Upandishaji wa madaraja kwa Watumishi wa Umma: Waziri wa Utumishi tunaomba utoe ufafanuzi

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Mhe. Waziri wa Utumishi, ili kuondoa manung'uniko, upotashaji na sintofahamu iliyotokea baada ya mishahara ya mwezi huu wa June kutoka huku baadhi ya watumishi wakiwa wamepandishwa madaraja na kupata mishahara mipya ila hali wengine hakuna kilichobadilika, nakushauri utoe ufafanuzi wa jambo hili kwa umma.

Msingi wa malalamiko na sintofahamu iliyopo inatokana na kauli yako ya kuhakikisha watumishi wote wanaostahili kupanda madaraja wanapanda na kulipwa mishahara mipya mwezi huu jambo ambalo halikutokea kwa watumishi wote

Inawezekana kuna changamoto zilijitokeza kama vile hela ya kuwalipa iliyotengwa haikutosha tofauti na matarajio yenu au kumekuwa na kasoro nyingine zilizopeleka baadhi ya watumishi(inaonekana ni wengi tu) kutopandishwa. All in all, kwakuwa watumishi hawaelewi, basi malalamiko lazima yawepo, hivyo ni bora kutoa ufafanuzi na kueleza mkakati uliopo kwa wale ambao hawakupandishwa madaraja.

Mpaka sasa teyari kuna maneno mengi: kuna wanaodai mnapandisha kwa awamu, waliobaki watapandishwa mwezi ujao wa July, System imewatema kimakosa baadhi ya watumishi(imewaruka) n.k. Hivyo, utagundua kuwa kuna sintofahamu kubwa tu kuhusu hali hii kwahiyo ni bora serikali ikatoa kauli.

Information ni tiba panapokuwa na sintofahamu.
 
Halafu hizo walizolipwa baadhi ya waliopandishwa vyeo zilipitishwa lini?maana bunge ndiyo limepotisha bajeti inayoanza kutumika tarehe 1.07.2021
 
Inauma sana unamkuta mtumishi mwenzako mnayestahili wote kupanda, amepanda! Halafu wewe hujapanda! Na hujui lini utapanda! Maana hakuna tamko lolote lile!! Kana kwamba mambo yako shwari kabisa.

Mbaya zaidi miaka ya nyuma ilikuwa unapewa barua mwezi Juni, then mshahara mpya unaanza kusoma Julai mwishoni!
Sasa walichokifanya safari hii, wanajua wenyewe.
Haishangazi kuona hata walimu wapya nao wakilalamikia mfumo uliotumika kuajiri!

Wizara ina changamoto nyingi sana hii!!!
 
Kwenye kuwachimba mkwara maafisa utumishi mchengerwa na mwenzake walikuwa msitari wa mbele. Ila sasa wamekaa kimyaaaaaa kama hawapo vile 😅😅
 
Halafu hizo walizolipwa baadhi ya waliopandishwa vyeo zilipitishwa lini?maana bunge ndiyo limepotisha bajeti inayoanza kutumika tarehe 1.07.2021
Zile ndege mlinunua kwa hela iliyopiyopishwa na bajeti ya mwaka gani?
 
Suala la kupandisha watu madaraja mnatakiwa muelewe kuwa linakwenda kwa kujiridhisha na sifa za wanaopandishwa. Hopefully mwezi ujao wengi watakua wamepandishwa. Tuache siasa kwenye utendaji.
 
Kuna uhuni mwingi kwenye hili zoezi,Maafisa Utumishi wametanguliza waliotoa Rushwa,washkaji zao na Mademu zao wengine tunapigwa visingizio tu na sababu kibao na hayo maneno ya Matumaini.Shida si waziri wala Katibu Mkuu aliyesema lolote wala kuchukua hatua yoyote ndiyo maana Wakurugenzi wengi na Maafisa Utumishi wamejenga Jeuri.
 
Inauma sana unamkuta mtumishi mwenzako mnayestahili wote kupanda, amepanda! Halafu wewe hujapanda! Na hujui lini utapanda! Maana hakuna tamko lolote lile!! Kana kwamba mambo yako shwari kabisa.

Mbaya zaidi miaka ya nyuma ilikuwa unapewa barua mwezi Juni, then mshahara mpya unaanza kusoma Julai mwishoni!
Sasa walichokifanya safari hii, wanajua wenyewe.
Haishangazi kuona hata walimu wapya nao wakilalamikia mfumo uliotumika kuajiri!

Wizara ina changamoto nyingi sana hii!!!
Acha maneno yako wewe
Mimi nilisoma miezi 10
Wengine miezi sita....4...
 
Kuna uhuni mwingi kwenye hili zoezi,Maafisa Utumishi wametanguliza waliotoa Rushwa,washkaji zao na Mademu zao wengine tunapigwa visingizio tu na sababu kibao na hayo maneno ya Matumaini.Shida si waziri wala Katibu Mkuu aliyesema lolote wala kuchukua hatua yoyote ndiyo maana Wakurugenzi wengi na Maafisa Utumishi wamejenga Jeuri.
Ni bora kukaa kimya
 
Kuna uhuni mwingi kwenye hili zoezi,Maafisa Utumishi wametanguliza waliotoa Rushwa,washkaji zao na Mademu zao wengine tunapigwa visingizio tu na sababu kibao na hayo maneno ya Matumaini.Shida si waziri wala Katibu Mkuu aliyesema lolote wala kuchukua hatua yoyote ndiyo maana Wakurugenzi wengi na Maafisa Utumishi wamejenga Jeuri.
Waziri au wasaidizi wa waziri, kama mnapita humu, haya ndio yanayoongelewa sasa kazi kwenu.
 
Back
Top Bottom