Ibrahimu Zuberi Mkondo
Member
- Sep 19, 2019
- 43
- 383
Bismillahir Rahmaanir Rahiim
SHURA YA MAIMAMU TANZANIA
KESI YA MASHEIKH LEO JUMANNE TAREHE 27. 04. 2021, MAHAKAMA KUU DAR
Leo Mashekh wamefikishwa tena Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kusikiliza mashtaka 11, yaliyobaki kwenye kesi baada ya kufutwa yale 14 mengine.
Hata hivyo shauri halikuzungumzwa kutokana na upande wa Jamhuri kushindwa kutimiza masharti yayotakiwa katika uamuzi ulitolewa Ijumaa.
Aidha baada ya hukumu ya tarehe 23/04/2021, iliyowapa ushinda mkubwa Masheikh kwa kufuta mashtaka makubwa 14, kati ya 25, yanayowakabili, upande wa Jamhuri walitakiwa leo kuwasilisha hati mpya yenye mashtaka 11, badala ya ile ya awali yenye mashtaka 25.
Hata hivyo upande wa Jamhuri haukutekeleza matakwa hayo ya kisheria na badala yake wameomba muda zaidi ili wapate kuyatekeleza.
Kufuatia hali hiyo Jaji ameakhirisha shauri hilo mpaka kesho saa 8 mchana ambapo wametakiwa kutekeleza matakwa hayo ya kisheria.
Aidha Shura ya Maimamu inawakumbusha wananchi kuwa karibu na mashauri haya ili kujifunza mambo kadhaa ikiwemo mfumo wetu wa Sheria, Uongozi na dhana ya Utawala Bora.
Ibrahim Z. Mkondo
Msemaji wa Shura ya Maimamu Tanzania.
0713118812*
SHURA YA MAIMAMU TANZANIA
KESI YA MASHEIKH LEO JUMANNE TAREHE 27. 04. 2021, MAHAKAMA KUU DAR
Leo Mashekh wamefikishwa tena Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kusikiliza mashtaka 11, yaliyobaki kwenye kesi baada ya kufutwa yale 14 mengine.
Hata hivyo shauri halikuzungumzwa kutokana na upande wa Jamhuri kushindwa kutimiza masharti yayotakiwa katika uamuzi ulitolewa Ijumaa.
Aidha baada ya hukumu ya tarehe 23/04/2021, iliyowapa ushinda mkubwa Masheikh kwa kufuta mashtaka makubwa 14, kati ya 25, yanayowakabili, upande wa Jamhuri walitakiwa leo kuwasilisha hati mpya yenye mashtaka 11, badala ya ile ya awali yenye mashtaka 25.
Hata hivyo upande wa Jamhuri haukutekeleza matakwa hayo ya kisheria na badala yake wameomba muda zaidi ili wapate kuyatekeleza.
Kufuatia hali hiyo Jaji ameakhirisha shauri hilo mpaka kesho saa 8 mchana ambapo wametakiwa kutekeleza matakwa hayo ya kisheria.
Aidha Shura ya Maimamu inawakumbusha wananchi kuwa karibu na mashauri haya ili kujifunza mambo kadhaa ikiwemo mfumo wetu wa Sheria, Uongozi na dhana ya Utawala Bora.
Ibrahim Z. Mkondo
Msemaji wa Shura ya Maimamu Tanzania.
0713118812*