updates


Updates


Makamanda, habari za muda huu. Mpaka sasa hivi tunaendelea kushughulikia sakata la kukamatwa kwa viongozi na wanachama walipokuwa kwenye misa jana Kawekamo.

Walioko lock up ni Katibu wa kanda ya Victoria, Mwenyekiti wa Ilemela, Katibu wa Nyamagana na wanachama wengine jumla yao ni 20.

Baada ya kumuona OCD asubuhi ya leo, alitwambia kuwa wanatuhumiwa kwa kufanya vurugu kanisani na kwamba alipigiwa simu na viongozi wa kanisa.

Ilibidi tukauone uongozi wa kanisa Katoliki jimbo la Mwanza, tumeonana na msaidizi wa baba Askofu na akatuwezesha kuongea na askofu Mkuu Renatus Kwande.

Askofu Nkwande amesikitishwa sana na uongo wa jeshi la polisi na kuthibitisha kwamba hakukuwa na vurugu yoyote kwenye misa hiyo. Na alipokea matoleo ya Wana Chadema na kusali pamoja nao. Akawakaribisha wale chakula.

Wakati wanakwenda kunawa polisi wakavamia eneo hilo na kuanza kukamata kila aliyekuwa na sare za Chadema.

Awali asubuhi, walikwishakamata wanachama watano akiwemo mama Pambalu ambaye naye alikuwa anaigia kanisani.

Baba askofu katupa msaidizi wake tukaenda naye Kirumba na ameongea na OCD, sasa ocd kageuza kwa si kanisa lilimpigia simu bali ni waumini wawili mmojawapo anaitwa Gerlad Joseph. Msaidizi wa Askofu kawasiliana naye na sasa Askofu amemtuma katibu wake Padre Nyanda, tunaendelea kumsubiri hapa kirumba.

Msimamo wetu ni:
1. Wawaachie wote bila masharti ya dhamana.

2. Au baba Askofu akawadhamini waumini wake.

Wanzagi
Sare za Chadema na kanisan wapinawapi.C tumeamua tusichanganye siasa na Dini? Yaan hao walitenda makosa wakaamua kukimbilia kanisan bila haya uyo kiongoz wa dini akaamua kuwatetea
 
Hata sikuelewi
Nimekuuliza wapi uliona raisi kavaa kijani kanisani
Unaniletea habari za wajinga,

Ccm wakifanya upumbavu na nyie mnaiga upumbavu huo.

Nacho pinga ni siasa (haijalishi ni chama gani) ndani ya kanisa (bilakujali ni kanisa/zehebu gani).
Kinacholalamikiwa hapa ni polisi kuingia kanisani wakati wa ibada na kukamata watu ambao wamevaa nguo za aina fulani na wanao muombea mtu wao. Huo ni uonevu kwa sababu hamna sheria waliovunja. Wenye mamlaka ya kuweka dress code ni wenye kanisa na si mwingine. Viongozi wa kanisa waliisha toa tamko kuwa uvaaji wa nguo za kisiasa hauzuiwi kanisani. Ni kawaida kwa kikundi fulani kuvaa nguo zinazo watambulisha wakati wanaombea jambo linalowahusu, k.m. kikundi cha wakina mama n.k. Kuwanyima haki hii sio ishara nzuri.

Amandla...
 
Akimalizana na Chadema atakutafuta wewe au ndugu yako

Hapo ndio utajua dikteta hana undugu

Wewe endelea kukenua mimeno tu
Mnatumia maneno makali pasipo na uhakika! Kila kiongozi asiyekubaliana nanyi mnamuita dikteta! Huyu kama ana udikteta upi? Mnafundishwa uzuzu na zuzu kuu Tundu Lissu na kutishia nyau na ICC! Acheni utoto
 
Sare za Chadema na kanisan wapinawapi.C tumeamua tusichanganye siasa na Dini? Yaan hao walitenda makosa wakaamua kukimbilia kanisan bila haya uyo kiongoz wa dini akaamua kuwatetea
 
Kinacholalamikiwa hapa ni polisi kuingia kanisani wakati wa ibada na kukamata watu ambao wamevaa nguo za aina fulani na wanao muombea mtu wao. Huo ni uonevu kwa sababu hamna sheria waliovunja. Wenye mamlaka ya kuweka dress code ni wenye kanisa na si mwingine. Viongozi wa kanisa waliisha toa tamko kuwa uvaaji wa nguo za kisiasa hauzuiwi kanisani. Ni kawaida kwa kikundi fulani kuvaa nguo zinazo watambulisha wakati wanaombea jambo linalowahusu, k.m. kikundi cha wakina mama n.k. Kuwanyima haki hii sio ishara nzuri.

Amandla...
Mpwa wanajitoa tu ufahamu, usifikiri kuwa hawajui
 
Hata sikuelewi
Nimekuuliza wapi uliona raisi kavaa kijani kanisani
Unaniletea habari za wajinga,

Ccm wakifanya upumbavu na nyie mnaiga upumbavu huo.

Nacho pinga ni siasa (haijalishi ni chama gani) ndani ya kanisa (bilakujali ni kanisa/zehebu gani).
Wewe ni mjinga! Jitoe ufahamu tu

images (2).jpeg
 
-kwasasa kodi yangu inatumika vibaya sana ,wapinzani wasipokuwepo,wakiwa ccm tu,kutakuwa hakuna ukamataji wa wapinzani na kuwasafirisha km zaidi ya elfu 1 na kuwalipa per diem askari wanaowasindikiza.

-Kesi za kubumba za uhujumu uchumi zitakuwa hakuna hivyo kesi zitakuwa chache,kutakuwa hakuna haha ya serikali kuajiri majaji wengi na kuwalipa misharara minono,hivyo hivyo kwa magereza multiplier effect ,fedha za kuhudumia wahabusu zitapungua.
Wakimalizana na upinzani watawageukia nyie
 
Wanzagi- sikutegemea CHADEMA kuonyesha ujinga wa kiasi hiki. Mnachotaka ni kulichonganisha Kanisa hasa RC na KKKT na serikali na waumini ambao siyo CHADEMA- tunajua wakristo hupenda kuleta chokochoko pale ambapo nchi inakuwa na rais ambaye si Mkristo SASA MMEANZA.- NI UJINGA MTUPU MNAOFANYA
Utter nonsense
 
Jeshi la Polisi Tanzania waache kutumiwa na CCM , hawaoni wenzao huko Zambia vyombo vyao vya dola vya ulinzi na usalama vilikataa kutumika vibaya na chama tawala kilichongolewa tarehe 12 August 2021.
Kiutaratibu au kimfumo chama tawala kikishindwa tu uchaguzi mara moja chama hicho hubadilika kuwa chama pinzani. Hivyo vyama vya upinzani Tanzania mwenzao kwa nchi ya Zambia ni chama kilichoshindwa na siyo chama kilichoshinda.
 
Back
Top Bottom