Update kesi ya Masheikh wa Uamsho | 27 Aprili 2021: Jamhuri yashindwa kuwasilisha hati mpya yenye mashtaka 11 baada ya mengine 14 kufutwa na Mahakama

Sep 19, 2019
43
383
Bismillahir Rahmaanir Rahiim

SHURA YA MAIMAMU TANZANIA

KESI YA MASHEIKH LEO JUMANNE TAREHE 27. 04. 2021, MAHAKAMA KUU DAR

Leo Mashekh wamefikishwa tena Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kusikiliza mashtaka 11, yaliyobaki kwenye kesi baada ya kufutwa yale 14 mengine.

Hata hivyo shauri halikuzungumzwa kutokana na upande wa Jamhuri kushindwa kutimiza masharti yayotakiwa katika uamuzi ulitolewa Ijumaa.

Aidha baada ya hukumu ya tarehe 23/04/2021, iliyowapa ushinda mkubwa Masheikh kwa kufuta mashtaka makubwa 14, kati ya 25, yanayowakabili, upande wa Jamhuri walitakiwa leo kuwasilisha hati mpya yenye mashtaka 11, badala ya ile ya awali yenye mashtaka 25.

Hata hivyo upande wa Jamhuri haukutekeleza matakwa hayo ya kisheria na badala yake wameomba muda zaidi ili wapate kuyatekeleza.

Kufuatia hali hiyo Jaji ameakhirisha shauri hilo mpaka kesho saa 8 mchana ambapo wametakiwa kutekeleza matakwa hayo ya kisheria.

Aidha Shura ya Maimamu inawakumbusha wananchi kuwa karibu na mashauri haya ili kujifunza mambo kadhaa ikiwemo mfumo wetu wa Sheria, Uongozi na dhana ya Utawala Bora.

Ibrahim Z. Mkondo
Msemaji wa Shura ya Maimamu Tanzania.
0713118812*
 
Wasiachie ao wataleta shida kwenye nchi yetu. ikiwezekana wanyongwe tuu
Acha roho mbaya,ujue wanafamilia zinawategemea kwahiyo wakinyongwa watoto wao unataka watunzwe na nani?.acha Sheria ichukue mkondo wake.Ingawa wakiachiwa na waanze tena harakati zao za uamusho na kuwachochea vijana kuchoma makanisa hapo ndipo wakamatwe wafungwe maisha ila sio kuwanyonga.
 
Hao watu wakatwe vichwa vyao si wa kuwaacha mtaani. UISLAM HUO HAUPO KOKOTE DUNIANI. MIMI NI MUISLAM SAFI KABISA ILA KWA HAO WAKATWE VICHWA VYAO. ALLAH (S.W) hajatupa elimu ya dini ili tulete mgawanyiko bali tuwasaidie wale wasiojua waweze pata kujua. Walikuwa wanatumika kisiasa badala ya kidini. Binafsi hata wakiachiwa mimi nitapambana mpaka niwe RAIS na nitume watu wakawatengue viuno vyao.

Upuuzi kama huu si wa kuuchekea hata kidogo. Gharama ya kuitafuta AMANI ni kubwa mno kuliko kuwapiga risasi za vichwa hao magaidi. Kuwaacha ni UPUMBAVU wa kiwango cha juu mno.

Mnaowatetea jaribuni kufatilia video zao YOUTUBE utapata mwanga fulani kuwa hawa si watu wa dini. Tunao mashekhe wa muda mrefu, Shekhe Sule, Mazinge, Khishki, nk wanajielewa mno. Wanakupa darsa na unaelewa juu ya ALLAH (S.W) pamoja na mtume wake Muhammad (S.W.A).
 
HAPA NAPITA maana kuachiwa kwao kunanukia lakini madai yao ya kutaka zenj ijitenge watayarudia tu na kujitenga na Tanganyika
Hapo ndipo patakuwa patamu
Basi ni jambo la heri kuombea watoke ili wasaidie kufanikisha huo mchakato wa hiyo Zenj kujitenga na Tanganyika. Muhimu tu watumie njia za amani na ushawishi kwa wananchi!

Na siyo kutumia njia ya kuhubiri chuki kwa wafuasi wao, na mwisho wa siku warudishe ule upuuzi wao wa kuwamwagia tindikali wakristu, nk.
 
Basi ni jambo la heri kuombea watoke ili wasaidie kufanikisha huo mchakato wa hiyo Zenj kujitenga na Tanganyika. Muhimu tu watumie njia za amani na ushawishi kwa wananchi!

Na siyo kutumia njia ya kuhubiri chuki kwa wafuasi wao, na mwisho wa siku warudishe ule upuuzi wao wa kuwamwagia tindikali wakristu, nk.
Ndio shida yao kubwa. Ndio maana mm nataka wasiachiwe hata kama ni waislam wenzangu ila wapuuzi
 
Back
Top Bottom